Kutokana na hii story yangu hauwezi nikuta humu nashabikia kutoa watoto EMs na ISs na kuwapeleka kayumba

Kutokana na hii story yangu hauwezi nikuta humu nashabikia kutoa watoto EMs na ISs na kuwapeleka kayumba

Na hii ligi wameingia Chaka vibaya mno, walianza na single mothers, wanasema hawafai kumbe hawajui hata mama zao waliolewa wakiwa single mothers, wakaenda kwa kataa ndoa wakakuta dada zao wanapigwa miti na washikaji zao, Leo wameingilia mambo ya taaluma kisa hawana pesa.
Hahaahh

Hatariiiio
 
Kila mzazi apeleke mtoto anapoona panafaa kulingana na kipato chake!!!! Binafsi wa kwangu nitaangalia sehemu ambayo watasoma huku nikiwaandalia future yao....
Usome kayumba, Ems , International
Inatakiwa upate elimu ambayo ukiileta mtaani ikupe matokeo chanya. Elimu utajayopata popote inatakiwa ui apply kazini, kwenye biashara, kilimo, na hata hapo ulipo kwa maana ya familia, Elimu hiyo itupe utofauti wenye tija.
Hakika
 
Mtoto wa EM hana chochote za ziada anachomzidi mtoto wa Kayumba ukiangalia kwa jicho la 3, hana. Mimi sio muumini wa matokeo ya As ama Bs ambazo zinapatikana EM kwa kuiba mitihani na mambo kama hayo. Mimi ni muumini wa analytics, watoto hawa wa EM zaidi ya matokeo hana kingine anachomzidi wa Kayumba.
 
Binafsi sijaelewa hii kampeni ni ya nini na ni kwa maslahi ya nani.

Je inaendeshwa na victims (watoto waliosomeshwa EMs wakalost kwenye maisha) au inaendeshwa na wazazi (wenye kupenda watu wafanane/wafuate mitazamo yao)
Inashangaza sana...mi naona kilamtu ajikune pale mkono unafikia
 
Bottom line is, usifanye chochote kilicho nje ya uwezo wako.

Ikiwa una uwezo wa kulipa private school, ni busara kumpeleka mtoto huko. Hakuna faraja kwenye ufukara. Kuna tofauti kubwa sana ya uelewa baina ya mtoto wa darasa la watoto 20 (private school) na watoto 120 (Kayumba).

Mimi nashukuru Mungu ni product ya English Medium (Olympio ya 90's, St. Mary's ya late 90's, Early 2000's na mwisho Uganda).

Ukiwa na chimbuko zuri la Primary, secondary unatoboa shule yeyote. Hili nililiona baada ya kuhamishwa toka St. Mary's na kupelekwa Uganda. Ilikuwa nikiliganisha baina yangu na wenzangu wa Tz waliotoka shule za kawaida, nilikuwa na advantage kubwa ya kuelewa ikizingatiwa mtaala wa Uganda ni wa kiingereza toka chekechea.

Mtoto wangu wa kwanza yupo Secondary (Form 2) toka nursery amesoma English medium na sekondari nimempeleka shule ya Serikali, so far hakuna gumu lolote analopitia kwa swala zima la uelewa.

Kiuhalisia kinachoangusha elimu ya Tz hasa primary ni lugha. Ni ngumu kwa mtoto kufundishwa kwa kiswahili toka chekechea halafu ghafla form 1 unabadili kila kitu kwenda kwa Kiingereza. Hatma ya huyo mtoto ni kukariri definitions kuliko kuelewa hasa kinachofundishwa. Na hii huendelea mpaka kwenye ajira.

Ni kawaida kukutana na mtu mwenye masters lakini uwezo wake wa kujielezea ni mdogo mno japo anajua kile anachopaswa kukielezea.

Ifike wakati serikali iende na wakati na kubadili mfumo wa lugha ya kufundishia na kuwa Kiingereza toka mwanzo. Na wale wanaojimithilisha na China kusema kuwa Kiingereza hakina umuhimu basi pia wamithilishe na uchumi wao.

For as long as sisi ni nchi maskini, kiingereza hakiepukiki katika kutafuta fursa za kidunia.

Watu wanahamasishana upumbavu, nafikiri wenye uelewa mdogo ndo watafuata ushauri wa kipumbavu
 
Naona wamiliki wa shule za EM's baada ya kuona mnaharibiwa soko la biashara zenu mmeamua kujibu mapigo
Wamiliki wa shule si maadui, wanatoa huduma, Wanalipa kodi na wanatoa ajira.

Tatizo nini? Serikali haiwezi kuhudumia mahitaji ya kielimu bila wadau kutoka sekta binafsi.

Yall taking everything personal!
 
Yani Dunia inakuelemea ukiwa katikati ya wanaojua Kingereza 😅😅😅sa hiyo huna wa kumlaumu. Uko peke yako, hujiwezi. Hadi Tell us about yourself inakutoa Jasho 😜😜😜😜😅😅
Hapo ndiyo shida inapoanzia. Timedaganywa kwamba kujua kingereza ni kuwa na Akili nenda China utashangaa waafrica bado tu watumwa wanl wazungu 100%
 
Kila mzazi apeleke mtoto anapoona panafaa kulingana na kipato chake!!!! Binafsi wa kwangu nitaangalia sehemu ambayo watasoma huku nikiwaandalia future yao....
Usome kayumba, Ems , International
Inatakiwa upate elimu ambayo ukiileta mtaani ikupe matokeo chanya. Elimu utajayopata popote inatakiwa ui apply kazini, kwenye biashara, kilimo, na hata hapo ulipo kwa maana ya familia, Elimu hiyo itupe utofauti wenye tija.
unao wangapi?
 
Make Kayumba schools great again.

Usijitese kusomesha watoto huko EMs, walete shule za jamii wapate Elimu bora huku ukiishi bila stress.

Binafsi nimesoma Taasisi za Serikali mwanzo mwisho, hata nilipokutana na hao waliosoma EMs hakuna walichonizidi zaidi ya kiingereza cha hapa na pale ila darasani hakuna walichonizidi.

LIKUD
Sahihi kabisa mkuu. Halafu mtoa Mada hajui hata Nini maana ya private school.

What is private about EMS kama hawatumii mtaala wao wenyewe wana tumia mtaala wa NECTA?

Unaposema wewe ni private school maana Yake hata mtaala wako pia unapaswa kuwa private.

Sio unasema wewe ni private halafu mtaala unatumia wa public

The only private thing about shule za EMs za kibongo ni majengo Yao lakini everything about them is public

Hata English yenyewe hazifundishi isipokuwa kinacho fanyika ni just mentioning. Yani masomo kwenye shule za EMs yanakuwa mentioned in English na Sio kufundishwa in English.

Mtu ambae Sio mzungumzaji WA lugha ya kiingereza Kwa kuzaliwa hana uwezo WA kufundisha somo lolote lile Kwa lugha ya kiingereza but he can mention it in English.


Kama Kweli mzazi upo serious na hiyo unayoita elimu Kwa kiwango hicho Basi shule zinazo fundisha Kwa mtaala wa Cambridge ambazo ada zake ni walau kuanzia milioni 25 Kwa mwaka.


Lakini hizi za kumilikiwa na wakina Muggetta za kulipa milioni 2, 3 au 4 Kwa mwaka ni upuuzi mtupu
 
Back
Top Bottom