Kuliko kuajiri mfanyakazi wa ndani tuwe na utaratibu wa kuchukua watoto wa ndugu kwa nia ya kuwaendeleza

Kuliko kuajiri mfanyakazi wa ndani tuwe na utaratibu wa kuchukua watoto wa ndugu kwa nia ya kuwaendeleza

Binadamu wengi hatufahamu jinsi ya kubadilisha negative situation into positive. Hawa mabinti faraja wakiipata shuleni na huko ndiko waliko kazia.

Kuna mwalimu wangu mmoja alinisimulia matatizo aliyoyapata ugenini. Baba yake alihamishwa kikazi na yeye ilibidi ahamie na kusoma kule. Kwakua lafudhi yake ilikua tofauti, akiongea watoto wenzake walimcheka darasani. Aliamua kufa na kitabu ndiyo ilikua faraja yake. Matokeo yake alikua wa kwanza darasani.
Yeah ofcourse hii inasaidia ila ni wangapi wenye hii spirit😀
 
Wengine tumekulia mazingira hayo watoto wa nyumba hio wao wanakula cakes na mayai asubuhi nyie mnakula magimbi. Wanalia sahani nyie mnapigwa kwenye sinia chini! Nyama za baba tu japo baba kanunulia familia nzima ile ila anapikiwa yeye na wanae nyie mwendo wa kabichi na maharage tu. Siku za shopping ya vyakula watoto wake wananunuliwa chocolates na pringles wanalia chumbani na kupangusa midomo mtakutana na maganda tu. Alfajiri uamke ufagie kiwanja na banda la mbuzi kisha unaenda shule hata chai hujanywa hupewi hata sh.100 utembee wao wanapandishwa school bus na buku ya kuspend on break time hapo washakula cakes, mayai na chai asubuhi! I don’t wanna remember that life aisee...Siwezi ruhusu mtoto wa mtu apitie ile hali akiwa kwangu! I rather not take him/her.
Shukuru hapa mtoto anakomazwa na anapata akili kinouma.sasa subiria miishakuwa wakubwa uliyekuwa unaonekana unateswa ndo unahimili mikiki ya life Ila wao Kama hawajashikwa mkono usikute wanakuomba msaada.
Mie naamini katika kukomazwa kwa dizaini iyo.
Hata mie nimekulia kwa bamdogo huyo mke wake ndo alinijenga na zile mishe za jkt.
Kwetu Niko strong kuliko wengine.kuna muda mdogo wangu ni mwanaume kabisa alikuwa around 28 Yuko town kiutafutaji,sijui ilikuwaje akijiliza kwa mama kuwa Hali mbaya nalala njaa. Na huku mie nishalala siku mbili bila kuweka kitu mdomoni sema nilichukulia Kama stepping stone nikapata maganzi makubwa how to fight.
We've unlimited potential
 
Shukuru hapa mtoto anakomazwa na anapata akili kinouma.sasa subiria miishakuwa wakubwa uliyekuwa unaonekana unateswa ndo unahimili mikiki ya life Ila wao Kama hawajashikwa mkono usikute wanakuomba msaada.
Mie naamini katika kukomazwa kwa dizaini iyo.
Hata mie nimekulia kwa bamdogo huyo mke wake ndo alinijenga na zile mishe za jkt.
Kwetu Niko strong kuliko wengine.kuna muda mdogo wangu ni mwanaume kabisa alikuwa around 28 Yuko town kiutafutaji,sijui ilikuwaje akijiliza kwa mama kuwa Hali mbaya nalala njaa. Na huku mie nishalala siku mbili bila kuweka kitu mdomoni sema nilichukulia Kama stepping stone nikapata maganzi makubwa how to fight.
We've unlimited potential
Yeah kusaidia imesaidia sana mzee japo ilikuwa unfair game! Wao walizaliwa Canada so wana uraia wa kule na kwa sasa walisharudi Canada kimaisha wako zao mtoni sie tunapambana Bongo!
 
