Kujenga nyumba ni ndogo ya kila maskini

Wenzako walisema hivyo hivyo na sasa wanalia wakiomba msaada, maana mwenye nyumba anataka kuwafukuza na pesa hawana.
 
Kwann? Nimesoma hii nyuzi dah
 
sasa kama mtu mwenyew una andika chizi = xhizi
unategemea zitakia timamu kichwani mwako emb toka kwanza apo kweny nyumba ya urithi ukapange uone uchungu wa kulipa kodi matterCall wewe!!...
 
Mtu kama anayo mapesa mengi ya kuweza kujenga nyumba nzuri na hapohapo anao na uwezo wa kuweka vitega uchumi,naye unamuweka kundi gani?Maana naona umeegemea sehemu moja tu.
 
Daah jeifu inakufa hivi hivi naona.......... threads za kijinga kama hizi mtu anapost post tu na mods wanauruhusu Uzi kama huu? Uhuru ukizidi unakuwa ujinga
Usichukulie maisha serious hivyo
 
😂😂😂😂mtoa mada unateseka ukiwa wapi nyumba ni nyumba tu iwe kubwa ndogo ni heshima kuwa nayo..
 

Wanaokushambulia hawajakuelewa tu manake uko sahihi. Kujenga nyumba ni uoga shauri ya umaskini. Kwa vile wewe ni maskini, ukiona maskini mwenzio amejikwamua kwa kupunguza hofu ya maisha na kujenga unapaswa ufurahie na ujitahidi na wewe ujenge, sio kuponda.

Halafu you have no manners! Umealikwa kwa watu unaenda kuponda baada ya kula ubwabwa wao! Im happy walikufukuza. Sasa maskini mwenzetu, ujenge na wewe acha kumbwela!
 
Mtu kama anayo mapesa mengi ya kuweza kujenga nyumba nzuri na hapohapo anao na uwezo wa kuweka vitega uchumi,naye unamuweka kundi gani?Maana naona umeegemea sehemu moja tu.
Huyu kujenga haki yake sababu ukiwa na kitega uchumi nyumba unajenga kwa muda mfupi tena ramani uitakayo tena unajenga sehemu uitakayo,ila kuna baadhi ya watu hawana uwezo wa kuendesha kusimamia hela wakizipata muda mfupi zinaisha kwa matumizi holela hao bora wajenge tu kisha waishi na wapangaji humo wachangie choo sebule waombane chumvi na wapangaji wao waombane mboga lakini kwa anae weza kuendesha biashara yake asijenge kwanza apange tu kisha biashara ikimalika ajenge

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mtoa mada upo sahihi japo uwasilishaji wa mada yako umeonesha dhihaka kwa watu wenye mitizamo tofauti na wewe

Ipo hivi ukipata mil 20 ukaamua kuanzia kujenga na mwingine akipata mil 20 akafungua biashara ndani ya miaka mitano Je mtakuwa sawa kimaendeleo
 
Kama hayo yote unayajua basi si vema kupangiana namna ya kuishi.Kila mmoja afanye mambo yake kadiri ya muitikio wa akili zake.Tukifanya hivyo tutakuwa tumepevuka katika ustaarabu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…