Kujenga nyumba na kununua magari ni sababu mojawapo ya Umasikini

Sio kweli sidhani kama uko sahihi dhamana ya milioni 200 upewe 50 hakuna kitu kama hicho
 
Sina hakika kama unafanya biashara usinielewe vibaya lakini kwa nia njema tu mfano biashara yako yahitaji mtaji wa kuzungusha (working capital) tuseme milioni 100 uta-save kwa muda gani uje uziingize kwenye biashara yako? Kingine nani alikwambia nia na madhumuni ya bank ni kukufilisi mbona biashara nyingi zimeinuka na kufanikiwa kwa kukopa labda kama hujawahi kufanya biashara na hujawahi kwenda taasisi za fedha.
 
Ukikopa mil 100, ukaiweka UTT , baada ya miaka 5 unakua na zaidi ya mil 300. lakini ukijenga nyumba ya mil 100 baada ya miaka 3 nyumba hiyo itakua na dhamani ha mil 50
Una uhakika mkuu?? Huko UTT ROI yao ni 1.2 to 1% ya mtaji wako, means kwa mwaka utapata mil 12, kwa miaka 5 utapata mil 60, hyo 300m umeipata kwa hesabu gani??
 
Kujenga nao Ni muhimu Sana mwak 2015 nilkuwa na access ya kujenga nikaona wacha niwekeze kwenye biashra aloo acha kbsa biashra bongo hazitabirikii kwa ujumlaaa
Uko sahihi 'uncertainties' zipo za kutosha kwenye biashara zetu za kibongo haitabiriki leo hiki kesho kile kuusoma upepo muhimu kwenye biashara bongo wengi wametoka nje ya reli.
 
Kujenga nyumba, kununua gari hayo yote ni mahitaji muhimu kwa mwanadamu wala sio utajiri.
Kuoa ni maamuzi pia ila kujenga extra yaani kuzidi kipato chako huo ni uzuzu, tumieni akili basi unafanya kazi posta unajenga madale.....

Jenga madale pangishia afu ile kodi lipia hapo hapo mjini, imeisha hiyo....
 
Hatima ya hivi vyote ni nini iwe kujenga au mtaji wa biashara?

Unapofanya chochote kile ndani ya hivyo kuna faida na hasara sasa sijui wewe unadhani maisha yataishi kwako tu na siyo kwa wanaondeleza kikazi chako.

Fanya mambo kwa upeo mkubwa hasa kuacha kizazi chako katika hali ya juu kimaisha,maisha siyo fedha bali mipango na kumbuka vyoote utaviacha duniani na je kizazi chako ni bora ukiachie biashara isiyo na kinga au mahali pa kuishi pa kudumu?
 
Naamini sisi watumishi ndio tunaongoza kutishana kuhusu biashara tunapeana vitisho vingi kweli sijui TRA,kila rais akiingia madarakani ana vipengele vyake,c mnawaona wafanya biashara wa k/koo wanavyohangaika.
Mwisho wa siku tunastaafu pesa inaisha ndio tunapata akili ya kufanya biashara, biashara ktk umri mkubwa baadae biashara hiyo hiyo inakupiga kofi mpaka kaburini
 
Shida ipo kwenye Mashirika yetu NHC, Watumishi Housing, TBA kama wangefanya kazi yao Watanzania wangekuwa mabilionea. Tunafurahi kwaa Dodoma maelfu ya majumba wanayojenga mtu huna haja ya kupoteza mamilioni kujenga wakati nyumba za Shirika zipo.
 
Mkuu haya kuyaongea kama motivational speaker ni rahisi ila kwenye vitendo kibongo bongo ni habari nyingine. Ila una mawazo mazuri
Shukrani ndugu.
Ila haya nimeyaandika kiuharisia kabisa na hali hairisi za maisha yetu ya Ki Tanzania.

Kuna baadhi ya vitu tukiviacha tutafika mbali.
Mfano: Kupoteza muda kwenye mambo ya kijifurahisha wenyewe ilihari hayana maana yeyote.

Angalia baadhi ya mafundi ujenzi na wengine wenye fani mbali mbali wanafanya kazi kwa kujituma laki ikifika jioni pesa anaipeleka kwa mchepuko au baa, kesho anaamka tena kutafuta kisha anaipoteza tena. Mwisho wa siku wa huyu mtu anaishia kwenye umaskini tu.

