Kutawala kwa picha ya Rais Samia uwanjani ni ishara ya mafanikio katika kujenga umoja wa kitaifa na kukubalika kwake

Kutawala kwa picha ya Rais Samia uwanjani ni ishara ya mafanikio katika kujenga umoja wa kitaifa na kukubalika kwake

Tuseme tu ukweli ni ushamba.
Hivi na kwa wenzetu wanafanya hivi?
Mliopo nchi nyingine mnijuze tafadhali
Ni ujinga tu mkuu, siku zinavyozidi kwenda ndio watanzania wanazidi kuwa wajinga.

Tumekuwa na shule na vyuo vingi nchini lakini unashangaa watu wanazidi kuwa wajinga tu, tena inashangaza zaidi wale waliopata bahati ya kupita huko vyuoni ndio wametoka wakiwa wajinga wabobevu.

Chunguza uone hilo wazo la kubeba picha za marais kwenye mpira huwa linatoka kwa nani utashangaa.
 
Ukweli gani?. Kiongozi anatakiwa kuwa challenged ili afanye kazi.

Sasa kila siku mapambio ya kijinga ndo maana hata mfumuko es bei hawahangaiki nao wanajua kuna wajinga kama wewe wanasifia kila kitu
Kwani kuongea ukweli ndio uchawa? Kwa hiyo wewe hapo unapinga pinga kila kitu ili upate faida gani? Tusijenge Tabia ya kuwakatisha Tamaa viongozi aina ya Rais Samia waliojitoa na kujitolea kututumikia watanzania kwa uzalendo mkubwa
 
Ni ujinga tu mkuu, siku zinavyozidi kwenda ndio watanzania wanazidi kuwa wajinga. Tumekuwa na shule na vyuo vingi nchini lakini unashangaa watu wanazidi kuwa wajinga tu, tena inashangaza zaidi wale waliopata bahati ya kupita huko vyuoni ndio wametoka wakiwa wajinga wabobevu.

Chunguza uone hilo wazo la kubeba picha za marais kwenye mpira huwa linatoka kwa nani utashangaa.

Kuna mambo yanaweza kufanya ukapoteza uzalendo kabisa. Wapuuzi sana
 
Hizo hoja mbadala ndio nataka na wewe uzilete ili Nasi tuzione na kutoa mawazo yetu lakini kwa Sasa nimeona namna mh Rais alivyojitahidi kuweka mikono yake katika kila secta ili ipate kuinuka na kuwanufaisha Watanzania wengi, ndio maana unaona hata secta binafsi mh Rais anajitahidi na kufanya kazi kubwa ya kuweka mazingira mazuri ili iweze kukua na kutoa mchango katika uchumi wetu na hata kutoa ajira kwa vijana wa kitanzania
Amefanya nn kuhakikisha vijana wanajiajiri Kwa kupata mikopo ktk fedha zinazokuja Kutoka hazina kwenda halmashauri na majiji??

Pesa za mikopo Kwa vijana wanapewa UVCCM wagawane.

Ili kijana apate sharti ajiunge CCM,

Nchi hii Si yenu, ni ya Watanzania wote bila kujali vyama.
 
Uwe na shukurani na kujifunza kupongeza, Hivi wewe huoni kuwa mh Rais amefanya kazi kubwa Sana katika kumsaidia mwananchi kiuchumi? Huoni alivyopambana kukabiliana na mfumuko wa Bei kwa kutoa Ruzuku ya mabillioni ya pesa za kitanzania? Huoni kazi kubwa aliyoifanya mh Rais kusogeza huduma karibu ya mwananchi na hivyo kupunguza adha ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma?
Wewe utakuwa unaishi nchi ya kusadikika, ni mfumuko upi wa bei alokabiliana nao kama leo mchele kilo moja ni shilingi 3,200/= na vingine vingi viko juu. Rais kamsaidiaje mwananchi kiuchumi wakati mtaani kila mtu ni kilio?

Ni huduma zipi Rais kasogeza kwa mwananchi, barabara mbovu, maji hakuna, madawa hospitali hakuna halafu unajinasibu kwa kujipendekeza, tuulizeni sisi tunaoishi na jamii kubwa ya Watanzania tuwaeleze life lilivyo gumu na huyo Mama haelezwi ukweli na wasaidizi wake.

