Kuwaita wafadhili wetu “mabeberu”, kabla hatujaweza kujitegemea, ni ushamba unaoweza kuliangamiza Taifa tusipokuwa makini!

Kuwaita wafadhili wetu “mabeberu”, kabla hatujaweza kujitegemea, ni ushamba unaoweza kuliangamiza Taifa tusipokuwa makini!

Ndiyo. Mzee Nyerere aliwaita mabeberu wakaiangusha bei ya zao la mkonge halina bei hadi leo. Alipokuja Mzee Mwinyi akabadilisha jina wakawa wahisani au wafadhali, Mzee Mkapa akawaita wawekezaji. Mzee Kikwete akawaita wadau wa maendeleo sasa awamu hii tunaanza kurudi kule kule kwa Nyerere ambaye walimtaiti mpaka akaukimbia urais
Ahahaha
 
Kuna jamaa alidai tutakimbilia kwa wazalendo wenzetu WaChina tuliowanyima bandari ya Bagamoyo kwani wao wana mapesa mengi mpaka ya kuwakopesha waMarekani. Sijui alikuwa nani yule utopolo?
 
Yeah....hata jina lenyewe mie naona linatutukanisha tu........kama 'wao' ni mabeberu (mbuzi dume), ina maana 'sisi' ni "mbuzi jike"? Haaaaa......
 
Baada ya kichapo cha mbwa mtu kwenye box la kura naona unaibuka na nyuzi za kitoto. Unajua nini maana ya Beberu? Unadhani kila mfadhili ni Beberu. Unafahamu dhana nzima ya Imperialism? Tumia akili zako unapofanya ukosoaji wa kiuchambuzi.
Ule nao unauita uchaguzi?
 
Wewe endelea kuota tu, eti maendeleo yatakuja na ufadhili. Tumefadhiliwa tangu tulipopata uhuru, lakini 2015 hapajakuwa na meandeleo yoyote. Nchi zilizokuwa nyuma ka,ma Korea Kusini, malaysia, Vietnam, etc zote zimeendelea kwa kutumia pesa za ndani tu. Wewe bado unatamani na kung'ang'ania kufadhili. Wewe ni sawea na baba wa familia anayeshindwa kulisha familia yake akitegemea misaada na kuhemea kutoka kwa ndugu na marafiki. ebu angalia kutegemea kwetu mapato ya ndani kumetufikisha wapi katika miaka mitano (UCHUMI WA KATI).Mtu mwenye aklili na kutaka kuendelea ataendelea tu kwa kutotegemea misaada peke yake. Kwanza hata hiyo misaada huwa ina masharti ya kuturudisha nyuma wakatyi mwingine. Jitegemee kwanza, mikopo iwe ni pla two.

hivi wewe ukitaka kuanzisha biashara (kujiendeleza) utategemea misaada tu. Kabla hata ya kupata mkopo inabidi waangalie uwezo wako wa kuwalipa, na una nini cha kuchukuwa ukishindwa kulipa.
Tatizo ccm mumejusahau na kulifanya Taifa la Tanzania kama kichwa cha mwendawazimu. Kila mwenyekiti wenu mpya anakuja kujifunzia kunyoa hapo toka uhuru. Sijui kama hata wewe mwenyewe unaelewa ulichokiandika.

Wapi nimesema maendeleo yatakuja kwa ufadhili? Toka uhuru hadi kufikia 2015 ndiyo mumefahamu?
 
Hata wanaotoa kauli hizo, wanajua wanazitoa kisiasa.

Njia rahisi ya kumtawala Muafrika ni kumtengenezea adui wa pamoja, yani hawa wakoloni weusi wa leo kina Magufuli wanaotutawala kwa kuiba kura wakishindwa kutatua matatizo ya wananchi, kimbilio lao ni kuzusha vita dhidi ya "mabeberu".

Hapo wanawachota wananchi.

Na utakuta watu masikini kabisa wanaokandamizwa na hii serikali, na wao wanaitetea, kwa sababu tu wamelishwa ujinga wa "kupigana dhidi ya mabeberu".

Kusema ukweli ubeberu kwa kiasi fulani upo. Dunia ina geopolitics, ina espionage, ina national interests. Kwa hiyo, dhana ya "mabeberu" si kweli kwamba ni ya uongo kabisa.

Ila, wanasiasa wanajua kuitumia kwa manufaa yao, si kwa manufaa ya taifa.

Wanajua kuutumia ukweli fulani mdogo (a kernel of truth) na kuukuza vibaya kwa manufaa yao ya kisiasa.

Maanay yake nini?

Chukulia Wamarekani kwa mfano. Nchi yenyewe imegawanyika. Kuna Democrats na Republicans.Kuna Conservatives na Liberals. Kuna watu wa mijini na wa vijijini. Hawa si wamoja, wenyewe wanapingana.

Kwa kuangalia "popular vote", mshindi, Joe Biden, mpaka sasa, hajafikisha hata 51% ya kura zote. Yuko kwenye 50.8%. Wakati Trump yuko 47.3%.

Katika serikali ya Trump, kuna watu wamejiuzulu kazi serikalini kwa kupingana na muelekeo wa serikali ya Trump.