Maisha ni utashi na Kila mtu anafanya kile ambacho anakiona ni sahihi kwake na kinampa manufaa ila kimtizamoo ni jambo jema sana
 
Asili ya binadamu ni majungu na wengine wanasahau hali zao. Na yeye anataka aishi kama Junior, ale chocopops kwa breakfast. Mkishindwana unamridisha kwao salama.

Eti umrudishe kwao! Utajua huwajui ndugu wewe.🤏[emoji2535][emoji36]
 
Ni jambo zuri sana ikiwa utapata watu wanaojitambua na kuelewa wajibu wao.
Kwa uzoefu wangu, ndugu au jamaa wanaweza kukupa kero na namna ya kushughulika na kesi zao inajumuisha watu wengi ambao inawezahatarisha mahusiano kwenye familia.

Ukipata anaejitambua, ni raha sana, lakini wengi wao wanakuja na mtazamo kwamba hapo wapo kwa ndugu yao na wao sio wafanyakazi, wanaweza kumvimbia wife ikawa tafran.

Nawasaidia lakini mmalawi lazima awepo kufanya wajibu ambao mahusiano yetu ni kazi na ujira.
Malawi Ishakuwa official,sio Iringa tena?

Wale wanajua kazi yao vizuri sana, tatizo off kila Jumapili.
 
Shukuru hapa mtoto anakomazwa na anapata akili kinouma.sasa subiria miishakuwa wakubwa uliyekuwa unaonekana unateswa ndo unahimili mikiki ya life Ila wao Kama hawajashikwa mkono usikute wanakuomba msaada.
Mie naamini katika kukomazwa kwa dizaini iyo.
Hata mie nimekulia kwa bamdogo huyo mke wake ndo alinijenga na zile mishe za jkt.
Kwetu Niko strong kuliko wengine.kuna muda mdogo wangu ni mwanaume kabisa alikuwa around 28 Yuko town kiutafutaji,sijui ilikuwaje akijiliza kwa mama kuwa Hali mbaya nalala njaa. Na huku mie nishalala siku mbili bila kuweka kitu mdomoni sema nilichukulia Kama stepping stone nikapata maganzi makubwa how to fight.
We've unlimited potential
Jirani yangu alilelewa na baba na mama wa kambo. Mama wa kambo alimfahamisha kabisa kuwa mle ndani hakuna mfanya kazi kwaajili yake. Ajue kufua na kupiga pasi nguo zake. Ajue kusafisha chumba chake. Akitoka shule apike ugali wake. Haya yote mama yake hakuwahi kumfundisha.

Anamshukuru sana mama wa kambo sasa hivi.
 
Achana na habari za kum control! Ukimsaidia mtu mwache free afanye anachopenda you guys mnafeli hapa...Unapomsaidia mtu usimuhenyeshe maana ile mantiki ya msaada inakuwa haipo kabisa na wala hizo thawabu unazozitaka hutazipata! Assist someone with a clean heart. Sio ndio umfanyishe makazi kama punda na kumkosesha amani!

Kuna watu wanakaa na watoto wa wenzao yani mtoto hawezi juta kuishi hapo sababu wote wanapata fair treatment! Sio mtoto wako shopping Mlimani wa mwenzio unampa hela aende Ilala Boma akanunue mtumba! Haya ndio mambo ya hovyo

Ulianza hovyo ila umehitimisha vema. Eti usimcontrol umuache free afanye anachotaka, huyu mtoto wa miaka 15-18 umuache free?

Hapo una jukumu la kumfunza mambo mengi tu, na utarajie upinzani mkali.
 
Ulianza hovyo ila umehitimisha vema. Eti usimcontrol umuache free afanye anachotaka, huyu mtoto wa miaka 15-18 umuache free?

Hapo una jukumu la kumfunza mambo mengi tu, na utarajie upinzani mkali.
Haimaanishi avunje vyombo au vioo vya gari kisha umtazame! Mtoto unaweza muelewesha kwa upendo kuwa namna nzuri ya kufanya mambo ni hivi na vile
 
Unakaa na mtoto kwa mkataba wa kumsomesha au kumuendeleza. Mnapanga muda wake wa kwenda shuleni au mafunzoni na muda wake wa kazi. Anaishi kama mtoto wa nyumbani, unamnunulia mahitaji yake madogo madogo. Sehemu kubwa ya mshahara unakwenda kulipia ada na Bima ya afya.

