Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Ajabu hakuna aliyekiri kuwa na hizi tabia!
Mi kiukweli nikienda ugenini kama nna njaa huwa sijivungi.... Nagonga msosi kisawasawa alafu hakuna kuangalia mtu usoni, nikija kuinua uso shoo imeisha najua huwezi kunisema live utaishia kunung'unika moyoni mwako
 
Aisee kumbe wote humu tuna tabia nzuri ktk ulaji Misosi sijaona wale walalamikiwa humu au wanapita kimyakimya...ila zamani utaratibu ulikuwa ni kula kwa pamoja inawekwa ngoma katikati inapigwa ni kasi yako tu na utimamu wako wa akili,miaka ilivyosonga daaaah ukabakia ni utaratibu wa mijini na usasa zaidi ndo sasa hiv mambo ndo haya....kwa sasa hivi usitegemee sanaaaa kushiba ugenini,watu wana bajeti zao wamepanga alafu pia kama una taarifa ya kuja kwa mgeni au wageni,lazima uangalie na aina ya hao wageni wanaokuja ndo unafahamu kiasi hiki kitakuwa kinatosha kwa wote hata akiongeza msosi kibao au kama wageni hamuwafahamu vema na chakula umekadiria kiasi tu,mnaanza kupakua nyie family members kwanza then wao ndo wanafuata au unawapakulia kila mmoja au ya mwisho msosi unapakuliwa kabisa jikoni sahani znaletwa uwanjani na kilichobaki pia kinawekwa mezani na kwa wageni wa ghafla mnawapakulia tu au ndo vle mnaanza kupakua nyinyi kwanza ukisema karibu jipakulie wengine ndo wanakuchinja kijapani kabisa kwani tafsiri vichwani na ustaarabu unatofautiana ndo badae unaanza kujinyonganyonga rohoni sababu ya msosi wakati ni mambo ya kutumia diplomasia ya kikwete tu na ustaarabu unaanza kwako ili nawe usiharibu kwengine......jamani kuna wengine ni kama wagonjwa kula kidogo atakufaaa,sasa kule kwetu kanda ya ziwa akija town huku ndo unaweza kumdhani vbaya kumbe kashazoea kwao kijijini anakula nusu kilo ya ugali,maziwa Lita moja,viazi kibao unampa slesi mbili unafkiri hatakimbia jikoni kwenda kula hadi mboga za mwakani au kwenye frija na kukomba vinywaji vyote hadi whisky.........
 
Mama alikuwa anasema ukialikwa mahali popote hata iwe harusi hakikisha unakula nyumbani kwako kwanza.

Usiende kwa watu na njaa yako ukiambiwa pakua unajaza sahani kama ndo pa kupakulia.

Au unafika ukumbini we unatoa mimacho kungojea muda wa kupakua.
Hivi ndivyo tulivyofundishwa.

..........Sio mtu unaenda msibani unaanza kuuliza muda wa kula ni saa ngapi?
 
Acha uchoyo pika chakula cha kutosha

Kama wali kilo 3

Samaki hot pot linajaa

Mgen anakula mpaka anashindwa kutembea

Sisi mgen akija kijijin,mbuz anachinjwa ,supu anakunywa ,main anakaangiwa ,kula nyama mpaka meno yanasema inatosha

Watu wamjin uchoyo uchoyo tu
 
watu wa DAR wanaishi kwa maneno sana,nakumbuka nilienda kwa familia moja walikuwa hawependi makande,lakin walikuwa wanapika kwa sa sababu ya mshua,bac cku wakipika makande ni watu wawil tu ndio tulikuwa tunakula,mzee na mm,bac mzee akishakula namalizia msosi wote,sasa mke wa mzee akaanza kuni sema kwa watoto wake kwamba ninakula sana makande,ilinibidi nivumilie adi nilipomaliza mda wangu apo home.
 
Hpo hpo usingemchelewesha ungempa makavu " samaki wapo wangapi na watu ni wangapi " unamaalizia kwa kumwambia " simama weka simu mezani na kila kitu ulichonacho mfukoni hivi ndivyo vitaenda kununua mboga ya wale ambao hawajapata mboga shwain mkubwa"

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Hapa ndio unasikia mgongano wa tamaduni.

Binafsi mimi kwetu Musoma, kwa kawaida unapikwa ugali mkubwa watu mnakaa round mnakula.

Sasa baada ya kuanza kuzurula kwenye mikoa ya watu nikaanza kupata changamoto.

1. Kisa cha kwanza, nilienda familia fulani wakati wa kula mimi nikawa namega tonge kubwa nakata ( maarufu kama chumba na sebule ) nikichunguza wenyeji wangu, wanamega tonge moja Moja. Ikabidi nijifunze na mimi kula kama wao. Ila sasa nikawa sometimes namega kubwa sometimes dogo 🤣🤣🤣 yaani ilikuwa tabu sana.

Nikawa sishibi kabisa, njaa muda wote.

