The redemeer
JF-Expert Member
- Jan 28, 2025
- 1,497
- 2,681
90% ya ndoa zote zimeshikwa na pesa ukitaka kujua hili check ndoa za wastaafu wanakufa mapema kwa sababu hawana tena cha kuwapa wake zao kama zamani
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Respect brotherNdoa ni tamu tena tamu sana. Ukio mtu unaempenda na anayekupenda. Ila ndoa ni ngumu pia sababu inabidi ujikane mwenyewe kwajili yake na yeye ajikane mwenyewe kwajili yako.
Kabla haujaoa sali, mwambie Mungu akuletee ataekuwa msaada wako. Na Mungu anakuletea anaefanana na wewe bandugu, hauwezi kuwa muasherti ukapata malaika utapata muasherati mwenzako kwahiyo kama
Unataka kamalaika inabidi na wewe uanze kuwa kamalaika kama unataka mdada mwenye akili inabidi nawewe uwe na akili.
Ukishaoa kuna kudumisha penzi, wengi mnadhani ukioa ndo umemaliza la hasha… ukitaka uyo mwanamke akuheshimu kila mwezi dumisha penzi nogesha penzi uyo mwanamke atakuhusudu
La mwisho ndoa ina siri nyingi, kadri utavtoweza kumbariki mkeo na familia ndivyo na wewe utabarikiwa. Wanawake hawana formula ila ukifanya maisha yake yawe mepesi na ukampenda haswa wanaume wengine atawaona kama mafala. Ila pia kuwa mkali, weka misingi yako, mimi nafanya a mpaka z, ikitokea mama umekiuka uaminifu wangu sina mazoea.. ni kwenu! Ajue mwanzo vitu vinavtoweza kuuua jitihada zako na kiweke hiki kipengele mbele kwamba huna msamaha… ila huwezi kisema huna msamaha afu na wewe janja janja wanawake wengine wanakutaka sio unawaendekeza ovyo
Pia ndoa inatunufaisha wanaume kuliko wanawake. Mimi tangu nimeoa naishi kama mfalme!, nina watoto wanasoma sijui ada shing ngapi ata mke tu anatoa kwenye account analipa, nyumba ina chakula muda wote nina wadada wa kazi wawili na mlinzi yani me kazi yangu kwenda kazini kwenye mishe piga madili saka hela weka kwenye account , mama ana vibiashara vyake duka nje tu ya nyumba ni frem. Leo nikisema tununue gari anasema we tafuta million 5 tunaenda. Tukihitaji kujenga natoa hela na mjenzi mama anasimamia sho mpare mbahili mkali hacheki na yeyote… nilivokuwa single nilikua nalipwa kazini million moja na nusu sielewi inaishaje leo nimeoa nina mishe tu ile hio hio mllion moja na nusu imezaa nyumba, magari, inasomesha na inalisha nyumba watu 7, huyu mama ameniheshimisha ila asivunjike moyo nampelekaga tu dubai, south africa.. kagari kadogo ka ist roho yake nyeupe. Kwa macho ya kawaida unaweza diriki kusema eti ana nufaika zaidi yangu? Walaaaa ila namgharamia maana haya yote ni ya watoto na ni maisha katengeneza yey me nimetafuta tu na kuweka mezani… ila ndo kupata kama huyu haumpati club wala wavuvi. Na mke wangu alikuwa mshamba me ndo nimsop sop mpaka sasa kimekaa kama kidada cha mjini kumbe mpare mmoja kutoka sanya juu alie na krismasi 5 tu Dar
Ndoa bila Mungu haiwezekani ndugu zangu, swali, sali. Kuweni na mtumishi mmoja mwaminifu (awe ameoa )wa kuwashikilia mkono maana mtakosana tu na mtahitaji mpatanishi.
Zingatieni haya ndo mtaichekelea bila hivyo kila siku mtalia
Inahitaji d2 kuelewa hii point yako mkuuNa ndoa yeyeto kama mama mkwe hanufaiki na hio ndoa itavunjika.
Ndoa ni uwekezaji
Mada imeishia hapa.. saluteSiku hizi hata wanaume wengi hawana uwezo wa kusimamia ndoa nayo nisababu kubwa Kwa wanawake kuwa nguvu,
Mfano mwanaume badala ya kumweka mke sawa ila yeye kazi yake mpaka aongee na mama yake au dada zake unategemea nini ? Badala ya kuongea na baba yake ampe mikakati ya kuishi na mkewe hakuna, mwanaume anamnunia mkewe kweli?😐😐😅😅 Hapo unategemea atakuwa na akili ya kutoa amri Kwa mkewe? Mme kama kichwa inatakiwa akisema hilo hapana ni hapana kweli, lakini nyie wa sasa m akaa na dada zenu na mama zenu mnamsengenya mke uwiii!!!!!
