Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Hii iliwahi nitokea
Niliweka ugali kwenye hotpot na mboga kwenye hotpot

Jamaa walikuwa wawili wakanawa wakasogeza hotpots zote wakapiga msosi nafika na visahani vyangu tukate ugali,
Shughuli imeisha
Hawa ndio wanaume wa shoka, kama uliwahi kusikia basi ndio hao.
 
Wakati wa likizo huu unapokea watoto wamekuja likizo. Asubuhi umezoea kuwakaangia watoto wako mayai manne lakini wenyewe umewafundisha kuwa ni lazima kila mtu apate.

Wanakuja watoto wageni wanamaliza mayai yote wanao wanabaki wanaangalia. Kama wangefundishwa wote wangegawana na wote wangepata hata kipande kidogo.
Unapopata wageni wenye Tabia kama wametoka Ethiopia zile main mboga kama kuku, nyama na samaki usiwe unapakua zote unaweza kupakua hata robo tabu. Wale wanaofikiria kuwa wenzao hawali wakishajaza lumbesa unaenda kumaliza na waliobaki wanapata. Kuhusu mayai kama sio watu wazima unaweza kukaanga yote na kukata vipande vipande. Samahani najibu huku nakula 🙄🙄🙄
 
Mwingine anaweza kujifanya mstaarabu anakula kwa adabu kumbe kwenye pochi kajibebea magimbi yake na viazi vitamu vya kuchemsha.... Mmelala ye anajigongea vitu vyake adoado.. Hiyo inaitwa usinichoshe nisikuchoshe
 
Kabisa mkuu....na unawekaje samaki 8 exactly na idad ya wageni buana....weka misamaki yakutosha kama una wagen usibanie

Mi bi mkubwa wangu akiandaa meza aisee..mnaweza kula had mkatambaa
Hao ndio wamama ambao walikotoka hamna njaa njaa...Ila simshangai mtoa mada sana, ndugu zetu wa Lushoto wana choyo sana mezani 😝 naongea ikiwa nimekulia familia yenye mama msambaa wa lushoto.

Alikuwa mtu wa kumaindi sana misosi.
 
Sema Shemeji wale samaki uliwawekea nini!!? Maana si kwautamu ule.alafu next time shemeji samaki wapakae chumvi na ndimu alafu waanike kabla ujawakaanga,

Alafu shemeji ulijuaje km samaki mi ndo ugonjwa wangu??

See you next weekend my favorite shemeji I can't wait to see you,
😝😂😂😝😝😂😂😂 shemeji atakoma
 
Shemeji siku nyingine upikege na wale kambare, huwa watamu sana hasa waliokaushwa wale ukiunga na nazi acha tu shemeji,,,ugonjwa wangu sana ule 😂😂😂😂😂😂
 
Bora tu umejichagulia utaratibu japo pia utasemwa jamaa kaona chakula chetu cha hovyo nini?
Chakula kizuri Ila sishibi Bora nikatae maana hawakunihesabu, wakinilazimisha nitawaambia ukweli kwamba hukunihesabu sishibi kwa hiyo sili na sili kweli
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Ulimwambia? Au ndo umekuja kumripoti huku kwenye mahakana ya JF?
 
Unapopata wageni wenye Tabia kama wametoka Ethiopia zile main mboga kama kuku, nyama na samaki usiwe unapakua zote unaweza kupakua hata robo tabu. Wale wanaofikiria kuwa wenzao hawali wakishajaza lumbesa unaenda kumaliza na waliobaki wanapata. Kuhusu mayai kama sio watu wazima unaweza kukaanga yote na kukata vipande vipande. Samahani najibu huku nakula [emoji849][emoji849][emoji849]
Kwani mkubwa hakatiwi hilo yai?, hapo wewe ndio unakuwa mpakuaji na unauliza hiki vipi kinatosha? Mboga nampakulia na yai nakata vipande husika, kuna wageni unaangalia wanaweza kulaza wengine na njaa
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Angalau leo nimekuelewa
 
[emoji13][emoji23][emoji23][emoji13][emoji13][emoji23][emoji23][emoji23] shemeji atakoma
Safari hii kabla sijaenda kwake napitia Gym kwanza kutanua utumbo,

Nitafurahi kweli weekend hii akipika Ugali na samaki wa kukaanga kachumbali pili pili asiweke nyingi iwe kwa mbali,
 
Ungemwambia Baba mdogo kaishi kwetu miaka na mamiaka hatujawahi muuliza anaondoka lini!
Aina maana, mwanamke mwenyewe waliachana, na sikumwambia faza Wala nin, alisema wameshindwana Tabia, kaondoka mi na faza undugu huko pale pale.
 
mtot anasoma boarding miaka yote mpak form 6, akitoka hapo jtk, huko hakuna kabisa nidham ya kula. kafanikiwaa chuo, uhuru wa kupitiliza.mtu akitafuna chakula mdomo wote wazi, kelele za chakula kikitafunwa mpk kero kwa jirani
 
Aisee nimecheka sana...lakini huo ndio ukweli! Mimi nilipata mgeni last two weeks lakini alikuwa wakipekeee...alikuwa anakuja na Taulo tena akiwa kifua wazi Mezani! Muda wote alikuwa akizunguka na Taulo na bila Vest ndani hata pale ambapo walikuja wageni zake kumtembelea! Hakika nilikuwa na wakati mgumu sana! Lakini finally nilitumia diplomasia kumuondoa!
Kweli Kabisa, mi wageni wa kiume home nawaogopaga sana, napenda wageni wa. Kike zaidi
 
Huyo atakua amezoea maisha ya kukaa kwenye chumba kimoja. Chumba, sebule na jiko vyote unaviona ukiamka asubuhi, hata kushinda na taulo ni sawa tu.
Licha ya hivo huyo kazoea maisha ya uswazi. Yan ni mswazi halafu hajitambui
 
Back
Top Bottom