Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Watu sijui kama wanaelewa haki ya lazima na wajibu wa lazima!

Kuna vitu ukizaliwa tu tayali unahaki ya kuvitumia bure ikiwemo ardhi na hewa!
Mengine ya kuumba ni wajibu ambayo tunalipishwa kodi kwayo!
Ardhi ni bure, kwann niilipie kodi?
... hewa haina mmiliki na kuitumia wewe popote ulipo haimnyimi mwingine fursa ya kuitumia.

Kinyume chake, ardhi ukishamiliki kipande ina-exclude wengine wote fursa ya kutumia the same kipande. Hiyo ndio tofauti ya ardhi na hewa.
 
Mada nzuri sana na nimependa wachagiaji wamechangia kwa busara bila matusi wala lugha za kukera,

Nimebaki njia panda kulingana na maoni ya wadau,
1. Ardhi isilipiwe sababu tumeikuta ni kitu cha Asili kama ambavyo hatulipii hewa

2. Ardhi inalipiwa sababu umekua mmiliki na ukiwa mmiliki ni wazi inakuletea faida na chochote kikupacho faida basi kilipiwe kodi,

Lakini kwanini nilipie ardhi kila mwaka wakati kinachonipa faida ni jengo na tayari jengo nalipia kila mwezi?
... sio kweli kwamba thamani ya ardhi ni majengo yaliyopo juu yake tu! Kile kitendo cha kui-own hata kama hujaweka chochote juu yake ni faida fulani kwako. Kama unaona haina faida iachie.
 
Mbona hewa hatuuziani lakini hakuna vurugu ushawahi kusikia sehemu watu 100 wanagombaniana kuvuta hewa basi Kama hewa kaumba Mungu hatugombaniani kila mtu ni yeye tu na ukubwa wa pua yake kwanini hio ardhi kuwe na kuuziana na umiliki

Hili la kununua mbona huja hoji unahoji la kodi
Hewa haionekani kwa macho ndugu,laiti hewa ingekuwa ina umbo maalumu,ina rangi na inakamatila wababe wangekuwa wanaiwahi na kuiweka ndani kwao
 
Mambo mengine mtu ukiwaza unaona kabisa maisha ni mepesi kimtindo lakini kuna baadhi ya wanadam wenye dhamana ya uongozi ndiyo waliyoyafanya maisha yawe magumu!

Tumeumbwa ardhi ilikuwapo, tumepata Uhuru, ardhi ilikuwapo milele hadi milele yote!

Sasa kwanini tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati tayali ipo BURE?
Huduma zingine za kijamii tunazolipia naelewa ni sawa zinazalishwa viwandani hivyo ni mhimu kulipia!
Sasa hili la kodi ya pango ya ardhi kwanini tulipie wakati tumekuja duniani ili tuishi kwenye ardhi halisi BURE?
yaani kwa lugha nyepesi Ardhi ipo kundi moja na hewa! Kama tunalipia kodi ya ardhi kwanini tusilipie na kodi ya hewa?

Naomba kueleweshwa! Vinginevyo naomba serikali ifute hii TOZO ya ARDHI ya ardhi mara moja!r
Ardhi Haipaswi kabisa kutozwa kodi TUMEPEWA BURE ! WACHA TUISHI NAYO BURE!
Umetafakari vyema, hata mimi pia niliwahi kuwaza hivyo hivyo kwann tulipie kodi ya ardhi? Nadhani hata kama serikali inawajibu wa kukusanya kodi katika kila nyanja basi kodi ya ardhi ingeondolewa kwa wale wanaoitumia kwa ajili ya makazi tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hewa haionekani kwa macho ndugu,laiti hewa ingekuwa ina umbo maalumu,ina rangi na inakamatila wababe wangekuwa wanaiwahi na kuiweka ndani kwao
Na kwasababu hio pia usiweke hewa na ardhi kwenye kundi moja kisa zimeumbwa na Mungu ni asili Kama ulivyokuwa unasema..... Ardhi ni kitu Tangible kina shikika, inakalika, inaonekana, ina milikika na kutathminika lazima iwe tofauti na kitu Kama hewa hivyo usisashangae kukunulika na kulipiwa kodi
 
NA kwanini tunainunua wakati tumeikuta bure?
Wakati vitu vingi thamani ina-depreciate, ardhi always inaongezeka thamani. Ukijua maana ya kauli hiyo ambayo ni sahihi huwezi kutumia neno BURE kwa ardhi.
 
