Kwa kuliokoa Taifa letu la sasa lenye Vijana 'Nyoro Nyoro' wengi naomba Mafunzo ya JKT yawe ni ya Lazima

Kwa kuliokoa Taifa letu la sasa lenye Vijana 'Nyoro Nyoro' wengi naomba Mafunzo ya JKT yawe ni ya Lazima

Ndio yale yale ya "mume"kumuomba "mke" perfume huko Dubai.
Vijana wengi wanapenda unyunyu na make up.
Mwanaume na make up???
 
Tuanze kwanza kupiga vita suala la ushoga ,matumizi ya dawa za kulevya,pombe kali kwa vijana wetu. Ukiwapeleka huko kwa lazima halafu ujumuishe mashoga,na watu waliounguza maini mbona watakufa mkuu
 
Utakuwaje na Taifa lenye Watu Shupavu ( tena kwa Vijana ) kama unakutana na Kijana wa Kiume kapanda DalaDala kutoka Makonde Mbezi Beach na anashukia Kituo kinachofuata cha Goigi huku akijiona ni Mjanja?

Nilikuwa najiuliza sana tu ni kwanini Vijana wengi wa Kiume Siku hizi ni Wavivu, hawapendi Shuruba ( Taabu ), wanapenda Kujiremba na kufanyiwa Scrub na Massage huko katika Masaluni, wakiongea wanabana Sauti, wanapenda Kujilambalamba Midomo yao, wakiagiza Chips hawali mpaka iwekewe Mayonaizi, wanapenda Kuvaa Suruali Modo na zinazowabana na hupenda kuwa karibu na Mabinti ila kwa nilichokiona leo Mchana nimepata Jibu.

Ngoja Junior wangu akue kue Kidogo ili nami Baba yake GENTAMYCINE nianze Kumlea Kijeshi / Kimedani kama ambavyo Baba yake nililelewa na Babu yake ili huko mbeleni asije kuwa Msukuma Ukuta kama walivyo Vijana wengi waliozaliwa kuanzia Mwaka 1990 na nianavyo huko mbeleni hali itakuwa mbaya mno na si ajabu hata Tanzania tukaja Kuongozwa na Msukuma Ukuta kwani dalili ya Mvua ni Mawingu.

Serikali kwa Kushirikiana na Jeshi ( JWTZ ) tafadhali GENTAMYCINE nawaombeni Tangazeni Mafunzo ya Kijeshi ya JKT ni lazima ili tukiokoe Kizazi cha Vijana wengi wa Kiume wa sasa ambao wanaonekana Kupenda na hata kutamani Kusukuma Ukuta na kufanana na Dada / Mama zao.
duh we jamaa kwahiyo hutaki wasukuma ukuta, hahaaaaaa aisee hili bandiko lako naona lina mashiko maana ukiangalia watu wenye akili timamu wote hawahusudu kabisa huu ukameruni, kama PUTIN etc
 
Back
Top Bottom