Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Unatafuta wakukejeli tu
Kwa kiasi hicho unahitaji kuangalia mazingira uliyopo kuna nini wenzako wanafanya ndicho
Biashara ya kuku nyepesi sana na hela yake ya uhakika sana ila omba sana wasipigwe ugonjwa, mama yangu anafuga kipindi anaanza kuna ugonjwa uliwapiga kuku tulikula mpaka tukawa tunagawa
 
Laki 8 ni nyingi sana kama unajicho pevu la tatu la kuziona fursa,binafsi nishaanzaga na mtaji wa Tsh40000(elfu arubain tu) right now nina ROI ya 7m kama faida every two weeks ni ngumu kuamini but thats it..anyway nisikuchoshe

Tafuta washing machine with dry cleaning system, used atleast ichukue kwa 400000 Huna haja ya kununu liquid soap you can make it by your own at your home.

Huna haja ya kukodi frem..tafuts eneo lavwazo hapo nyumbani kwako au chumba cha wazi
Tafuta hosteli na vyuo vyenye mkusanyiko wa watu wengi maeneo ya karibu yako..bandika ads kwamba unafua na kupasi nguo za wanafunzi na watu wengine kwa bei nafuu na ofa maalumu plus nguo za aina yoyote..lets say unafua na kupasi T-shirt na jeans kwa 2500 each@1250 plus ofa ya kufua boxer na vest/sidiria na chupi bure kwa mhusika mmoja..

400000 ivunje kama ifuatavyo: toa 50000 nunua baiskeli toa 100000 ingia mkataba wa miezi mitano kwanza na kijana mdogo kutoka uswekeni ambaye hana ajira wa kumlipa 20000 kila mwezi plus allowance ya 500 kwa kila complete order anayoileta(ya 2500)..mpe baiskel kwaajili ya kuchukua na kurudisha order za watu.huyu kijana usisahau kumpa motisha za malazi chakula na matibabu.
Imebaki 250000:Ivunje kama ifuatavyo

Toa 50000 nunua pasi na perfumes mbili moja ya kike na moja ya kiume(perfume ni mbwembwe tu kwa wateja wako)
Toa 30000 nunua enga za bei rahisi au tafuta muuza mitumba akuelekeze material ya kununua kwa ajili kutengeneza enga za gharama nafuu..hizi enga zitumike kutudukia na kudeliver nguo za watu..ila zisibaki kwa wateja.

Toa 30000 tengeneza kijikabti au sanduku nyuma ya ile baiskeli kwaajili ya kucollect na kudeliver order za watu.
Imebaki 140000 toa 50000 ingia mkataba na muuza maji wa karibu yako kuchukua dumu tatu kwa hesabu ya 750 kila siku za kazi kwa muda wa miez miwili..NB:Kama una'access na maji ya bure hii ni salama yako

Imebaki 90000 toa 40000 kwaajili ya kununua liquid soap materials pamoja na jiki material ya kutengeneza jiki nyumbani..
Imebaki 50000 toa 35000 iweke iwe pesa ya kulipia gharama za umeme kwa kipindi cha atleast mwezi mmoja na nusu..na 15000 kwaajili ya yale mabandiko ya printed white paper kama matangazo NB:inabidi wewe na yule kijana muwe nembo muhimu ya kuitangaza biashara yenu msitegemee mabandiko tu.

Kilichobaki ni kuanza kazi na kusubiri mvua ya wateja itakayo kuwa ikimiminika hapo ulipo..
Zingatia huduma nzuri kwa wateja wako.Na pia zingatia ulichowekeza na utakachokuwa ukikipata kama faida...pia zingatia ghatama nafuu kwakila huduma ya kuzisafisha nguo za wateja wao..lengo ni kuwa'outstand major dry cleaning franchises na kuprovide huduma kama yao ila kwa bei nafuu..Zaidi ya hapo SEE YOU AT THE TOP..WISHING YOU ALL THE BEST much great
 
Habari watanzania Mimi nikijana mdogo nipo Kibaha Mlandizi nataka kufanya biashara nahitaji mawazo ya biashara gani nifanya inayo toka nainawateja kwa hapa Mlandizi naiwe yenye kutuanzia mtaji mdogo Kama laki moja ushuriwenu pls nataka nijikwamue kimaisha
 
Angalia changamoto zilizopo kwenye eneo lako zaidi pitia kwenye hili jukwaa zipo threads mbalimbali zenye mawazo mazuri ya biashara kwa mtaji ulioutaja.

