Kwa muda mfupi sana kiongozi wa Tanzania alipata maadui wengi sana

Kwa muda mfupi sana kiongozi wa Tanzania alipata maadui wengi sana

Kwanza kabisa ni wanachama wenzake ambao walishazoea kupiga madili makubwa. Hawa walishazoea kukwapua mabil ya shilingi na wao huona kama wamekwapua shilingi elfu moja. Hawa walishamchukia sana kwa kuziba mianya yaou ya upigaji.

Pili ni wanasiasa wa upinzani ambao baada ya kusambaratisha vyama vyao nao wakawa hoi kisiasa. Na vyama vyao vikwa vimeyumba kisiasa na kiuchumi.

Tatu ni wananchi ambao wengi walimuona kama kiongozi ambae ni dikteta hawa wengi walidai kupoteza jamaa zao au ndugu zao kwa kile kilichodaiwa ni watu wasiojulikana.

Nne ni wafanyabiashara ambao walizoea kuhujumu uchumi kwa kutengeneza bidhaa bandia, kukwepa kodi, wengi walikamatwa na kukwepa kodi na walikuwa magerezani kwa kuhujumu uchumi

Tano ni matapeli na wapigaji hawa walishazoea kulipwa mabilioni ya senti kwa kuwa na kampuni za mfukoni na walikuwa wakilipwa hata kama hwajafanya kazi.

Kwa ujumla kiongozi alikuwa na maadui wengii sana kwa muda mfupi.

Hivi ndivyo Africa ilivyo.

Umesahau
Wauza madawa ya kulevya.

Majangili wa nyara za serikali, mfano meno ya Tembo.

Mashoga

Waliokuwa wanajiita mamesheni tauni (sijui kama nimepatia jina).

Michepuko ya wanene waliopangishiwa masaki.

Wazee wa bandari
 
sijui una umri gani kiongozi,ila wewe ni kati ya watu wazima wajinga sana.

nyinyi wazembe wachache ndio matokeo ya tz hii ilipo zaidi ya miaka 50 ya uhuru.
Sio kweli matokeo haya ni ya nyerere alitutia umaskini na viongozi wenye mtazamo kama wako na meko mungu amchome moto huko aliko wa kutuyumbisha na kutupeleka mnavotaka. Watu walipoteza matumaini mana alisimamisha maisha ya watuili ajenge nchi alaf sijui alete wazungu waje kutumia hizo rasilimali. Mana km ni kwa ajili ya watanzania hakupaswa kuzuia kupanda kwa mishahara,hakupaswa kuzuia ajira zisitoke na hakupaswa kuficha vitu ambavyo vinatumia fedha zetu na kufanya anavyotak. Sheria ziliekwa kutuongoza na kuleta usawa na sio kupeleka ujinga wake chato sasa nendeni burigi uko msilete thread za kijinga hapa. Legacy haitetewi!!!
 
Wachina walikwenda hivi kwa miaka isiyopungua 20 na leo tunawaona wako hapa ila sie miaka 5 tu ndg yetu washamuwaisha ahera, haitatokea tukajitegemea watanzania na daima tutaendelea kutawaliwa na kuonewa. Tumechukua upande wa wakataa pema sasa pabaya pametuita rasmi
Hata tungepewa 100 na Bwana yule tusingesonga.China amesonga baada ya kuzitupa sera chakavu za dikteta Mao za kuendelea kwa kuwa kisiwa.Huwezi endelea pasipo kuliwa.
 
Wachina walikwenda hivi kwa miaka isiyopungua 20 na leo tunawaona wako hapa ila sie miaka 5 tu ndg yetu washamuwaisha ahera, haitatokea tukajitegemea watanzania na daima tutaendelea kutawaliwa na kuonewa. Tumechukua upande wa wakataa pema sasa pabaya pametuita rasmi
Muda utasema tu kiongozi tatizo la watanzania wengi hawana uzalendo na wanapenda kuishi kiujanja ujanja na kifisadi bila kufanya kazi.
 
