Kuhusu Mungu na chanzo cha Ulimwengu, kuna mahali hatuna taarifa kamili/sahihi?

Kuhusu Mungu na chanzo cha Ulimwengu, kuna mahali hatuna taarifa kamili/sahihi?

kipawa kinachowezesha kufikiri, kuelewa, kuwasiliana, kujifunza, kupanga na kutatua matatizo.
Ulijuaje kinaitwa akili?

Au umekuta jina tu kipawa hicho kikiitwa akili?

Aliyekiita kipawa hicho akili alijuaje anacho na kuthibitisha kinaitwa akili kweli?

Au alibuni jina tu " Akili" na kuamua kuita hivyo, kipawa hicho cha kufikiri, kuelewa,kujifunza na kuamua?
 
Ulijuaje kinaitwa akili?

Au umekuta jina tu kipawa hicho kikiitwa akili?

Aliyekiita kipawa hicho akili alijuaje anacho na kuthibitisha kinaitwa akili kweli?

Au alibuni jina tu " Akili" na kuamua kuita hivyo, kipawa hicho cha kufikiri, kuelewa,kujifunza na kuamua?
Nadhani imetosha kukupa maana ya neno akili. Kama bado hujaelewa basi ni juu yako.
 
Subri apigwe na ugonjwa tu kama wa kisukari, kansa au figo uone kama ataendelea na ngonjera zake hapo juu.

Wewe hauwezi hata jiongezea japo umri ufikishe miaka 200, halafu unaanza kuvimba dhidi ya aliyeviweka vyote hivi tunavyoviona na tusivyoviona.

Hizo imani zote lengo mama ni kumuabudu na kumtafuta Mungu mkuu muumba wa vyote ingawa zinatofautiana utaratibu, hivyo inawezekana wote wakawa sahihi.
 
Akili ni neno la kufikirika tu.

Si kitu ambacho kinaonekana au kipo kwenye ubongo wa mwanadamu.

Ufanyaji kazi wa ubongo ndio ulipachikwa jina "Akili"

Ukipasua kichwa cha binadamu huwezi kuta hiyo akili
Akili ni sawa na ubongo? Yani unafananisha Mind na Brain? Nadhani unapaswa kufanya tafiti ya kina kuhusu akili/Mind.
 
NIELEWE KWA MAKINI SANA.

Mungu wa Israel
Mungu Allah,
Mungu wa wabudha,
Miungu ya kale pale misri,
Na Mungu au Miungu yote ambayo inaabudiwa ikiwemo mizimu na isiyo mizimu, ikiwemo hai na isiyo hai.

Ukweli mchungu ni huu, pamoja na ufahamu wetu wote tulionao lakini bado hatufahamu kuhusu Mungu ama chanzo cha ulimwengu.

Sisemi kuwa Mungu yupo au hayupo hapana, bali naandika kuhusu giza la ufahamu tulilonalo juu ya yupi ni Mungu sahihi ama kipi ni chanzo sahihi cha ulimwengu!

Nafahamu watu na imani zenu mnaona kama naandika maandiko yasiyosahihi!,ila naomba utulivu wa fikra zako japo kwa uchache tutazame vitu kwa undani zaidi.

Hebu fikiri imani uliyonayo sasa, najua wengi wenu mmeirithi toka kwenye jamii ulipozaliwa hivyo ulivyo laiti ungezaliwa katika jamii inayoabudu budha nawe ungeamini na kuabudu na pia ungejiona upo sahihi, imani ambayo ingekuwa tofauti nawe ungeona Kama ni uongo tupu!

Ulishawahi kujiuliza kwanini?
Jibu baki nalo!

Swali zuri nalotaka ujiulize ni kwanini tuna aina nyingi hivi ya Mungu/Miungu? Na wakati ukiangalia kiuhalisia sisi sote ni binadamu wamoja, mazingira mamoja, tunavuta hewa moja n.k.

Kwenye vitu vidogo vidogo hivi tunafanana lakini hili kubwa tunatofauti sana!

Anaeabudu tofauti nawewe unamuona sio sahihi, nayeye pia anakuona wewe sio sahihi!

So yupi ni sahihi?

Kipi kinathibitisha kuwa wewe sio au ndio unaeamini mahali sahihi?

