Kuhusu Mungu na chanzo cha Ulimwengu, kuna mahali hatuna taarifa kamili/sahihi?

Kuhusu Mungu na chanzo cha Ulimwengu, kuna mahali hatuna taarifa kamili/sahihi?

NIELEWE KWA MAKINI SANA.

Mungu wa Israel
Mungu Allah,
Mungu wa wabudha,
Miungu ya kale pale misri,
Na Mungu au Miungu yote ambayo inaabudiwa ikiwemo mizimu na isiyo mizimu, ikiwemo hai na isiyo hai.

Ukweli mchungu ni huu, pamoja na ufahamu wetu wote tulionao lakini bado hatufahamu kuhusu Mungu ama chanzo cha ulimwengu.

Sisemi kuwa Mungu yupo au hayupo hapana, bali naandika kuhusu giza la ufahamu tulilonalo juu ya yupi ni Mungu sahihi ama kipi ni chanzo sahihi cha ulimwengu!

Nafahamu watu na imani zenu mnaona kama naandika maandiko yasiyosahihi!,ila naomba utulivu wa fikra zako japo kwa uchache tutazame vitu kwa undani zaidi.

Hebu fikiri imani uliyonayo sasa, najua wengi wenu mmeirithi toka kwenye jamii ulipozaliwa hivyo ulivyo laiti ungezaliwa katika jamii inayoabudu budha nawe ungeamini na kuabudu na pia ungejiona upo sahihi, imani ambayo ingekuwa tofauti nawe ungeona Kama ni uongo tupu!

Ulishawahi kujiuliza kwanini?
Jibu baki nalo!

Swali zuri nalotaka ujiulize ni kwanini tuna aina nyingi hivi ya Mungu/Miungu? Na wakati ukiangalia kiuhalisia sisi sote ni binadamu wamoja, mazingira mamoja, tunavuta hewa moja n.k.

Kwenye vitu vidogo vidogo hivi tunafanana lakini hili kubwa tunatofauti sana!

Anaeabudu tofauti nawewe unamuona sio sahihi, nayeye pia anakuona wewe sio sahihi!

So yupi ni sahihi?

Kipi kinathibitisha kuwa wewe sio au ndio unaeamini mahali sahihi?

Mtu aliekinyume na imani yako ambae amezaliwa nakuamini tofauti unafikiri amefanya kosa lipi kwa Mungu wako kwa kutokumuamini kuwa ndie Mungu sahihi, ikiwa hakupata ufahamu wowote juu ya Mungu wako?

Je, unafikiri kati yako na Mungu nani alistahiri kumtoa kwenye tope mwenzake nakumleta mahali sahihi?

Maswali haya nikuchokoza ubongo wako ili ufikiri na uelewe nini namaanisha.

Je, huyo Mungu wako mwenye uweza haoni kama ana hatia kwa kuiachia Miungu mengine iabudiwe na kuwapoteza watu wake na hata kuja kuwapa adhabu watu hao?

Ukweli mchungu mwengine ni huu, mpaka Sasa binadamu hatufahamu Mungu sahihi na ndio maana bado tuna Miungu mingi tunayoabudu!

Laiti kama usahihi wa Mungu kweli ungeonekana kati ya Miungu tunayoijua basi binadamu asingekuwa kiumbe mwenye kutapatapa ktk imani!

Kwani kusingekuwa nashaka juu ya Mungu husika kwenye vichwa vyetu!

Tumezaliwa nakukuta vitu hivi vya imani, tumerithishwa tukavipokea (wapo wasiopokea) na tukaviamini (wapo wasioamini pia).

Jiulize, kwani imeshindikana nini kumfahamu Mungu mmoja wa kweli pasipo kurithishwa?

Imagine uzaliwe ujue kunyonya,ujue kupumua ujue kutazama ila Mungu wa kweli usimjue bali urithishwe.!😀
Kimekosekana nini mpaka Tushindwe kumjua Mungu ndani yetu pasipo kufundishwa?

Binafsi mpaka hivi sasa katika Mungu na Miungu ambayo nimeilist hapo juu hakuna hata mmoja ambae logics zake zimeniingia akilini na kunishawishi kuwa yeye ndie Mungu wa kweli!

Hata robo ya ulimwengu jinsi unavyofanya kazi bado hatujaujua ama siri na kanuni za ulimwengu unavyofanya kazi bado hatujazijua!.
MIUNGU wengi tulionao tunaowaabudu bado hawana majibu juu ya chanzo chao pia na ulimwengu kiujumla! Nafikiri zipo sheria mama za kiulimwengu ambazo tukizigundua basi tunaweza kuujua ukweli wote!

Tunajikuta katika lindi la imani hizi kwasababu Kuna kitu hatujajua bado! Giza la ufahamu mbele yetu ndilo linatuweka katika matokeo haya!