Unasema huvyo kwa sababu hukuwahi kuguswa wakati wa utawala wa yule shetani. Mimi ni mhanga niligombea nafasi Fulani ndani ya chama Fulani tena ni chama cha wafanyakazi tu. Kilichotokea ni maajabu. Kwa kuwa walihisi nipo upande wa pili, nilitekwa nikalazimishwa kujiunga na upande wa kijani. Niliyoyaona huko sithubutu hata kumuomba dua yule kayafa. Mungu amlaze mahali panapostahili.
Acha ufedhuli nani akuteke wewe au ulitekwa na maisha.
 
Kwanza kabisa ni wanachama wenzake ambao walishazoea kupiga madili makubwa. Hawa walishazoea kukwapua mabil ya shilingi na wao huona kama wamekwapua shilingi elfu moja. Hawa walishamchukia sana kwa kuziba mianya yaou ya upigaji.

Pili ni wanasiasa wa upinzani ambao baada ya kusambaratisha vyama vyao nao wakawa hoi kisiasa. Na vyama vyao vikwa vimeyumba kisiasa na kiuchumi.

Tatu ni wananchi ambao wengi walimuona kama kiongozi ambae ni dikteta hawa wengi walidai kupoteza jamaa zao au ndugu zao kwa kile kilichodaiwa ni watu wasiojulikana.

Nne ni wafanyabiashara ambao walizoea kuhujumu uchumi kwa kutengeneza bidhaa bandia, kukwepa kodi, wengi walikamatwa na kukwepa kodi na walikuwa magerezani kwa kuhujumu uchumi

Tano ni matapeli na wapigaji hawa walishazoea kulipwa mabilioni ya senti kwa kuwa na kampuni za mfukoni na walikuwa wakilipwa hata kama hwajafanya kazi.

Kwa ujumla kiongozi alikuwa na maadui wengii sana kwa muda mfupi.

Hivi ndivyo Africa ilivyo.
Kwa alipokuwa yule Shetani anatupeleka,ni dhahiri kungetokea Vikundi vya Waasi na Kigaidi.
Mungu hakuruhusu hilo litokee
 
Propaganda haziwezi kumpaiza mtu yoyote. Subirini wajinga ndio muwalishe hizo propaganda. Yule alikuwa dhalimu sio zaidi ya hapo.
Subiri tuone wasiokuwa wadhalimu wataifanyia Tanzania, wewe ni mbinafsi usiokuwa na future ya baadae hayati alikuwa anaandaa mazingira mazuri kwaajili ya watoto wetu na vizazi vitakavyokuja kumbuka ata china ilipitia magumu mangapi.
 
Kwanza kabisa ni wanachama wenzake ambao walishazoea kupiga madili makubwa. Hawa walishazoea kukwapua mabil ya shilingi na wao huona kama wamekwapua shilingi elfu moja. Hawa walishamchukia sana kwa kuziba mianya yaou ya upigaji.

Pili ni wanasiasa wa upinzani ambao baada ya kusambaratisha vyama vyao nao wakawa hoi kisiasa. Na vyama vyao vikwa vimeyumba kisiasa na kiuchumi.

Tatu ni wananchi ambao wengi walimuona kama kiongozi ambae ni dikteta hawa wengi walidai kupoteza jamaa zao au ndugu zao kwa kile kilichodaiwa ni watu wasiojulikana.

Nne ni wafanyabiashara ambao walizoea kuhujumu uchumi kwa kutengeneza bidhaa bandia, kukwepa kodi, wengi walikamatwa na kukwepa kodi na walikuwa magerezani kwa kuhujumu uchumi

Tano ni matapeli na wapigaji hawa walishazoea kulipwa mabilioni ya senti kwa kuwa na kampuni za mfukoni na walikuwa wakilipwa hata kama hwajafanya kazi.

Kwa ujumla kiongozi alikuwa na maadui wengii sana kwa muda mfupi.