Mtu aliekinyume na imani yako ambae amezaliwa nakuamini tofauti unafikiri amefanya kosa lipi kwa Mungu wako kwa kutokumuamini kuwa ndie Mungu sahihi, ikiwa hakupata ufahamu wowote juu ya Mungu wako?

Je, unafikiri kati yako na Mungu nani alistahiri kumtoa kwenye tope mwenzake nakumleta mahali sahihi?

Maswali haya nikuchokoza ubongo wako ili ufikiri na uelewe nini namaanisha.

Je, huyo Mungu wako mwenye uweza haoni kama ana hatia kwa kuiachia Miungu mengine iabudiwe na kuwapoteza watu wake na hata kuja kuwapa adhabu watu hao?

Ukweli mchungu mwengine ni huu, mpaka Sasa binadamu hatufahamu Mungu sahihi na ndio maana bado tuna Miungu mingi tunayoabudu!

Laiti kama usahihi wa Mungu kweli ungeonekana kati ya Miungu tunayoijua basi binadamu asingekuwa kiumbe mwenye kutapatapa ktk imani!

Kwani kusingekuwa nashaka juu ya Mungu husika kwenye vichwa vyetu!

Tumezaliwa nakukuta vitu hivi vya imani, tumerithishwa tukavipokea (wapo wasiopokea) na tukaviamini (wapo wasioamini pia).

Jiulize, kwani imeshindikana nini kumfahamu Mungu mmoja wa kweli pasipo kurithishwa?

Imagine uzaliwe ujue kunyonya,ujue kupumua ujue kutazama ila Mungu wa kweli usimjue bali urithishwe.!😀
Kimekosekana nini mpaka Tushindwe kumjua Mungu ndani yetu pasipo kufundishwa?

Binafsi mpaka hivi sasa katika Mungu na Miungu ambayo nimeilist hapo juu hakuna hata mmoja ambae logics zake zimeniingia akilini na kunishawishi kuwa yeye ndie Mungu wa kweli!

Hata robo ya ulimwengu jinsi unavyofanya kazi bado hatujaujua ama siri na kanuni za ulimwengu unavyofanya kazi bado hatujazijua!.
MIUNGU wengi tulionao tunaowaabudu bado hawana majibu juu ya chanzo chao pia na ulimwengu kiujumla! Nafikiri zipo sheria mama za kiulimwengu ambazo tukizigundua basi tunaweza kuujua ukweli wote!

Tunajikuta katika lindi la imani hizi kwasababu Kuna kitu hatujajua bado! Giza la ufahamu mbele yetu ndilo linatuweka katika matokeo haya!

Hatujui usahihi wa kweli ipi ndio maana tunatofauti katika Mungu tumuabudie!, kweli huwa haina mashaka ila uwezo wa ufahamu wako ndio unaamua ubebe kipi na uache kipi.

Kwa akili naufahamu wako umeamini kuwa wapo watu wameteuliwa kuwa karibu na Mungu, hivyo wanaweza kukusogeza karibu na Mungu! Kwanini sio wewe mwenyewe ikiwa wewe ni asili toka kwake?

Siamini katika Mungu wa mashaka ambae toka binadamu amekuwepo ktk dunia hii tunaambiwa yupo ila anawashukia wachache na hali ipo Kama hivi ilivyo! Hata kuthibitika kwake bado imekuwa ni mashaka au matendo yake hayathibitiki bali masimulizi!

Mungu ambae ameumba ulimwengu wenye sayari lukuki na akamtupa shetani katika dunia ambayo inaviumbe wake wapendwa! Mungu ambae anasema kwamba shetani amekuja kutujaribu hivyo ni kazi yake mwenyewe anaipima na Kama hukuwa sahihi basi unapewa adhabu! Sa nani hayupo sahihi ikiwa mimi nilieumbwa au yeye alieniumba?

Haitoshi yupo Mungu na Miungu iliyobumbwa kwa vito ambavyo vimetoka hapahapa duniania na tunaambiwa wao ndio walituumba!

Nfikiri tunasafari ndefu ya kufahamu ukweli juu ya nadharia ya Umungu na Mungu mwenyewe pamoja na chanzo cha ulimwengu.

