Kuna hatari kizazi hiki kikaaminishwa kuwa Tundu Lissu ni moja ya Watu wabaya na sio wazalendo kwa Taifa

Mimi si mwana CCM ila sikukubaliana na Lissu kabisa kwenye suala la kuwatetea Acacia kwenye makinikia pamoja na suala la kutetea ushoga.
1. Lakini makinikia yapo ndugu?

2. Lisu hajatetea ushoga, ispokuwa kasimama kama katiba YETU. Lisu amesema atatenda kwa mujibu wakatiba.

Hivi kuheshimu na kufuata katiba nikosa? Au hukuelewa? Au unazusha?
 
Always statements za Lisu ni facts

Ispokuwa wajinga hawamuelewi, I mean ccm.
 

Wajinga bado wengi
Huu uzi unathibitisha ukweli wa madai ya Lisu
 
Always statements za Lisu ni facts

Ispokuwa wajinga hawamuelewi, I mean ccm.
Lissu hamna kitu kabisa kwenye kichwa chake kama alivyo jidhihirisha kwenye suala la 'MIGA'. Bungeni Prof. Kabudi alimwambia nitaleta matokeo yako hapa akakuja mkia na hajawahi kumjibu hadi leo. Si mwanasheria mzuri ila ni mpayukaji mzuri asiyekuwa na maarifa yoyote, ukiangalia rekodi yake ana kesi nyingi za kushindwa kuliko kushinda.
 
Mbona kimeshaaminishwa mkuu!! Soma tu comments za watu humu jamvini utajua kuwa watanzania siyo critical thinkers.
 
Wajinga bado wengi
Huu uzi unathibitisha ukweli wa madai ya Lisu
Lissu ni mpayukaji hana maarifa yoyote ila nyinyi nyumbu kawaaminisha ni kichwa. Kiboko yake Prof. Kabudi alimwambia bungeni alaleta matokeo yake ya chuo kama ataendelea na jeuri ya upayukaji, Lissu alikaa kimya na hajawahi kumjibu hadi leo.
 
Nimependa "Jingaman".
 
Wenye roho ya shetani pekee ndio wamemfanyia ubaya,na kumsemea ubaya,na wale bendera fuata upepo wanaoamini katika roho mbaya, kutofuata wala kupenda kuona haki ikitendeka.
 
Watu wajinga ndio wataweza kudanganywa.
Mzarendo gani,huyu aliyekuwa anakaa upande wa mabeberu kutishia serikali kuwa tutashitakiwa miga,mala tutanyorewa na vipande vya chupa pasipo maji, mzarendo gani anayeweza kukaa upande wa maadui wa taifa.Lissu ni kibaraka tu.
 
Always statements za Lisu ni facts

Ispokuwa wajinga hawamuelewi, I mean ccm.
Wewe nawe hujitambui. Rekodi ya Lissu kwenye kesi ni ushahidi tosha ni mpayukaji hana maarifa yoyote, ana kesi nyingi za kushindwa kuliko kushinda, wakati mwenzake Kibatala ana kesi nyingi za kushinda kuliko kushindwa.
 
Wewe nawe hujitambui. Rekodi ya Lissu kwenye kesi ni ushahidi tosha ni mpayukaji hana maarifa yoyote, ana kesi nyingi za kushindwa kuliko kushinda, wakati mwenzake Kibatala ana kesi nyingi za kushinda kuliko kushindwa.
Wenye roho mbaya mkimwona najua dhamira zinawasuta,ila hapa najua hamwezi kusema.
 
Mbona kimeshaaminishwa mkuu!! Soma tu comments za watu humu jamvini utajua kuwa watanzania siyo critical thinkers.
Ila bado naimani na Rais Samia, wakati fulani ukifanikiwa kumrejesha mtu kama huyu kwenye hali yake unakuwa umeponya mioyo ya Watu wengi Sana kwa maramoja. Mama bila kujali makosa ya mwana wa Tanzania huyu tafadhali mrejeshe kwenye hali yake nimegundua Kuna space kwenye ubongo wa Lissu inahitaji upendo wa nchi yake kabisa na si kwa mwingine ikitoka kwa Rais itakuwa dawa na mwanzo mpya kwa Tanzania yenye matumaini.....huyu mtu kakosa upendo wa nyumbani jamani.
 
Ukweli ni kwamba Tanzania watu wenye Akili, weledi na misimamo thabiti hupigwa vita na wajinga wengi waliomo CCM
Hilo la Lissu kuonewa watu wanalijua sana tatizo ni wale wasiopenda kukosolewa watakupiga teke hata ukiwaambia shati lako kanyea kunguru, wataenda hivohivo wakikutukana badala ya kulifuta.
 
Hatasalia hata mwovu mmoja bila kuumbuka
 

..Magufuli alikuwa akifanya vituko vingi sana na usipokuwa makini unaweza kutekwa akili zako.

..Chukulia hoja yake kwamba kuna "msaliti" anatuma txt kuomba data. Halafu akaendelea kudai mawasiliano kati ya "msaliti" na DEO MWANYIKA yamedakwa!!

..Halafu anaendelea kusema "msaliti" hatakiwi ku-survive, anatakiwa auwawe kama inavyofanyika kwa askari waliokengeuka wakiwa mstari wa mbele.

..Kwanza niulize hivi tume ya uchunguzi haikutafuta data toka kwa Accacia / Barrick wakati wakiandaa ripoti yao?

..Wakati wa majadiliano hakukuwa na ubadilishanaji wa data kati ya timu ya serikali na timu ya Accacia / Barrick?

..Sasa kwa akili za Magufuli huyu "msaliti" anastahili kuuwawa, lakini Deo Mwanyika mtumishi wa Accacia / Barrick anastahili kuishi, na kupitishwa kuwa mgombea ubunge wa CCM!!

..Je, wanaosema Magufuli ana faili Mirembe wanakosea?

..Jambo lingine ni suala la kuwafungia watendaji wa serikali waliokuwa wajumbe kwenye tume yetu ya majadiliano na Accacia / Barrick.

..Majadiliano yale yalifanyika kwa MIAKA MITATU mpaka kufikia conclusion. Je, Magufuli alikuwa kawafungia wajumbe wa tume muda wote huo?

..Tatizo ni kwamba Magufuli alikuwa anasema mambo ya UONGO ambayo hayapaswi kusemwa na kiongozi anayeheshimu wananchi wake.

..Ni bahati mbaya kwamba wale waliojenga ujasiri kumrudisha Magufuli kwenye mstari ndio hao mnaowaita wasaliti, na kuunga mkono wauwawe kinyama.

NB:

..Magufuli hakukamata kampuni yoyote ya mabeberu. Tayari alishanywea baada ya kukutana CEO wa Barrick.

..Na kama Barrick ni kampuni ya kibeberu ambayo ni hatari kwa usalama wetu, tujiulize aliyeileta hapa Tanzania ni nani kama sio CCM ya Magufuli na washirika wake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…