Kumbuka ukiwa mgeni wenyeji hawawezi kushiba wote halafu wewe ukabaki unendelea kula ni Aibu.

( Ndio maana kwa Musoma mostly, mgeni hawezi kula peke yake na wewe kama mwenyeji hupaswi kuacha kula hata umeshiba mpaka mgeni ashibe )

2. Kisa cha pili, wewe probably kwenu huwa chakula kikitengwa ni kula tu, na wengine wanasali kwanza: sasa uko ugenini chakula kimetengwa kabla hawajasali wewe ushamega, wanaanza kusali wewe tayari una tonge umeshiiiria kwa AIBU. Hili limenikuta sana.

3. Kisa kingine kilimtokea Mshkaji wangu, yeye alienda zile familia za kujipakulia mwenyewe. Sasa chakula chenyewe wanapika kidogo. Na kibaya zaidi hizi familia nyingi za Pwani huwa usiku wanakula chai na chapati.

Sasa wameweka chapati 6 mezani, jamaa kachukua 4 mwenyewe vila kujua. Yaani tayari akawa katia hasara mtu mmoja kakosa.

Ukiachana na hayo, mimi kwetu siyo ufahari mtu kwenda chooni watu wanakuangalia. Nilivyoanza kuzurula kwenye mikoa mikubwa, nilipata tabu sana, unaamka asubuhi unakuta watu wamekaa nje yaani 🤣🤣 na wewe unataka kwenda chooni. Tabu sana

Kutembea na kujifunza tamaduni za watu pia ni vizuri maana kunafungua akili na kukufaya uweze kuwa na utu na ku embrace diversity.
 
Kwahio mlikuwa mnapika kuku wangapi maanake mapaja yako mawili tu. Kula mapaja mawili au manne ni kujaza choo tu kiwango kinachohitajika ni kidogo sana. Ni Sawa na mtu anaekula ugali mwingiiii anajaza Choo tu.
Kujaza choo hyo unajua wew....sis tulikua tunakula tu hakuna kupangiwa...na kwetu kulikuwa na ndugu kama wote..yaan mzee wangu amesomesha ndugu zake karib kijij kizima...wakitoka kijijin wanafkia nyumban.so nmekua nikishuhudia familia kubwa..na wote tulikua tunashiba had tunajinyea..na hata sku1 mama hajawai mpangia mtu kupakua..unakula had unaacha mwenyew mkuu namii ukiniita kwako kama una vibudget kwenye kula..utaaibika mkuu....mim nafukia na sio bonge
 
Samaki sio mboga ni kitoweo.
Jifunzeni Kiswahili hasa kwa awamu ya tano
Mkuu mbona wewe complicator hivyo kwa taarifa yako kiswahili nilipiga banda , hivyo sina shida, nilikomaa zangu na makabeji(CBG), kwahiyo pitia kitu kinaitwa synonym/s(Kisawe/visawe) na wewe uache ulafi, Njooni niwafundishe ufugaji wa samaki bure ikiwa ni mkakati mojawapo wa kuondoa food insecurity(uhaba wa chakula unaoleta udumavu wa mwili, akili pia na Kiroho pia), karibu mwalimu wa kiswahili.
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Good, ujumbe safi.
 
Hivi watu wanawezaje kufanya hivyo ugenini au ndo ucheshi na uchangamfu? sitasahau siku 1 nilipo karibishwa chakula mezan tuko watu 5 nilipakua chakula kidogo kuliko wenyeji na nikadanganya kuwa nimeshakula huko nilipo toka.
Baada ya dakika 10 akaingia mtt wao katoka shule akakuta chakula kimeisha alilia sana hata alipo ambiwa asubir apikiwe chake bado aliendelea kulia huku ananiangalia kwakweli nilijiskia vbaya sana, baba wa mtoto akamtandika mtoto wake kwa kosa la kutokua na adabu na Mimi nikiwepo ndo nikaendelea kukosa amani kabisa nikajiona Mimi ndo chanzo Cha yote.
Hadi leo hii nikiwa ugenini ukifika mda wa kula ndo muda ninao uchukia zaidi na ninaweza kukataa kula kabisa kama ikiwa tu ni sehem nilienda kusalimia na kupita
Wewe upo kama mimi kiukweli muda wa kula chakula ugenini ni adui yangu mkubwa sana, siupendi huo wakati huwa nakosa amani na furaha hata radha ya chakula huwa sisikii kabisa km ntalazimishwa kula, nikifikia kwa ndugu labda mkoa huwa nakula kabisa mbali na kwa wenyeji wangu, sipendi kuwa kero kwa wengine hasa upande wa chakula
 
