Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Mamaa'amiiiina!
FB_IMG_16882473244337768.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 


Huyo hapo Mrisho Mrisho akielezea kilichofanyika tayari bandarini mwezi Juni tu.

Sasa huyo Maria asijifanye anatoa siri kwa kitu kilichowazi na kimeelezewa na bandari yenyewe.

Sasa wewe unachomlalamikia Maria hapa ni kitu gani?

Amejisifu wapi?
 
Yaani mnyama tunamuwinda sisi, jasho linatutoka sisi, kisha DP World anakuja kutuconvince kuwa yeye ana kisu kilali zaidi tumuachie mnyama atatumegemea mapande ya nyama na sisi tunakubali. Kama huu siyo uzwazwa ni nini?

Siyo hapo tu hata Taifa gas anawekeza 200 million dollars Kenya lkn fedha ni ya kwetu sisi ndiyo tume guarantee mkopo maana yake ni kwamba akishindwa kulipa deni anayedaiwa ni Serikali ya JMTZ na siyo Taifa gas ingawaje faida inakwenda kwake na ajira Kenya, think about that kama siuo evil ni nini?
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.
Una uthibitisho wa hili?
DP World wanafanya kazi Kwa maslahi ya kibiashara pekee..
Lengo kubwa ni ku control trade kupitia mikataba yenye ahadi hewa na zisizotekelezeka..

Silaha Yao kubwa ni mikataba mibovu yenye kuwalinda ,Kinyonyaji na kutisha nchi zinazoingia Kwa ushawishi wa ahadi kemukemu..
 
Umeambiwa report za World Bank na CAG. Tulipewa fedha $21M kwaajili ya mifumo na DP World ndio wametajwa watekelezaji! Jamani hapa hatufanyi siasa! This is very serious National matters. Binafsi sijasoma hizo report lakini kwa credibility ya Maria hawezi kusema jambo linalogusa taasisi nyeti bila ushahidi.

Inaogopesha sana!
Haya Basi. Kumbe DPW walishaweka pua zao huko siku nyingi, wakisubiri tu wakati ili waje kijumla kutumbua!

Ila sasa jinsi walivyokuja, kufuatana na yale "makubaliano" wameona ni bora wazoe kabisa, na wala siyo kutumbua pekee!
 
Acha kuwa mmpumbavu... Unajadilije uafanisi ambao haujauona?, Tahira wewe.
Huna hoja.
Unazani DPW ndo wanaanza kufanya kazi za bandarini kwa mara ya kwanza hapa Duniani ?
kama huwajui sema tukupige shule uwajue. Nyie mnaviashiria vya ufisadi na mnajua kwa uwepo wa DPW hamtoiba kirahisi.
 
Siyo hapo tu hata rostamu anawekeza 200 million dollars Kenya lkn fedha ni ya kwetu sisi ndiyo tume guarantee mkopo maana yake ni kwamba akishindwa kulipa deni anayedaiwa ni Serikali ya JMTZ na siyo rostamu ingawaje faida inakwenda kwake na ajira Kenya, think about that kama siuo evil ni nini?
Asante.

Mwisho wengi wetu wataelewa tu namna ya haya mambo yanavyofanyika juu ya migongo yetu.
 
Unadhani DP WORLD Hizo Pesa watazitoa Wapi?!!! Au unadhani kuna mwekezaji anatumia his own money ? Usishangae yeye akatumia collateral ambao ni huo mradi kwenda kukopea kwa financiers kwahio mwisho wa siku ni asset yako wewe mwenyewe ambayo ime-facilitate huo mradi..
Possible

Lakini serikali yako ipo restricted ndio kwanza credit ratings wameipa B+ it’s a junk bond hakuna bank atakayokupa hela. Wewe unabaki na makusanyo yako, IMF, WB na donor countries; kama source yako ya revenue.

Sasa kama DPW anaweza pata mkopo huko shida yako ni good terms za ‘project agreement’ na transferable skills anazowaachia vijana wako nchini muda wake ukiisha na kuamua kutokuongezeka.
 
Wamekiweka kwenye maandishi ama mdomoni ili wakulainishe moyo wako. Usiwe biased. Huyo mkurugenzi anaweza akapigwa fungu la maisha milele atetee una uhakika
Yapo kwenye appendices 1 ya IGA uwekezaji watakaofanya DPW.
 
Possible

Lakini serikali yako ipo restricted ndio kwanza credit ratings wameipa B+ it’s a junk bond hakuna bank atakayokupa hela. Wewe unabaki na IMF, WB na donor countries.

Sasa kama DP anaweza pata mkopo huko shida yako ni good terms za ‘project agreement’ na transferable skills anazowaachia vijana wako nchini,
Whaat ?!!!!