Ila nikupe ukweli wote Dini ni matrix iliyotengenezwa na wachache wanaoujua ukwel ili kutawala wengne, soul zetu zimetoka kwa Mungu kweli na zinatambua Hilo, Ila akili zetu zimetekwa na matrix huku duniani, Cha msingi apo nikufanya juhudi binafsi za kiroho ili kujitambua wewe Ni Nan umetoka wap,umekuja kufanya nin na utaenda wap? Kumeditate Ni muhimu ili kuwa na utulivu na kufungua Soul zetu.
Unajuaje ulimwengu una mwanzo?
 
MUNGU wa kweli ni Mungu wa Mbinguni, wanamwita Yaweh, Jehovah, ambaye pia ndiye Mungu wa Abraham, Mungu wa Isaka na Mungu wa Israel. Aliyeumba Mbingu na Dunia na Viumbe wote wanaoonekana na wasio onekana, vilivyohai na visivyohai. Yeye ndiye Asili ya yote, Hana mwanzo na hatakaa awe na Mwisho.

Ukielewa chukua, hutaki endelea na majizingaombwe ya Dunia.
 
Nimekwambia hivi, ufanyaji kazi wa ubongo ndio ulipachikwa jina Akili.

Hiyo mind unaweza kuthibitisha ni nini?
Hakuna tofauti kati ya Mind, akili au intellect. No vitu ambavyo huwezi ona kwa macho.

Lakni Brain ni physical na Ina kazi tofauti kama ku sence.
 
Unajuaje ulimwengu una mwanzo?
Mzee Wa maswali.... Yaani wewe Kila topic jamaa yangu badala ya kujibu hoja unaanza kumuhoji mtoa hoja.... Aseee... Why can't u just quit or skip the topic... We are not here to question each other rather to add inputs on what posted.... Nevertheless you better know questioning has never being the measure of intelligence. Reasoning is.
Hebu grow up Sasa!
 
MUNGU wa kweli ni Mungu wa Mbinguni, wanamwita Yaweh, Jehovah, ambaye pia ndiye Mungu wa Abraham, Mungu wa Isaka na Mungu wa Israel. Aliyeumba Mbingu na Dunia na Viumbe wote wanaoonekana na wasio onekana, vilivyohai na visivyohai. Yeye ndiye Asili ya yote, Hana mwanzo na hatakaa awe na Mwisho.

Ukielewa chukua, hutaki endelea na majizingaombwe ya Dunia.
Habagui dini wala kabila, yeye ni Mungu wa wote na kwake tutarejea.
 
Hakuna tofauti kati ya Mind, akili au intellect. No vitu ambavyo huwezi ona kwa macho.
Ndio maana nilikwambia Akili ni jina tu la ufanyaji kazi wa ubongo.

Huwezi kutaka uthibitishiwe akili ipo au haipo kwa vile akili ni neno tu.
Lakni Brain ni physical na Ina kazi tofauti kama ku sence.
 
Ndio maana nilikwambia Akili ni jina tu la ufanyaji kazi wa ubongo.

Huwezi kutaka uthibitishiwe akili ipo au haipo kwa vile akili ni neno tu.
Hatakama ni neno tu, Bado akili ipo na kama hauamni kwamba ipo basi kwako ndy itakuwa haipo.
 
Mzee Wa maswali.... Yaani wewe Kila topic jamaa yangu badala ya kujibu hoja unaanza kumuhoji mtoa hoja.... Aseee... Why can't u just quit or skip the topic... We are not here to question each other rather to add inputs on what posted.... Nevertheless you better know questioning has never being the measure of intelligence. Reasoning is.
Hebu grow up Sasa!
Kwenye kujibu hoja kuna namna nyingi.

Kuna Socratic Method, tunakwenda wote mdogo mdogo kwa kuulizana maswali mpaka tunaelewana.

Unajuaje ulimwengu ni lazima uwe na mwanzo?

Kama hujajibu swali hili, hoja zote kuhusu "mwanzo wa ulimwengu ni nini?" zinakuwa zina mapungufu makubwa.

Kama uso wa dunia hauna mwanzo au mwisho, ni mfano wa tufe la mviringo ambalo ukizunguka unaweza kurudi palepale ulipoanzia, swali la kuuliza "uso wa dunia umeanzia wapi?" ni swali lisilo na msingi katika ukweli. Ni swali linalotokana na ujinga tu wa kutokujua kwamba uso wa dunia hauna mwanzo.

Sasa, tunarudi kwenye hoja ya ulimwengu, unajuaje ulimwengu una mwanzo?
 
Back
Top Bottom