Kutawala kwa picha ya Rais Samia uwanjani ni ishara ya mafanikio katika kujenga umoja wa kitaifa na kukubalika kwake

Kusema ukweli siyo uchawa, Wala kumpongeza mh Rais kwa kujenga umoja wa kitaifa haliwezi kuwa kosa la jinai
Nachozungumzia mimi ni wingi wa picha ambazo walizigawa wenyewe uwanjani na hoja iliyotolewa, sio kwamba namnanga Rais no asikubali watu wanaompa sifa za kijinga kijinga ambazo huwezi kuprove kitaalam kuwa ndio kigezo cha kukubalika.
 
Ila nikusifu maana hupanic, unajibu kistaarabu. Ingawa sipendi theme za mada zako.
Sina sababu za kupanic Wala kumtukana mtu hata akinutukana matusi ya aina yoyote Ile maana sote tuna Nia njema ya kuona Tanzania inakuwa Bora Zaid ya Leo na kwamba kila mtu anainuka kiuchumi, siyo tufe na njaa wakati tuna Mito kila mahali na maziwa ambayo tunaweza fanya kilimo Cha umwagiliaji tukapata chakula Cha kutosha na tukauza kingine na kupata fedha za kigeni zitakazo tusaidia katika manunuzi ya vitu vingine Kama vile baadhi ya madawa hospitalini

Hatutaki kuona wanafunzi wetu wakikaa chini wakati tuna Miti ya mbao maelfu kwa maelfu huko iringa tunayoweza kupasua mbao na kutengeneza madawati ya wanafunzi wetu na wakakaa vizuri wakati wanajifunza darasani

Hatutaki mtoto wa masikini akae nyumbani kwa kukosa Ada wakati tuna uwezo wa kufuta Ada ili kila mtoto apate haki na fursa ya Elimu

Ndio maana nampongeza mh Rais wetu mpendwa mama Samia kwa kuwa ameonyesha dhamira ya dhati katika kuona kila mtanzania ananufaika na fursa zinazopatikana katika nchi yetu, lakini pia serikali ya mama Samia inafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kuwa inagusa maisha ya mtanzania mnyonge anayehitaji kusaidiwa, maana kazi ya serikali Ni kusaidia watu na siyo kuumiza watu wake, hiki ndicho afanyacho mama Samia kuhakikisha anasaidia watanzania kuinuka kiuchumi
 
Nachozungumzia mimi ni wingi wa picha ambazo walizigawa wenyewe uwanjani na hoja iliyotolewa, sio kwamba namnanga Rais no asikubali watu wanaompa sifa za kijinga kijinga ambazo huwezi kuprove kitaalam kuwa ndio kigezo cha kukubalika.
Hakuna ubaya wowote ule kwa mtu kupongezwa afanyapo vyema, ndio maana ya uanzishwaji wa tuzo mbalimbali Duniani Kama sehemu ya kutoa motisha kwa watu
 
Umeandika ila inategemea upande uliopo kwenye shilingi, upande wa uongozi au kwa wananchi.

Umesema mafanikio mengi tunashukuru ungeweza kutuletea data zinazo onyesha positive move towards maendeleo unayozungumzia kama elimu (ubora wa elimu), fursa, njinsi serikali imegusa wanyonge n.k.
 
Yote Ni maisha tu yawe Ni ya dagaaa au samaki au mlenda au mihogo, lakini pia hata Kama mtu anadaiwa siyo dhambi maana ndio ukubwa wenyewe na utu uzima, Sasa Kama wewe unamcheka mtu ukiona anadaiwa Basi utakuwa hujaanza kuyaishi maisha halisi na hujapitia shida, pia usimcheke Wala kumdharau mtu kwa kuwa anapitia shida au matatizo ya kiuchumi hata Kama umepanga Naye jirani chumba

Ukiwa na nafasi na ukaona mtu anateseka au anahangaika msaidie kwa kadri ya uwezo wako japo huwezi kumsaidia kila mtu lakini unaweza ukasidia hata mmoja ambaye akafurahi katika moyo wake na kubaki anakuombea kila siku ili mwenyezi Mungu akubariki

Pia hata ukimsaidia mtu usisubiri fadhira kutoka kwake maana awezaye kukulipa wewe Ni Mwenyezi Mungu pekee, hivyo usimdharau mtu kwa kipato chake au Hali yake ya umaskini maana kupata Ni Majaliwa,Aliyekupa wewe ndio aliye mnyima Yule unayemdharau na hujuwi atampa lini

Naona umeniita kenge, Hata hivyo Naheshimu mtizamo wako na ninaendelea kuheshimu michango yako humu maana tunaweza kubishana kwa hoja bila kutukanana
 
Nakupa mfano mmoja unaonihusu Mimi mkulima, mwaka Jana mbolea ilikuwa Bei juu Sana mfano mbolea ya DAP iliuzwa kwa laki na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa elfu 70 tu baada ya utolewaji wa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini, Hapa mh Rais Amegusa maisha ya mtanzania mnyonge moja kwa moja kwa kuwa secta ya kilimo ndio mahali utakapokuta kundi kubwa la watanzania linategemea secta hii kuendesha maisha yao, hapa Ni Kama wakulima tulipewa pumzi Safi
 
Kubali tu kuwa mh Rais Samia anakubalika na kupendwa Sana na watanzania
 
Sasa ndio inavyotakiwa kutoa hoja zako safi sana, Angalia na vingine virkezee hivyo hivyo hoja inapata mashiko zaidi
 
 
Nasubili kuja kumpigia kura uchaguzi ujao na kumpigia kampeni mitaani nyumba kwa nyumba na mtaa kwa mtaa kwa miguu yangu

Hahitaji kura, anahitaji vyombo vya dola na tume isiyo huru ya uchaguzi kumtii basi. Akipata hayo anakuwa rais kwa kishindo hata kama hakuna mtu yoyote atajitokeza kupiga kura.
 
Nonsense.
 
Hahitaji kura, anahitaji vyombo vya dola na tume isiyo huru ya uchaguzi kumtii basi. Akipata hayo anakuwa rais kwa kishindo hata kama hakuna mtu yoyote atajitokeza kupiga kura.
Hata ije tume kutoka marekani kusimamia uchaguzi bado Rais Samia atashinda kwa kishindo maana anakubalika na kupendwa Sana na watanzania
 
Mimi bado nashangaa Kama wengine wanavyoshangaa.....kuwa ukiwa na picha ya Rais unashinda mechi yako.au kutoa draw. Nashauri Yanga waende nazo Tunisia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…