Kumlipa Clinical Officer laki 6 sio haki hata kidogo

Kumlipa Clinical Officer laki 6 sio haki hata kidogo

Hao hao form 4 failures waliopata div.3 na 4 ndio unataka walipwe zaidi?

Si haki kabisa kuwapeleka watu wenye ufaulu mdogo kushughulika na usalama wa Afya zetu.Serikali komesheni huu upuuzi.
Mmeanza tena mnataka kuwaita watu vilaza,kuna watu wenye ufaulu mdogo wanapokuwa kazini wanafanya kazi kwa ufanisi kuliko wewe mwenye ufaulu mkubwa.
 
Wazee wa kugugo Diagnosis na kusoma prescription kwenye vitabu.

Kila Diagnosis ni UTI [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Hawa watu bana.

Nurses wanakomaa na Labour, RCH, CTC, Triage

Vituo visipokuwa na pharmacist wao ndio wanakaa kubabakee,[emoji1787]

Halafu kinatokea ki-CO kimoja na shule yake ya Tandabui kinaona mshahara hautoshi[emoji1787]
Hahahaha ety tandabuhi....mbona hata ma co wanazalisha
 
Hakuna kitu kizuri kama kila mwisho wa mwezi una uhakika wa hiyo hela.
Imagene kwa mtu jobless au muuza nyanya na vitunguu?
[emoji848][emoji848] though kuna wanaopiga pesa nene kuliko hio laki 6 kwa mishe za kitaa.
 
Ukiona unatumia nguvu na muda kupata pesa isiyokidhi mahitaji yako, jua hiyo sio kazi, achana nayo.
 
Mie nakubaliana na ww asilimia mia ,ila ukiangalia kwa undani mishahara inapangwa kulingana na level ya elimu.cha muhimu Fanya kazi kwa mda kasome MD .ulipwa hiyo 1.5 M

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
Mishahara inapangwa kutokana na hali ya uchumi wa nchi kwa ujumla, taasisi husika na kada husika ikichochewa na uzalishaji wa faida. Elimu bila kuzalisha, ina maana kuna sehemu inabidi wazalishe ili huyo CO alipwe
 
Mishahara inapangwa kutokana na hali ya uchumi wa nchi kwa ujumla, taasisi husika na kada husika ikichochewa na uzalishaji wa faida. Elimu bila kuzalisha, ina maana kuna sehemu inabidi wazalishe ili huyo CO alipwe
Mishahara inapangwa kutokana na hali ya uchumi wa nchi kwa ujumla, taasisi husika na kada husika ikichochewa na uzalishaji wa faida. Elimu bila kuzalisha, ina maana kuna sehemu inabidi wazalishe ili huyo CO alipwe
Of course, ndio hivyo. Ukiona unalipwa zaidi ya unavyozalisha maana yake kuna watu wanazalisha unapewa wewe.

Na ndio maana mashirika yanayozalisha wana Payscale zao, wanalipana kutokana na wanavyozalisha.
 
Hivi sekondari zetu ada zinapishana kulingana na masomo?Kwamba hapa Bagamoyo sekondari anaesoma PCB analipa ada kubwa kuliko yule wa HGK?.Hii mimi leo ndiyo naisikia
Ada zinatofautiana ,na kitu kinachofanya ada iwe kubwa ni kwenye lab huko zile specimens mf panya, Mendes,vyura, nge nk Bado chemicals hapo .
 
Sasa hivi hawa watu ni wengi mnooo mtaani.

Kuna mmoja amekaa home mpaka amechoka, eti akaamua kwenda kusoma ADDO[emoji1787]

Yaani CO ameamua kwenda kusomea kuuza dawa[emoji1787]
Sio huyo tu..wengi tu mimi na dogo alipiga addo sasahivi yupo anauza duka la madawa na co yake..wafamasia wakae mkao chonjo kazi zao zimevamiwa na co waliokosa kazi.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
In short, kama una uwezo wa kuzalisha pesa kubwa kwa mwezi kuliko kile unacholipwa kazini, ACHA KAZI.

Ila usije ukaacha kazi ukafikiri IDEAS na MOTIVATIONAL QUOTES zinalipa BILLS.

