Je katiba mpya ni takwa la wanasiasa au la wananchi......??
Ni maoni yako. Kuna ambao wanapata maisha bora kupitia katiba hii hii. Kuna watendaji wanaongeza pato la taifa kupitia katiba hii hii.Nani amekwambia tunatafuta perfection ya 100%?
Tunachosema ni kuwa katiba ya siasa siyo muafaka wa kitaifa wa nmna tunavyotaka nchi yetu iongozwe.
The only reason CCM na Rais hawataki katiba mpya ni kwa sababu wanaitumia katiba hii kupora chaguzi za wananchi, kutapanya resources za Taifa kupitia mikataba ya kifisadi bila consequences.
Hakuna reason ya msingi ya wao kukataa katiba mpya!
Sema kimeumana..hahahahhahaha..nmefurah sana..mama anaupiga ule ule wa mzee baba sema kwa saut ya kinyonge sana.saf mama samiaMkuu kuna dikteta mwingine Ikulu anayedhani ana haki ya kutuamulia Watanzania vile atakavyo yeye kinyume na Katiba ya Nchi.
Unafikiri katiba mpya itasababisha mshinde uchaguzi? kwa nini usiamini katika kujenga vyema chama chenu? Je unafahamu kwamba Vyama vingi vya upinzani hapa nchini ni vya hovyo hovyo tena bado hawajitambua? Je malengo yenu ya katiba mpya yanalenga nini zaidi ya kutaka kushinda uchaguzi? Nitajie katiba mpya ya nchi yoyote ilivyosaidia graduate wote wa nchi hiyo kupata ajira,Nani anataka kupiga kura yake ya kuchagua Rais, Mbunge au diwani kisha kura hiyo ikaibiwa kwa mtutu wa bunduki? Chama kiko madarakani kwa miaka 60 sasa kimefanya lipi katika kuboresha uchumi wa nchi katika hiyo miaka 60? Ajira hakuna graduates wanasaga lami, elimu yetu ni ya hovyo sana, matibabu pia ni hovyo sana, usafiri pia ni hovyo sana. Mishahara ya wenye ajira ni ya chini mno miaka sita sasa bila nyongeza. Hebu tia akili kichwani japo KIDUCHU badala ya KUKURUPUKA.
Ni ngumu sana nchi hii kupata katiba nzuri kwasababu agenda yenyewe imetekwa na wanasiasa, tena uchwara.Je katiba mpya ni takwa la wanasiasa au la wananchi......??
Kuiheshimu katiba iliyowekwa kwa mujibu wa sheria ni kiapo chake, hilo halina mjadala, wala hahitaji kuomba ushauri kwetu
Ila tunachomwambia ni kuwa kuna sheria ya mabadiliko ya katiba, inabidi aitekeleze hiyo wananchi tupate katiba mpya, hilo nalo siyo hiari yake
Magwanda yanapwelepweta leoHATUTAKI KATIBA WALA MIKUTANO YA SIASA.
KILAUMBELE NI UCHUMI
Mama umenifurahisha sana leo, mabavicha yanakanyagana huko
Hii katiba ipo toka mwaka 1977 ingekuwa nzuri basi CCM wasingeiweka kwenye ilani ya uchaguzi mwaka 2015 ibadilishwe. Ofcourse tunajua kuwa Serikali ya Magufuli na Samia akiwa makamu wake ilifanya uhuni na kukataa kutekeleza suala hilo!Ni maoni yako. Kuna ambao wanapata maisha bora kupitia katiba hii hii. Kuna watendaji wanaongeza pato la taifa kupitia katiba hii hii.
Rwanda hana katiba nzuri lakini nchi yao inapaa kiuchumi.
Unafikiri katiba mpya itasababisha mshinde uchaguzi? kwa nini usiamini katika kujenga vyema chama chenu? Je unafahamu kwamba Vyama vingi vya upinzani hapa nchini ni vya hovyo hovyo tena bado hawajitambua? Je malengo yenu ya katiba mpya yanalenga nini zaidi ya kutaka kushinda uchaguzi? Nitajie katiba mpya ya nchi yoyote ilivyosaidia graduate wote wa nchi hiyo kupata ajira,
Mwisho naungana na wewe ukitaka katiba mpya ingawa malengo yako hayajaangalia masilahi ya walio wengi.
Samia ni mccm tu, Katiba Mpya na Tume huru ni kitanzi kwa CCM.Rais Samia anasema eti suala la kipaumbele kwake ni uchumi kwanza halafu mambo ya katiba mpya ni ya baadae huko mbeleni.