Hivi ndivyo Africa ilivyo.
Umesahau aliyotendea watumishi wa umma
 
kila ninapotaka kuandika kitu najikuta nafuta na kuanza tena kuhusu huyu kiongozi

sijawahi kufaidi chochote katika siku zake za utawala, wala siku za wenzake walipokuwa wanatawala nchi!

kuna kijana wa kigogo mmoja (ni tajiri sana huyu mzee) wakati wa awamu ya nne alisema kitu kwa kijana wangu wa kazi, nilimtazama na kumfikiria kama dakika 5 nikakosa cha kujibu na kufanya. siku hiyo niliona uchungu wa kuwa mwananchi.

huyu kiongozi alivyoingia madarakani, baada ya mwaka, huyu mzee aliwekwa ndani. kuna mambo alikuwa anajihusisha nayo ambayo hayakuwa yamekaa vizuri. na mtaani watu walikuwa wanajua ila wenye dhamana hawakuweza kumfanya chochote! kijana alichanganyikiwa sana, na mambo yake mengi yaliyumba!

mawazo yangu baada ya kuona yanayowezekana kufanyika Tz:

1. wenye pesa na viongozi, msilee watoto kwa maigizo na mazoea, leo mpo, kesho hampo. mtawaachia mizigo vijana wenu ambayo itawapelekea pabaya. msilewe sana pesa ama uongozi, jitambueni na hao vijana watajitambua kutokana na misimamo yenu!

2. jamii wafundisheni vijana waogope na watetemeke wakisikia Polisi/Takukuru/TRA/NSSF n.k hivi vyombo sio rafiki ya watu. hivi vyombo vipo ilikunyoosha wananchi wenye akili potovu. na pia sehemu Tanzania kama nchi kupata mshiko wake, kuachiliaya kodi!

3. tujue kuwa US, UK, Singapore zimeendelea kutokana na faini kali mbali mbali pamoja na ukusanyaji wa kodi.

4. tumkaribishe mwekezaji na mfanyabiashara nchini lakini tusiwakumbatie na kuruhusu mali pamoja na wananchi wetu kuchezewa! marsharti na taratibu zipo wazi. kama watashindwa basi waseme yanayowakwamisha. ila wasimtegemee mtu bali wategemee taasisi kwani somo kuu la leo ni kutokumtegemea mwanadamu kwani taratibu za nchi haziozi ila mwanadamu hutoweka!

nitamkumbuka kwa maudhi, mabaya na mazuri yake, kama tu viongozi wengine. lakini zaidi, kwa yale aliyo tekeleza na kusimamia ambayo yalikuwa yana manufaa kwenye jamii hasa kwa wale wa hali ya chini!

taarifa ilipowafikia wananchi kuwa hatupo naye, namkumbuka mama mmoja kwenye televisheni akiombea usalama wake anapotoka nyumbani na kurudi nyumbani usitoweke na tusirudi nyuma! hii ilinigusa sana.

saa zingine kilicho 'basic' kwako, 'it's not so basic' kwa jirani yako.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kabla huyu mwamba wenu hajaingia madarakani nilikuwa nikienda kumsalimia bibi kule nyanungu kwa kupita mbugani basi ilikuwa nalipa 30000 mpaka Tarime.
Alipoingia tu mwamba garama ikapanda ikafika 50000 eti wanaopita huko wote walipishwe kama watalii Wa ndani.
,utadhani anawakatia majani hao wanyama.kwa hili Mimi nkageuka kuwa adui wake.
Aisee. Pole sana. Wengi wana machungu yao wameamua kukaa kimya tu. Ndiyo maana sherehe ziliibuka mpaka ikabidi wazuie na kulazimisha kuomboleza
 
..Vyama vya siasa hupenda kupenyeza watu wao ktk vyama vya wafanyakazi, wanafunzi, etc etc.

..Sio jambo la ajabu chama cha kijani, au kile kingine, kuwa na interest na uchaguzi wa viongozi wa chama cha wafanyakazi.
Wajiulize kwa nini TLS, TUCTA na vyama vingine vya wafanyakazi na vya kitaaluma huwa vinaingiliwa na vyama vya siasa? Hata chaguzi za vyuo vikuu tu huwa inakuwa hivyo.

Nahisi unajadili na watu wenye uelewa mdogo sana achana nao.
 
Back
Top Bottom