Kuvaa Hijab ni dini au udhaifu wa wanaume?

Kuvaa Hijab ni dini au udhaifu wa wanaume?

Mafundisho ya baadhi ya Dini yamepitwa na wakati.
Shida iko hivii, kama ukimkosea baba utaadhibiwa na baba mwenyewe, kama ukiikosea serikali utaadhibiwa na serikali, lakini kama ukimkosea Mungu kuna watu wamejipa kazi ya kuadhibu kwa niaba ya Mungu, hii haiwezekani iwe hivyo, maana kazi ya kumjua na kumhukumu mkosefu mbele ya mungu anayo Mungu mwenyewe, hajaikasimu kwa mtu wa aina yoyote. Aliyemuua aliyevaa vibaya hijab alifanya hivyo kwa niaba ya nani? je, Mungu anashindwa kumuadhibu yeye mwenyewe?
 
Ulichoandika hakina maana ni uchafu mtupu!! Haya usivae nguo uone ,Hayo mambo ni katika kuslow down mahaswi kutokana na Tamaa za kibadamu kinaweza kuchochea uzinifu .

Hakuna mahali umelazimishwa ila kama unataka kuifuata uislamu basi tii Sheria hyo kwa mwanamke kwa nn unapenda kufuatilia vitu havikuhusu ,nenda kaangalie masisters wanavaaje kanisani kama hujui hekima ya wao kuvaa ile hijabu ni ishu za kujistiri angalia na mapadre ulishawai kuona wapo padre kavaa kipensi, nenda hata ofisini uvae kipensi uone .
Hawaja lazimishwa kua ma Padre au ma sister. Ni utashi wao nahata leo wakiamua kuvaa vipens na vimini hawata uwawa Ila kanisa lita wafukuza kwa kutoendana na Sheria za kinisa sio kuwauwa
 
Huyo Mokiti Kazi yake kubwa humu ni kupotosha hata umuelimishe vipi na utamkuta karibia kila uzi unaohusu uislamu ,haelimiki yeye anaganda kwenye analolitaka ndio maana watu wengi humu tunampuuza comments zake tunazipita kama hatuzioni na tunamquote pale kwenye ulazima tu ili kubainisha upofu wake akiwa mbishi anataka ligi tunamfungia vioo tu.
Naweka nukuu halisi, na weka ushahidi wazi kabisa , ndio maana wengi mnaniogopa Sana mnataka watu wasio jua chochote kuhusu Uislamu mumuingize Chaka

Kama hapa umeona wazi nimeweka maandiko yenu yanasema Umar ndio muanzilishi wa hijab , mnatakiwa kupinga maandiko yenu sio kupambana na niliyeyatumia Kuweka ushahidi
 
Kuvaa hijabu ni amri ya Mwenyezi Mungu kwa wanawake wote wa Kiislamu. Na hii inawasidia wenyewe wasiudhiwe hasa kutokana na maungo yao kuwa ya kuvutia kwa hivyo wakijisitiri hawapati usumbufu.
Haya mavazi ndio hayo hayo aliyoyavaa Mama yake Issa/Yesu (Yaani Mariamu) na ndivyo wanavyo vyaa masista wa katoliki.

QURAN 33: 59
" Ewe Nabii! Waambie wake zako, na binti zako, na wanawake waumini wajiteremshie nguo zao. Hivyo kutafanya watambulikane (kuwa ni wenye kujiheshimu) wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu."
Huyo Mungu Kama anapenda sana wanawake wajistir angefanya namba wazaliwe na hijabu kabisa
 
Binadamu wote wake kwa waume wanazaliwa wakiwa uchi kabisa, kuvaa nguo ipi na ivaliwe wapi na nani kwa sababu gani ni utashi tu wa wanajamii wenyewe. Bahati mbaya au nzuri Mwenyezi kuna maeneo na viungo vya mwili ambavyo alishavifunika yeye mwenyewe kwa sababu zake kwa kutumia nywele ndefu na nywele fupi kutokana na umuhimu wake na sababu zake. Mfano, Mungu amekifunika kichwa cha kila mtu kwa nywele ndefu bila kujali jinsia yake, kabila wala dini yake, Mungu akakifunika kinena cha kila mtu aliyebalehe kwa nywele ndefu tunazoziita mav*zi. Hakuishia hapo akakifunika kidevu na kifua cha mwanaume kwa nywele ndefu pia kwa sababu zake mungu mwenyewe. Hakuishia hapo akaifunika ngozi ya mwili ya watu wote kwa nywele fupi tunazoziita malaika kwa sababu zake pia, akatupa pia nyusi, kope na nyweli puani bila ya kumuomba. Hivyo kila nywele ilikuwa na sababu yake na ilitosha kabisa kuifanya kazi iliyokusudiwa kufunikwa na kukingwa. Hii ni kuonyesha kuwa Mungu anayajuwa mahitaji yetu yooote.

