Kuna sehemu hatari kuishi kama South Africa?

Ongea yote usikanyage MEXICO......south africa ina subiria mbali sana ukiangalia kwa video zao wakiwa wanafanya mauji sidhani kama south africa inawakuta
Mexico Kundi za DRUGS DEALER ndo ishu ila ukiamua kuishi kwa hamsini zako bila kuingilia Anga zao hakuna tabu utapata
Ila sasa SOUTH kuna VITA aina nyingi sana ambavyo vinaweza kukutoa UHAI wako muda wowote
 
Nchi za huko unazoweza kutembelea ni Argentina harafu inafata Brazil ingawaje Brasil nao wana wauza sumu wengi tu huko sijui Colombia,Bolivia,Venezuela na ndugu zake hakuna Nchi hata moja yenye usalama huko...
 
Congo ni cha mtoto kwa South africa wacongo ni vibaka tu lkn South Africa ni wahuni

Sent from my PRA-LA1 using JamiiForums mobile app
Kiukweli maisha ya mtaani ya SA siyajui mkuu. Nakuja mara nyingi SA ila nafikia hotelini na kurudi. Nimekuja Capetown mara 4, Pretoria mara 2 na Jobug mara 2 na mara nyingi nafikia hotels zilizoko CBD so maisha hasa ya street sijayui sana.
 
Elewa mantiki ya member kuleta uzi huu

Yeye anaongelea SA kwa sababu ni sehemu ambayo kibongobongo unaweza kwenda kubeti maisha; sasa Haiti na El Salvador kuna wabongo wanakwenda kutafuta maisha huko?
Umesoma title ya uzi ilivyo andikwa au unakurupuka?

Title inasema hivi 👇

"Hivi kuna sehemu hatari ya kuishi kama south Afrika"

Ukishaweka neno "sehemu" hiyo ni worldwide.
 
🚨🚨
"Wananchi wa Kigamboni wanataka Katibu wao wa Kamati ya Wananchi Paul Mwikambe aachiliwe‼️
Inasemekana anashikiliwa na JWTZ kikosi cha baharini (Navy)
Ishu ya ardhi ni hatari tupu!"
mhe: Maria T Sarungi
 
Mexco ni kwenye mitaa ya wauza unga, kama wewe sio police na wala sio muuza unga haaana shida na wewe, Sasa South tu mambo ya kuchukuliana wanawake hii ni kosa kubwa.
Unapoambiwa Mexico sio salama jua hivyo mkuu na usidanganywe sijui mitaa ya Wauza unga pekee ile Nchi isikie hivyo hivyo na ina wanawake wazuri nao wanauana sana kwa sababu ya Wanawake muuza Sembe anachukua pisi yeyote anayoitaka tofauti na SA wauza sumu wanauana kwa ajili ya biashara sio Wanawake...
 
Mexico Kundi za DRUGS DEALER ndo ishu ila ukiamua kuishi kwa hamsini zako bila kuingilia Anga zao hakuna tabu utapata
Ila sasa SOUTH kuna VITA aina nyingi sana ambavyo vinaweza kukutoa UHAI wako muda wowote
Mexico Kuna biashara haramu na uhalifu wa kila aina , hao drug cartels wanamiliki territories na wanafanya uhalifu kama utekaji ,ujambazi ,human trafficking ,biashara haramu ya viungo vya binadamu , black mail nk
Kiufupi ukiona hili neno "Cartel" ujue ni organized crime gangs
Cartels za Latin America zinafanya kila biashara haramu siku hizi
Wewe unaweza ishi sehemu yenye ujambazi ,au utekaji ili walipwe ransom ,au utekaji na mauaji ya watu ili kupata viungo kama maini , mapafu ,figo nk ? ,bila shaka hautakuwa safe kwa namna yoyote ile kukaa eneo hili , mfano kwa sasa hayo magenge ya wahuni yanatoza ushuru mpaka wale wahamiaji haramu wanakimbilia Marekani kwa kupitia porini au miji ambayo hao wahuni wanaishikilia kama territories zao , Newyork times waliwahi andika mwaka huu kwamba hayo magenge yamepata zaidi ya dollar billion moja kama makusanyo ya hizo tozo za wahamiaji wanakimbilia Marekani
Sasa imagine hicho ni chanzo kimoja tu cha mapato , bado hawajauza cocaine na madawa mengine , hawajafanya kidnapping nk , bila shaka hao wahuni watanunua silaha nzito ,vifaa na kuongeza nguvu kazi zaidi na kujitanua na kuwa hatari zaidi .
 
Mbona unajiita "RiskTaker", kupitia Uzi wako nakuona ni "Risk-Averser". Hao wa SA achungu ya ubaguzi bado yako ndani. Ni mifumo yao ya uchumi inawaganya wengi kuwa vibarua tu. Bongo kila mtu anaweza kuanzisha duka mbele ya Baraza lake au kuweka Banda sehemu ya wazi Hata mbele ya ikuku.

Jibu swali la mdau hapo juu kuhusu sleep over 😁 watu wanataka waende kwenye mechi ya wananchi na Masandawana kama sababu
 
Hao Los zetas ,Kuna documentary niliona walituma mpaka timu ya wauaji Texas na Arizona kuua watu waliokuwa wanataka kuwaua
The impunity and ruthlessness , halafu yanaua vibaya mno
Ubaya ni wanajeshi tena special force waliofundishwa na USA na Mexico kisha wakaasi na kutengeneza genge lao la kuuza madawa ya kulevya
 
National Geographic walionyesha documentary moja mwaka huu jinsi hao wahuni wanavyofanya money laundering Kwa biashara wanayofanya ya kuingiza madawa ya kulevya Marekani , wanashirikiana na wafanyabishara wachina , yaani madawa yanaingizwa Marekani na hao wahuni halafu yanauzwa pesa cash anapewa mchina halafu hao wahuni wanapata pesa zao kwa network ya wafabiashara wa kichina wanaofanya biashara kwenye nchi la latin America mfano Mexico nk
So wanaavoid detection Kwa namna hiyo
Na kwa madawa mfano methamphetamine ambayo raw materials zinatoka china , hao wahuni wanawatumia wafanyabiashara wa kichina ambao wananunua huko kwao China na kuingizwa kwenye hizo nchi kupitia mizigo ya hao wafanyabishara wa kichina
 
Uhalifu upo kiwango cha kitisha.
 
Uhuni kama huo ulianza kuota mizizi hapa tz kipindi cha JK. Alipokuja Magu akaagiza polisi and kupokonya bunduki toka kwa wahalifu.

Akasema polisi mzima unazidiwa na jambazi kwanini usimnyang'anye bunduki yake? Akimaanisha ua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…