Hongera kwa uthubutu wako ulioonyesha kama kweli una nia utafanikiwa..laki moja nayo ni pesa..thamani ya pesa uliyonayo huwezi kuiona mpaka utakapoikosa ama kuitumia..
Kwanza kabisa elewa kuwa kwa maisha ya sasa laki moja inahitaji budgeting kwa kias chake..ila uweke usistadoo pembeni kwanza ndo utafanikiwa..ushauri wangu ni kama ufuatao;
kulingana na hela uliyonayo unaweza kufanya biashara zifuatazo;
Nunua jiko la mkaa.-10000/-
karai la kuchomea maandazi 5000/-
mafuta ya kupikia lit 3...12000/-
mkaa debe 6000/-
unga kg 2 2500/-
hamira 500/-
baking powder 500/-
kibao cha kusukumia 5000/-
kontena ya kuwekea 3000/-
sukari nusu kg 1000/-
Jumla 45,500/-
hivi ni kwa kuanzia tu kwanza utaongeza kadri siku zinavyokwenda..
unaweza kukaanga maandazi ama half keki nzuri..
SOKO
Sijui unaishi.mazingira gani au maeneo gani huko mtaani kwenu sijui kumekaaje ila ninavyojua dar kuna sehemu nyingi sana za chai kila kona cafe zile..wengi huwa wanapelekewa vitafunio wao wanauza na huwa hawatengenez vyote.nakushauri mdogo wangu ongea na mmojawapo wa mhusika wa hivo vihotel mwambie mpango wako wa kupeleka maandazi ama half cake kila siku asubuh.unaweza kumuuzia 200 yeye akauza 300 ama zaid atajua mwenyewkg 2 ua unga inatoa piece 40/30 kwa size ya kawaida hapo ukimuuzia 200/300 una elfu 8-10 kwa siku.unatengeneza kibubu chako ukifika unaiweka hela yote kwenye kibubu kwakua bado una chombeza mtaji ile hela iliyobaki kama 50500/- utaendelea kununua unga na mafuta na mkaa kama ni kutumia na nauli n.k hii ni kwa vile unaanza lazima ujaribu soko likichanganya unaongeza vipimo.
Sehemu nyingine unayoweza kuuza ni kwenye maduka ya kina mangi utakachofanya utanunua unga, mafuta. sukari n.k hapo dukani kwake then yeye anakuuzia bila kukata hela yeyote..hii ndo huwa hivi..
soko lingine unaweza kutembezea majirani zako asubuh majumbani mwao na wakishazoea utaenjoy maana utatafutwa..cha muhim ni ubora wa bidhaa yako tu.
soko lingine unaweza kuweka kastuli hapo nje ya geti na majirani wakiona watanunua tu..
Zingatia kuwa:, usiangalie ni wangapi wanaofanya biashara kama hii kila mtu na bahat yake na ubora wa bidhaa yako..mfano mimi no mfugaji wa kuku karibu majirani wotee shamban kwangi wanafuga lakini nauza mpaka kuku 300 kwa wiki sasa utaona kwann inakua hivi wakat wote tinafuga kuku walewale?
Ukitaka kufanikiwa usichague kazi fanya kile kilichopo mbele yako mradi kiwe halali..ka ni maandazi nimeuza sana na ninaijua sana hii biashara.maana kama una uwezo wa kupata elf 10/15 kwa siku unataka kaz gani tena ndugu? na wakati wapo wanaooga na kukipaka mafuta asubuhi wanatoka na wanarud jioni mshahara elf 50-80 sasa wewe kwa mwez una lak3-4.5
Nipo na vibaby vinanisumbua hapa kidogo nlitaka nikuandikie na biashara nyinginenyingine ila kwa baadae vumilia ntaitembelea tena thread yako.
Kila la kheri na ulete feedback..usikatishwe tamaa thubutu utafanikiwa.