Kujenga nyumba na kununua magari ni sababu mojawapo ya Umasikini

Kujenga nyumba na kununua magari ni sababu mojawapo ya Umasikini

Kama hauna familia sawa anza kufanyabiashara ila kwa wakina sisi tulioanzaga mchezo mbaya mapema tulijikuta tupo chuo mwaka wa pili tu tayari tuna mke na mtoto.
Hadi unakuja kupata kazi unajikuta familia inakuforce uwe na nyumba ukicheki kupanga nyumba nzima ni gharama sana inakubidi uanze kujenga maana kuishi kwenye chumba na sebule ni udhalili.
Nakumbuka nilijimeki within 6months nikanunua plot, kisha tukafunga mkanda kuanza ujenzi ilikuwa kila mwisho wa mwezi naenda kulipia tofali hardware to make story short.
Ndani ya miaka mitatu mfululizo nilikuwa nishamaliza boma kupaua na fence kusema kweli baada ya kupachika grills plasta na floor nilihamia kwangu mambo ya finishing nilifanya nikiwa humohumo maana nilijiapizaga kuwa sitaki kuanza kusomesha hukunikiwa nyumba ya kupanga.
Ushauri kwa vijana kujenga sio matumizi ya hovyo ya pesa maana nyumba ni pumziko, heshima, utulivu, kituo cha kudumu cha familia yako, kitunza dhiki na shida zako.
Mwenye macho na aone na mwenye masikio asikie😊
 
nilitaka kuongea point kama hii,kufanikiwa kwa yule jamaa yao aliyetumia principles za finance haiwezi kuwa formula kwa watu wote,kama hiyo formula inasaidia watu wote ilitakiwa na wao baada ya kumaliza mijengo yao wangeitumia pia ili watajirike.
Kuna formula zingine zinafaa zina application ulaya huko kwa bongo ni ngumu sana.
Bongo kuna factors nyingi sana ambazo zinaleta variations kwenye business aspects kwa mfano utawala ukibadilika na mifumo yote inabadilika,miundombinu,mambo ya kodi,rushwa yote haya yana affect business na kufirisika ni rahisi sana.
Refer wale wafanyabiashara wa kariakoo walivyotoa vilio vyao na baadhi mitaji yao ilikuwa ni billions of money.
Hizi principles za kuwekeza kwenye bonds na vipande vya UTT nimezisikia tangia 2003., nikiwa graduate tayari Kabla ya hapo sikuzijua. Lakini sijawahi zifuata. Ila mleta mada namsapoti lakini dah ni ngumu kuzitekeleza ktk umri mkubwa na majukumu mengi. Nashauri vijana mzifuate. Jambo baya ninaliliona ktk jamii zetu ni watu kujenga kwa kutafuta misifa. Kuna sababu gani kijana ndio umeoa au kuolewa, mtoto wenu ndo ana umri chini ya mwaka. Unajenga nyumba ya vyumba vitatu au vinne vyote self na servant quarter! Compound nzima inagharimu Mio kama TZs 80! Wakati Kipato chako kinakuwezesha kulipa kodi ya TZS 150 kwa mwezi? Ukiangalia hiyo compound ukataka kuikodisha, gharama yake ya pango ni TZS 500,000 hadi TZS 600,000 kwa mwezi! Kwa nini usijenge nyumba inayolingana na uwezo wako wa kulipa kodi, hiyo nyingine ukawekeza ktk ardhi?
 
Hizi principles za kuwekeza kwenye bonds na vipande vya UTT nimezisikia tangia 2003., nikiwa graduate tayari Kabla ya hapo sikuzijua. Lakini sijawahi zifuata. Ila mleta mada namsapoti lakini dah ni ngumu kuzitekeleza ktk umri mkubwa na majukumu mengi. Nashauri vijana mzifuate. Jambo baya ninaliliona ktk jamii zetu ni watu kujenga kwa kutafuta misifa. Kuna sababu gani kijana ndio umeoa au kuolewa, mtoto wenu ndo ana umri chini ya mwaka. Unajenga nyumba ya vyumba vitatu au vinne vyote self na servant quarter! Compound nzima inagharimu Mio kama TZs 80! Wakati Kipato chako kinakuwezesha kulipa kodi ya TZS 150 kwa mwezi? Ukiangalia hiyo compound ukataka kuikodisha, gharama yake ya pango ni TZS 500,000 hadi TZS 600,000 kwa mwezi! Kwa nini usijenge nyumba inayolingana na uwezo wako wa kulipa kodi, hiyo nyingine ukawekeza ktk ardhi?
Unapojenga nyumba faida yake na umuhimu wake utakuja kuuona miaka kadhaa mbele usipigie hesabu za leo.
Kwa mfano sasa hivi kwa vile una mtoto mmoja mdogo kwa hiyo haitakiwi kujenga nyumba kubwa?lakini kumbuka baada ya miaka 10 huyo mtoto atakuwa anakaribia miaka 15 na atakuwa na wadogo zake wawili kwa hiyo ukiwa na nyumba kubwa haitakupa stress ya kuanza kujenga upya nyumba nyingine na pesa utakayokuwa unaipata utaamua ufanyie miradi gani.
Pili umesema kwa vile unafanya kazi na una uwezo wa kulipa kodi ya laki 2 kujenga hakuna umuhimu?Kumbuka hiyo kazi unayofanya sasa hautafanya milele kuna kufukuzwa kazi,kuna kuugua,kuna ajali so haya yakitokea kazini watakuchoka na kukuachisha kazi na pia vile vile baba mwenye nyumba atakuchoka pia maana anahitaji kodi yake na wewe uwezo wa kulipa hautakuwa nao.
Lakini ukiwa na nyumba yako itakusitiri hata kama uko jobless mke wako anaweza kuanzisha kibiashara kidogo tu nyumbani kwako hata cha kuuza barafu na Ice cream mnapata hela ya kula maisha yanasonga.
 
