Kuomba mchango wa harusi ni matusi makubwa

Kuomba mchango wa harusi ni matusi makubwa

Wagalatia huwaambii kitu kuhusu huo ushamba wanapenda ufahar wakati kipato duni.
Umenikumbusha mbali sana, kuna jamaa akawapa kadi washikaji, sasa yule mmoja hakutoa kabisa yaan pamoja na shughuli kupita yule jamaa alikuwa anadai gharama za kadi aliyochukua, jamaa akamtolea uvivu ndio akapotelea mbali
 
Ukiwa mtu wa kutaka attention ni kweli utasumbua watu wakuchangie.
 
Nacheka kama mazuri.....juzi jamaa angu kafunga ndoa,kahenyeka kupata michango.

Haya sasa sherehe imeisha nikamuuliza umepata sh ngapi nikutafutie ata kausafiri used...Looh eti ana 2ml afu budget ya harusi ilikuwa 10ml
 
Jumapili au Jumamosi funga ndoa kanisani rudi nyumbani na mwenzi wako muishi kwa amani na furaha. Nendeni ofisi ya DC fungeni ndoa mrudi nyumbani muishi kwa amani.
Au fungeni ndoa nyumbani kwa binti murudi nyumbani mukaishi kwa amani.
Kama unataka kufanya sherehe ruksa, fanya kwa uwezo wako. Mchangishane wana familia, hiyo ndio heshima na busara. Marafiki mutualike tu, kwakuwa tunajua mnaanza maisha hatutakuja mikono mitupu. Pesa mtapata ambazo mtafungulia biashara au kuanza ujenzi. Vyombo mtapata pia.
Hii ya kukabana michango mwisho wa siku ikipatikana millioni 20 yote wanakula ma MC, wapambaji, catering, wapiga picha nyie mnabakiwa na laki 6 .
Hakuna zawadi ya maana rafiki au workmate alitetoa mchango atakuletea.
Sherehe utaiandaa kulingana na kiasi cha fedha. Wengine wameanza maisha ya ndoa kwa mkosi wa madeni .
Hiyo ndoa itajaa madeni, madeni, madeni mpaka ivunjike.
Hakika
 
Basi na isizidi laki mbili
Mahari hutegemea hadhi ya mtu wako hadi wa elfu tano wengine hadi milioni 20 hadi 50

Katafute wa saizi yako mbona wako wengi tu wa bei hiyo

Usitarajie mtoto kasomeshwa acadeny International schools nk aje aolewe na wewe choka mbaya kwenu mumejaa kunguni na viroboto kwa mahari ya laki mbili

Mpuuzi katafute maskini wenzio size yako ukaoe huko kwa hizo laki mbili zako
 
Wagalatia huwaambii kitu kuhusu huo ushamba wanapenda ufahar wakati kipato duni.
Hakika, ukitaka kugombana na wagalatia ongelea vibaya harusi na michango yake ya mbwembwe nyingi hadi za kukabana koo.
 
Sa tusipofanya harusi na kukesha na matarumbeta majirani watajuaje kama tumeolewa😊.....

Mi ntaolewa lulu majizzo style.watu wachcahe pande zote mbili,vinywaji na catering ya watu 50 tu
Hata Kwa budget ya mil 3 unafanya mwenyewe Tena nyumbani.usiku mnene Kila mtu arudi kwao.ismeisha

Mipango mingi mume mwenyewe sina
Mume niko hapa my dear
unataka kuolewa mwaka huu au mwakani?
 
Ungesema tu wakristo ndio wapo hvyo kwasababu hawana jambo dogo yaani hata hamjuani kashakuletea kadi ya harusi na kiwango kaweka ila unaweza ukawa na rafiki muislamu akaoa wala usijue.

Kuna group moja la kazini sijawahi kuona mchango wa muislamu ila ni wakristo tena wanawake mpaka send off ila hawa jamaa kwenye msiba ndio balaa keneza tu million 2.
 
Back
Top Bottom