Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Ardhi ni Mali ya umma, na Rais ndo amekabidhiwa kama msimamizi thus wote tumekodishiwa kutumia tena kwa muda maalum. Ndo mana kuna hati za miaka 33, 99 ndo mana tunalipa kodi. Ukipata muda pitia sheria ya, Ardhi ya mwaka 1999 na maboresho yake.
Shukrani sana The Broker kwa ufafanuzi,
Nitaipitia hiyo sheria
 
Kinacholipiwa kodi ni UMILIKI; OWNERSHIP. It is entitled to you and not to someone else. Kikishakuwa ni chako mwingine hana fursa nacho sharti ukilipie. Hiyo ndio kanuni.

Na ndio maana maeneo ya public hayalipiwi kwa sababu ni free to everybody kama ilivyo hewa.
Hapa sasa umeeleweka,
Ardhi ikishakua yangu inakua yangu hakuna mtu ataweza kuimiliki tena, kwa hiyo nitalipia ule umiliki wangu,
Ndio maana nikitaka kuuza nitauza umiliki wangu kwa mtu mwingine,

Safii
 
Kodi ya pango la ardhi inatozwa ili wewe mmiliki upate ulinzi wa dola katika kipande chako za ardhi. Bila ulinzi wa dola mtu mwingine ye yote mwenye nguvu za misuli au fedha anaweza kuvamia eneo lako na kukunyang'anya na ukakosa wa kukusaidia.

Hivyo serikali inatoza kodi ili iendelee kukulindia kipande chako unachomiliki. Na kwa kufanya hivyo kupunguza migogoro ambayo ingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.
Sijui unaongea kitu gani! Serikali kwamba imeweka dola kulinda eneo langu!
Kazi ya kupewa title ( hati ya kiwanja nini?)
Hati maana yake ni ulinzi wa kisheria katika kipande cha ardhi!

Sasa kodi ya ardhi inalindaje kwa dola mkuu!
Tuache majibu mepesi ndugu!

Dola ni mamlaka in general kwa RAIA na Mali zao! Tunalipa kodi kwenye manunuzi ya kila siku ya Mali!

Ardhi ni urithi tunarithishana kwa kumilikishana! Sasa kwanini tulipie kodi kila mwaka ardhi ambayo hatujatia mkono wa kibinadam kuifinyanga?
 
Ndio ni kwa mujibu wa hao wakusanya kodi ndio waliitunga hiyo sheria,lakini bado swali la mtoa mada litabaki palepale ni kwa nini iwe hivyo wakati ardhi yote iliumbwa na Mungu ili binadamu waitumie?
Mungu ni suala la dini, Serikali haina mambo ya dini ina Jeshi.
 
Ndugu mwana JF
Ukitaka kujuwa serikali nini tokewa na mambo haya hapa.

Shamba lako likibainika lina-Alimasi linakuwa mali ya Serikali.
Ila shamba lako likibainika lina-Bangi hiyo ni mali yako mkuu! 😀
Naomba niishie hapa siwezi kuendelea hadi aje mwanasheria wangu!
 
Kwa nini tukodishwe na Serikali wakati Ardhi tumeikuta na Kama ilivyo hewa ndio urithi wa mwanadamu?
Kama tunakiri kuwa wakoloni walitwaa ardhi zetu, wakagawa vipande na kuweka Serikali zao, zikajiendesha kwa kodi za dhulma kama hii, kwa nini Serekali yetu inaendeleza ukoloni ule ule kwa watu wake?
Suala la kodi zipi ziwepo na zipi zisiwepo ni suala la sheria. Hatuna kodi ya hewa ila tulikuwa na kodi ya kichwa kilichobeba pua na mdomo inayovuta hewa, tukaifuta. Hata ya ardhi tunaweza futa.

Ila ili ifutwe mara zote huwa kuna mbadala. Bajeti yake itafidiwa na nini? Serikali haijali sana jina la kodi, inajali kiasi kinachoingia. Ikipata mbadala wa kodi ya ardhi CHAP CHAP TAYARI WANASIASA WATAPATA MTAJI WA KUOMBEA KURA NA MADARAKA. VICHWA VYA HABARI VITAKUWA: " SERIKALI CHINI YA RAISI........YAFUTA KODI YA ARDHI, RAISI ASEMA NI UONEVU KWANI ARDHI IMETOKA KWA MUNGU"
 
Mungu ni Mungu na dini ni dini.
Kwani kuna mtu ambaye hajui kwamba ardhi iliumbwa na Mungu?bila kujali dini yake ni ipi
Ndo tunarudi pale pale kuwa huwezi sema serikali ifute hiyo kodi sababu ardhi tumepewa bure na Mungu.

