Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Umenikumbusha mbali sana na issue ya chapati.nilijaribu kujifanya nataka nipike l.ebwana eeh ikatoka kama zile nani(yale machapati ya kuvunjika.Ngumu hiv.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ukipigwa nalo shavuna lazima shavu litoboke [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Acha kudanganya watu ...faida ya 25,000......

Mnaandika tu huku kufurahisha umma si ndio
Mimi ni shahidi wa haya ninayozungumza.

Nilianza na mtaji wa 50 kwa siku nilikiwa naweka zaido ya elfu 8.

Uuzaji wa maziwa fresh. Nadamkia maeneo riverside nanunua maziwa kwa 1200 nauza kwa 1900.
Nilianza na lita 15 nkafika mpaka 40.
So inawezekana.
Biashara mwisho saa 4 asubuhi.
 
Tuma picha Badoo
 
River side maeneo ya stendi ya kwenda mbagala,hiyo laki mbili ana nunua maziwa hapo anaenda kuuza mtaani kama ana wateja wengi ishirini anafikisha kama faida,sisi tulikuwa tunatoa hapo River side tunauzia mbagala vichochoroni faida ina fika 10 kwa siku.
 
Inawezekana hata zaidi ya hio usikariri.
Kwani mama uji anaingiza bei gani kwa siku.
Vipi akiifungulia vijiwe vya kuuza uji,na vitafunio mbona hata huo mtaji wa laki2 still bado ni Mkubwa.
Akiweza uza vikombe 100 kwa siku asubui vikombe 50,jioni vikombe 50 kwa siku anapita hio 20 kwa siku.
Location kariakoo, magufuli stand, makumbusho stand, pugu mnadani, Buguruni sokoni, Ilala sokoni, soko la karume, ferry kivukoni, kigamboni fery,
Utajiri ni kutupa aibu pembeni.
 
Popote penye makundi ya watu kuna pesa, wapelekee nini wanataka.
Utajiri ni uwezo binafsi wa kukusanya pesa kutoka kwa mtu mwingine.
Umasikini ni kitendo cha kushindwa/ kukosa mbinu ya kuchukua pesa toka kwa mtu mwingine.
 
Yes yes. Mkuu hela ipo ila ukijituma na ukubqli hasara mwanzoni
 
Tafuta baiskeli used ambayo ipo katika hali nzuri hata 50,000 unapata inayobaki nunua mayai trei 20 kwa 7,000 itakua 140,000 na 6,500 itakua 130,000.
Zunguka kila chocho kila duka la mangi kila genge kila banda la chipsi asubuhi na mapema ukiacha namba na ukichukua namba za wateja wako.

Nakuhakikishi itafika kipindi kila trei 50 utakua unazisambaza kwa masaa machache tuu.
Faida yake huwa ni (500 mpaka 1000) kwa trei kwa mwanzo usitake faida kubwa anza na 500 tuu utengeneze wateja ila baadae utakua ushajua wafugaji wanaouza mayai kwa bei nafuu na utaanza pata faida ya 1000 kwa kila trei.. ukifika level hii sasa ukiuza trei zako 20 tuu hiyo ila yako ya siku unayoisema utaiingiza kirahisi na muda mfupi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…