Kufukuzwa Membe CCM: Hakika siasa ni Mchezo kama ilivyo Karata na Draft

Kufukuzwa Membe CCM: Hakika siasa ni Mchezo kama ilivyo Karata na Draft

Naaaam, wananchi wenzangu!

Nimefikiria kwa kina na kusoma comment za wananchi wenzangu dhidi ya maamuzi ya mwenyekiti wa CCM, kumfuta uanachama Mh. Bernard Membe.

Nimesoma jinsi watu wengi wanavyo comment kwa mihemuko ya kumhurumia Membe.

""JAMANI CCM WANA MBINU NYINGI MNO ""

Hili ni lazima wananchi wenzangu ambao ndiyo wapiga kura, tuamke na kuelimisha wenzetu hasa huko mitaani na huko vijijini.

Kila mwaka wa uchaguzi, CCM hujipanga vyema kupitia makada wake, mbinu kadhaa wa kadhaa, safi na chafu, za siri na za kuelimisha ilimradi kushinda uchaguzi.

Chambo ya Membe haina tofauti na ile ya Lowasa.
Kwa mtazamo wetu sisi wapiga kura, ni kama CCM na Mwenyekiti wake, wamehitalifiana vibaya sana na Membe, hilo si kweli hata kidogo, huyo wamemtuma ili kudhohofisha upinzani na kutugawa wapiga kura.
Na kwa mpango huu Magufuli atashinda kwa urahisi sana uchaguzi huu ujao.

Wanachofanya CCM, ni kumuandaa kada mmoja wenye nguvu, kabla ya uchaguzi aonekane mwenye ugomvi na serikali au chama, halafu atangaze kuhamia upinzani.

Membe atahamia ACT WAZALENDO, hata Zitto anavyoonekana mpinzani mkubwa wa serikali na CCM, yawezekana kabisa katika kipindi hiki lao ni moja, ila wanao umia ni wananchi/wapiga kura.

Naishia hapa, fungue macho, sumaye, lowassa ni mifano tu, iliyotumika kutugawa na kupunguza makali ya kura zetu bila sisi kujua na hivi sasa wanakula pension zao.

Nawakilisha, kukubaliana kutokukubaliana ni BUSARA muhimu .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo nimekuja na hoja kuwahusu watu wanaojiita wana CCM wa huku mtadaoni ambao asilimia 90% niwanafiki na hawajui chochote kuhusu CCM

Mpo wapi mliomtukana Lowasa 2015 alipo i challenge CCM aliporudi mmesemaje?

kama upo humu uliyesema Lowasa mgonjwa kajinyea embu jiite James delicious ( Yule shoga maarufu )

mpo wapi mlioleta umbea kwa SUMAYE ?

Mko wapi mliokuwa mnawatukana wapinzani ambao leo wapo kwenu?
mfano waitara, Bashiru, na madiwani ?

kama kuna wanaume tuliobaki na msimamo toka zamani kuhusu siasa za kibongo naomba sana tujipige mkono kifuani tuseme hakika sisi sio mashoga.

bila kusahau wale ambao usiku wanaombea nchi ipate US AID alafu wakiwa nyuma ya keyboard wanamuita pompeo BEBERU.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwenye macho aliona, mwenye masikio alisikia

Nakumbuka ilikuwa mwaka 2015 mwanzoni tulishuhudia mvunjiko wa kamati kuu ya ccm ikiongozwa na mzee wetu Edward Lowasa na baaday kufuatiwa na Frederick Sumaye na washirika wengine ambao waliachana na chama chao kilezi na kujiunga na upinzani, Lowasa alijitahidi kuleta upinzani chama tawala na kwa mara ya kwanza Tanzania tulishuhudia ushindani mkali kutoka upinzani.

Tukumbuke ilikuwa 2015 uchaguzi mkuu. na hii ya mvunjiko wa Membe imetokea 2020 uchaguzi mkuu...

Swali... kwanini hii migogoro na mivunjiko inakuwa mingi kipindi cha uchunguzi? Isije ikawa ndio mtego kwa wapinzani waingie kichwa kichwa kwa Membe mwisho wa siku wamsahau muwakilishi wao kama ilivyokuwa 2015 kwa Dr. Slaa

huu ni mtego wapinzani wawe makini
 
Kutokana nakufukuzwa uanachama kwa mwana CCM mkongwe ndugu Bernard Membe,sababu nyingi zimetajwa kufukuzwa kwake kubwa zaidi ni kuonekana kumhujumu Rais na uchaguzi wa 2020 Kama ndivyo, huyu mhujumiwa amepitishwa tayari kuwa mgombea was urais 2020?

Hili pia limetajwa na mwenyewe Membe kuwa sababu ni Urais, je'ccm hawaingii kwenye Kura zamaoni? ukiangalia adhabu ya mzee Kinana zinafanana hii pia ukiangalia inafanana na ya mzee Lowasa, he democracies ndani ya CCM haipo?