Unatak tushindee balaaa na Kulaaa mbunyeeee...!!
 
Ulitumia miaka mitatu kujenga means by 2016 ulikuwa umemaliza. Kuanzia 2016 hadi leo miaka zaidi ya sita bado haujawa stable, kama ulijenga kwa miaka mitatu imagine hii miaka sita ungekuwa makini ungesave kiasi gani!! Inaonekana ni wewe ndio mwenye shida.

Kujenga bongo ni rahisi sana, na ni risky sana kufanya biashara au kuinvest hilo halipingiki (of course ukitoboa umetoboa).. hizi principle za usijenge invest kwanza zinafaa Marekani na Ulaya ambako kujenga ni ghali sana. Bongo ukipata pesa jenga uepushe aibu za hapa na pale.
Kukopa niwew tubkulipa unaweza lipa ata mkopo wako miaka 20 hasa kwa wafanya kazi si kuna dada alikopaga 40m kumbe alimkopea ki ben ten chake kilivopewa mkwanja kikapenya kijamaa na mzigo wote dada bado analipaga tu mwaka wa saba huu
 
Ukikopa mil 100, ukaiweka UTT , baada ya miaka 5 unakua na zaidi ya mil 300. lakini ukijenga nyumba ya mil 100 baada ya miaka 3 nyumba hiyo itakua na dhamani ha mil 50
wewe mtu emu muogope mungu mfuko gani wa UTT Amis unatoa return kubwa kiasi hiko................
 
hizo tunaita rat Race.... tafuta kazi oa chukua mkopo jenga chukua mkopo nunua gari anza kulipa mikopo yako ..ukiimaliza watoto washakuwa anza kulipa ada....lipwa kiinua mgongo kufa baada ya miaka mitano
Na pia watoto na wao waanze kujitafuta kivyao...hili ni tatizo kubwa sana kwenye jamii zetu. Ndo maana ni vigumu sana kuvunja Generational Poverty cycle.,umaskini unarithishwa kizazi hadi kizazi. unless tuanze kubadili Mindset zetu.
 
Kuna jamaa yangu Kaenda jenga bonge la mjengo mbondole. Katumia pesa nyingi sana kupambania mjengo ule. Kazi anafanyia posta. Jamaa kashindwa kabisa kuhamia mjengoni badala yake kamuweka mtu amtizamie.

Angetumia ile pesa kuinvest angekuwa mbali. Sasa hivi analalamika maisha yanamchapa anashindwa kula bata kumbe pesa alikopa na anakatwa pesa ndefu ya mkopo.
kwanini usimshauri aipangishe?
 
Na hapa ndipo vijana tunapopotelea. Kuna intake yangu wamekopa pesa bank wakaenda kujenga, unakuta 30 milion inakata na nyumba haijaisha wakati huohuo mshahara unakatwa, anaishi kwa madeni.
 
Na hapa ndipo vijana tunapopotelea. Kuna intake yangu wamekopa pesa bank wakaenda kujenga, unakuta 30 milion inakata na nyumba haijaisha wakati huohuo mshahara unakatwa, anaishi kwa madeni.
kwa ujenzi wa sasa ,30m ni ndogo sana ,hapo lazima waishi kwa madeni,angalau ukiwa hujatumia mkopo unaweza kujivuta kwa savings zako ukamalizia finishing taratibu.
 
