Kwani CCM siyo mali ya watanzania ?Leo Jumatatu Shirika la reli linafanya majaribio ya safari za treni ya abiria toka Moshi kwenda Arusha. Mgeni mualikwa ni katibu mwenezi wa ccm Humphrey Polepole.
Nimejiuliza tu kumbe TRC ambalo ni shirika la umma, ni wakala wa CCM siku hizi?...
ALiyezuia isije huku Moshi ni nani?Train haijatembea huko miaka 25 Sasa kijana wa miaka 30 lazima ashangae kwa hiyo kuzinduliwa ni sawa. Inazinduka baada ya miaka 25.
Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Pole pole anahangaika sana na watu wa Moshi na Arusha. Aende usukumani huko hata maji ya kunywa hawana
Kwahiyo kutoka Dar mpaka Arusha ni treni? Price Tsh ngapi?Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM ndugu Polepole leo anazindua Huduma ya usafiri wa treni kati ya Moshi na Arusha.
Mkoa mzima umetulia kimya na watu wote wameelekea stesheni kushuhudia treni ya kwanza ya TRC iliyobeba makada wa CCM ikianza safari ya kihistoria.
Chanzo: Channel ten.
Maendeleo hayana vyama!
Moshi kwenda Arusha wananchi wanatumia coaster bus TSH 3,000 kwa kutumia masaa 1.30 kuingia arusha.sasa train kutoka Moshi kwenda Arusha itatumika masaa 4 Nani wa kuisubiri? Itapalia abiria kwa TSH 330 au?
Apande huyo slow slow na mke wake!
Na mwisho wao wa kukaa uraiani ni pale Lissu akiapishwa kuwa rais, haya makando kando yote waliyoyafanya ccm yatawacost
Siasa za kishamba Sana. Swali langu Ni moja tu Hivi nikweli wanaamini watatawala milele bila kupigwa chini?? Siku itafika ujanja ujanja wote utaisha kwa kuwa Hakuna kitu Cha kudumu maishani hata uhai wetu Ni wa muda TU sembuse utawala!!? Nachofurahi wajinga wengi wameamka usingizini.
Nawasifu tu CCM kwa kuwa na Mikakati ya namna hii kwani hakuna asiyejua kuwa Kilimanjaro na Arusha walikuwa hawapendwi sasa watapendwa.
Kwani Kilimanjaro wanaishi Wachagga tu?Wachagga siyo wapumbavu kiasi cha kwenda kushangaa ujinga bwashee!
Yani mangi aache kuchoma nyama, manka aache kupeleka ndizi kiboriloni aende kumshangaa ki-homo eractus kutoka zama za mawe kati kikizindua garimoshi lililokuwapo miaka ya nyuma kisha wakaliua hao hao wanaodai kulizindua Leo?
Wapendwe kwa hiyo treni outdated Kaka! Watu wa huko wameamka miaka mingi nyuma. Mtu aache kusafiri na Youtung lenye AC ndani kwa muda mfupi, apakie treni la masaa 18 Ms-Dar? Halafu kupendwa ni kitu automatic na sio kwa vitu. Kuna mwanamke nilikuwa nampenda balaa hapo mlimani, kanilia sana hela zangu, lakini alikuwa anampenda muhuni wake muuza mitumba hapo Mwananyamala, tena muhuni mwenyewe alikuwa hapo kitu.
Hao wanaoipenda ccm wataendelea kuipenda, ila wanaopenda upinzani wataendelea hata wakifungiwa mabomba ya maziwa ndani. Usitegeemee Simba ikichukua makombe, basi mashabiki wa Yanga wataipenda.
na heri huo ujinga angefanya ukanda wa wasukuma huko kaskazini anapoteza muda wake tu
Mosh sio washamba to that extent unless wameambiwa kuna nyama ya kitimoto.
Polepole kuzindua hii kitu wapi na wapi?
Ndiyo maana Tundu Lissu anawapaga MATAGA za uso halafu wanaishia kulialia!
Watu wa Moshi ndio wanashangilia bwashee!Wewe ni zuzu. Unashangilia kazi iliyofanywa kwa kodi yako?
Nipo Kishapu naona jinsi mlivyopigikaNani kakwambia ?
Nalisikia ndio linaingia Arusha town saa hii na honi kama zote.Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM ndugu Polepole leo anazindua Huduma ya usafiri wa treni kati ya Moshi na Arusha.
Mkoa mzima umetulia kimya na watu wote wameelekea stesheni kushuhudia treni ya kwanza ya TRC iliyobeba makada wa CCM ikianza safari ya kihistoria.
Chanzo: Channel ten.
Maendeleo hayana vyama!
Hongera sana Magufuli kwa kweli,unastahili sifa zote.Mmm,Nyerere,Mwinyi,Mkapa na Kikwete waliturudisha nyuma sana kwa kweli.Hii ni hukumu kwao wote, popote walipo, hata kama sio ya mahakamani.Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM ndugu Polepole leo anazindua Huduma ya usafiri wa treni kati ya Moshi na Arusha.
Mkoa mzima umetulia kimya na watu wote wameelekea stesheni kushuhudia treni ya kwanza ya TRC iliyobeba makada wa CCM ikianza safari ya kihistoria...
Duh! mr price imefungwa zamani!!!!! huko Moshi weweNdio maana nimepita maeneo ya ushirika na kwa mr price kinyaa watu hakuna. Jamaa a yangu yupo Uchira anasema wamekodi Coaster kwenda kuishangilia treni. Ccm hoyeeee