Yaani undhani Serikali hii haikuopesheki; Unadhani Hao Walamba Asali wa Awamu hii huko wanakozunguka kila kona wanafanya nini ? Na since tuna asset za kufa mtu ambazo waasisi hawakutaka kuzifuja (unadhani kwanini baadhi ya watu walitoa tahadhari kwa kinachoendelea kwamba kuna siku tutaamka asubuhi tukute tumeuzwa)
 
Kuna kamati za bunge ndo zina utafiti neenda ukasome hasadi uone how bandari ya Dar inavo kua under utilised na mapato serikalini ni kidogo sana wizi ufisadi ndo umejikita sana pale......manaake tumeshindwa kuendesha hiyo bandari, kwanza niambie tulishawahi kufanikisha kuendesha nini?
Mkuu bado hujajibu swali langu!
Wanaohusika moja kwa moja na uendeshaji wa bandari wanapatikana kwa utaratibu gani?
 
Hii ni kutoka report ya Worl Bank .................................BY MARIA SARUNGI

Muhimu kuhusu DPW na mradi wa Benki ya Dunia

Pesa za mkopo wa @WorldBankAfrica zimetumika (na kukamilika)
👉🏽 kupanua na kuimarisha Gati 1-7 na kujenga gati mpya Gerezani
👉🏽kupanua mlango wa bandari hadi Gati 11
👉🏽kuboresha na kuunganisha na reli
👉🏽 Kupanua na kuimarisha Gati 8-11
👉🏽Kuna RORO terminal ilijengwa na kukamilishwa

Sasa tuangalie wanachodai DP World kufanya kwa mujibu wa IGA
Cha kwanza kikubwa eti kujenga, kuendesha na kusimamia RoRo terminal na Gati 1-4 na gati 5-7
🙄
Yaani pesa zote zimewekezwa za walipa kodi kupitia mradi wa sasa wa WB alafu wao wanakuja kuendesha na kusimamia? Wanawekeza nini??

Ndiyo maana mkataba haujawekwa thamani ya uwekezaji wao 😄 kumbe wanadandia mradi unaoelekea kukamilika waje wajisifu!

YAANI KIUFUPI WANAKUJA KUTEKELEZA MRADI WA PESA ZA MKOPO WA WORLD BANK

Nyieeeeeeeeee!
Mnaotetea mkataba huu mnajua kuwa mnatumika kutetea ulaji wa genge ndogo!?
Ila #TutaelewanaTu
Nimekuwa nauliza haya haya!
Kwanini baada ya kuwekeza zaidi ya Trillioni mbili za Kitanzania tena za mkopo tunaenda kuwagawia hawa Waarabu bandari yetu?

Kwa kweli mpaka kieleweke.
 
Hapana hao DP world wana kuja na mitambo yao pamoja na technology yao wana fanya oparation mantainance and investment manaake wata panua bandari iwe kubwa zaidi
Kwa hiyo serikali ilipoboresha bandari kwa mkopo wa IMF haikununua mitambo wala tekinolojia?
 
Ingekuwa ni Rahisi hivyo Dp wananunua tu Mahali crane kwanini Ujerumani, Uingereza, Canada, China hawawezi nunua ZAO? Kwanini wamempa Dp?

Hivi vitu ni complicated sana ila sisi tunajifanya tu wajuaji sana.

Kampuni Zote kubwa Duniani zinapo Outsource hivi vitu lazima ziwe na mikataba ya kupewa Exclusivity Atleast Kwa Muda fulani

Naomba nikusahihishe kidogo konecranes ni kampuni ambalo inatengeneza na kuzalisha vifaa mbalimbali Kwa matumizi ya bandarini ikiwemo mobile harbor cranes [emoji911] za aina zote pamoja na rubber gantry crane (rtg) na pia wanajihusisha na mambo ya port solutions na kampuni hii ipo Finland na pia ipo kampuni nyengine inayoitwa kalmar ambayo hii pia inajihusisha pia na utengenezaji wa reach stacker,terminal tractor,straddle carriers,rmg crane, pia ipo kampuni kubwa kutoka China [emoji630] ambao ni wazalishaji wa crane za ZPMC ambazo ukienda hata huko Arab na bandari zetu za Africa zimejaa kibao cranes zake
 
Jamani huu mkataba alie nao anitumie niusome,ikibidi uwe umetafsiriwa kwa lugha yetu maridhawa.

Maana mpaka asaivi sijui kitu
 
Mkataba huu ukipitishwa naomba wananchi tuungane kuiweka CCM pembeni
 
Back
Top Bottom