Ni nani ambae hataki kumuona mwanamke ambae asiyefunika nywele zake? Je, ni mwanamke mwenyewe kwa sababu zipi? Je, ni mwanaume kwa sababu zipi na je, ni Mungu aliyetufanya tuzaliwa uchi lakini akatufunika kwa nywele kwa sababu zipi?

Utafiti wangu kwenye hili ni kwamba, sio Mungu anaetaka wanawake wavae Hijab bali ni wanaume tu kwa sababu ya wivu na kujifanya kuwa wao ni dhaifu kwa kutazama tu nywele, matiti, mapaja na vitovu vya wanawake wakasahau kuwa Mungu angetaka asingeshindwa kuwafanya wanawake wazaliwe wakiwa na hijab tayari. Tuache ujinga wa kuwadhulumu wanawake kwa kujificha kwenye kichaka cha dini. Nini sio Hijab wala nywele za mtu.

Ona haya mauaji na maandamano ya kijinga kabisa, eti msichana hakuvaa hijab.


Nawaza moyoni kama mtoa mada alivoyosema. au naongeza umuhimu wa mwanamke kuvaa nguo za heshima, lakini kuvaa hijabu mpaka kufunika miguu na uso, naona kama ni uonezi mkuu sana kwa wanawake.
Kwa upande wangu nafikiri mwanzilishi wa dini inawezekana kuwa alichangia kwa kuwa yeye pia alikuwa na bidii sana katika uhusiano na wanawake (alioa wanawake 9 na vile vile alikuwa na masuria kibao). Msifikiri na kashifu kiongozi wa dini hii, la hasha, bali naeleza ukweli aliokuwa nao, nafikiri Ili kupunguza hilo (kwa mawazo yake) ni kuwafanya wanawake wajifunike mwilini mzima, ili wanaume wasitamani wanawake (sijui na yeye pia?) Kumbe tatizo sio tu wanawake kujifunika bali moyo ukiharibika hauna dawa mpaka Mungu pale anavyoweza kuingilia kati. Nchi zenye sheria kali kuhusu ngono zinapunguza tabia hii kwa namna fulani, lakini nadhani sio hijabu iliyopunguza, kilichopunguza ni sheria kali. Kama si hivyo walegeze sheria lakini waruhusu hijabu kama tabia ya uasherati haitapanda. Ubaya wake sheria hizi kali zimelenga upande mmoja tu wa wanawake wala sio wanaume.
Kwa kutojua mtu anafanya biashara ya nguo anajifunika uso, mara nyingine najiuliza huyu amekuja kufanya biashara ya nguo, karanga au? Biashara inaendana na uchangamfu wa mtu, uso wake unapooneka. Lakini wengine kwa ujinga wao kuelewa Qur'ani ni kujifunika uso ndio kunampeleka mbinguni.
Dini kwa sehemu kubwa inawakandamiza sana wanawake, ingawa wanawake hawajui hilo. Kwa dini ya Kiislamu hakuna mbingu ya wanawake, ni ya wanaume tu, ambao watakuwa na mabikira huko. Jamani usipande jazba nimetoa yale niliyosoma na kufikiri kama mtu mwenye akili za mtazamo wangu, wala usifikiri mimi wa dini fulani inayopinga Uislamu. Naandika juu ya uonezi wa wanawake kidini.
 
