Kuna watu wanamshauri huyu kijana upumbavu mpaka unashangaa kama huu ushauri umetoka kwa mtu mzima mwenye akili timamuu au wale wenye mihemko?
Eti "nunua bando la halichachi, weka ufanye nauli ya kambini,ka beti n.k" wale wote waliomshauri hivi huyu kijana kwa mtaji wake wa elfu 50 nadiriki kusema ni WAPUMBAVU wa akili na kufikiri"
Kwenye Biashara hakuna ela ndogo ni wewe tu na juhudi yako ya kuitafutia soko tu.
Mdogo wangu, hongera kwanza na nakusihi usikatishwe tamaa na wapuuzi wachache wa JF, wewe umeonyesha nia na akili zaidi inayowashinda hata Graduate wabeba bahasha,zipo vingi vya kufanya ila nitaviorodhesha baadhi
* kama upo Dar amka asubuhi sana nenda katika masoko makubwa ya mitumba kama Soko la Ilala boma n.k muda huo ndio mitumba hufunguliwa na kuuzwa kwa bei nafuu sana, tafuta hata Nguo za watoto kwa buku buku na ukaziuze mtaani kwa kuzitembeza nyumba kwa nyumba hata kwa elfu 2 mbili tayari utakua unakuza mtaji wako taratibu Sana lakini wenye matumaini na kuendelea kujitanua.
*kwa kua sasa hivi ni msimu wa mihogo nenda sokoni asubuhi sana kanunue roba lako la mihogo (hapa yakupasa uwe makini ya kutambua aina ya mihogo kama ni mitamu + inaiva kwa haraka) nunua hata mihogo ya elfu 10 tu kwa kuanzia,
Karai lako La elfu 5 na kuni bila kusahau mafuta , anza kukaanga mihogo taratiibu utapata chochote kitu
*Nenda k/koo kwenye maduka ya vyombo ya jumla AU Maduka ya urembo na viatu (simple shoes za akina mama na watoto wa kike) kanunue vitu vichache tu na anza kuvitembeza na kuvikopesha kwa akina mama wa mitaani (hawa hupenda kukopa sana) alafu waambie utapitia kila siku buku buku, utajikuta unasogea
*tafuta karai size ya kawaida tu, nunua mafuta na uamke asubuhi kwenda machinjio ya kuku, nenda kanunue kuku huko hata kwa kuanzia na wa 3 sio mbaya mfano niliwahi nunua kuku wa kizungu kwa elfu 6, anza biashara mdogo wangu hapo hapo mtaani kwenu
Siku zote muheshimu sana Mtu anayeanzia chini kwenye biashara maana kiu yake ni kubwa mno kufikia mafanikio, naamini na wewe kiu hiyo unayo, Allah akuongoze vyema InshaAllah