Kwa mara ya kwanza nchini KM 2035 zinajengwa kwa wakati mmoja

Kwa mara ya kwanza nchini KM 2035 zinajengwa kwa wakati mmoja

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Kwa mara ya kwanza Tanzania inaandika historia chini ya Rais Samia Suluhu kwa kutekeleza ujenzi wa Kilometa nyingi za barabara kwa wakati mmoja. Serikali inaenda kutekeleza miradi mikubwa yenye Jumla ya kilometa 2035 ambayo itaanza kutekelezwa Kwa wakati Mmoja na itagharimu shilingi trillioni 3.7.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa wakati wa uwasilishaji wa bajeti ya Wizara ya ujenzi kwa mwaka wa fedha wa 2023/24.

Sambamba na ujenzi wa miundombimu ya barabara, serikali imeendelea na ujenzi wa madaraja makubwa pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR. Uboreshaji wa miundombinu unaunganisha nchi na kufungua fursa za kiuchumi kwa kurahisisha usafiri wa watu na usafirishaji wa bidhaa na malighafi.

Hakika awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu hakuna kilichosimama, utekelezaji unaendela na kazi inaendelea.

1684762494393.png
 
Ujenzi makubwa hivi jaman hauwezi kweli kuvunja regency yetu pendwa??
 
Hujaisikiliza bajeti vizuri, total bajeti ya wizara ni tril 3.7 ambapo 1.1trl inaenda SGR, nyingine za kulipa madeni, kujenga na kumalizia miradi iliyopi ie Kigongo, airports.

June wanazindua ila haitaanza kujengwa zote kwa pamoja.

Uzuri wa Bajeti ni EPCF ya barabara ya Dar Morogoro
 
Hongera sana Mama kwa kazi kubwa sana, Allah akulipe kwa kazi hii njema kwa Taifa lako
 
Cha ajabu Waziri wa hiyo wizara watu hata hawamjui-jui kabisa.

Kuna kama ungejengwa katika awamu yake, basi angendaa ziara ndefu ya ardhini kuamzia Dar hadi Tinduma huku kila mkoa akisimama si chini ya mara sita akitukana wananchi, wapinzani, wafadhili hadi mabibi na mababu zenu.

Halafu angefika pale Tunduma angemalizia kwa kumtukana rais wa Zambia na babu zake, halafu huyooo, angerudi zake kule kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa.

Maana yule bwana ilikua hata 6ausi wakitaga na kutotoa ilikua lazima dunia ijue
 
Hujaisikiliza bajeti vizuri, total bajeti ya wizara ni tril 3.7 ambapo 1.1trl inaenda SGR, nyingine za kulipa madeni, kujenga na kumalizia miradi iliyopi ie Kigongo, airports...
Huyo mleta uzi amekuja hapa kutafuta kiki baada ya Samia kusema huwa anapita humu Jf.

Amesahau tu kuweka namba.
 
Haijawahi kutokea tangu nchi hii ipate uhuru, mama yupo kazini.
 
Ila kwa yule bwana hatofikia! Ile ilkua ngoma nagwa
 
Mwisho wa mwaka bajeti itakuwa imetekelezwa Kwa 34% sio kazi rahs kama unavyofkria inahtaji mkono wa chuma
Halafu watakuja na kisherehe chao na CAG wanatusomea walivyobunya pesa.
 
Hujaisikiliza bajeti vizuri, total bajeti ya wizara ni tril 3.7 ambapo 1.1trl inaenda SGR, nyingine za kulipa madeni, kujenga na kumalizia miradi iliyopi ie Kigongo, airports...
Imeshapata mzabuni au bado!

Vipi maandalizi yake yataanza mwaka huu?
 
Alie buni malipo kwa control namba, kwenye hii nchi aliona mbali sana.
 
Back
Top Bottom