Vijana wasasa kaeni na watoto wenu wawe wanaume sio mtoto wa kiume.
Mama wa kibongo akioza bintie yake kwako kafanya uwekezaji thus ni lazima waulize anafanya KAZI, biashara gani?Inahitaji d2 kuelewa hii point yako mkuu
Uko sahihi, ukienda hivi utaambiwa una roho mbaya Kwa mkeo, mtemi, mbabe n.kSiku hizi hata wanaume wengi hawana uwezo wa kusimamia ndoa nayo nisababu kubwa Kwa wanawake kuwa nguvu,
Mfano mwanaume badala ya kumweka mke sawa ila yeye kazi yake mpaka aongee na mama yake au dada zake unategemea nini ? Badala ya kuongea na baba yake ampe mikakati ya kuishi na mkewe hakuna, mwanaume anamnunia mkewe kweli?😐😐😅😅 Hapo unategemea atakuwa na akili ya kutoa amri Kwa mkewe? Mme kama kichwa inatakiwa akisema hilo hapana ni hapana kweli, lakini nyie wa sasa m akaa na dada zenu na mama zenu mnamsengenya mke uwiii!!!!!
Vijana wasasa kaeni na watoto wenu wawe wanaume sio mtoto wa kiume.
Kila raheri maisha ni kuchagua, endelea kutafuta pesa Kisha uje kula na mijusi 😅😅😅😅(ila kuoa sio lazima )Ni kweli unayosema ila yote hayo nimesha yafikiria na nimeona ni batili,rafiki wa kweli ni pesa tu hata watoto nao utafika umri wataenda kujitafutia maisha yao kwahyo bado utabaki mwenyewe kama ulivyo kuja mwenyewe ndio utakavyo ondoka mwenyewe.
Wanandoa wengi hawaongei wengine viburi wengine mie ndiyo mwanaume, kila mtu anabeba lake lakini kila mtu aseme mie nataka hivi mwingine hivi Kisha mchague hakuna, na.hili jiji letu watu wanazurula weee mpaka usiku hoi nyumbani kunadodaUko sahihi, ukienda hivi utaambiwa una roho mbaya Kwa mkeo, mtemi, mbabe n.k
Nashindwa kuelewa tufanyeje
Lakini zigo lote kwa mke badala ya kujiuliza sababuMada imeishia hapa.. salute
Mbona kama kuna muda unaingia kwenye mfumo alafu unatoka hivi?Kila raheri maisha ni kuchagua, endelea kutafuta pesa Kisha uje kula na mijusi 😅😅😅😅(ila kuoa sio lazima )
😄😄😄😄 Si hautaki kuoa?Mbona kama kuna muda unaingia kwenye mfumo alafu unatoka hivi?
KATAA NDOA ALUTA CONTINUA😄😄😄😄 Si hautaki kuoa?
Kuna mwana JamiiForums ameelezea Hizi point ukipata wasaa kaa chini uzisome kwa kutulia bila mihemko,kwa Era ambayo tupo sasa ndoa ni mtego na wana ndoa wengi wameingia kwenye ndoa ili kuficha maovu yao si wanawake si wanaume😄😄😄😄 Si hautaki kuoa?
Umeandika mengi mpka yanachosha kusoma, wewe tabia njema unazo ? Au unataka mwanamke ndiye azifanye peke yake? Unazani yeye hapendi amani ya moyo?Kuna mwana JamiiForums ameelezea Hizi point ukipata wasaa kaa chini uzisome kwa kutulia bila mihemko,kwa Era ambayo tupo sasa ndoa ni mtego na wana ndoa wengi wameingia kwenye ndoa ili kuficha maovu yao si wanawake si wanaume
Kukosa amani ya moyo kwa kusababishiwa na mkeo kwa makusudi ili kupima misimamo yako, utapewa presha za bure taka usitake hakika
2: Maomivu ya moyo kutokana na mkeo kukupa stress zisizo na mpangilio kila siku, kukudhohofisha ili tuu aweze kukutawala
3: Kuchapiwa, utachapiwa mkeo na bado utakalishwa chini na wazee na kuambiwa kuchapiwa ni siri ya ndani jiangalie ulipomkosea mkeo na vumilia huo ndiyo ukubwa
4: Utanyanyaswa kimwili na kiroho, kulala njaa na kunyimwa unyumba ndiyo zitakua asante zake kwako baada ya kumuhudumia kwa kisingizio cha kuugua, uchovu au ugomvi au vyovyote vile mkeo atakavyopenda kukunyanyasa
5: Mwanamke atakua kinyume chako kwa kila kitu pia atakua ananukuu maongezi yako ili apate pakukuadhibia kisawaswa, haijalishi utaongea kwa wema au kwa utani atakunyoosha sana pindi akinukuu vibaya maongezi yako
6: Hela za mwanamke wako zitakua ni zake peke yake na ndugu zake. wewe hela zako zitakua zenu wote na ole wako usitoe hela utasaidiwa majukumu na vijana wa mjini kwa namna mkeo atakavyotaka yeye
