Kwa mshahara huu, Mo Dewji utajiri wako unatokana na unyonyaji wa wafanyakazi wako

Kwa mshahara huu, Mo Dewji utajiri wako unatokana na unyonyaji wa wafanyakazi wako

Ni Kweli kuna TAJIRI ana wiwanda vikubwa kibarua anamlipa Tsh 3000 kwa siku,mie nashangaa Waziri wa kazi/Ajira na Waziri wa Viwanda wapo tu kutwa kwenye Majukwaa kupiga bla bla za chama badala ya kwenda field kutetea maslahi ya wafanyakazi,hivi 3000 kwa siku inatosha?
hivi kwa kuuza vijuisi hivyo tanzania tu watu wanataka kulipwa na sawa na kampuni kama puma au adidas ambazo zinauza bidhaa dunia nzima gharama ni kubwa sana za uzalishaji kiwandani kibaya zaidi serikali inategemea kupata kodi kubwa zaidi viwandani ndo mana wawekezaji hawategemei kipato kimoja
 
hivi kwa kuuza vijuisi hivyo tanzania tu watu wanataka kulipwa na sawa na kampuni kama puma au adidas ambazo zinauza bidhaa dunia nzima gharama ni kubwa sana za uzalishaji kiwandani kibaya zaidi serikali inategemea kupata kodi kubwa zaidi viwandani ndo mana wawekezaji hawategemei kipato kimoja
Nani kasema walipwe sawa na kampuni ya puma au adidas?
Wewe unaona ni sawa dereva kulipwa 130,000?
 
Mkuu naomba nifafanue hapa kuhusu hicho Kidogo wanachopata. Hii nafasi ya hawa SalesPerson cum driver, wanapewa Allowance ya Tsh. 100 katika Kila Carton 1 ya Maji au Soda. Akiuza Carton 100 kwa siku Ana Tsh. 10,000/= x siku 26 ni 260,000/= kwa mwezi, wakati mwingine hata Jumapili wanaingia kazini. Hapo ni kama Ameuza Cartons 100, wapo ambao wanauza mpaka cartons 500 per day. Ukiangalia huu mfumo ndo wenzetu wa Nchi zilizoendelea wanatumia, yani mtu alipwe kulingana na alichozalisha. Utaona kwa sisi ambao tunapenda Kazi ya Sales, hatuangalii Mshahara, Tunaangalia percentage on Commission based. Ugonjwa mkubwa wa Watanzania waliyo wengi anataka aone fixed salary ili apate mtelemko kila mwisho wa mwezi. Yani ufanye kazi usifanye mwisho wa mwezi hela yako iingie. Huu Upuuzi ambao matajiri wengi walishaachana nao. Hata ningekua ni Mimi lazima nione unachozalisha katika kampuni ndo nikupe mshahara mzuri. Watanzania Tubadilike. Vijana wengo mnaotoka chuoni mkiambiwa njoo ufanye kazi ya Commission hamtaki kwasababu mnapenda mitelemko. Dunia imebadilika. Mwisho, Hiyo 130,000/= wanalipwa kama hela ya Kujikimu tu In case hajafanya mauzo mwezi mzima, lakini kinyume chake Commission wanazopata ni kubwa maradufu kuliko mshahara ambao ww umelalamikia hapa. Asante


Eddy Love unasemaje juu ya hili, ni kweli ilikuwa hivi wakati unafanya kazi huko!??
 
Wabongo hatueleweki tunataka nini kwa kweli Rais Akisema amuamshie Dude uyo Mo Dewji ili mpate mishahara minono then mo Aka react na kufunga biashara mtakuja kupiga kelele apa kuwa anafukuza investors wanaotoa ajira, Akisema aache ili muendelee kulipwa hio hio bado mnaona mnaumizwa je mnataka nini nyie kasuku?!!! Wahindi hao ni washezi hata dangote cements inasimamiwa na mhindi ni wanyonyaji by nature hapo anaweza kuwa hamlipi io 130 ila anaandika kiasi iko kidogo kukwepa Kodi mana kwa 130k hata tax apo serikali haichukui
 
Maisha yanabadilika kila siku.

Gharama za Maisha zipo juu sana.

Kama ni kweli, kwa MSHAHARA huo!

Nafikiri hapo unamfundisha DEREVA wako akuibie
 
Kwahiyo mm ninaemlipa dereva wangu wa daladala 120000 nina afadhali kuliko mo dewji[emoji30]
We nae ni muongo tu,tangu lini dereva wa daladala akalipwa mshahara,tena inaelekea hata hujawahi kufanya biashara ya basi.
 
Ku
bonas mkuu hazitambuliki kisheria, zinaweza kuwepo au zisiwepo.

Mshahara gani upo chini ya kima cha chini kwa kampuni ya Tajiri namba moja?

Huu ni unyonyaji mtupu.
n
Kuna sales commission na sales appraisal. Hizi huzidi salary hata mara 10, kwenye sales &marketing industry huwa hivyo, lengo ni kumfanya staff awe na bidii
 
Mshahara mdogo unaufuata wa nini si unakwenda ulipoona maslahi makubwa? Ajira ni mkataba so ni hiyari yako kuuchukua au kuacha. Japo kima cha chini kipo kisheria, lakini mbona hata serikali haitimizi maslahi yote ya waajiriwa wake kwa 100%. Mwenye njaa ataweza kwenda kudai kima cha chini ilhali kazi yenyewe kaipata kwa zengwe? Usisubiri usawa dunia hii, mengine ni maandishi tu ambayo yapo kwa sababu ni lazima yawepo. Tumikia kafiri pata mtaji wako jiweke huru.
 
Hizo hasira unazitoa wapi? Dont take life so serious. Hii ni blog
Sio hasira man,ila nataka kumweleza tu huyo asikariri maisha madereva wa vidala wengi ss hivi wanalipwa,na yote hiyo mwenye gar uweze kumpa dreva masharti ya kazi
 
Back
Top Bottom