Naweka nukuu halisi, na weka ushahidi wazi kabisa , ndio maana wengi mnaniogopa Sana mnataka watu wasio jua chochote kuhusu Uislamu mumuingize Chaka

Kama hapa umeona wazi nimeweka maandiko yenu yanasema Umar ndio muanzilishi wa hijab , mnatakiwa kupinga maandiko yenu sio kupambana na niliyeyatumia Kuweka ushahidi
Kuna levo ya ujinga na ubishi mtu akifikia basi hastahili kujibiwa ndio na hii ndio kawaida yangu.
81rm4i7UXRL._AC_SX425_(2).jpg
 
Umesoma vizuri maandiko lakini au unataka tu kubishana
Embu wewe na adriz mjibu kwa weledi kwa Hadith hii mnatujuza nani ndie alianzisha wazo la hijab

Kumbuka hili sio andiko langu, nimeweka mpaka nikipo litoa kwenye vitabu vyenu

Umar said:.... , both righteous and evil doers enter your wives, so why don't you tell them to observe the hijab? Then the verse of hijab was revealed. ...... and it was revealed like that. Musnad Ahmad 157
 
According to hadith za kiislam...Umar (Rafiki ake mtume/Swahaba)ndio alitaka wanawake wafunike uso.
Alimfata Muhamad na kumsihi apitishe sheria hii ila muhamad akawa kama haitaki vile.

Umar siku moja akaenda mahali wanakojisaidia wanawake (Enzi hizo hamna vyoo, kulikuwa kuna maeneo tu huko jangwani ya kwenda kujisaidia)
Akapambana mpaka amuone mke wake Mtume akijisaidia...Alipomuona akamuambia "Wewe Aisha nimekujua"

Akaenda kumsimulia hilo tukio Mtume na kumwambia kuwa angejifunika uso, Umar asingemtambua.

Basi Ewala...Mungu fundi, Usiku huo huo Malaika Jibril akashuka na Aya za kuwalazimisha wanawake wafiche sura zao.
Allahu Akbar.
Wewe ulimuna huyo jibril unaweza ukaleta selfie uliyo pigs nae
 
Nakuweka maandiko yenu , wewe unasema ni ujinga 😂😂
Kuweka maandiko sio shida mtu anaweza kutumia Qu'ran kusema jambo halali ni haramu na haramu ni halali kwa uchache wa uelewa ,ujinga na upumbavu wake .Hata Kiswahili naweza kusema wale wote wanawake halafu ni wanaume watu wakanielewa vibaya lakini wanawake mimi nimemaaanisha kuwa wametoa yaani wanawake kama ilivyo kusema wanawatoto .

Kosa la kwanza unatafsiri maandiko kwa utashi wako na namna unayoitaka sasa ingekuwa hivyo waarabu wasingejifunza elimu ya 'Qu'ran exegesis' kwa vile ipo katika lugha yao na wanaelewa moja kwa Moja .

Leo unaleta hadithi wakati kuna siku nilionyesha Qu'ran imemtaja Nabii Yaquub (Upon him be peace) kama Israel wewe unataka nionyeshe kivipi umebadilika kutoka Yakubu mpk Israeli kwa kutumia Qu'ran na nikakuuliza chanzo ni Qu'ran pekee Ktk Uislamu ?leo hii ww unaleta hadithi sasa kama sio mjinga ni mtu gani?
 
Kuweka maandiko sio shida mtu anaweza kutumia Qu'ran kusema jambo halali ni haramu na haramu ni halali kwa uchache wa uelewa ,ujinga na upumbavu wake .Hata Kiswahili naweza kusema wale wote wanawake halafu ni wanaume watu wakanielewa vibaya lakini wanawake mimi nimemaaanisha kuwa wametoa yaani wanawake kama ilivyo kusema wanawatoto .

Kosa la kwanza unatafsiri maandiko kwa utashi wako na namna unayoitaka sasa ingekuwa hivyo waarabu wasingejifunza elimu ya 'Qu'ran exegesis' kwa vile ipo katika lugha yao na wanaelewa moja kwa Moja .

Leo unaleta hadithi wakati kuna siku nilionyesha Qu'ran imemtaja Nabii Yaquub (Upon him be peace) kama Israel wewe unataka nionyeshe kivipi umebadilika kutoka Yakubu mpk Israeli kwa kutumia Qu'ran na nikakuuliza chanzo ni Qu'ran pekee Ktk Uislamu ?leo hii ww unaleta hadithi sasa kama sio mjinga ni mtu gani?
Baada ya kushindwa Kuweka ushahidi wako kwa Koran nilikutaka uweke kwa chanzo chako ukatoka nduki kama kawaida yenu

Natambua Kuna Hadith na Kuna Tafsir kwenye kusoma Koran maana Koran kama yenyewe haieleweki na haijitoshelezi ukiitegemea verse nyingi utatoka kapa hutaelewa

Ila leo tupo na maelezo yenu mnasema hijab ni wazo la Umar , una Cha kuongea.

