Kutoka kwenye familia tuliyosomeshwa kwa gharama kubwa kumeniathiri kiuchumi, Kupeleka watoto kayumba ni aibu, Napambana kukwepa aibu

Pole sana kaka kwa unayopitia kwa wakati huu na nikutoe hofu almost waajiriwa wengi wanapitia hapo na wapo ambao umewazidi maana umefikia hatua unatembelea IST yako mwenyewe.

Ushauri wangu kwako
1. Ni hatari sana kiuchumi kwako na familia kama unasomesha watoto private school kwa sababu tu wew ulipitishwa huko au unaogopa watakuonaje watu waliokuzunguka.

Uhatari huu utauona katika viashiria viwili
i. Unakopa ili kulipa ada
ii. Unaairisha moja ya mipango yako ili kulipa ada.

Nivema uweke tathimini za kiuchumi na kama upo kwenye moja ya kundi hapo juu nivema kufanya uamzi wa busara juu ya uchumi wako, binafsi sioni shida katika shule za Umma maana wengi tumesoma huko na ziko vizuri japo kuna changamoto ambazo ni za kawaida.

2. Nakushauri pia soma vitabu hivi viwili vitakusaidia sana katika ufumbuzi wa changamoto yako

i. Usichokijua kuhusu Malezi Kimeandikwa na mwanasaikolojia Mtanzania Deogratius Sukambi

Kitabu hiki katika sura yake ya pili (mtego wa upendo) kitakusaidia sana kuepuka kuingia katika mtego wa kudhania kuwa ukiwapelek huko private school ndio utakuwa umewapatia kilichobora
Sura yake ya Sita (Vifungo hisia) itakuwezesha kuepuk na hisia ulizonazo kuwa ulipopitishwa ndipo unabid na wew upitishe wengine

Lakini kwa ujumla wake kitabu kitakusaidia sana katika kujua wajibu upi n sahihi kwa mzazi kwa watoto wake na watoto pia kwa wazazi

ii. Millionare next door by Dr Thomas J Stanley & Dr William Danko

Kitabu hiki katika sura yake ya pili (Frugal Frugal Frugal) itakusaidia namna ya familia yako binafsi inaweza kuishi chini ya kipato chako ili kuweza kuwekeza amount ya pesa nyingi hatakama mna kipato kidogo au kikubwa

Katika sura yake ya tano (Economic Outpatient Care) itakusaidia kujua namna private school zinawafany wazazi wengi kuishia kuwa maskini lakini pia kuzarisha vizazi vinavyokuja kuwa katika truck hii ya private school mentality. (wakiamini ndio shule bora)

Hapo utaona ametolea mfano wa Ndoa ya Marry and Lamar walivyokuwa na hiyo mentality na wakawa masikini

Kitabu hiki kwa ujumla kina lenga tafiti zilizofanywa nchini malekani na hawa Doctrate wawili kujibu swalinla kwa nini watumishi wengi richa ya kulipwa pesa nyingi bado wanakufa masikini au wanakuwa dependent leaving in paycheck na wakistafu hawanauwezo wa kumudu maisha yao. Kisome chote nikitabu kizuri

Asante
Regards
M. Miguel
 
Ndio maana tunasema muende shule nzuri "pwenti"ndio Nini🤔?
Duh shule nzuri uliyo soma imeshindwa kukuongoza kuelewa kwamba "pwenti" ni neno lisilo rasmi linalo tumiwa na vijana wa kitanzania kumaanisha " point" ?

Mnalipa mamilioni ili kukariri sio? 😁😁😁
 
Duh shule nzuri uliyo soma imeshindwa kukuongoza kuelewa kwamba "pwenti" ni neno lisilo rasmi linalo tumiwa na vijana wa kitanzania kumaanisha " point" ?

Mnalipa mamilioni ili kukariri sio? 😁😁😁
Hamna Cha vijana Wala cha Nini wewe sema tu umeandika mbiombio hamfundishwi kuhariri maandiko yenu kabla hamjayapeleka public!hebu hamisha watoto Hizo shule wasije rithi hili tatizo🤔
 
Tuondolee maisha ya maigizo wewe
 
Hamna Cha vijana Wala cha Nini wewe sema tu umeandika mbiombio hamfundishwi kuhariri maandiko yenu kabla hamjayapeleka public!hebu hamisha watoto Hizo shule wasije rithi hili tatizo🤔
Duh inaonekana wewe mtoto wa geti kweli kweli yani hujawahi kabisa kusikia neno " pwenti" maisha yako yote?