Akili kichwani.
Bado hujaelewe..nikwamba pamoja na kusubiri hizo laki 4 kwa mwezi..kuna magap yanatokea ofisini ingawa sio siku zote..yanaweza kumpa hela mtu ya kutosha kuzidi hata mshahara..kupitia hiyo hiyo kazi aliyoajiriwa kama mtumishi...kuna semina kuna warsha maakongamano na other deals.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Zaidi ya Miaka nane kwenye Cheo kimoja"!....Hizo takwimu ulizoongea ni za lini?
Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni.Mh Raisi Samia kafanya kazi kubwa sana kupandisha watumishi Madaraja Mwaka huu, Hiyo Miaka 8 sijui kama atakuwepo hajapanda?!?! Pia Waziri alisema, "Mtumishi akiwa ana sifa ya kupanda, lazima apande"

Sasa Mkuu, embu jiUpdate...ili uwe unaandika kulingana na muda.
Jikite kwenye mantiki ya hoja, watumishi kulalamika kucheleweshwa kupanda madaraja, kutopata annual increments, madai ya likizo na posho na stahili nyingine lukuki hakujaanza leo. Ndo ninachosema hapa kwamba maslahi ya watumishi yangekuwa yanatekelezwa kwa wakati yangeweza kufunika madhira ya kulipwa mishahara midogo kama hiyo wanayolipwa CO.
 
Jikite kwenye mantiki ya hoja, watumishi kulalamika kucheleweshwa kupanda madaraja, kutopata annual increments, madai ya likizo na posho na stahili nyingine lukuki hakujaanza leo. Ndo ninachosema hapa kwamba maslahi ya watumishi yangekuwa yanatekelezwa kwa wakati yangeweza kufunika madhira ya kulipwa mishahara midogo kama hiyo wanayolipwa CO.
Nijikite vipi kweny Hoja! Wakati wewe umechomekea vitu ambavyo haviko sahihi?

Soma comment yako, angalia maneno yako ya Cheo kimoja and da da da.
 
CO anatakiwa apewe 1.2 m
MD apewe 3m...
Nurse degree apewe 2.5
Mfamasia ..2.5m
Dentist ...3m
Lab scientist 2.5m
.......
Itatokea ...pale maisha yatakapopanda sana ambapo hakutakuwa na tofauyi na sasa
.......hii mishahara ya mwisho wa mwezi jnafanya asubuhi mpaka jioni ...sikunyingine mpaka usiku ni uchawi yu.....
Mkuu, at least hivi viwango ulivyopendekeza vipo reasonable angalau kwa mtu anayeanza kazi.......lakini kwao wanaona kumlipa mbunge na kiongozi wa kuteuliwa mil. 12 ni bora zaidi kuliko kumlipa mtaalamu reasonable salary kutokana na hali ya uchumi ilivyo na changamoto za kazi zinazomkabili. Ndo maana leo ukienda kupata huduma hospitalini watu wanafanya kazi kama wamelazimishwa, motivation kwa watumishi ni hovyo kabisa......
 
Ukiona unalipwa kidogo halafu hutaki kujinasua huko.. jipige kifuani useme mimi ni mnyonge..

maisha hayawezi kuwa malaini kwa kulalamika bila kuchukua hatua.

Mshahara mkubwa hauji hivi hivi bila kuupambania. Na hapo unalalamika kuna kazi tamu za mishahara minono kila siku zinatangazwa kwenye NGOs sema umeamua kuwa mlalamishi.

Keep it up, uone kama ulalamishi utalipa bills. Maisha hayapo fair, na equation ndo ipo hivo wala hata usijisumbue kuhoji kwanini..

Probably solution ya haya masuala itakuja miaka mia inayokuja.. utakuwa hai? Kama la.. dont try to fight the status quo... utajiumiza na kufa mapema..
 
Nijikite vipi kweny Hoja! Wakati wewe umechomekea vitu ambavyo haviko sahihi?

Soma comment yako, angalia maneno yako ya Cheo kimoja and da da da.
Hizo changamoto zipo na ni sugu, and that is the truth!
 
Back
Top Bottom