Umar said:.... , both righteous and evil doers enter your wives, so why don't you tell them to observe the hijab? Then the verse of hijab was revealed. ...... and it was revealed like that. Musnad Ahmad 157
 
Baada ya kushindwa Kuweka ushahidi wako kwa Koran nilikutaka uweke kwa chanzo chako ukatoka nduki kama kawaida yenu

Natambua Kuna Hadith na Kuna Tafsir kwenye kusoma Koran maana Koran kama yenyewe haieleweki na haijitoshelezi ukiitegemea verse nyingi utatoka kapa hutaelewa

Ila leo tupo na maelezo yenu mnasema hijab ni wazo la Umar , una Cha kuongea.

Umar said:.... , both righteous and evil doers enter your wives, so why don't you tell them to observe the hijab? Then the verse of hijab was revealed. ...... and it was revealed like that. Musnad Ahmad 157
Kwanza aya inajieleza cha pili Weka screenshot uliyosema niweke hadithi kama unasema kweli ?
 
Kwanza aya inajieleza cha pili Weka screenshot uliyosema niweke hadithi kama unasema kweli ?
Koran haijitoshelezi ndio maana Kuna vyanzo nje ya Koran , Hadith na Tafsir za ma skola , Rudi kasome utakuta nimekwambia weka chanzo chako ukakimbia

Ila leo tupo na maelezo yenu mnasema hijab ni wazo la Umar , una Cha kuongea.

Umar said:.... , both righteous and evil doers enter your wives, so why don't you tell them to observe the hijab? Then the verse of hijab was revealed. ...... and it was revealed like that. Musnad Ahmad 157
 
Nawaza moyoni kama mtoa mada alivoyosema. au naongeza umuhimu wa mwanamke kuvaa nguo za heshima, lakini kuvaa hijabu mpaka kufunika miguu na uso, naona kama ni uonezi mkuu sana kwa wanawake.
Kwa upande wangu nafikiri mwanzilishi wa dini inawezekana kuwa alichangia kwa kuwa yeye pia alikuwa na bidii sana katika uhusiano na wanawake (alioa wanawake 9 na vile vile alikuwa na masuria kibao). Msifikiri na kashifu kiongozi wa dini hii, la hasha, bali naeleza ukweli aliokuwa nao, nafikiri Ili kupunguza hilo (kwa mawazo yake) ni kuwafanya wanawake wajifunike mwilini mzima, ili wanaume wasitamani wanawake (sijui na yeye pia?) Kumbe tatizo sio tu wanawake kujifunika bali moyo ukiharibika hauna dawa mpaka Mungu pale anavyoweza kuingilia kati. Nchi zenye sheria kali kuhusu ngono zinapunguza tabia hii kwa namna fulani, lakini nadhani sio hijabu iliyopunguza, kilichopunguza ni sheria kali. Kama si hivyo walegeze sheria lakini waruhusu hijabu kama tabia ya uasherati haitapanda. Ubaya wake sheria hizi kali zimelenga upande mmoja tu wa wanawake wala sio wanaume.
Kwa kutojua mtu anafanya biashara ya nguo anajifunika uso, mara nyingine najiuliza huyu amekuja kufanya biashara ya nguo, karanga au? Biashara inaendana na uchangamfu wa mtu, uso wake unapooneka. Lakini wengine kwa ujinga wao kuelewa Qur'ani ni kujifunika uso ndio kunampeleka mbinguni.
Dini kwa sehemu kubwa inawakandamiza sana wanawake, ingawa wanawake hawajui hilo. Kwa dini ya Kiislamu hakuna mbingu ya wanawake, ni ya wanaume tu, ambao watakuwa na mabikira huko. Jamani usipande jazba nimetoa yale niliyosoma na kufikiri kama mtu mwenye akili za mtazamo wangu, wala usifikiri mimi wa dini fulani inayopinga Uislamu. Naandika juu ya uonezi wa wanawake kidini.
Tuliweke sawa hili pia. Ngono sio tabia mbaya, ni mpango mahasusi wa Mungu kwa viumbe vyake vyote, alikasimu kazi ya kutengeneza watu kwa wanawake na wanaume. Bahati nzuri ni kwamba Mungu alitengeneza wanaume wachache na wanawake wengi kwa idadi, lakini mungu akaliweka sawa hili la uwiano kati ya wanawake na wanaume kwa kuwapa wanaume uwezo mkubwa wa kuzaa na wanawake wengi kwa wakati mmoja kwa kupewa mbegu (manii) nyingi za kiume kuliko wanawake, hii ni kila mwanamke asikose mbegu pamoja na wingi wao kuliko wanaume. Agizo hili la kila mwanaume awe na wanawake zaidi ya mmoja ni kwa viumbe vyote, hata jogoo, beberu, nk wanatii agizo hili.
 