7: Ukimpendezesha mkeo atatongozwa na atajiona alikosea kuolewa na wewe, atajiona ni mzuri bila kujua wewe ndiye uliyemfikisha hapo. Ataanza kukudharau na kuwapenda wa nje na wewe kubaki kuwa siyo type yake
8: Utasalitiwa kiroho na kimwili taka usitake kwa kisingizio cha kulipiwa kisasi iwe ulifanya baya au jema hakika utalipiziwa ni kitendo cha muda tuu
9: Mkeo akiwa mfanyakazi atamsikiliza boss wake na akiwa muumini wa dini kiongozi wake wa imani ( dini) kuliko wewe mume wake hao ndiyo watakuwa waume zake halali
10: Daima mkeo atakuona kikwazo kwenye uhuru wake na maendeleo yake binafsi. Ataona wewe ndiye unaye mkwamisha kwa kila kitu
11: Gubu halitokaa liishe hiyo ndiyo fimbo ya kuchapiwa wewe daima na milele kwa sababu kukupiga hawezi
12:Huyo mwanamke uliye muoa atataka akae kwenye nafasi yako akuongoze na kukufunga kauli kwa njia yeyote ile iwe hata ya kukuloga, kikubwa ni akutawale tuu
13: Mkeo atakuona una chukia ndugu zake , haijalishi ndugu zake watakuja kuleta uharibifu kwako ila daima atakuona wewe una chuki na ndugu zake pindi utakapoongea kusahihisha makosa ya ndugu zake.
14: Baba yake na mkeo atajiona ana nguvu kwenye ndoa yako, atapindisha mawasiliano na kuyapekeka direct kwa mkeo ili tuu uonekane sikitu siichochote kwa mwanae. Atafanya hivyo ili mkeo awe anakupa taarifa na siyo kuomba ruhusa kwako kama mume wake
15: Mkeo atakuambia aliacha ndugu zake ili aje kwako hivyo hana chakupoteza kwako, hata ogopa kuachiaka kwasababu nyumbani aliambiwa hajafukuzwa, akishindwa huko kwenye ndoa kuliko aumizwe akirudi watampokea ni mwanao.
16: Mkeo atashindana na wewe daima taka usitake, atakua mbishi sana na mwenye malumbano na wewe mwanaume kuliko hata kabla hukumuoa, utii kwake utakua ni utumwa
17: Kuulizwa ulikua wapi , kwanini unanijia sasa hivi hiyo ndiyo salamu yake kwako pindi utakapochelewa kurudi nyumbani, haijalishi hata huko ulipokuwepo ulinusurika kupigwa risasi, uliopolewa kwenye ajali au ulikua matatani ila salamu yake utakua niambie ulikua wapi au ulikuwa kwa malayer zako
18: Utasusiwa na kususwa kwa kila hali, utadharauliwa na kunyong'onyeshwa daima na mkeo, mkeo hatokua na msaada na wewe
19: Mkeo atakutingisha sana kwa makusudi kwa kila kimbwanga na ukichechemea atakuona huna msimamo kama mwanaume, na ukiwa na msimamo atakuoana wewe ni mkoloni, mbabe na siyo romantic
20: Daima wewe mwanaume utanyonywa kila mahali na mkeo, utanyonywa kitandani na bado utanyonywa hela zako, utanyonywa akili yako na nguvu zako mpaka ubaki chakari mtupu hufai tena
21: Mkeo atakunafikia sana kuishi na wewe kwa upendo kwasababu bado hajapata kile anachokitaka kutoka kwako, siku akikipata popote pale ataondoka kwa dharau na kukuacha ukiwa hoi taabani
22: Ukikosa hela mkeo ataenda kudanga na ukiuliza atakuambia hakuna kitu unampa so ulitaka afanyaje wewe ni mwanaume gani, iga wanaume wenzako au wewe ni mwanaume suruali
23: Mkeo atakua ana kuuliza kila wakati ukifa utatuachaje, maombi yake yatakua daima ni weww ukifa utawaachaje, mbaya zaidi kama una mali atakuambia andika mirathi usije ukafa ukanisumbia tuteseke.
24: Watoto wako watakudharau, watakuona siyo kitu kwao, watampenda mama yao na kukuchukia wewe baba mzazi haijalishi ulishinda njaa ili wao wale pia ukizeeka watakuona wewe ni kero kwao na ikibidi watakutelekeza hakika
25: Huyo mkeo atafanya makosa daima na ukimwambia ukweli atayageuza kuwa ni makosa yako na wewe ndiye sababu ya yote hata kama ukiwa umekufa atageuza makosa yake kuwa yako na wewe kuwa ndiye sababu ya yeye kukosea