Habari,

"Tafuta kiwanja, Jenga, Oa/Olewa, nunua mkoko", njia hii na mawazo haya yamekuwa kwa vijana wengi wanaoanza maisha, hususani waliobarikiwa kupata ajira au biashara zao binafsi ambazo zinawapa kipato flani cha kuendesha maisha yao. Kwa uzoefu wangu hii imekuwa kati ya sababu moja kubwa zinazosababisha watu kuwa maskini na kushindwa kufikia uhuru wa kifedha.

Lakini tujiulize swali la msingi, kwanini watu wengi wameamua kuchagua njia hii ya maisha. Nimefanikiwa kuwahoji watu wengi kidogo kuhusu hili na majibu niliyoyapata mengi yalikuwa kama ifuatavyo:

  • Gharama ya kupanga nyumba ziko juu sana, ni bora kujenga ya kwako.
  • Nyumba ni asset.
  • Usafiri ni shida sana eneo niliko jenga ni bora kuvuta gari yangu.
  • Mama/baba mwenye nyumba ana gubu sana.
  • Nikiwa na kwangu nakuwa na uhuru mkubwa sana.
  • Siku nikifukuzwa kazi au biashara ikiyumba nibaki na pakulala na familia yangu.

Sababu hapo juu nyingi ni za maana kabisa ila tatizo ni kwamba njia zilizotumika kutatua hizo changamoto zinaongeza changamoto zaidi, kivipi?. Ngoja tujadili mambo machache kuhusiana na maisha ya watu wengi hususani mijini (e.g. Dar):

- Wengi wananunua viwanja maeneo ya mbali kutoka mahali wanapofanyia shughuli zao zinazowapa kipato.
- Baadhi ya hayo maeneo yana changamoto za miundombinu ya maji, umeme, barabara na hata kiusalama.
  • Wengi wanajenga kwa kuunga unga sana, unaweza jenga nyumba hata miaka sita au zaidi. Kuna msemo wanasema "nyumba haiishi".
  • Nyumba nyingi wanazojenga watu kukaa zinakuwa ni kubwa na za kifahari bila kukumbuka lengo la mwanzo lilikuwa ni makazi tu na sio jengo la maonesho (Hapo utajibiwa kuwa tunajenga mara moja ya kuzeekea)

Kuzingatia hizo hoja hapo juu, yafuatayo yanakuwa ni matokeo ya gharama za maisha baada ya huyu mtu kuhamia kwake:

  • Gharama za usafiri au mafuta zinakuwa juu ukilinganisha na awali.
  • Mazingira yanakuwa sio rafiki kwa familia kuishi, maana nyumba nyingi zinakuwa bado hazijaisha (Wengine wanasema unakuwa unaishi site).
  • Kama una gari, gharama za matengenezo zinakuwa juu kwa sababu ya pengine barabara kuwa mbaya, lakini kwa kuwa unasafiri umbali mrefu kila siku, basi hata service ya gari utafanya mara nyingi zaidi.
  • Pia kama una gari utalazimika kuendesha gari umbali mrefu kila siku, hii si nzuri kwako kiafya.
  • Gharama za umeme na maji pia zinaweza kuongezeka kwa kuwa nyumba ni kubwa sasa na pengine maji hayajafika.
  • Maeneo mengine hata watu hawajahamia wengi hivyo hata usalama unakuwa hatarini.
  • Mara nyingi unaweza ukajikuta mbali na huduma bora za kijamii ikiwemo hospitali, shule, n.k.

***NOTE: Gharama zinaweza kuongezeka ukilinganisha na mwanzo.

Kwanini kuna hofu ya kuwekeza hizo pesa?

Tujiulize swali hili la msingi. Ni kweli baadhi ya watu wanatamani sana kuffanya biashara, lakini wengi wanasema, BIASHARA HAZITABIRIKI. Ni kweli kabisa, lakini ukweli ni kwamba hilo sio tatizo la watu kutokuwekeza.
SHIDA KUBWA NI WATU KUTOKUWA NA ELIMU YA FEDHA. Hili ni jambo la muhimu sana kwa vijana kupata elimu. kwanza kabisa sio kweli kwamba ukitaka kuwekeza ni lazima ukafanye biashara fulani kama kuuza nguo, vinywaji au duka la mangi. Unaweza ukafanya uwekezaji kwa njia nyingi sana ambazo hazitahitaji your active time kuweza kusimamia ila mwisho wa siku ukaja kuwa na uchumi mkubwa kabisa. Uwekezaji huu ni kama mifano ifuatayo:

  • Kununua viwanja na mashamba (Kumba muda unavyokwenda ardhi inapanda thamani lakini nyumba inashuka thamani)
  • Kununua hisa za makampuni
  • Tressury Bonds and Bills
  • Mifuko ya uwekezaji ya pamoja (e.g. UTTAMIS)
  • Fixed deposits accounts
  • Kuwekeza kwenye elimu (Hii sio lazima zile za darasani, inaweza kuwa hata kujiendeleza katika fani flani)
  • N.k.

