Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

Kuna wageni ambao hawana ustaarabu mezani saa ya chakula

We ukija kwetu utaishi kwa tabu sana

Bi mkubwa wangu ukipakua paja moja la kuku anakuongezea yeye mawil..hahahah..hata muwe wangap kwenye meza.....sasa sis wengne tumeendeleza hyo tabia..


Hahah natania.......ila kwel bi mkubwa wangu sis watoto wa kiume alikua anatuoverload mda wa kula sana...
Kwahio mlikuwa mnapika kuku wangapi maanake mapaja yako mawili tu. Kula mapaja mawili au manne ni kujaza choo tu kiwango kinachohitajika ni kidogo sana. Ni Sawa na mtu anaekula ugali mwingiiii anajaza Choo tu.
 
Mwingine anaweza kujifanya mstaarabu anakula kwa adabu kumbe kwenye pochi kajibebea magimbi yake na viazi vitamu vya kuchemsha.... Mmelala ye anajigongea vitu vyake adoado.. Hiyo inaitwa usinichoshe nisikuchoshe
[emoji23][emoji23]
 
Nimepitia comments zote nimeona jinsi nilivyosumangwa 😔

Mungu atawalipa tu
 
Mimi utaratibu wangu nikienda kutembea kwa watu.mda wa kula unakuta kabla ya hapo nilipita sehem nikajipigia kitimoto na balimi mbili murua kabsa,kwa hyo wakileta chakula napakua punje 6 tu za wali,samaki ntaweka mifupa,nawambia mi sio mlaji sana.(kinachonicost tu nna tabia ya kuchomeka toothpick kichwan af nasahau kwa hyo wakiona vile wanajua uyu mwamba Kuna sehem kagonga heavyfood.


Kuna dogo alisanua et aliniona wanapouza kitimoto ilihali m mgeni kwenye huo mji.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwani mkubwa hakatiwi hilo yai?, hapo wewe ndio unakuwa mpakuaji na unauliza hiki vipi kinatosha? Mboga nampakulia na yai nakata vipande husika, kuna wageni unaangalia wanaweza kulaza wengine na njaa
Point, Mambo ya kulazana na njaa hapana.
 
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Ukitaka kumfahamu mtu kastaarabika vipi basi mwangalie wakati wa kula jinsi anavyobehave. Meza ya Chakula ni mojawapo ya kipimo kizuri sana cha tabia ya mtu.
 
Ni wapi huko nasie tuhamie maisha ya mjini hayataki masihara Ndugu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Poleni sana watu wa Dar, sisi huku mikoani mgeni akikaribishwa na akajipakulia Lumbesa ndiyo furaha yetu na faraja ya kumkirimu mgeni, hatuna takrima zingine mbali na msosi lumbesa.

Huko Dar chakula ni ghali mno hiyo ndiyo sababu ya manung'uniko yenu.

Mimi siwezi kuishi Dar katika hali ya kawaida, huko nasikia Embe dodo moja ni sh 1000---1500, wakati huku nilipo ni shs 250---300 nk.[emoji1787]
 
Unamchana LIVE tu sasa mbona umechukua vipande vya samaki vitatu wakati kuna wengine HAWAJAPAKUA? 😳
Unakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa katikati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.

Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.

Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.

Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
 
Tabia nisiyoipenda kwenye kula ni wale wanaotafuna kwa kutoa sauti na wale wanaokula huku wanajilambalamba vidole na mikono.
 
Kweli mkuu mi pia nilikua na tabia hio lkn sku moja niliadhirika kwasababu nilipakua chakula kingi Sana mpk wengine wakakosa ikabidi dada wa kazi akaange chips za fasta ili wale
Lkn mungu hataki dhambi kile chakula nimekula nusu tu kikaanza kunishinda
Kwakweli ilikua aibu kubwa Sana
Tangu siku hio nimejifunza
 
Kuna wale wanaotafuna chakula utadhani mtu anatembea kwenye matope, arggg wananikera kinyama
 
Back
Top Bottom