Namshukuru Mbunge wa Geita Mjini Mh. Constantine Kanyasu majuzi alipata ujasiri wa kusema waziwazi ni kwa namna gani wananchi wana hali ngumu ya maisha tofauti na Mama anavyolishwa matango pori
 
ni tabia za kike ndio zinawasumbua mashabiki wetu! duniani kote mpira unapigwa lakini huwezi kuona picha za marais wao! pale mchezo wa soka ambao rais wake ni karia ,motsepe,na infantinho,kwa nn wasibebe mabango ya hao? shame!
Biashara ni matangazo.
 
Wewe utakuwa unaishi nchi ya kusadikika, ni mfumuko upi wa bei alokabiliana nao kama leo mchele kilo moja ni shilingi 3,200/= na vingine vingi viko juu. Rais kamsaidiaje mwananchi kiuchumi wakati mtaani kila mtu ni kilio? Ni huduma zipi Rais kasogeza kwa mwananchi, barabara mbovu, maji hakuna, madawa hospitali hakuna halafu unajinasibu kwa kujipendekeza, tuulizeni sisi tunaoishi na jamii kubwa ya Watanzania tuwaeleze life lilivyo gumu na huyo Mama haelezwi ukweli na wasaidizi wake. Namshukuru Mbunge wa Geita Mjini Mh. Constantine Kanyasu majuzi alipata ujasiri wa kusema waziwazi ni kwa namna gani wananchi wana hali ngumu ya maisha tofauti na Mama anavyolishwa matango pori
Mfumuko wa Bei mh Rais amekabiliana nao kwa ustadi mkubwa Sana , mfano katika Nishati ya mafuta mh Rais alikuwa anatoa Ruzuku ya billion Mia moja kila mwezi, Hatua hii ilisaidia Sana katika kumpa ahueni mwananchi mnyonge ambaye ndio mhanga kunapotokea mfumuko wa Bei, maana mfanyabiashara hupanga Bei kulingana na gharama alizotumia kuongoza mzigo nchini, pia Ikumbukwe kuwa siyo serikali ya CCM iliyopandishaa Bali Ni Bei katika soko la Dunia iliyotokana na Vita huko ukrein

Ukija katika kilimo nako unakuta juhudi na mikakati thabiti iliyofanywa na mh Rais kukabiliana na mfumuko wa Bei za pembejeo, Hapa mh Rais ametoa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini hatua iliyopelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni zaidi ya nusu, mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu wakulima tunapata mbolea hiyo kwa elfu 70 tu,

Ukija katika Elimu mh Rais amefanya kazi kubwa Sana ikiwepo kujenga shule mpya maeneo ambako shule zilikuwa mbali au zilikuwa chache,lakini pia kumekuwepo na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya elfu nane vilivyojengwa nchini kwote, hatua hii imesaidia wanafunzi wote wanaofaulu kwenda shule kwa wakati tofauti na zamani ambapo walikwenda muhula wa pili na kuwa nyuma kimasomo ukilinganisha na wenzao waliotangulia

Hapa pia mh Rais amafuta Ada mpaka kidato Cha sita na hivyo kusaidia watoto wote hata wanaotoka familia za kipato Cha chini kupata Elimu bila kikwazo chochote kile

Ukienda katika Afya nako mh Rais kafanya kazi kubwa Sana ikiwepo ujenzi wa zahanati kila Kijiji na vituo vingi tu vya Afya Kama ambavyo majuzi hapa vituo vya Afya takribani 234 vimejengwa nchini

Kila eneo utakapokwenda utakuta mh Rais kaweka mikono yake, na hapa Ni ndani ya muda mfupi Sana tangia alipoapishwa kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania
 
Ibada zenu zinaongozwa na njaa munazoendekeza. Kupinga au kutofautiana mitazamo, hoja katika maisha ndio uhalisia na sio kosa. Kama hujui ndio demokrasia ya kweli.
Ndicho kinachotakiwa tupingane kwa hoja na siyo matusi na kukashifiana
 
Amefanya nn kuhakikisha vijana wanajiajiri Kwa kupata mikopo ktk fedha zinazokuja Kutoka hazina kwenda halmashauri na majiji??