Vipi na kuhusu neno " Piwa" kumaanisha " Pure"?

Anyways hayo ndo madhara ya kukariri darasa.

Umezidiwa maarifa mpaka na mababu zetu.

Wazungu walipo kuja Tz waliwaambia babu zetu kwamba nguo ya kuvaa juu inaitwa " Shirt" ( sheet!)

Babu zetu wakawaambia acheni ujinga nyinyi, mbona mwahangaika kutumia nguvu nyingi sana kuelezea simple term kama hiyo? Kwanini msiseme tu " Shati" mbwa nyinyi, ( sheet) ndio mboga gani tena?


Hawakusikia wazungu wakaja tena na neno ( Cupboard)

Babu zetu wakawaambia hivi nyie mna shida gani nyie mabwege?

Cupboard ndio nini tena?

Kwanini msiseme tu " Kabati"


Sasa wewe ndio wale waswahili walio kariri uzungu.

Narudia tena kwa mara nyingine " pwenti" inamaanisha " point" acha kukariri
 
English medium zina faida kwenye hilo hakuna ubishi

Ushawahi sikia binti wa english medium kapewa mimba na boda?

Pambania.
nishaona mzee tena nimesoma nae class moja advance akiwa analea Mtoto kwao.alinipa stories ilikuwa kivumbi kwao nusura mama yake na yeye wote wafukuzwe Nyumbani mana baba yake alimind vibaya sana
 
Hamna Cha vijana Wala cha Nini wewe sema tu umeandika mbiombio hamfundishwi kuhariri maandiko yenu kabla hamjayapeleka public!hebu hamisha watoto Hizo shule wasije rithi hili tatizo🤔
Duh
 
Dadeki noma sana.

Hivi watoto huwa wanawasaidia nini maishani?? Zaidi ya wengi kulalamika, sionagi watu wakisifia uwepo wao.
(Tafiti nimeifanyia jf na mtaani)
Ukishazeeka kimwili na kiakili ndio utajua mzee.
 
Kupeleka mtoto Private ni zaidi ya kufaulu kwenye mitihani, Hata vijijini kwenye shule wanazokaa chini wapo vipanga wanaofaulu zaidi.

Ni suala la kumrahishia maisha mtoto, kuhusu kufaulu hilo ni jambo lingine.

soma uzi mzima.
Nadhani hapa wazazi wengi tunalenga katika kuwaandaa vijana wetu kuwa raia wa dunia(global citizens) ili kutumia uwanda mpana wa dunia kujikwamua kiuchumi. Ni kazi ngumu mtoto aliyesoma shule za umma kuanzia chekechea hadi chuo kikuu kuweza ku interact na dunia kama mwenzake wa private school.


Jambo la kuzingatia ni uwezo wako wa kiuchumi maana haina faida kuingia kwenye madeni yaliyokuzidi kimo ili kumpeleka mtoto private school.
 
Hizi pepsi za sasa za take away zina ladha gani?? Mbona mbaya hivi..

Ni kweli mkuu pambana..
 
Huyo wa mwisho muanzishe government kuliko kumpeleka private kisha yakakushinda na kuamua kumpeleka government
.

Ni heri aanze huko huko.
 
Darasa moja wanafunzi 100.
Zaidi ya 100, kuna baadhi ya shule darasa moja utakuta wanafunzi mia nne ,dawati la kukaa wanafunzi watatu wanajibana wanakaa watano wengine wanakaa chini ndio maana wengi wao huwa ni wachafu sana
 
Uongo, mfano halisi ni mm mwenyew, mm nmesoma kayumba, lkn nilipitia meng kipind chote cha masom yang, nilihangaika sana kutafuta walim wa ziada kunipunguzia mzig wa syllibus wkt marafk zang wanaosoma shule za gharama walikua wanafundishw kila kitu darasani, yani wanapewa kila kitu ibaki wenyew kufanya revision t lkn kwa upande wang nilikua nahangaika sana kutafuta matuition na walim wa ziad na kila asbh natakiw niwah shule ilhali shulen walim hawafundish kama wanavopaswa kufundisha, nili ishia kupata div 3 form 4, lkn niliamn kMa ningelisomea shule za privTe bas nilikua na uwezo wa kufaul vizur zaid,
 
Hivyo vyote vinapatikana kayumba kasoro usafiri ambao hata kwa shule za English Medium za kibongo ni yaleyale. Ninafikiri wazazi wengi wanapeleka watoto English Medium kwa sababu ya peer pressure.
100% Fact
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…