Imani isikupofushe,kinamzuia nini kuvaa hijab huyo kahaba?kama ndani ya hiyo hijab anabeba bomu atashindwaje kuvaa hijab?hijabu ina tofauti gani na dera?
Hujielewi pita kushoto, naongelea context ambazo hijabu inatumika ni kama vazi la heshima ,haya mavazi mengi status tumeyapa wenyewe tu binadamu wa watu wa jamii fulani ,usikariri ndo maana nikauliza nawe unaropoko ni kwamba context za kufanya ukahaba huwezi kuvaa hijabu wakati unatangaza biashara ya uchi
 
Hizi dini ya kulazimishana vaa kile, usile hiki zimepitwa na wakati.

Kwanini musiwaache watu wahukumiwe na Mungu waliomkosea ?
 
Embu wewe na adriz mjibu kwa weledi kwa Hadith hii mnatujuza nani ndie alianzisha wazo la hijab

Kumbuka hili sio andiko langu, nimeweka mpaka nikipo litoa kwenye vitabu vyenu

Umar said:.... , both righteous and evil doers enter your wives, so why don't you tell them to observe the hijab? Then the verse of hijab was revealed. ...... and it was revealed like that. Musnad Ahmad 157
Wew elewa ulivo elewa inatosha tusibishane bila sababu
 
Marekani anazidi kuwachokonoa waislamu , huku anampelekea Moto Putin , Irani naye yupo under hot soups, 😁😁😁 badae atamfinish North Korea kiulaiiiiiiiiiiiiini
Sasa wewe jamaa!!!

Hapo Iran askari wao tena kitengo husika kilichowekwa special kwa ajili ya kusimamia sheria za dini kimekamata mtuhumiwa aliyevunja taratibu za dini,wakamsulubu wenyewe wakitumia sheria ya dini kwenye kituo chao kilichopo kisheria mpaka kumtoa damu masikioni mwisho roho ikamtoka lakini wewe unakuja hapa kusema ni Merikan imefanya hayo una akili sawasawa kweli?

Kwanini baadhi yetu Waafrika tunazidi kuganda akili zetu?kama hapa jambo lipo wazi kabisa ila kwa ulemavu wa akili alio nao Mwafrica anapindisha ukweli,kwa manufaa gani?
 
Huyo Mokiti Kazi yake kubwa humu ni kupotosha hata umuelimishe vipi na utamkuta karibia kila uzi unaohusu uislamu ,haelimiki yeye anaganda kwenye analolitaka ndio maana watu wengi humu tunampuuza comments zake tunazipita kama hatuzioni na tunamquote pale kwenye ulazima tu ili kubainisha upofu wake akiwa mbishi anataka ligi tunamfungia vioo tu.
Kumfungia vioo tu
 
Pole sana uislamu upo tofauti na iyo dini yako ..Kwenye uislamu hakuna mbora bali yule amchaye mwenyezi mungu wapo watu apa tanzania wana elimu kubwa ya dini kuliko wale waliozaliwa makah au madina..uislamu hauna mmiliki kwenye hii dunia isipokuwa mwenyezi mungu pekee na waislamu wote wanafuata sheria na mafunzo ya mtume muhamad s.a.w .. nije kwenye mada walichofanya askari wa doria apo Iran ni dhambi na siku ya mwisho watawajibika kwa kitendo walichokifanya uislanu una hukumu zake na sheria zake ... mimi ni muislamu lakini walichokifanya wale askari ni kinyume na mafundisho ya Qurani na sunah.
Uislam haina mmiliki? Mbona Quran imeandikwa kwa lugha ya kiarabu?
 
Back
Top Bottom