Rais George W. Bush, a conservative and Republican, ndiye rais aliyeisaidia Africa kuliko marais wote, kuliko hata Obama. Hususan kwenye mambo ya kupigana na magonjwa kama Malaria na AIDS.

Sasa watu hawa very complex. Tuukiwashutumu, basi na shutuma zetu ziwe complex.

Siyo mtu unaiba kura, Wamarekani wakikusema umeiba kura, unajitetea kwa kuwaita mabeberu.

Wakati hata wananchi wako wengi tu wanalalamika umeiba kura na umezima mitandao ya kijamii.

Sasa hao wananchi wako nao ni mabeberu?

Kuiba kura na kuzima mitandao ya kijamii nako si ubeberu?

Beberu ni lazima awe mzungu au Mmarekani?
Well said.
 
Wewe endelea kuota tu, eti maendeleo yatakuja na ufadhili. Tumefadhiliwa tangu tulipopata uhuru, lakini 2015 hapajakuwa na meandeleo yoyote. Nchi zilizokuwa nyuma ka,ma Korea Kusini, malaysia, Vietnam, etc zote zimeendelea kwa kutumia pesa za ndani tu. Wewe bado unatamani na kung'ang'ania kufadhili. Wewe ni sawea na baba wa familia anayeshindwa kulisha familia yake akitegemea misaada na kuhemea kutoka kwa ndugu na marafiki. ebu angalia kutegemea kwetu mapato ya ndani kumetufikisha wapi katika miaka mitano (UCHUMI WA KATI).Mtu mwenye aklili na kutaka kuendelea ataendelea tu kwa kutotegemea misaada peke yake. Kwanza hata hiyo misaada huwa ina masharti ya kuturudisha nyuma wakatyi mwingine. Jitegemee kwanza, mikopo iwe ni pla two.

hivi wewe ukitaka kuanzisha biashara (kujiendeleza) utategemea misaada tu. Kabla hata ya kupata mkopo inabidi waangalie uwezo wako wa kuwalipa, na una nini cha kuchukuwa ukishindwa kulipa.
Umetaja mataifa ambayo yalikuwa masikini kama sisi wakati wa uhuru, lakini sasa wako juu. Halafu tatizo ni beberu
 
Kama kungekuwa na "going back to future" ya ukweli, sidhani kama ungeiwaita mabeberu, nadhani ungewaita mashetani, wabakaji, wauaji, wezi, waporaji, na kama sikosei matusi makubwa zaidi kuliko hayo...
Hao jamaa unaodai wameendelea siyo watu wazuri kabisa, ni binadamu wenzetu sawa ila wana tabia za kikatili mno, sana sana..
Jaribu kusoma history kidogo ujuwe siri za utajiri na maendelea yao labda ukirudi tuweze kuongea kivingine...
 
BEBERU sio matusi mzee ......kwa kiingrerza tunawaita imperialist....


Kumuita mtu Beberu inafanana (an analogy) na kumuita mtu mwizi, kama ni mwizi na ushahidi unao basi kumwita mwizi sio tusi lakini kama huna ushahidi basi kumwita hivyo ni tusi. Mtu anakuwa beberu pale ambapo anafanya ubeberu vinginevyo beberu, kwa tafsiri ya nchi zinazofuata misingi ya kijamaa, ni tusi.
 
China imeendelea sana
Ilipewa misaada?
Badilisha mtazamo
Umatonya ni fikra mgando

yan unaongelea nchi ya pili kwa utajiri duniani unafananisha na nchi iloyopo kwenye nchi kumi za mwisho kwa umaskin duniani mkuu upo sawa upstairs ??

Nan alokwambia china haijawah kupewa msaada ??
 
Usengelema mkubwa kuliko wote kila likitajwa hilo neno "BEBERU" ndugu zetu wa CCM wanahusisha na jambo baya, ila hao hao kina kabudi wakiwa wanapikea misaada wanawaita WAHISANI , sasa swali langu kwanini wakati wanapokea misaada wasiseme "MABEBERU" wameleta hela hizi na hizi, SOMETHING SOMEWHERE IS NOT OKAY, ila kuna mbwa kutoka ccm itakuja kutetea huo upuuz.
 
Ndiyo. Mzee Nyerere aliwaita mabeberu wakaiangusha bei ya zao la mkonge halina bei hadi leo. Alipokuja Mzee Mwinyi akabadilisha jina wakawa wahisani au wafadhali, Mzee Mkapa akawaita wawekezaji. Mzee Kikwete akawaita wadau wa maendeleo sasa awamu hii tunaanza kurudi kule kule kwa Nyerere ambaye walimtaiti mpaka akaukimbia urais
Ninyi watu mnakaririshwa haya mambo au mnafuatilia historia sahihi?
Kuna raisi wa Tanzania ambaye amemzidi Nyerere kwa kupata misaada toka magharibi na mashariki mwa dunia?

Hakuna hata aliyefikia nusu yake...
Nyerere alikuwa mtu wa diplomasia hasa, juu ya yote alikuwa na kiburi na jeuri ya kukataa misaada yenye mashariti ya kijinga.
 
Nilidhani kila mtu hapa anajua kilichopo nyuma ya kuitana majina mabaya!

Ad hominem fallacy.
 
Back
Top Bottom