Kila la kheri.
 
Habari watanzania Mimi nikijana mdogo nipo kibaha mlandizi nataka kufanya biashara nahitaji mawazo ya biashara gani nifanya inayo toka nainawateja kw ahapa mlandizi naiwe yenye kutuanzia mtaji mdogo Kama laki moja ushuliwenu pls nataka nijikwamue kimaisha
Anzisha biashara ya kufua au kufua na kupasi nguo.
Nunua sabuni ya MAQ BOX KUBWA LA TSH 5000/
BESENI MOJA SH 5000/
NDOO NDOGO 2 . 3000/
GLOVES NGUMU 7000/
CHUKUA BOX ANDIKA HATA KWA MAKER PEN
ANZA KAZI MKUU UFURAHIE MAISHA
 
Wazo zuri Sana, hizo gloves zinaitwaje na zinapatikana maduka gani?
Anzisha biashara ya kufua au kufua na kupasi nguo.
Nunua sabuni ya MAQ BOX KUBWA LA TSH 5000/
BESENI MOJA SH 5000/
NDOO NDOGO 2 . 3000/
GLOVES NGUMU 7000/
CHUKUA BOX ANDIKA HATA KWA MAKER PEN
ANZA KAZI MKUU UFURAHIE MAISHA
 
Mkuu Nenda Sokoni Kisutu kuna Korosho nzuri safi zilizokaangwa(Rosted and Salt) zinauzwa Elfu 9 hadi 10 Kwa Robo kilo nunua vifuko special vile vidogo vinauzwa elfu Tano kwa pcs 50 yaani kimoja ni Mia Korosho unaweza nunua robo kilo unajaza kwenye kifuko kwa kutumia Mzani ile midogo digital gram 20 ukimaliza kujaza vifuko vitatoka vifuko 25 kila kifuko kilichojaa Korosho utakiuza kwa bei ya Shs 1,000/= so ukifanikiwa kuuza vyote mauzo yatakuwa elfu 25,000/= gharama za Matumizi ya kuandaa bidhaa itakuwa 5000/=vifuko,Korosho 9,000/= Jumla 14,000/= Faida itakuwa 11,000/= Hapo unaweza tumia akili zako kama umezaliwa nazo ukaenda kwenye maduka ukawauzia kwa bei ya jumla kifuko komoja ukawauzia mia 600 au 700 upate faida ya 400 au mia tatu kwa kila kifuko au unaweza omba mwenye duka akuuzie faida mgawane n.k but unatizama mauzo yakiwa fresh unaongeza mzunguko wa kutafuta masoko ila hakikisha Korosho zile Tamu na Safi ikiwezekana unachambua unaondosha zile mbaya ukiendlea unaweka na namba yako ya simu kwenye vifuko maisha yataenda... ukiwa na mkono wa Biashara hiyo pesa unaweza rudisha mkopo ndani ya siku kadhaa tu. Nimekupa Mtaji mdogo kabisa wa kuanzia ambapo ni robo ya ulichonacho.

kama Umependa Gonga Like. Utashukuru ukifanikiwa
vifuko 25 vya kg 20unahitaji nusu kilo ya korosho sio robo mkuu, wazo zuri linawezekana kutekelezwa hata km mtu yupo busy
 
Wapendwa ninaomba kupata wazo zuri la biashara kwa mtaji wa laki tano

Huku manyara wilaya ya Mbulu( Haydom) ningependa kuanzisha biashara huku vijijini ila bado sijapata wazo zuri la biashara

*Nimejaribu kufikiri ila nikaona kidole kimoja hakivunji chawa karibuni kwa maoni yenu
maxresdefault.jpg
 
Chipsi zinalika huko.!???

Au uza kitimoto..

Thank me later
 
Naona watu wanakula chips sema vbanda vingi sana huku alafu wanakula sana nyama choma
 
Back
Top Bottom