Serikali inataka mapato na ili ufute hayo mapato unahitaji mbadala wa hayo mapato. Mbadala ukipatikana haraka haraka wanasiasa utawaona majukwaani wakitaka kodi iondolewe ili waitumie hiyo kama mtaji wa siasa.

Kinyume na hapo Ukija na stori za Mungu katupa ardhi jibu ni jepesi tu serikali haina dini.
 
Ndo tunarudi pale pale kuwa huwezi sema serikali ifute hiyo kodi sababu ardhi tumepewa bure na Mungu.

Serikali inataka mapato na ili ufute hayo mapato unahitaji mbadala wa hayo mapato. Ukija na stori za Mungu jibu ni jepesi tu serikali haina dini.
Ungesema serikali hawana Mungu labda ila ukisema hawana dini bado wanaye Mungu ambaye anawawezesha kuamka kila siku asubuhi na kwenda kutunga sheria.
 
Ndiyo mana wana jeuri ya kununua magari ya kifahari na likipata jeraha tu wanauziana wenywewe,
Unapanga frem na Bado unaambiwa
ulipe tena Kodi ya pango, hiyo ni tofauti n tra na ukienda manispa unakutana na Kodi ukirudi mtahani kuna Kodi tena ya taka na ulinzi Bado mitaro unasafisha!
Alafu unaambiwa vijana mkaajiajiri wakati ukifungua duka hata ujaanza tu unakadiriwa Kodi!
 
Mungu ni Mungu na dini ni dini.
Kwani kuna mtu ambaye hajui kwamba ardhi iliumbwa na Mungu?bila kujali dini yake ni ipi
Hata kama hana dini! Hiyo ardhi akiiona anafikili iliagizwa ulaya? Ardhi ni urithi tumerithishwa ili tuwarithishe wengine kwa kupeana fidia! Ni kitu ambacho kipo pasipo hiari yetu!

Ardhi ni ya wote, usipotaka utaikanyaga, utailima, utaivuna na mavumbini utarudi!
Sasa huyu anaetoza kodi ya ardhi hana aibu hata kidogo
 
Ungesema serikali hawana Mungu labda ila ukisema hawana dini bado wanaye Mungu ambaye anawawezesha kuamka kila siku asubuhi na kwenda kutunga sheria.
Hapo unaingiza kwenye imani yako sasa boss.
 
Ndiyo mana wana jeuri ya kununua magari ya kifahari na likipata jeraha tu wanauziana wenywewe,
Unapanga frem na Bado unaambiwa
ulipe tena Kodi ya pango, hiyo ni tofauti n tra na ukienda manispa unakutana na Kodi ukirudi mtahani kuna Kodi tena ya taka na ulinzi Bado mitaro unasafisha!
Alafu unaambiwa vijana mkaajiajiri wakati ukifungua duka hata ujaanza tu unakadiriwa Kodi!
Broh mi nasema maisha ni mepesi sana lakini kuna watu wanatuwangia! Makodi ya ajabu hata kwenye vitu vya bure
 
Ana changanya! Hakuna anaepinga kodi! Tatizo unachukua kodi kwenye nini!
Mfano kodi ya mifugo, kodi ya ardhi, kodi ya jengo zote hizi hazina tija kabisa ni wizi!

Already existing on its nature! Kwanini uombe kodi!
Zamani kulikuwa na kodi ya kichwa! Vyote hivi ilikuwa ni unyama wa hali ya juuu! VIFUTWE VYOTE
Wala sijachanganya mada,kuna mtu nilikuwa nimemjibu hiyo comment,aliniambia kuwa mimi sijui umuhimu wa kodi wala maana ya kodi ndio nikamjibu yeye anayejua umuhimu wa kodi ameona wapi hiyo kodi ikifanya kazi ipasavyo
 
Hata kama hana dini! Hiyo ardhi akiiona anafikili iliagizwa ulaya? Ardhi ni urithi tumerithishwa ili tuwarithishe wengine kwa kupeana fidia! Ni kitu ambacho kipo pasipo hiari yetu!

Ardhi ni ya wote, usipotaka utaikanyaga, utailima, utaivuna na mavumbini utarudi!
Sasa huyu anaetoza kodi ya ardhi hana aibu hata kidogo
Boss, kodi ya ardhi ipo kisheria kupitia bunge lako tukufu. Hakuna aibu hapo kuna sheria. Kama hatuitaki ni suala la kushinikiza mbadala bungeni pawepo mswada sheria ibadilike.
 
Hapo unaingiza kwenye imani yako sasa boss.
Wala sijataja dini yangu hapo,niko neutral.
Labda uniambie kwamba kuna mtu yeye anaamini uhai amejipa mwenyewe,na ardhi pia kuna watu wameitengeneza.
 
Back
Top Bottom