Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Mie ndo maan siwezi kula kwa watu, yaan ni kuwekewa masharti na kuchorwa tyuuuh aaaaah
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Mimi mara zote huwa ninakuwa na wasiwasi sana na watu ambao akli yao iko concentrated sana kwenye mambo ya chakula mezani. Ni kwa sababu utafiti wangu wa kina ulishanithibitisha pasipo shaka kabisa kuwa kawaida watu hawa huwa wana shida kubwa sana mahali fulani kichwani
 
Tatizo lenu mnapika chakula kidogo mboga kidogo akitokea tu mgeni roho mkononi sijui atachukua kiuno cha samaki? Uchoyo tu usukumani mbona haya hayapo mnakwama wapi bandugu?
 
Noted. Ila mimi sipendi kabisa kula kwa watu. Na ikitokea basi huwa napakuwa chakula kiwango kidogo kadiri nitakavyoweza. Ni bora nisishibe ugenini, nitaenda kujazia mbele ya safari (nyumbani).
Ukiwa unaenda kwa watu, fabya backup hata ya kiepe au fruits, ukifika unapakua kiasi.
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
wapakulie kabisa
 
dah'table manner inamatter sana'watu wengi nilokutana nao sehemu mbalimbali kiukwel hili suala ni changamoto especially wanaume yaani wanavitabia vinakera sana wakati wa chakula
 
Ustaarabu ni Relative Term, ukute mwenzio alichokifanya ndio ustaarabu wake!
 
Kwenye kila family kuna yule mwamba
Huwa anaambiwa .

Pakua chakula kidogo wenzio hawajala
 
Kweli mkuu mi pia nilikua na tabia hio lkn sku moja niliadhirika kwasababu nilipakua chakula kingi Sana mpk wengine wakakosa ikabidi dada wa kazi akaange chips za fasta ili wale
Lkn mungu hataki dhambi kile chakula nimekula nusu tu kikaanza kunishinda
Kwakweli ilikua aibu kubwa Sana
Tangu siku hio nimejifunza
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kabla sijapakua mboga uwa nascan bakuli kwanza kwenda chini kupata idadi kamili ya yaliyomo kama yamo

Nacross multiplication vs number of remaining candidates
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]

Apo nikipanda juu na kijiko shughuli imeisha


Remember this is a very quick assessment [emoji23]
 
mimi ni mtumia smart phone wakati nakula ila nafanya hivo kama wenyeji ni wa umri wangu vijana wenzangu na tuwe wachache
 
Mama alikuwa anasema ukialikwa mahali popote hata iwe harusi hakikisha unakula nyumbani kwako kwanza.

Usiende kwa watu na njaa yako ukiambiwa pakua unajaza sahani kama ndo pa kupakulia.

Au unafika ukumbini we unatoa mimacho kungojea muda wa kupakua.
 
Hapo kwenye smartphone inamaana mtu asijibu ujumbe wa mtu aliotumiwa

Ufipa group mna nongwa😀😀😀
 
Samaki sio mboga ni kitoweo.
Jifunzeni Kiswahili hasa kwa awamu ya tano
Sijui ni ulafi au Uzungu, wewe kama umepika wachache si shida ni yako? kwanini usiweke kwenye sahani na mkashea hasa kwenye upande wa mboga? Hivyo vipande vitatu ni vya gram ngapi kila kimoja? Chakula cha manung'uniko bhana mwisho mtu anigwe na mfupa kisa jicho la usuda la kuchukua samaki mmoja (tena kagawanywa vipande vitatu) mwenye gram 400.

Kwani haufahamu siku hizi chakula ni mboga, YAANI MBOGA INAKUWA KUBWA ZAIDI YA WALI/UGALI?
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Hatufundishwi ustaarabu wa kula, na suluhisho acha kwenda kwenye nyumba za watu, nenda kwa hotel kula unachotaka, au nunua nyumbani kwako. mambo ya kuingia ingia kwenye nyumba za watu acheni.
 
Back
Top Bottom