Ningependa kumkumbusha rais Samia kuwa, hoja ya katiba mpya ni hoja nyeti, ni suala muhimu sana na haliwezi kuwa option ya pili katika mambo yanayopaswa kufanyika nchini kwa sasa. Na hii ni kwa sababu zifuatazo
1. Katiba mpya haizuii kujenga uchumi
Rais anaposema eti tumpe muda ajenge uchumi kwanza ndo afikirie katiba mpya, tungependa kumueleza rais kuwa kuwa na katiba mpya hakumzuii yeye au serikali yake kukjenga uchumi, Labda Rais atueleze, je katiba bora iliyo nzuri inazuiaje yeye kuvutia wawekezaji, inazuiaje kuboresha utalii, inazuiaje kujenga miundo mbinu?. Hapa kimsingi rais hana hoja yenye mashiko kabisa juu ya kukataa kuwapa wananchi aina ya katiba wanayoitaka.
2. Mchakato wa katiba mpya si hisani ya rais bali ni hitajio la kisheria
Ipo sheria ya mwaka 2012 inayogovern mchakato wa mabadiliko ya katiba mpya, Sisi wananchi tunamtaka rais atekeleze sheria hiyo, asifanye hili suala kama hisani yake binafsi, hili ni hitajio la wananchi wengi.
3. Hofu ya rais ni ya kisiasa na si kimaslahi ya kitaifa
Kauli ya rais ya kukataa kuipa katiba kipaumbele ilianza kwenye awamu ya tano ambayo yeye alikuwa makamu wa rais, rais wa wakati huo na yeye alisema hoja hizohizo za kujenga uchumi kwanza kabla ya kuleta katiba mpya, leo hii tuna miaka mitano bado tunapigwa kalenda hizohizo za ngoja tujenge uchumi. Huhitaji kuwa genius kuona kwamba hofu ya viongozi hawa ni hofu za kisiasa tu, za kuhofia hatma zao na vyama vyao kisiasa iwapo Taifa litapata katiba mpya, ni dhahiri wahafidhina ndani ya CCM hawataki. katiba mpya, lakini kama alivyowahi kusema katibu mkuu mstaafu wa CCM, Hoja ya katiba mpya haitakufa mpaka ipatikane.
4. Kujenga uchumi bila kuwa na katiba ya kuulinda ni kazi bure
Hii katiba tuliyonayo inampa rais mpya power za kuvunjilia mbali mafanikio ya serikali zilizopita, anaweza kusitisha mradi wa kimkakati, anaweza kuingia mikataba ya siri isiyo na faida, anaweza kutapanya rasilimali zetu na asishtakiwe. Kwa hiyo ni dhahiri hata ujenge uchumi mzuri kivipi, bila katiba nzuri huwezi kuulinda uchumi huo, ndiyo maana hitajio letu la katiba mpya ni muhimu sana
5. Watanzania hatuko tayari kurudi katika utawala wa kidikteta aina ya awamu ya tano
Ktk utawala wa awamu ya tano tuliona matendo ya kinyama na kiuonevu yaliyofanyika, sababu mojawapo ya matendo hayo ni kuwa na katiba inayotoa mwanya mtawala kuvunja sheria bila consequences ikiwemo kushtakiwa, Katiba hii imetoa mamlaka makubwa kwa rais, na kiukweli ni katiba ya kidikteta, Hatuwezi kuruhusu scenario ya kupata aina ya uongozi wa awamu iliyopita, na guarantee bora ya kutofika huko ni katiba mpya na si maneno matamu tu ya rais Samia
Mimi nilisema Mkuu Maza sina imani naye sasa maneno yangu yametimia Mkuu.
Hiyo ni sawa na kumwuliza mtu kama anataka usingizi mzuri au godoro zuri.Mumewauliza wananchi kama wanataka Katiba mpya au wanataka uchumi?.Wananchi wengi,tunataka uchumi,tupate mkate wetu wa leo na kesho,mambo ya Katiba ni yenu nyinyi wanasiasa,sisi wananchi bora mkono uwende kinywani.Hebu anzeni nyinyi wanasiasa muwaulize wananchi,hata kwa kupiga kura,kwenye maeneo yenu.
Hao wanasiasa wanapigania katiba mpya kwa maslahi ya nani.....??Ni ngumu sana nchi hii kupata katiba nzuri kwasababu agenda yenyewe imetekwa na wanasiasa, tena uchwara.
Wananchi wamewekwa pembeni.
Je unadhani wananchi wana uelewa wa umuhimu wa katiba na faida za moja kwa moja zitokanazo na mabadiliko ya katiba mpya.......na kipi ni kipimo cha wananchi cha uelewa wao juu ya katiba mpya......??Nchi ina mfumo wa vyama vingi tangu 1992 kwanini maccm waendelee kufanya uhuni wao kwa miaka 30 sasa kukumbatia katiba ya mfumo wa chama kimoja? Kwanini Butiku na Warioba ambao ni maccm damu damu wanaunga hoja ya kuwa na Katiba mpya. Kwanini Bashiru kabla ya kuwa Katibu Mkuu wa maccm aliona umuhimu mkubwa wa kuwa na Katiba mpya?