Hatujui usahihi wa kweli ipi ndio maana tunatofauti katika Mungu tumuabudie!, kweli huwa haina mashaka ila uwezo wa ufahamu wako ndio unaamua ubebe kipi na uache kipi.

Kwa akili naufahamu wako umeamini kuwa wapo watu wameteuliwa kuwa karibu na Mungu, hivyo wanaweza kukusogeza karibu na Mungu! Kwanini sio wewe mwenyewe ikiwa wewe ni asili toka kwake?

Siamini katika Mungu wa mashaka ambae toka binadamu amekuwepo ktk dunia hii tunaambiwa yupo ila anawashukia wachache na hali ipo Kama hivi ilivyo! Hata kuthibitika kwake bado imekuwa ni mashaka au matendo yake hayathibitiki bali masimulizi!

Mungu ambae ameumba ulimwengu wenye sayari lukuki na akamtupa shetani katika dunia ambayo inaviumbe wake wapendwa! Mungu ambae anasema kwamba shetani amekuja kutujaribu hivyo ni kazi yake mwenyewe anaipima na Kama hukuwa sahihi basi unapewa adhabu! Sa nani hayupo sahihi ikiwa mimi nilieumbwa au yeye alieniumba?

Haitoshi yupo Mungu na Miungu iliyobumbwa kwa vito ambavyo vimetoka hapahapa duniania na tunaambiwa wao ndio walituumba!

Nfikiri tunasafari ndefu ya kufahamu ukweli juu ya nadharia ya Umungu na Mungu mwenyewe pamoja na chanzo cha ulimwengu.

Ila nikupe ukweli wote Dini ni matrix iliyotengenezwa na wachache wanaoujua ukwel ili kutawala wengne, soul zetu zimetoka kwa Mungu kweli na zinatambua Hilo, Ila akili zetu zimetekwa na matrix huku duniani, Cha msingi apo nikufanya juhudi binafsi za kiroho ili kujitambua wewe Ni Nan umetoka wap,umekuja kufanya nin na utaenda wap? Kumeditate Ni muhimu ili kuwa na utulivu na kufungua Soul zetu.
Kwanini watu huanguka mapepo?, na kwanini wengine hupandisha mapepo, makanisani wanapoombewa.

Kama mapepo yapo na malaika wapo.

Kama mapepo yapo na shetani yupo

Kama malaika wapo na Mungu yupo

Kama shetani yupo na Mungu yupo

Na Mungu ndiye mfalme na mkuu wa wote na vyote, Mungu mmoja muumba wa mbingu na nchi

Na dini zipo kuelimisha watu kuhusu Mungu na matakwa yake.(Yani Mungu anataka tuishije, tufanyaje na tuweje ili mwisho tuweze kufika kwake mbinguni)
 
Kwenye kujibu hoja kuna namna nyingi.

Kuna Socratic Method, tunakwenda wote mdogo mdogo kwa kuulizana maswali mpaka tunaelewana.

Unajuaje ulimwengu ni lazima uwe na mwanzo?

Kama hujajibu swali hili, hoja zote kuhusu "mwanzo wa ulimwengu ni nini?" zinakuwa zina mapungufu makubwa.

Kama uso wa dunia hauna mwanzo au mwisho, ni mfano wa tufe la mviringo ambalo ukizunguka unaweza kurudi palepale ulipoanzia, swali la kuuliza "uso wa dunia umeanzia wapi?" ni swali lisilo na msingi katika ukweli. Ni swali linalotokana na ujinga tubwa kutokujuabkwambabuso wa dunia hauna mwanzo.

Sasa, tunarudi kwenye hoja ya ulimwengu, unajuaje ulimwengu una mwanzo?
Haya Mkuu nimekubali kabisa ... Daaah my hands are up on you!!!
 
Mzee Wa maswali.... Yaani wewe Kila topic jamaa yangu badala ya kujibu hoja unaanza kumuhoji mtoa hoja.... Aseee... Why can't u just quit or skip the topic... We are not here to question each other rather to add inputs on what posted.... Nevertheless you better know questioning has never being the measure of intelligence. Reasoning is.
Hebu grow up Sasa!
Nadhani wewe ni mgeni humu JF,

Ni sawa unataka kumfundisha Albert Einstein au Isaac Newton physics.

Halafu Ukianza kuwekewa calculations ngumu ngumu za kifizikia na kihisabati utakimbia mwenyewe.

Kiranga ni next level kwenye maswala ya kujenga hoja.
 
Nadhani wewe ni mgeni humu JF,

Ni sawa unataka kumfundisha Albert Einstein au Isaac Newton physics.