Akihitimu mafunzo unamuwezesha kujitegemea na unatafuta mwingine. Kama ndugu zako wote mambo safi unaweza kuchukua vijana wa kijijini kwenu. Hii ni njia ya kurudisha katika jamii na kukwamuana kimaisha.
🎼Mama Mdogo aliponichukua kijijini, alimuahidi Mambo mengi, dada yaaakeeee🎵kwamba atanisomeshaaaa
🎶Kumbe ni kunirudishia Nyuma Maisha yaanguu ya badaeee

🎼Tulipofika mjini mamaaaa🎶Tulipofika mjini mama kanigeuzia kibao 🎵
Hakuna Cha shuleee🎶wala darasaaa🎤
 
Kutumwa kazi hakuna uhusiano na kuteswa ila kama mtajiondoa by 100% kwenye hizo kazi sababu yeye tu yupo lazma alalamike! Haiwezekani watoto wa rika lake wapo wanaangalia igizo halafu umnyanyue yeye akalishie kuku. Kazi wafanye collectively wakwake na wako halafu uone kama atalalamika.

Msaidiane kazi sio mumpe mikazi yote kwa vile mnamsaidia kumsomesha!

Kwa mujibu wa mada hii, lengo kuu ni kupata mfanyakazi ila awe ndugu ili kumwendeleza… kwahiyo huyu ni mfanyakazi na analipwa kama wengine ila kwa sababu ya undugu ndo atadhani ana haki sawa na Junior.

Ni changamoto sana kubalansi hapo.
 
Kwa mujibu wa mada hii, lengo kuu ni kupata mfanyakazi ila awe ndugu ili kumwendeleza… kwahiyo huyu ni mfanyakazi na analipwa kama wengine ila kwa sababu ya undugu ndo atadhani ana haki sawa na Junior.

Ni changamoto sana kubalansi hapo.
Kwahio wewe unaona kwako ni sawa kumchukua mtoto wa kaka yako na kumfanya shamba boy hapo kwako?
 
Kwahio wewe unaona kwako ni sawa kumchukua mtoto wa kaka yako na kumfanya shamba boy hapo kwako?
Ni hivi anasafisha mazingira ya nyumbani, lunch anakula anapaswa kwenda kwenye mafunzo na jioni kama hajachoka anaweza kukaa sebuleni kuangalia hotuma ra Mheshiwa Rais pamoja na familia.
 
Haya ndio mie nayapinga haswa..,kuna watu wavumilivu kama watoto wa kike watakausha ila sasa wakishaondoka hapo uhusiano umekwisha hutaona wakikanyaga tena hio nyumba! Mjomba wao wataonana nae misibani na kwenye harusi za watu.

Huo ni ushenzi na wanawake wengi ndio wana tabia hii kwa ndugu wa mume!

Leo nipo na wewe tu Mzee.[emoji16]

Acha kuwa negative sana, pamoja na kuvaa maronya lakini umeambiwa hao mabinti walifanikiwa kusoma hadi kupata kazi…. umewaza pengine maronya yalisevu hela iende kwenye ada?
 
Leo nipo na wewe tu Mzee.[emoji16]

Acha kuwa negative sana, pamoja na kuvaa maronya lakini umeambiwa hao mabinti walifanikiwa kusoma hadi kupata kazi…. umewaza pengine maronya yalisevu hela iende kwenye ada?
Sawa sijakataa mi nalalamikia ile fairness! Kwani wangevaa woolworth wasingesoma hadi kupata kazi?
 
Kwahio wewe unaona kwako ni sawa kumchukua mtoto wa kaka yako na kumfanya shamba boy hapo kwako?

Kama lengo langu ni kutafuta shamba boy na nikaona nikimweka yeye atafaa, kwa maana ningeweza kuleta yeyote ila nimechagua ndugu ili angalau naye nimsogeze mahali.
 
Back
Top Bottom