Kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma Makao Makuu, wote imekuwa ni njia moja Dar

Kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma Makao Makuu, wote imekuwa ni njia moja Dar

Mkuu kwa mtazamo wangu mm huyu mama hawezi kua rais bora kabisa kwa kifupi mm smukubali hata kidogo nimejipa mda ili nijirizishe kwanza na utendaji wake.
Akheri yako bado unampa muda; mimi naelekea ukingoni kutegemea lolote la maana kwa nchi yetu katika miaka yake hii minne.
 
Magufuli hayupo tena , cha muhimu ni kuipata katiba mpya, msiongee kama kwamba Magufuli na familia yake ndio walikua katiba ya Nchi, HAPANA, Magufuli alikua kiongozi wa nchi na alishaenda zake, tuliobaki ndio inatupasa kuisaka katiba mpya vinginevyo tuna safari ndefu sana.
Kwani magufuli alikukataza kuitafuta acha uoga
 
Bwana yule alikua anaenda Sana chato mbona mawaziri wake hawakuiga kwenda huko kitovuni?
Si ajabu, baadhi yao (mawaziri), walianza kutafuta viwanja Chato, wakiamini makao makuu yatahamia huko!
Waziri wa utalii huenda hata msingi wa nyumba yake alishajenga huko!
 
Tatizo liko kwa aliyefikiria kuwa Dodoma kuwa Makao makuu.Tangu mwanzo yeye mwenyewe kamalizia miaka yake zaidi ya 20 akiwa Bongo Daslam sasa anakuja jamaa kurupu twendeni Dom.Thubutu.Kukaa Dodom inahitaji Moyo.Hao wabunge wa Dodoma akina Ndugai wikiend wako Dar. Hata Mwendazake siku alizokaa Dodoma ni chache kuliko alizokaa Dar.Kwa ufupi hakuna Mtazania asiyependa kukaa Dar.
Aliyefikiria ni Julius Nyerere waliofuata walikuwa hawana mapenzi na watanzania. Akaja aliyezaliwa huko kijijini akatekeleza, ameondoka bahati mbaya sana na funguo za Ikulu ndio maana kila wakiingia wanaona mauzauza. Wataikwepa Ikuklu ya Chamwino lakini ndiko angalau funguo za kuchonga zinaweza kutengenezwa na kazi ikaendelea. Kaacha barabara nyingi za mitaa iliyokuwa ya kienyeji lakini zimetandikwa barabara za zege (Mfano Mazense, Magomeni, Vingunguti, Kigogo, Sinza, Mwananyamala, Kinondoni nk)
 
Huwa nawashangaa sana watu wanaodai katiba mpyaa...mnashindwa kujua shida iko wap..hata ukiwa na katiba bora kama nn..bila kuwa na watu wanaoiheshimu ni kaz bure..katiba haijindeshi yenyewwwe..wapo watu wanaisimamia hiyo katiba..kama hao watu ni hovyoo baas wataikanyagaa tu hiyo katibaaa...hivyoo kinatakiwa ni mind set za hao watu zibadilike hapo ndipo katiba itasaidia..la sivyo ni kutwanga maji kwenye kinu..
Hii iliyopo tu inasiginwaa mchana kutwaa..
Hizi kelele za katiba ni kutafutia watu ulaji tu ili hiyo katiba wanayoitaka ilazimishe nao wateuliwe kuwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya pia wawe mawaziri hamna kingine na kabisa wapo nje ya uwanja ndio kabisa njaa imewapiga kweli kweli, hizo ni drama tu na kutuvurugia amani yetu tuwaapuuze na tuchape kazi.
 
Hizi kelele za katiba ni kutafutia watu ulaji tu ili hiyo katiba wanayoitaka ilazimishe nao wateuliwe kuwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya pia wawe mawaziri hamna kingine na kabisa wapo nje ya uwanja ndio kabisa njaa imewapiga kweli kweli, hizo ni drama tu na kutuvurugia amani yetu tuwaapuuze na tuchape kazi.

..siyo kweli.

..moja kati ya mapendekezo ya katiba mpya ni kuondolewa kwa nafasi za wakuu wa mikoa na wilaya.
 
Wananchi ndio wenye madaraka yote, ndio wanaowaweka hao viongozi wanaoapa kuisigina katiba, na kwa hiyo wananchi wanao uwezo wa kuwawajibisha.

Hili nalo ni gumu kwako kulielewa?

Kama uingereza hawana Katiba kabisa, lakini wana sheria zinazotungwa na bunge; hizo sheria zinakiukwa na hao viongozi wanaowekwa na wananchi?
Kwani Katiba ni nini, siyo sheria?

Kama "Trump alivunja katiba" jambo ambalo siyo kweli, eleza sasa yupo wapi?

Unatafuta tu njia za ku'justify' uvunjaji wa sheria wa hao unaosema wanaapa kuilinda katiba, halafu wasiwajibishwe!
Unaongea mambo theoretical zaidi ambayo ndiyo mwanzo wa false expectations. Ni kweli wananchi ndio waliowaweka viongozi madarakani, lakini walifanya hivyo wakati wa uchaguzi. Wananchi hawana power ya kumwambia kiongozi kuwa umefanya makosa tunakufukuza kazi na tunaajiri kiongozi mwingine kirahisi namna hiyo. Itabidi wasubiuri uchaguzi mwingine (miaka mitano ijayo).

Uingereza hawana katiba lakini serikali inafuata sheria. Hilo ndilo swala la kujiuliza, je sheria tunazoijiwekea zinafuatwa na serikali? ndiyo maana nikasema katiba ni kitu kimoja, na utekelezaji wake ni kitu tofauti. Usimamizi wa sheria ni kazi ya serikali. Sasa hivi sheria inasema makao makuu ya serikali ni Dodoma, kwa serikali isiitekeleze sheria hiyo kama ilivyo? katiba mpya itasaidia nini kwa serikali kutimiza jukumu lake la kusimamia sheria?

Kwa hiyo wewe hujui kuwa Trump alichochea watu kubomboa ofisi za bunge, ambalo siyo tu kuwa ni kosa la jinai lakini pia ni kinyume katiba ya marekani inayotenganisha Article 1 na Article 2. Vile vile hutambui kuwa wakati wa utawala wa Trump safari zote za jeshi la marekani kuelekea Ujerumani zilikuwa zinalazimishwa kulala Scotland kwenye hotel za Trump ambayo ni kinyume cha Katiba. Vile vile huelewei kuwa Pence alipokwenda safari ya kikazi huko Ireland alilazimika kulala hoteli ya Trump kinyume cha katiba. Kuna msululu mrefu wa mambo ya uvunjaji wa katiba na sheria yaliyofanywa ambayo bado yanashhughulikiwa. Trump aliondolewa madarakani baada ya miaka minne kwa njia ya uchaguzi uliofuata.
 
a hiyo wewe hujui kuwa Trump alichochea watu kubomboa ofisi za bunge, ambalo siyo tu kuwa ni kosa la jinai lakini pia ni kinyume katiba ya marekani inayotenganisha Article 1 na Article 2. Vile vile hutambui kuwa wakati wa utawala wa Trump safari zote za jeshi la marekani kuelekea Ujerumani zilikuwa zinalazimishwa kulala Scotland kwenye hotel za Trump ambayo ni kinyume cha Katiba. Vile vile huelewei kuwa Pence alipokwenda safari ya kikazi huko Ireland alilazimika kulala hoteli ya Trump kinyume cha katiba. Kuna msululu mrefu wa mambo ya uvunjaji wa katiba na sheria yaliyofanywa ambayo bado yanashhughulikiwa. Trump aliondolewa madarakani baada ya miaka minne kwa njia ya uchaguzi uliofuata.
Baada ya kuyaona yote haya, na wananchi wakaona upuuzi wakamwondoa kwenye uongozi, bado huoni kwamba sheria zao zinafanya kazi, ikiwa ni pamoja na katiba yao?
Baada ya kukariri yote hayo aliyokuwa akifanya Trump, bado unashindwa kutambua kwamba alikuwa 'impeached', tena mara mbili?

Katiba yao haiweki madaraka yote kwa mtu huyo mmoja kiasi cha mtu huyo ndiye aamue kila kitu na hawezi kuwajibishwa, hili hulioni? Trump hata leo anaweza kufikishwa mahakamani kwa makosa aliyofanya akiwa rais, hilo halina maana kwako?
Uingereza hawana katiba lakini serikali inafuata sheria. Hilo ndilo swala la kujiuliza, je sheria tunazoijiwekea zinafuatwa na serikali? ndiyo maana nikasema katiba ni kitu kimoja, na utekelezaji wake ni kitu tofauti. Usimamizi wa sheria ni kazi ya serikali.
Sasa angalia mfano kama huu ulioweka hapa, sijui unataka kueleza kitu gani katika kutetea hoja yako, kama siyo kuipinga moja kwa moja bila kutambua kuwa unajipinga mwenyewe.
Huko Uingereza kuna kitu gani kinachowafanya viongozi wa huko watii sheria wanazojitungia, ambacho sisi hapa hatuna?
Una maana kwa vile hapa viongozi hawafuati hizo sheria zinazotungwa, tuache kuhimiza sheria zisifuatwe na kutafuta njia za kuwafanya wafuate hizo sheria, ikiwa ni pamoja na kuondoa udhaifu uliomo kwenye hizo sheria ili ziwabane zaidi wasiweze kuzikiuka?
 
Labda wanamjaribu mama, au dodoma hawapapendi.
 
Yaani kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma makao makuu - wote imekuwa ni njia moko Dar - Magari yenye bendera za Mawaziri na Watendaji wengine wa Serikali wamerudi Dar kwa kasi kubwa mno. Yaani haipiti saa tatu ukiwa Morogoro kila siku unaona gari la kiongizo liko spidi kutoka au kwenda Dar na Dodoma. Matrafiki siku hizi hawana hata mpango wa kuyasimamisha tena. Wamechoka wanaangalia tu.

Gharama hizo za magari kukimbia njia ya Dar Dom ninaona ni kuwa mno kiasi kwamba angekuwepo Mwendazake isingekuwa hivi - wengine hadi juzi wamediriki kuamua kurudisha Ofisi zao Dar - Waziri yule kaitoa Ofisi Moro kuipeleka Dar badala ya Dodoma. Ninamkumbuka sana Mwendazake jamani!

Hivi leo hii tukiitisha roll call ya Viongozi Dodoma ni Mawaziri na Wanaibu Waziri na Makatibu Wakuu wangapi watakuwepo Dodoma leo?
Kumbuka juzi tu karibu wote walikuwa Dar kwa Sabasaba - leo Ijumaa tayari wanne wamepanga ndege na kuna magari zaidi ya 6 yanaelekea Dar now bila hata sababu yeyote. Pumzika kwa Amani Mwendazake! Tumekumiss sana sana!
We kiboko kweli, umemmiss nani!
Mtu anakufanya uishi kama mtumwa ndani ya nchi yako mwenyewe, wewe unammiss! Fimbo ni kwa mgongo wa mpumbavu"

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Dar imeshakuwa na watu wengi sana kiasi kuwa shughuli za serikali zinakuwa ni kero kwa raia. fikiria unatoka nyumbani kwenda mishe mishe zako, unakuta traffic wamefunga barabara kwa sababu kuna msafara wa rais. Halafu hujafikia mtaa wa pili unakuta barabara zimefungwa kuwa kuna msafara wa makamu wa rais: ni kero sana. Ndiyo maana nchi nyingi sana zilizojengwa miaka ya karibuni hutenga eneo la makao makuu liwe ni tofauati na vitovu vya biashara. Ni nchi za zamani sana ambazo makao makuu ya mfale yalegeuka kuwa vitovu vya biashara na ikabaki hivyo, kwa mfano, Tokyo, London, na nchi kadhaa za ulaya. Na hata hivyo katika miji hiyo bado sehemu za serikali zimetengwa sana na sehemu za biashara.
Asante elimu nzuri mkuu.
 
Hapo sasa ndo mana nikasema huwez elewa nilichoandika..
Unasema wananchi hawana utambuzi wakati mm nazungumzia utambuzi kwa wenye madaraka..Farewell bro...
 
Viongozi bakini huko huko Dodoma huku Dar mnafuata nini??
 
Dar imeshakuwa na watu wengi sana kiasi kuwa shughuli za serikali zinakuwa ni kero kwa raia. fikiria unatoka nyumbani kwenda mishe mishe zako, unakuta traffic wamefunga barabara kwa sababu kuna msafara wa rais. Halafu hujafikia mtaa wa pili unakuta barabara zimefungwa kuwa kuna msafara wa makamu wa rais: ni kero sana. Ndiyo maana nchi nyingi sana zilizojengwa miaka ya karibuni hutenga eneo la makao makuu liwe ni tofauati na vitovu vya biashara. Ni nchi za zamani sana ambazo makao makuu ya mfale yalegeuka kuwa vitovu vya biashara na ikabaki hivyo, kwa mfano, Tokyo, London, na nchi kadhaa za ulaya. Na hata hivyo katika miji hiyo bado sehemu za serikali zimetengwa sana na sehemu za biashara.
Kweli ee!
 
Yaani kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma makao makuu - wote imekuwa ni njia moko Dar - Magari yenye bendera za Mawaziri na Watendaji wengine wa Serikali wamerudi Dar kwa kasi kubwa mno. Yaani haipiti saa tatu ukiwa Morogoro kila siku unaona gari la kiongizo liko spidi kutoka au kwenda Dar na Dodoma. Matrafiki siku hizi hawana hata mpango wa kuyasimamisha tena. Wamechoka wanaangalia tu.

Gharama hizo za magari kukimbia njia ya Dar Dom ninaona ni kuwa mno kiasi kwamba angekuwepo Mwendazake isingekuwa hivi - wengine hadi juzi wamediriki kuamua kurudisha Ofisi zao Dar - Waziri yule kaitoa Ofisi Moro kuipeleka Dar badala ya Dodoma. Ninamkumbuka sana Mwendazake jamani!

Hivi leo hii tukiitisha roll call ya Viongozi Dodoma ni Mawaziri na Wanaibu Waziri na Makatibu Wakuu wangapi watakuwepo Dodoma leo?
Kumbuka juzi tu karibu wote walikuwa Dar kwa Sabasaba - leo Ijumaa tayari wanne wamepanga ndege na kuna magari zaidi ya 6 yanaelekea Dar now bila hata sababu yeyote. Pumzika kwa Amani Mwendazake! Tumekumiss sana sana!
Sasha miaka yake 5 kisha itakua vizuri awapishe wanamapinduzi kuendesha nchi kimagufuli. Bila hivyo mafanikio yote yatapotea.
 
Uamuzi wa kuhamia Dodoma ulifanyuka bila upembuzi yakinifu.
Ila sasa ndio tushahamia. Vigogo wasiturudishe dar. Ni suala la rais tu kua mkali na kua mfano yeye mwenyewe.
 
Back
Top Bottom