Kuna ulazima hayo mashindano ya Quran yafanyike Mkapa Stadium? Siku ya mchezo Simba vs Orlando!?

Aisee hili jambo nimewaza katika angle tofauti sana aisee. Kama kuna mazindiko yaliyofanya hizi timu za kariakoo ili wawe wanashindaga mechi, je mazindiko yao yarabaki salama kwa vile visomo vya watu zaidi ya 100? Kama havitakuwa salama na wakachekewa kumaliza mashindano itawapelekea timu ya kariakoo kushindwa kupata wasaa wa kutosha kufanya marudishio yao.
 
Ule ni uwanja wa michezo bhana. Hivyo hayo matamasha yenu ya injili na hayo mashindano ya Quran, mnalazimisha tu kufanyia humo.
Mkuu uwanja kama ule unajengwa kwa shughuli za kijamii ikiwemo michezo, matamasha,shughuli za kisiasa nk.
Sasa Wewe unataka population ya Watu labda 400000 ikakae msikitini au kanisani?
 
Kwani kuna mtu kasema lisifanyike? Suala ni mahali linapofanyikia kwa siku hiyo sio mahali sahihi sababu hiyo sehemu kwanza ni kwa ajili ya michezo na siku hiyo kuna mchezo. Je utaunga mkono ikiamuliwa wakafanyie shuleni na masomo yaahilishwe?
 
Hii mechi haitaanza muda husika, lazima itasogezwa mbele. Watu 60,000 kuingia ndani ya muda huo uliobaki ni kilio
 
Kwa nini ya Kishki hauyafagilii na kuyakubali ya Mama Sururu ? nipe info maana nilishawahi kumsikia Ostadh wangu ambaye alishawahi kutoa Moja ya washindi Ktk mashindano ya Kishki akisema kama ulivyosema ila sikupata kudadisi vizuri.
 
Kwa nini ya Kishki hauyafagilii na kuyakubali ya Mama Sururu ? nipe info maana nilishawahi kumsikia Ostadh wangu ambaye alishawahi kutoa Moja ya washindi Ktk mashindano ya Kishki akisema kama ulivyosema ila sikupata kudadisi vizuri.
KISHK NI MSANII...SIRI ILIYOPO NI KWANZA ANATANGAZA SHULE ZAKE...ALHIKMA BOYS N GIRLS,

PILI WANAFANYAGA KILA MBINU NA WAO WAPATE MSHINDI KUTOKA KATIKA SHULE ZAO...KUMBUKA MWAKA JANA ULIKUWA UNA LAWAMA SANA...

DHULMA HIZI ZINAANZIAGA CHINI KWENYE MCHUJO...

HII NI TAASISI YA KIDINI INAYOTEGEMEA UFADHILI WA NDANI NA KIMATAIFA (Nchi za kiarabu).

HAYO MASHINDANO NI KWA AJILI YA KUJITANGAZA KWA AJILI YA SPONSORS N DONORS...ILI IONEKANE TAASISI INAFANYA KAZI VIZURI NA IPO UNATAMBULIKA KIINCHI NA KISERIKALI NDIO MAANA HUWAALIKA VIONGOZI WAKUBWA WA SERIKALI...

KIUFUPI UJANJA UJANJA MWINGI...HAMNA DINI NI DUNIA KWENDA MBELE...BIASHARA KUBWA SANA...PESA WANAYOINGIZA NI MARA NYINGI YA GHARAMA...

WACHACHE SANA WANAANGALIA DINI...LABDA YA AISHA SURURU...NAYO SINA HAKIKA...
 
Naamini hakuna uwanja wa Dini,
Wanaweza kutumia hata huo wa Mkapa ila sasa kwanini siku hiyo ya game?
Kilichotikea hawa wa mashindano ya qur an walipewa uwanja kabla ya ratiba ya mechi kutangazwa, pili kuhusu kumaliza saa saba ni miaka yote iko hivyo maana kuna swala ya saa saba lazima wakasali
 
Kwani kipi kilianza!? Kunankimoja kimekuja ghafra..!? Simba na Wasauzi ilijulikana kabla, mashindano hayo vipi!?

Naanza kuona lawaza za UDINI zitaelekezwa kwa wasio waislamu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…