Mwisho Ile kauli ya mama yetu makamu wa Rais namjumbe wa kamati kuu ya CCM mama Samia kuwa wasifukuze watu wakati wa kuelekea uchaguzi kwakufanya hivyo kunaipunguzia Kura CCM akasihi yaliotokea 2015 hawapendi yatokee 2020,na je'nimpango wakimkakati wakumtoa Membe?

kwakuwa huwenda akajiunga navyama vingine nakama nimpango huwenda akatumika kupunguza kura za upinzani? mfano akijiunga na ACT akapewa nafasi ya Urais atakuwa mpinzani mwenye nguvu ndani ya upinzani,nahii kufanya kuzipunguza kura za ushindi kutoka kwa chama chenye nguvu CHADEMA, nahapa ndipo viongozi wa upinzani wanapaswa kuwa makini kwa maamuzi kuelekea uchaguzi huu wa 2020.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siasa za bongo ni sawa na bongo movie maana mtazamaji unakua na uwezo wa kujua kitakachofuata lengo ilikua ni Bernard membe afukuzwe ili asigombee urais 2020 wengine walijumlishwa kama chambo but target ni Membe
 
FK21,
Wasubiri siku ya uteuzi wa wagombea inakaribia. Ndo siku watamjua Magufuli ni nani na wataamini tuliyowaambia kwamba, chama kimetekwa na mtu mmoja.

Sasa anaandaa mazingira ya kila kitu. Atawachagulia wagombea wa ubunge, udiwani, mawaziri, spika na mpaka gereza la kuwafunga wana CCM wenye viherehere.
 
MgumuNgara, Hao wote uliowataja hakuna alieanzisha vuguvugu ndani ya CCM ikafikia atuhumiwe kuwa NI msaliti na kuitwa kwenye kamati ya maadili akahojiwa na mwisho kufukuzwa uwanachama wa CCM.
kwa hiyo unavohisi, sio vitavokua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Salaam,

Kama inavyofahamika kuwa Mh. Membe jana amefutwa uanachama na Chama chama chake cha CCM hali inayomfanya achague mawili, ama kuachana kabisa na siasa ama kuhamia upinzani.

Membe akienda chama chochote cha upinzani na kupewa nafasi ya kugombania Urais ni wazi uchaguzi utachangamka sana na kuwa na mwamko na hari ila tuangalie ki undani.


Mosi, Membe ni Shushushu nguli na ndiyo kazi yake ya kwanza hivyo kuna uwezekano kabisa akatumwa na chama chake kudhoofisha upinzani na kisha baada ya uchaguzi kupita ikasemekana ameomba msamaha na kurudishwa katika chama chake cha CCM.

Pili, iwapo la kwanza si sahihi...hili la pili pia tulitazame iwapo Membe ataingia upinzani na kupewa nafasi ya kugombea Urais je kuna tija?

Lowasa alipoingia upinzani kulitokea mtafaruku mkubwa kwa Cdm kiasi cha kumpoteza katibu mkuu wake, Cuf kukatokea migogoro na kugawanyika na mwisho wake mzee akarudi nyumbani CCM huku upinzani ukibaki na majeraha.

Ni wakati muafaka wa kufanya tafakuri ya siasa yetu na kuacha mambo ya mihemko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wasubiri siku ya uteuzi wa wagombea inakaribia. Ndo siku watamjua Magufuli ni nani na wataamini tuliyowaambia kwamba, chama kimetekwa na mtu mmoja. Sasa anaandaa mazingira ya kila kitu. Atawachagulia wagombea wa ubunge, udiwani, mawaziri, spika na mpaka gereza la kuwafunga wana CCM wenye viherehere.
Hapa ndipo panaotwa utamu kunoga. CCM watajuta kushabikia udikteta.
 
Ilo lipo wazi Membe ni usalama wa taifa, kama ilivyokuwa kwa Mrema mwaka 1995

System wamemshauri Magufuli Vile ili kuweka mtego

Upinzani watafute mtu makini kama Tundu Lissu lakini sio makapi.
 
hahahahaa hivi ni vichekesho shida sio membe shida ni uraisi walioko madarakani wanajua membe atawazid kura na atawaangusha ndo maana wamemtoa uchaguz ukiisha watamrudisha ahahaha.

Hii picha kali sana kununua wapinzani na kuwatoa na kuwatisha wale wenye nguvu eti kisa wao kutinzana na mawazo ya watawala mzee mwenyekiti haya muambie arudishe kadi ili tujue umemfukuza au ni picha la kihind unalolicheza hahaha wanzania hatudanganyiki sasahivi tunataka haki ya kutoa mawazo kwa kila mtu iheshimiwe na sio kutishana ahahaha
 
Kwa maslahi ya mtu mmoja tu

Hakuna demokrasia CCM ni ubabe na udikteta
 
Back
Top Bottom