Kwa 'body language' tu ya Mama azungumzapo huhitaji Akili Kubwa kujua ya kwamba...

Kwa 'body language' tu ya Mama azungumzapo huhitaji Akili Kubwa kujua ya kwamba...

Msishindane na marehemu fanyeni yenu ya onekane. Marehemu alifanya na yalionekana Mijizi na Mafisadi ndio hawakuona hilo. Sasa mnapomnanga marehemu tunajiuliza ndio tuseme mijizi na mafisadi wamechukua hatamu tena? Je mlioko serikalini na utumishi wa umati wa Watanzania ambao hamkubalini na majizi na mafisadi mtakaa muangalie kinyonge kinyonge na msifanye lolote?
Yeye mwenyewe the Late alikuwa mwizi na mjomba wake plus Bashite by then
 
Wakati ukiwa jangwani una kiu na umekata tamaa, Mungu anateremsha maji kwa njia ya ajabu kabisa.

Mungu ana maguvu sana
 
Kilicho muhimu siyo vyama vya siasa, siyo CCM, CHADEMA au ACT au chama kingine chochote BALI ni
kwa Taifa letu kuwa na viongozi wazuri na mifumo mizuri ya kiutawala.

Sina shaka kabisa Rais Samia ni kiongozi mstaarabu anayejua thamani ya utu wa mwanadamu. Anayetakbua kuwa kazi ya kiongozi ni kuwajengea mazingira watu wa makundi yote, ya kuweza kuijenga nchi yao, kuyajenga maisha yao na ya familia zao. Wananchi wana haki ya kuyafurahia maisha yao hapa Duniani kwa muda ambao Muumva wetu alitupangia alimradi hatuvunji sheria tulizozitengeneza.

Mh. Rais Samia ana uwezo wa kuliunganisha Taifa. Umoja katika Taifa letu ndiyo utakaoushinda umaskini.

Rais asisahau kujenga mifumo imara ya kiutawala ambayo italilinda Taifa dhidi ya watawala wabaya ambao wanaweza kuja kutokea hapo baadaye.

Tuachane na siasa za chuki, tumkosoe Rais wetu, tumshauri inapobidi, lakini kumpa ushirikiano ni jambo jema zaidi. Na hili livuke mipaka ya imani na ushabiki wa vyama. Taifa letu ni muhimu kuliko CCM, CHADEMA au ACT.

Mungu wetu, umjaze hekima Rais huyu mwanamke wa kwanza katika Africa Mashariki. Aongozwe na upendo wa kweli kwa Taifa lake. Ajue kuwa wanaomshangilia, wanaomsifia, wanaomkosoa, hata wanaomkejeli, wote ni watu wake.
 
Yeye mwenyewe the Late alikuwa mwizi na mjomba wake plus Bashite by then

Mjomba wake ni Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara kwa uhamisho. Bosi wake kapanda cheo ni namba bee. Khalafu unakuja na hizi hadithi. Unataka kuipa jamii taswira gani kuhusu Mh Rais wa JMT?
 
1. Baba Mbabe alikuwa hamshirikishi na huenda hata alitamani Kuachana nae.

2. Ushauri wake ulikuwa ukipuuzwa na kudharauliwa na Baba.

3. Hali ngumu ya Maisha imemkwaza Mama japo Baba aliona anatukomesha.

4. Aliwaamini sana Waliodharauliwa na Baba ambao walikuwa Weledi kuliko aliyowateua Yeye Baba.

5. Kuna Siri nyingi za Upigaji wa Miradi ya Baba ila alishindwa Kumwambia kwakuwa alishagundua anadharaulika nae.

6. Baba Kukitenga sana Kisiwa anakotoka Mama kulimkwaza akiamini hata Kisiwa pia kina Haki ya Keki Tamu na Nono ya Ardhi ya Tanzania.

7. Mama ameiva vyema Kidiplomasia na Kiustaraabu japo ana Ukali wa Kiumakini tofauti na Baba aliyekuwa na Ukali, Kukomoa, Chuki na Ujeuri wa Kibabe.

Ni mapema mno Kumpongeza Mama ila tusikatae kuwa dalili ya Mvua ni Mawingu na ' Body Language ' ya Mama inaonyesha kuwa Kilio cha Ugumu wa Maisha ya Watanzania ( Vyuma Kukaza ) hata na Yeye (Mama) inamuuma.

Hivyo Kipaumbele chake sasa ni Kuturudishia Tabasamu lililopotea katika Sura za Watanzania tokea tarehe 25 Oktoba, 2015 hadi 17 Machi, 2021.
Hii kitu inafikirisha mkuu 🤔🤔🤔
 
Kujaribu kuchukua rasilimali za Tanganyika " Tanzania" kuzipeleka Zanzibar ni udwanzi
 
Hapo kanigusa sana na pia vitakuwa huru sasa, uhuru wa Habar ulipotea sana

Acha tu nilikuwa najua tangia awali ,wazanzibar wana hofu ya Mungu,hawapendi uonevu,ukiona mzanzibar chakaramu basi ujue huyo amekulia bara ila wazawa wenyewe wanapenda haki.

Mh SSH atatuongoza vizuri ila namuomba asicheke na hawa "CHAWA aka WAPIGA MAPAMBIO" watampoteza, asimamie misimamo yake aliyoonyesha kwamba macho malegevu lakini yanaona ,ukimzingua na yeye anakuzingua ,bango moja DED/RC anakwenda na maji.
 
Waliokua wanawadanganya watanzania kuwa wapinzani kazi yao ilikuwa nikupinga tu, wajiulize kwanini wanampongeza kiongozi wasasa nawakati nimwana ccm?
 
Aisee watu walikua wanajituma sana tu lakini njia za mafanikio zilizimika kabisaaaaa. Lamda wewe ulikua kwenye mkondo wa neema ya wanayokula wenye nchi, au kunamisha fulani uliyakuta kutoka kwa familia yako au ulishaneemeka kipindi cha kikwete na ile msemo wa tembo hata akikonda hawezi kuwa kama mbuzi. Ila watu tunapambana brother na tunajibana sana lakini ilikuwa sio kazi nyepesi kwa mtu anayeanza maisha kutoboa kwenda level nyingine.
Naomba nikwambie tuu mie n muhanga wa maisha na niliathirika na transformation ya "The Magufuli effects" Ila Jambo jema nikuwa from day one kipindi anahutubia bungen siku ya kwanza Kama Rais nilimuelewa na nikajipanga katika line za maneno yake aliyokuwa anasema nilienda shambani japo kiubishi nikaumia nikarud mtaan ikawa ngumu nikatafuta kazi nikaajiriwa ikala kwangu nikarud mtaan Tena nikapata majanga maisha yakawa ngumu kama jiwe.

Ila nikaamua kubadilisha shida kuwa fursa karibu na watu wanaonizunguka TAFADHALI NAOMBA NIELEWE Tanzania Ni nchi nzuri Sana ukiwa mwaminifu na ukajituma jua wewe Ni mtaji mkubwa sana hapa Tanzania.

Sitaki kukwambia mwangalie mkuu wa mkoa wa simiyu ndugu Anthony mtaka na jiulize kwann yeye na simiyu nasio wengine na mikoa yao au hata wilaya utajifunza kitu na ANZA KUBADILIKA.
 
Back
Top Bottom