Kuna wenye nyumba wana roho mbaya usiombe

Misuko suko ya aina hii inapelekea kumiliki nyumba yako.
 
Wewe wasema
 
Bora huyo wa kwako mkuu. Kwenye moja ya biashara zangu, kuna fremu nimepanga lakini mwenye nyumba mjinga sijawahi ona.

Kama alikuwa anakudai hata elfu 10 na akaona wateja wamejaa kwako anakufata kuja kukuomba pesa yake ili watu wajue kuwa unadaiwa.

Na wakati mwingine biashara yako ikienda vizuri, ghafla atakuambia chumba chako anampango wa kukitumia, na hata kodi ikiisha anaomba uendelee.
 
Wengi wao wana vielement vya kichawi huwa siyo bure
 
Huyo wako ana wazimu[emoji23],
 
Hapo mwaka ni 84 au 94 faza na bado unasema ulikua una machalii wawili...
Nimemaliza shule 1978 ilunda primary school mwaka 1981 nikaozeshwa mwaka 1982 tukajaliwa kupata watoto mapacha hao wawili mwaka 1983 nikapata mchongo kwenye magari ya chama cha ushirika nyanza nikapiga kazi miezi kama 9 hivi nikakutana na jamaa mfanyabishara enzi hizo akanichukua tukaanza kazi ya kwenda kuchukua bidhaa kisumu na hapo ndiyo nikapata kupanga mitaa ya uhuru
Nikakutana na hayo masaibu ya baba mwenye mjengo
 
Daah wewe ni Uncle angu umri wa wajomba zangu huo...mwaka 1978 nina miaka miwili nafungwa nepi tuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…