Pesa za mikopo Kwa vijana wanapewa UVCCM wagawane.

Ili kijana apate sharti ajiunge CCM,

Nchi hii Si yenu, ni ya Watanzania wote bila kujali vyama.
Katika suala la mikopo la halmashauri serikali imekuwa ikiweka msukumo kuhakikisha kuwa zile 10% kwa ajili ya vijana 4%, akina mama 4% na watu wenye ulemavu wanapata na pesa zinatolewa kwa vijana husika baada ya kukamilisha kwa taratibu zote ikiwepo kuandaa katiba, kufungua account, kuwa business plan ya kitu wanachohitaji kukifanya, na vitu vingine vidogo vidogo.

Ndio maana serikali pia imekuwa mbogo kwa watendaji wanaochezea pesa hizo kwa manufaa yao binafsi ikiwepo uundaji wa vikundi hewa ili wachote pesa kwa maslahi yao binafsi badala ya walengwa tajwa hapo juu,
 
Ndugu zangu Rais Samia hakika amefanikiwa kujenga umoja wa kitaifa, amefanikiwa kuliunganisha Taifa, amefanikiwa kuwaweka watanzania pamoja, amefanikiwa kuishi katika mioyo ya watanzania , Amefanikiwa kupanda mbegu ya Uzalendo katika mioyo ya watanzania

Sasa picha ya Rais Samia inashangiliwa uwanjani Tena katika mchezo mkubwa siyo tu Tanzania Bali katika Bara Zima la Afrika, picha ya Rais Samia inaleta furaha na Tabasamu kwa mashabiki uwanjani, picha ya Rais Samia inakuwa sehemu ya burudani na furaha ya mchezo, mashabiki wote wa timu zote wanafurahi kuona picha ya Rais Samia ikiwa inapepea uwanjani

Hii ni kutokana na kuwa kila mtu na kila shabiki wa mpira anamuona Rais Samia kuwa Ni Rais wake na kiongozi wake, Hakuna mwenye chuki na Rais Samia, Hakuna mwenye kinyongo na mama Samia, hakuna mwenye Hasira na mama Samia. Kila Shabiki akiona picha ya Rais Samia mbele ya uwanja anaona furaha na Tumaini, kila mtu anahisi Rais Samia Ni mshabiki wa timu yake na anajisikia fahari,

Hakika Rais Samia Ni kipenzi Cha watanzania, Ni Tumaini la watanzania, furaha ya watanzania ,kiongozi aliyeteka mioyo ya watanzania, kiongozi anayekubalika na watu wote vijana kwa wazee. Ukifanikiwa kupenya katika mioyo ya wanamichezo maana yake umefanikiwa kukaa katika mioyo ya watanzania maana mchezo wa mpira ndio mchezo unaopendwa na watu wengi Sana Tanzania na unao waunganisha watu bila kujari itikadi zao za kisiasa

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
This must be coming from Chawas.
 
Ukweli gani?. Kiongozi anatakiwa kuwa challenged ili afanye kazi.

Sasa kila siku mapambio ya kijinga ndo maana hata mfumuko es bei hawahangaiki nao wanajua kuna wajinga kama wewe wanasifia kila kitu
Suala la mfumuko wa Bei limekabiliwa kishupavu na mh Rais kwa kutoa mabillioni ya pesa za kitanzania ili kuukabili mfumuko wa Bei Kama tulivyoona utoaji wa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini katika mbolea na kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni

lakini pia hata katika Nishati ya mafuta ya petrol Dizel na mafuta ya Taa nako mabillioni ya Ruzuku yamekuwa yakitolewa kupunguza ukali wa mfumuko wa Bei mtaani
 
Mimi Ni mkulima mwenyewe kwa hiyo nasi wakulima tulikuwa tumechoka kupata hasara kila mwaka, Tunamshukuru Rais Samia kwa kuhakikisha kuwa wakulima tunapata soko la uhakika na kwa Bei nzuri na hivyo kutusaidia kuinuka kiuchumi. Kilimo Ni biashara, unakaribishwa kulima maana Tanzania tuna ardhi yenye rutuba na yakustawisha mazao mbalimbali maeneo mengi
Mkulima mda wote una type ushubwada, unalima sangapi?
 