Kiukweli sisi wa Africa tunapoteza muda mwingi na utajiri kwenye mambo yasio na maana.

Angalia wenzetu nchi zilio endelea mfano China, hutokuta wadada wamejiongeza mashepu, wameridhika na maisha yao, na wanafanya kazi kwa kujituma.
Njoo sasa huku kwetu Africa kila kukicha tunawaza kuongeza mashepu, wanaume nao wanaongoza kutamani kuongeza miili yao na nguvu pia. Kiufupi fahamu zetu zimelala hapo. Hata tukipata pesa tumejitahidi sana tunakimbilia kujenga na kununua ki IST au Vitz, hapo tunaona tumesha fanikiwa kumbe tunahitaji kuwekeza kwa muda mrefu ili watu tujikwamue na umaskini.

Ndiyo maana nchi zetu za ki Africa tunaishia kuwa wachawi/roho mbaya tu, kwa maana hakuna tunachokiwaza zaidi ya mambo ya ajabu tu, hats ikitokea mmoja kafanikiwa lazima ashusshwe tu, wakati inabidi tumtiye moyo na kumuuliza kafikaje ili tujifunze lakini wapi.

Wadada/Wakaka wa Hong Kong wanaolewa/kuoa wakiwa na umri mkubwa, si kwamba hawana mihemko ila fahamu zao mda mwingi wanawaza maendeleo. Ndiyo maana zama hizi midoli ya uume au uke wa bandia zipo nyingi kwasababu wameweka ubusy mwingi kwenye mambo ya maana, miemko ikiinuka tu wanajimaliza wenyewe, ni kama kitu kizuri ila ni kibaya sana kiafya, ila wanatamani kuwa matajiri. Africa kwa hapa tumeshinda tunaoa mapema na kuishinda miemko yetu, sasa jambo la kufanya ni.

Kubadilisha fahamu zetu, tujikite haswa kwenye uwekezaji, kujifunza mbinu mbali mbali za kujikombowa kutoka katika maisha tuliyo nayo, nakuhakikisha kila kata ikiwa na vijana hata 50 wanaojitambua ndani ya mwaka 1 kuna vijana 100 wataongezeka, mwisho wa siku Africa yetu na Tanzania tutakuwa mbali sana.

Usikimbilie kujenga na kununua magari bali jifunze kuwekeza kwanza. Fanya uwekezaji kwenye mambo ya msingi ambayo utayamudu, baada ya hapo jenga na nunua vitu vya thamani uvipendavyo hapa utakuwa umesha wapa vijana wenzio motisha na wao pia watatamani kuwa kama wewe. Vinginevyo tutakuwa na vijana wa hovyo ambao wanatamani majumba mazuri na magari, ilihari hawajuwa kanuni ya kuvipata, tutakacho zidi kukizalisha ni mambo ya ajabu kwa vijana wetu.
 
Kwa maoni yangu, kumiliki nyumba na gari ya kutembelea ni kati ya mahitaji ya msingi (basic needs). Ukishakuwa na hivi vitu unakuwa na utulivu wa akili wa kufanya mambo ya maana ikiwemo uwekezaji.

Usifananishe na Ulaya. Huko, usafiri wa umma ni wa uhakika. Kila baada ya dakika kadhaa kuna chombo cha usafiri, mfano treni (tram) inapita, hivyo usafiri wa uhakika kwa muda muafaka unapatikana.

Sasa nenda pale Kkoo, Posta au Makumbusho saa 12 jioni, utasimama kituoni zaidi ya saa 1 au 2 unasubiri daladala, tena ya kupanda kwa kupambana, halafu kwa kuwa hizo daladala zinafuata ruti za kupangiwa bila kujali kama kuna foleni kali, unaweza kuchukua masaa mengine kadhaa hadi ufike. Ndiyo sababu kama uwezo unaruhusu unanunua gari Ili kupata ufanisi.

Kumiliki nyumba kunakupa security, hasa kama unaishi na wategemezi.
 
Watu wanafukia sana hela hii nchi
 
Kila mtu ajue namna ya kutumia pesa aliyoitafuta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…