Kwa vichwa vilivyopo Wizara ya Fedha sasa, Tanzania itakuwa mbali sana kiuchumi kufikia 2030

Kwa vichwa vilivyopo Wizara ya Fedha sasa, Tanzania itakuwa mbali sana kiuchumi kufikia 2030

Nimefanya utafiti kidogo juu ya habari mbalimbali zinazoandikwa juu ya Tanzania kiuchumi kwa kipindi cha miezi 3 sasa. Kusema kweli hakuna habari mbaya utakayoikuta juu ya Tanzania kiuchumi. Wachambuzi wote wa nje na ndani ya Afrika wanaisema vizuri sana Tanzania. Sio kwenye uwekezaji sio kwenye ukuaji wa uchumi.

Nikaja eneo la pili kujiuliza kwa nini haya yanatokea sasa? Nimekuja kugundua pale Wizara ya Fedha, Rais kaweka watu makini sana ambao kwa maoni yangu bila shaka hawa ndo wanasababisha haya yote yatokee

Rished Bade, Lawrence Mafuru na sasa Nehemia Mchechu watakuja vikwa nishani kama sio 2029 basi 2030.

Wanafanya Mwigulu Nchemba aonekane Waziri wa Fedha mahiri sana kwa Afrika Mashariki na kati kwa sasa.

Walioshauri hawa financial gurus wawekwe kwenye mfumo wa serikali wa uchumi wanastahili pongezi sana.

Kwa hali hii, kuna kila sababu ya kusema Samia anaweza kuja kuwa Rais bora kabisa kuwahi kutokea Tanzania. Hali ya kiuchumi ya nchi inaenda vizuri sana kwa kweli!
Safi kabisa sio yule paka aliyekuwa anatujazia wasukumaa
 
Kwani wewe unaonaje Mzee? Mwigulu ndio Waziri Bora wa Uchumi kuwahi kutokea.


Usipende kunakili nakili kila maandishi na kuyaleta humu kama zuzu

Serikali kuongeza bajeti kwa 7% ama hata 50% sio ishu, mfano, bajeti ya mwaka jana uliona ulikuaje, makusanyo halisi yalikuaje? I mean utekelezaji wa bajeti ulifikia 100%? Kama hakuna kuna tija gani kuongeza 7% kama ya mwaka jana, mwaka juzi, mwaka mwingine ule utekelezaji wa bajeti haukufika hata 80%?

Mtu mwenye akili unapaswa kujiuliza hivyo sio unanakiri tu maandishi na kuyaleta humu.
 
Basi sawa
1575C3A9-DB19-4EF4-8E69-95CD9C0337DE.jpeg
 
Back
Top Bottom