Hivi watu wanawezaje kufanya hivyo ugenini au ndo ucheshi na uchangamfu? sitasahau siku 1 nilipo karibishwa chakula mezan tuko watu 5 nilipakua chakula kidogo kuliko wenyeji na nikadanganya kuwa nimeshakula huko nilipo toka.
Baada ya dakika 10 akaingia mtt wao katoka shule akakuta chakula kimeisha alilia sana hata alipo ambiwa asubir apikiwe chake bado aliendelea kulia huku ananiangalia kwakweli nilijiskia vbaya sana, baba wa mtoto akamtandika mtoto wake kwa kosa la kutokua na adabu na Mimi nikiwepo ndo nikaendelea kukosa amani kabisa nikajiona Mimi ndo chanzo Cha yote.
Hadi leo hii nikiwa ugenini ukifika mda wa kula ndo muda ninao uchukia zaidi na ninaweza kukataa kula kabisa kama ikiwa tu ni sehem nilienda kusalimia na kupita
Huna tofauti na mm nachukia sana nikifika ugenini muda wa kula
 
Mama alikuwa anasema ukialikwa mahali popote hata iwe harusi hakikisha unakula nyumbani kwako kwanza.

Usiende kwa watu na njaa yako ukiambiwa pakua unajaza sahani kama ndo pa kupakulia.

Au unafika ukumbini we unatoa mimacho kungojea muda wa kupakua.
Mimi nikipakuliwa chakula katika sherehe/msiba kamwe siwezi kuongeza hata kama sijashiba. Niliwahi kuandika humu watu wakaanza kunitukana
 
Mwingine anaweza kujifanya mstaarabu anakula kwa adabu kumbe kwenye pochi kajibebea magimbi yake na viazi vitamu vya kuchemsha.... Mmelala ye anajigongea vitu vyake adoado.. Hiyo inaitwa usinichoshe nisikuchoshe
[emoji1787][emoji39][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mwingine anaweza kujifanya mstaarabu anakula kwa adabu kumbe kwenye pochi kajibebea magimbi yake na viazi vitamu vya kuchemsha.... Mmelala ye anajigongea vitu vyake adoado.. Hiyo inaitwa usinichoshe nisikuchoshe
Nikiwah kwenda ugenini....sasa sijui ilikuwa wananikomoa maana kiukweli chakula nilichokuwa naekewa hata mtoto hashibi mwanzoni niliona pengine wamekosea..huko mbeleni nikaona isiwe tabu cha kujitesa nn....nikila pale najivuta mtaani nazuga naenda kuangalia mpira napitia kibandani nakandamiza chipsi yai fresh, heeee! Sikh tupo sebleni dogo si akaropoka, Duuuh, uncle mchoyo sana chakula chetu tunampa ila yeye akila chipsi zake kule barabarani anajificha...dogo asijue nilikuwa namtoa shemeji hela kila asubuhi aongeze kwenye bajeti ya msosi licha ya kuachiwa hela na mumewe...hakuna siku nilijisikia noma kama siku hiyo[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ukweli ni kwamba waandaji mnatukosea waalikwa..
Unamualika mtu chakula cha mchana may be na unajua nyakat hzo ni njaa sana alf unatenga vi-hotpot vyenye chakula kidg kdg..hapa anaeumia huwa ni wa kwanza kupakua au wa mwisho..

Wa kwanza atapakua kukadilia wenzie wanaofata wa mwisho anaweza kutana na chakula kimebaki kdg,so hawa wanaweza wasishibe..

ukiamua kualika watu pika chakula cha kutosha hata wanapoondoka usibaki na manung'uniko,huwa mnatupa tabu ya kwenda kuongeza mlo mwngne vibandan huko kufidia nafas iliobaki wazi
 
My dear Sky Eclat

Ndio maana siku zote wazazi huwa wanashauriwa kuwa wanakula meza moja na watoto wao ili wawafundishe TABLE MANNERS ikiwamo kuwafikiria wengine na hata namna ya kutafuna chakula.

Inawezekana hao wageni ndio wale waliopelekwa boarding wakiwa bado wadogo sana (darasa la tatu) wakakosa muda wa kufundishwa tabia njema na wazazi/walezi wao.

Sikubalina na wewe tena waliokwenda boarding wana adabu kali sana mimi nina table manner na nimesoma boading................ hao hawajui maana ya sharing
 
Ndo mana ukiwa na watoto unatakiwa ule nao wote mezani saa ya kula kila mtu ale kwa ajili ya kufundishana table manners
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Me nikiwa naenda popote huwa nahakikisha nimekula kabisa japo nipo half way full. Ili nikienda kwa watu niwe comfortable wakati wa msosi au kama ni mtoko tuweze agiza hata chakula simple kama bites au dessert.

Lakini unapokwenda kwa watu na njaa zako hii huwa inakufanya kuwa na akili ambayo haipo under control. Hebu imagine unakwenda kwa rafiki yako halafu haujala tokea asubuhi ulipokunywa chai kavu.

Halafu unafika unakuta wameandaa msosi unaopenda. Hapo kujicontrol itakuwa ngumu sana kwakweli. Maana utaona kazi kweli kweli kujizuia unajikuta unajiachia tu bila kujua kuwa unachafuka CV.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom