Kwa sisi wanaume tuliooa, ukiacha tendo la ndoa, mke wako anakusaidia kwa lipi?

Kwa sisi wanaume tuliooa, ukiacha tendo la ndoa, mke wako anakusaidia kwa lipi?

Ndipo swali lilipo; kwa sababu kwa nyakati hizi, nje ya tendo la ndoa wengi wao hawana msaada mwingine.
Ukimpata 'wautulie' waweza pata nanufaa ya kusaidiwa kazi ndogo ndogo, msaada pale unapougua ama matatizo mengine ya kilimwengu, kukulelea familia nk nk.

Lakini ukipata mwanamke wa hovyo, hakuna lolote la maana analokusaidia, sana sana ni kukuvuruga saikolojia na kukubebesha majukumu yasiyostahili kama usingelikuwa naye.

Maana hata tendo la ndoa lenyewe si msaada wala manufaa.
 
Tutumie njia zipi kupata mke mkeo? Kwa sababu najua hapo ndipo kwenye shida

Ni swala la kuomba Mungu tu akupe wa kufana nawe.

Ndoa za sasa ni changamoto.

Wengi wanaishi na wake zao lakini hawajui behind the scene mauchafu wanayoyafanya siku wakigundua ndipo matatizo yanapoanza...kuomba Mungu kupata mwanamke aliyetulia ,mwanamke akitulia na kuwa MKE MKEO na mwanaume naye anatulia na ndiyo maana vitabu vya dini vinasema Mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe so anayevunja ndoa siku zote ni mwanamke ,UKIONDA NDOA IMEVUNJIKA ujue aliyeivunja ni mwanamke.
 
Wanaume wengi hufa mapema sababu ya direct au indirect pressure toka kwa wake zao. Mwanaume akipata maendeleo kinachofuata ni ndoa ilihali mwanamke akifanikiwa kinachofuata ni talaka. Wanawake wengi wakiwa huru kiuchumi huwa hawana time na ndoa.
Mwanamke akipata financial freedom lakwanza ni kuondokana na mwanaume maishani mwake. Hatari hawa viumbe. Ni kuwagegeda tuu
 
Swali zuri sana..... nami naomba kujibu kama ifuatavyo, ndoa sio tendo la ndoa tu, sasa ukiacha tendo la ndoa yapo yafuatayo:

1. Ulinzi wa mali zako, mwanamke aliye mke wako atajitahidi kulinda mali zako huku akifikiria kuna kesho maana yake anawaza future ya maisha yenu, wengi wakiambiwa kuna kesho huwa wanawaza labda kufa, hata usipokuwa kesho inakuja.

2. Anakupatia watoto, hii unaweza sema aah! nitazaa huko nje, mke akizaa anakuwa na kiu ya kuongeza uzao wako na anawatunza watoto kwa mapenzi yote kwa sababu anajua mume wake uko pembeni, kumbuka kuzaa sio kazi, kazi kulea mwana.

3. Mwanamke ataunganisha familia, kiuhalisia kuna familia ndugu hawaelewani, uwepo wa mke anakuwa mtu kati(mediator) na hapa upate mke sahihi wengine wanakuja kugombanisha.


4. Mke ni msaidizi wa mwanaume, na hapa sio usaidizi wa kazi za ndani noo, ni kumsaidia mwanaume kutimiza malengo yake, kumbuka malengo ya mwanaume ndo huwa malengo na msimamo wa familia, mwanamke hawezi kuja na ya kwake lazima atasimama na kumsupport mume, kumbuka hakuna mwanamke atapenda kusemwa kwamba hapo shost ulikosea kuchagua, kwahiyo hata kama mwanaume hayuko njema kiuchumi, atasaidiwa, tuna mifano kuna wanaume hata mahari walisaidiwa na wake zao.

5. Mke anakuletea Heshima katika jamii, sio heshima tu na kuaminika, kuna nyumba ukienda kupanga hujaoa au kuolewa huruhusiwi kwanini unaonekana huna heshima, huwezi kuwa Raisi wa nchi hii hujaoa, ukiachana Katoliki mengine huwezi kuwa Askofu hujaoa: Kiufupi kama haujaoa au kuolewa unawekwa kundi la wahuni, kama ndugu zangu kataa ndoa
Umeandika mambo mazuri lakini ni irrelevant na characters za wanawake wa kisasa
 
Wengi tulikuwa tunatamani kuoa, tukiamini baada ya kuoa maisha yatakuwa full starehe na hakutakuwa na migogoro.

Wapo waliofanikiwa kwa kupata watu sahihi, mpaka wakikaribia kuzeeka sura zao zinakuwa zinafanana.

Pia wapo waliokosa watu sahihi, na kujikuta wameingia kwenye ndoa yenye changamoto; ambao ukikutana nao njiani, sura zao zimekuwa nzito na zimejaa majukumu mazito na ghadhabu za kuingia kwenye ndoa.

Na wengi tunaoteseka kwenye hizi ndoa ni wanaume, sema huwa tunavumilia ndio maana ata takwimu zinaonyesha wanaume wanakufa haraka kuliko wanawake.

Sasa tujiulize swali; Kwa sisi wanaume tulio oa, ukiacha tendo la ndoa, mke wako anakusaidia kwa lipi?​
Hakuna kitu, maana, kwanza wengine tunaishi mbali, mkoa mwingine, hiyo huduma tunapata kwa vitoto vya 2000,kitu pekee ni kupikia na kutunza watoto, na kuhudhulia jumuia,
Thank God, kazi yangu inaniweka bize, na ni kitu ninachokipenda, kama kula wali kuku,
Ndoa za siku hz, headache tupu, mabinti wanaolewa, kusafisha nyota,basi, maana, kwao,tendo la ndoa, limeishawakinai! Wanapigwa pipe tangu primary! Hakuna kitu
 
Hakuna kitu, maana, kwanza wengine tunaishi mbali, mkoa mwingine, hiyo huduma tunapata kwa vitoto vya 2000,kitu pekee ni kupikia na kutunza watoto, na kuhudhulia jumuia,
Thank God, kazi yangu inaniweka bize, na ni kitu ninachokipenda, kama kula wali kuku,
Ndoa za siku hz, headache tupu, mabinti wanaolewa, kusafisha nyota,basi, maana, kwao,tendo la ndoa, limeishawakinai! Wanapigwa pipe tangu primary! Hakuna kitu
Hii inawezekana labda ni kutokumpata mtu sahihi
 
Kabla hujaoa either umempata mjini au kijini,awe na mali asiwe na mali,hakimisha IQ yake ipo vzr kuna watu darasa la 7 lkn wewe wa chuo unaweza usiwe namawazo km yake sometimes becomes,huyo ndio wakuoa
Asilimia kubwa, wengi hukimbilia kuoa kutokana na muonekano wa mtu; je uko tayari kuoa mtu ambaye hajakuvutia ila ana IQ kubwa?
 
Back
Top Bottom