Kama upo dar na unaweza kupata kasehemu ukaweka meza mtaani kama genge, iyo laki 3 unaweza kuanza kuuza karoti, ndizi, machungwa na nyinginezo za chakula. Bidhaa zako uzinunue mojakwa moja kutoka kwa mkulima. Wala si mbali, nenda apo Ruvu unapata mzigo wa kutosha. Huhitaji ela nyingi sana. Kumbuka tu kwamba laki inajengwa na elfu,milioni inajengwa na laki, nk.
Kwa uchache tu, kwa mfano saivi chungwa 1 wanauza sh. 30 shambani. Ukinunua gunia machungwa kama 1200) ni elfu 36 au tufanye 40 elfu. Weka usafiri kama elfu 10. Garama ya gunia unapata kama elfu 50.
Bei ya gengeni chungwa 1 ni sh. 200. Ukiuza 1200 unapata 1200x200=240,000. Ukitoa garama elfu 50, unabaki na faida ya sh. 190,000. Hiki ni kitu kimoja tu, bado hujaweka karoti. Nafikiri unajua bei ya karoti moja.
Kwa mtazamo wangu, huhitaji mtaji mkubwa ili utoke. Kidogo ulichonacho ukikusanya kwa malengo kitakua kikubwa. Usidharau iyo laki 3, inategemea unaipangilia vipi. Swala ni kujipangia muda tu na wewe kuwa tayari.
Mi nafahamu mtu aliyeanza kufanya biashara ya kuuza mifuko ya rambo Arusha miaka ya 1990 kwa bei ya rejareja, badae kaanza kusafiri kuchukua mifuko hiyo kutoka Zenji na kuiuza kwa jumla Aru. na nairobi, akaongeza biashara ya kuuza nguo, kwa sasa ana ghorofa kariakoo na anasafiri kwenda china kununua mali.