La muhimu ni kupata elimu sahihi ya mambo ya fedha ili ujue jinsi ya kufanya maamuzi ni vipi utumie pesa yako.


Ngoja nitoe mfano halisi mmoja ulio hai kabisa kwa lengo la kupata uhalisia wa ninacho kisema:

Mwaka 2013 niliajiriwa mahali na tulikuwa kama waajiriwa sita wapya katika hiyo kampuni, mwenzetu mmoja alikuwa na uelewa mkubwa sana wa mambo ya fedha, na mara nyingi alikuwa anatushauri kuhusu haya mambo lakini tulikuwa tunamuona kama kachanganyikiwa: Mimi na wenzangu wengine wa tano tulikwenda mahali tukanunua viwanja na kuanza kujenga kwa kasi sana na badae tukachuku na mikopo kuongeza kasi hiyo. Kwa haraka haraka kwa wastani tuliweza kutenga kama milioni moja kwa mwezi kila mmoja wetu kwa ajiri ya miradi ya ujenzi. Mungu si athumani baada ya miaka mitatu paka minne wote watano tukawa tumehamia kwenye site zetu huku tukiendelea na finishing.

Jamaa alikuwa kila mwezi anaweka milioni moja kwenye mfuko mmoja wa uwekezaji wa pamoja na alikuwa anapata average interest kama ya 11.85% kwa mwaka. Badae akawa ananunua na bond za serikali pamoja na mambo ya kununua mashamba mbali kidogo na mji yakichangamka anakata na kuyauza. Kiufupi jamaa ana zaidi ya milioni 200 kwenye mfuko anaoweka pesa pamoja na kuwa na asset ya viwanja na mashamba na benki ana pesa chafu.

Turudi kwetu tuliojenga na sasa tuna mikoko yetu, umbali wa kwenda na kurudi nyumbani ni 50 Km kila siku. Na pia siwezi pata picha ile hofu ya kwamba nikiachishwa kazi bado ipo maana siwezi nikala nyumba.

Kwa ajili ya muda niishie hapa kwa leo, nipate mawazo ya watu wengine pia. Kiufupi mimi naona kuna mitaji mingi ya biashara na uwekezaji inapotea kwa huu mwamvuli wa kujenga na kununua hii mikoko.

Ahsanteni!!!
Elimu nzr,umepita mulemule. Ila nipo pale nasubiri
 
Nmekuleta site kwangu uone hatua niliyofika umekuja kutangaza huku

Sasa elimu ya biashara sina ulitaka ifilisike uje kunicheka tena huku

DAH
😀 😀 ndio mana sipeleki rafiki site kwangu hata siku moja hata ndugu hawafiki seuse rafiki
 
😀 😀 ndio mana sipeleki rafiki site kwangu hata siku moja hata ndugu hawafiki seuse rafiki
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Yani mtu anaona biashara ni ya kila mtu anaweza kufanya tu
Yani nikose vyote biashara na makazi bora nibaki na hilo hilo boma
Kuliko kuja kuweka million 30 halafu niishie kutajirisha watu tu
Ashasema mtu anafanya kazi posta alitaka biashara isimamiweje
Kuna muda unaona bora tu ninune kiwanja nijenge kitakuja nistiri baadae.

Halafu vijamaa snitch kama hao unakuta anaandika andika JF na bado mkikutana anakulamba mzinga wa Bia. Jokes
 
Na pia watoto na wao waanze kujitafuta kivyao...hili ni tatizo kubwa sana kwenye jamii zetu. Ndo maana ni vigumu sana kuvunja Generational Poverty cycle.,umaskini unarithishwa kizazi hadi kizazi. unless tuanze kubadili Mindset zetu.
naamini umaskini ni mind set... jamii nyuingi zina mdudu huyu kichwani ubinafsi ujinga unaoshindwa kujua which is which..aset and liability.... mtu anamaliza hela kwenye home housing anasota kukopa mtaji benk alipe kwa riba na ile nyumba imekuwa colateral...home housing is liability and no one agree...
 
naamini umaskini ni mind set... jamii nyuingi zina mdudu huyu kichwani ubinafsi ujinga unaoshindwa kujua which is which..aset and liability.... mtu anamaliza hela kwenye home housing anasota kukopa mtaji benk alipe kwa riba na ile nyumba imekuwa colateral...home housing is liability and no one agree...
Kabisa mkuu,nini kifanyike ili watu waanze kufikiri tofaut.
 
Back
Top Bottom