Hapo umeamka zako saivi godoro ulilo lalia limebonyea katikati ukilala chaga zinagusa mbavu, dagaa wameisha na tu-unga tumebaki kidogoo kwenye kamfuko keusi.

Wapangaji wenzako wanakudai buku mbili ya umeme unawapiga chenga tu siku ya nne leo, endelea kulala usingizini kenge wewe
 
Mfumuko wa Bei mh Rais amekabiliana nao kwa ustadi mkubwa Sana , mfano katika Nishati ya mafuta mh Rais alikuwa anatoa Ruzuku ya billion Mia moja kila mwezi, Hatua hii ilisaidia Sana katika kumpa ahueni mwananchi mnyonge ambaye ndio mhanga kunapotokea mfumuko wa Bei, maana mfanyabiashara hupanga Bei kulingana na gharama alizotumia kuongoza mzigo nchini, pia Ikumbukwe kuwa siyo serikali ya CCM iliyopandishaa Bali Ni Bei katika soko la Dunia iliyotokana na Vita huko ukrein

Ukija katika kilimo nako unakuta juhudi na mikakati thabiti iliyofanywa na mh Rais kukabiliana na mfumuko wa Bei za pembejeo, Hapa mh Rais ametoa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini hatua iliyopelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni zaidi ya nusu, mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu wakulima tunapata mbolea hiyo kwa elfu 70 tu,

Ukija katika Elimu mh Rais amefanya kazi kubwa Sana ikiwepo kujenga shule mpya maeneo ambako shule zilikuwa mbali au zilikuwa chache,lakini pia kumekuwepo na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya elfu nane vilivyojengwa nchini kwote, hatua hii imesaidia wanafunzi wote wanaofaulu kwenda shule kwa wakati tofauti na zamani ambapo walikwenda muhula wa pili na kuwa nyuma kimasomo ukilinganisha na wenzao waliotangulia

Hapa pia mh Rais amafuta Ada mpaka kidato Cha sita na hivyo kusaidia watoto wote hata wanaotoka familia za kipato Cha chini kupata Elimu bila kikwazo chochote kile

Ukienda katika Afya nako mh Rais kafanya kazi kubwa Sana ikiwepo ujenzi wa zahanati kila Kijiji na vituo vingi tu vya Afya Kama ambavyo majuzi hapa vituo vya Afya takribani 234 vimejengwa nchini

Kila eneo utakapokwenda utakuta mh Rais kaweka mikono yake, na hapa Ni ndani ya muda mfupi Sana tangia alipoapishwa kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania

Hebu niambie hiyo ruzuku ya bilioni 100 kwenye mafuta kila mwezi ilimnufaisha vipi mwananchi wa hali ya chini maana hatukuona nauli za vyombo vya usafiri kupungua badala yake ama zilibaki pale pale au ziliendelea kupanda.

Hicho kilimo unachokisema sijui mbolea na vitu vingine, vimeleta ahueni ipi kwa Mtanzania kama bei za vyakula ziko juu na zinaendelea kupanda?

Ukija kwenye elimu kilichofanywa si kujenga shule bali ni kujenga majengo kujaza waliofeli, leo hii unakuta shule moja asilimia 70 ya wanafunzi wa kidato cha pili hawajui kusoma wala kuandika na bomu lingine linakuja la elimu ya msingi kuishia darasa la sita na hakuna mtihani wa kuwapima bali kwenda moja kwa moja kidato cha kwanza.

Tutegemee mengi zaidi ya ile slogan ya 'BIG RESULT NOW' ambayo matunda yake ndo yanaonekana kwa LST lakini makazini huku tulipo ndo tunaona vilaza wengi sana wa hiyo slogan.

Kwenye afya na kwenyewe ni kujenga majengo tu yakanakshiwa na rangi nzuri kilichomo ndani Mungu ndo anajua maana mkunga ndo Daktari, hiyo ndo utaita Kituo cha Afya?
 
Back
Top Bottom