Halafu Ukianza kuwekewa calculations ngumu ngumu za kifizikia na kihisabati utakimbia mwenyewe.

Kiranga ni next level kwenye maswala ya kujenga hoja.
Hatuwezi fanana katika kutazama jambo. Wapo wanaomsifia Makonda wapo wanaomponda. Maisha yapo hivyo.

Relax!!!!!
 
Si kwamba akili ipo, bali ni kwamba ufanyaji kazi wa ubongo wako upo.

Kitu ambacho hata kwa wengine kipo.

Wewe mfano ukifa huwezi tena kusema una Akili kwa sababu ufanyaji kazi wako wa ubongo umekufa.
Ubongo na akili ni vitu tofauti vyenye kazi tofauti. Chizi ana ubongo lakini hana akili.
 
Hatuwezi fanana katika kutazama jambo. Wapo wanaomsifia Makonda wapo wanaomponda. Maisha yapo hivyo.

Relax!!!!!
Wewe ndio inabidi u relax!!!

Na uchambue maoni yako kwa kina.

Kabla ya kufanya "ad hominem attack" kwa mtu, Hakikisha kwanza huyo mtu hoja zake umezielewa sio umekurupuka tu kumshambulia pasipo kuchunguza ukweli wa hoja zake.
 
Ubongo na akili ni vitu tofauti vyenye kazi tofauti. Chizi ana ubongo lakini hana akili.
Chizi sio kwamba hana akili, ila ufanyaji kazi wa ubongo wake una dosari kidogo.

Kwani wewe hujawahi kuona watu waliokuwa machizi wamepona na kurudi hali zao za kawaida?

Je madaktari walirekebisha akili ya huyo chizi kwa kuishika na kuitibu?

Au walitibu ubongo wa chizi ukafanikiwa kurudi katika hali yake ya kawaida ya ufanyaji kazi?
 
Chizi sio kwamba hana akili, ila ufanyaji kazi wa ubongo wake una dosari kidogo.

Kwani wewe hujawahi kuona watu waliokuwa machizi wamepona na kurudi hali zao za kawaida?

Je madaktari walirekebisha akili ya huyo chizi kwa kuishika na kuitibu?

Au walitibu ubongo wa chizi ukafanikiwa kurudi katika hali yake ya kawaida ya ufanyaji kazi?
Ubongo sio akili, haiwezekani kutazamana katika ramani ya shuhuli za ubongo na kutabiri au kujua emotions au ufahamu na uelewa wa mtu. Hiyo yote ni kazi ya Mind.
 
Ubongo na akili ni vitu tofauti vyenye kazi tofauti. Chizi ana ubongo lakini hana akili.
Mkuu mimi ninaona hiyo situation kuwa chizi amepata hitilafu ya kiafya katika ubongo wake hivyo ufanyaji kazi wake umepata shida na hivyo utendaji kazi wa ubongo huo kwasababu unaenda ukiwa una hitilafu, basi hata akili inayotokana na utendaji kazi wa ubongo huo nayo inatoka ikiwa na hitilafu.
 
Maswali ya kijinga haya. Kwahiyo unataka ufananishe ushahid wa uwepo wa akili na uwepo wa mungu?
Nami nikuulize unaamini una DNA? Umewah kuziona?
Lengo lilikuwa kumfahamisha mto mada kwamba haijalishi kwasababu kitu hakionekani basi hakipo.

Kuhusu DNA, Naamini ninayo na sijawahi kuziona.
 
Mkuu mimi ninaona hiyo situation kuwa chizi amepata hitilafu ya kiafya katika ubongo wake hivyo ufanyaji kazi wake umepata shida na hivyo utendaji kazi wa ubongo huo kwasababu unaenda ukiwa una hitilafu, basi hata akili inayotokana na utendaji kazi wa ubongo huo nayo inatoka ikiwa na hitilafu.
Kumbuka Brain ni physical, ili ipate hitilafu basi sababu inakuwa physical pia.
Sasa nadhani unafahamu kuna watu wamepata uchizi bila hata kuguswa physically.

Kupata uchizi ni matokeo ya kuvugika kwa mfumo wa akili, yani bado brain inakuwa inafanya kazi vizuri tu na ina sence na kutafsiri vitu kama maumivu,harufu, sauti na mengineyo.
 
Ubongo sio akili, haiwezekani kutazamana katika ramani ya shuhuli za ubongo na kutabiri au kujua emotions au ufahamu na uelewa wa mtu. Hiyo yote ni kazi ya Mind.
Bila ubongo unaweza kutumia hiyo akili yako kufikiri?

Kama ubongo sio akili, Tukutoe huo ubongo kichwani halafu utumie hiyo akili yako kufanya vitu.

Je Hilo linawezekana?
 
Back
Top Bottom