Wakati vitu vingi thamani ina-depreciate, ardhi always inaongezeka thamani. Ukijua maana ya kauli hiyo ambayo ni sahihi huwezi kutumia neno BURE kwa ardhi.
concept ni Nani ana mamlaka ya kuiuza ardhi tuliyoikuta, anayeuza aliitengeneza? Kama unaweza kununua kitu kilichoumbwa bure basi kilipie na kodi
 
concept ni Nani ana mamlaka ya kuiuza ardhi tuliyoikuta, anayeuza aliitengeneza? Kama unaweza kununua kitu kilichoumbwa bure basi kilipie na kodi
... kama concept ndio hiyo basi everywhere pawe free for everybody which is not the case kama baadhi wanavyojaribu kuilinganisha ardhi na hewa.

Kitu kikishakuwa na ownership ambayo inamnyima fursa mwingine kuki-own; lazima kilipiwe kodi.
 
Mambo mengine mtu ukiwaza unaona kabisa maisha ni mepesi kimtindo lakini kuna baadhi ya wanadam wenye dhamana ya uongozi ndiyo waliyoyafanya maisha yawe magumu!

Tumeumbwa ardhi ilikuwapo, tumepata Uhuru, ardhi ilikuwapo milele hadi milele yote!

Sasa kwanini tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati tayali ipo BURE?
Huduma zingine za kijamii tunazolipia naelewa ni sawa zinazalishwa viwandani hivyo ni mhimu kulipia!
Sasa hili la kodi ya pango ya ardhi kwanini tulipie wakati tumekuja duniani ili tuishi kwenye ardhi halisi BURE?
yaani kwa lugha nyepesi Ardhi ipo kundi moja na hewa! Kama tunalipia kodi ya ardhi kwanini tusilipie na kodi ya hewa?

Naomba kueleweshwa! Vinginevyo naomba serikali ifute hii TOZO ya ARDHI ya ardhi mara moja!r
Ardhi Haipaswi kabisa kutozwa kodi TUMEPEWA BURE ! WACHA TUISHI NAYO BURE!

Haya wataitoa kodi ya pango, makodi mengine je!!!! Hii ni dhulma ya wazi kabisa, aise ni wachache sana wataingia peponi

 
Mambo mengine mtu ukiwaza unaona kabisa maisha ni mepesi kimtindo lakini kuna baadhi ya wanadam wenye dhamana ya uongozi ndiyo waliyoyafanya maisha yawe magumu!

Tumeumbwa ardhi ilikuwapo, tumepata Uhuru, ardhi ilikuwapo milele hadi milele yote!

Sasa kwanini tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati tayali ipo BURE?
Huduma zingine za kijamii tunazolipia naelewa ni sawa zinazalishwa viwandani hivyo ni mhimu kulipia!
Sasa hili la kodi ya pango ya ardhi kwanini tulipie wakati tumekuja duniani ili tuishi kwenye ardhi halisi BURE?
yaani kwa lugha nyepesi Ardhi ipo kundi moja na hewa! Kama tunalipia kodi ya ardhi kwanini tusilipie na kodi ya hewa?

Naomba kueleweshwa! Vinginevyo naomba serikali ifute hii TOZO ya ARDHI ya ardhi mara moja!r
Ardhi Haipaswi kabisa kutozwa kodi TUMEPEWA BURE ! WACHA TUISHI NAYO BURE!
Duh kama ardhi ingekuwa haina kodi, saivi tusingerithi chochote , manake kila mtu angekuwa ameshajikatia zake kilomita za mraba 10,000 akajimilikisha , yaani kusingekuwa na ardhi yoyote iko tupu.
 
Duh kama ardhi ingekuwa haina kodi, saivi tusingerithi chochote , manake kila mtu angekuwa ameshajikatia zake kilomita za mraba 10,000 akajimilikisha , yaani kusingekuwa na ardhi yoyote iko tupu.
Point! Kodi inasaidia pia kupunguza walafi wa ardhi.
 
1.Kwa nini mfalme atoze kodi ya pango la ardhi wakati ardhi huyo mfalme ameikuta?
2. Mfalme ni binadamu au taasisi aliyoiunda ambayo imepewa ardhi na mungu kama ilivyo kwa wananchi wake, kwanini mfalme atoze kodi kwenye ardhi ambayo wote tumeipata bure?.

Kwa hiyo uelewa wako ni kwamba ardhi haina thamani hivyo ni ya buree!?
 
Ushuru wa magari n.k

Kodi za kipumbafu zisizo na maana mpaka stand za mabasi tunalipishwa watembea kwa miguu, magari n.k

Kodi za mapango, viwanda na manyumba dah watatumaliza aise
 
Duh kama ardhi ingekuwa haina kodi, saivi tusingerithi chochote , manake kila mtu angekuwa ameshajikatia zake kilomita za mraba 10,000 akajimilikisha , yaani kusingekuwa na ardhi yoyote iko tupu.

Uko sahihi kabisa mkuu. Kenya na Zimbabwe ni mifano halisi. Mfano Kenya, akina Kenyatta na wazungu wanamiliki wilaya kadhaa.
 
Ngoja tusubiri ufafanuzi kutoka kwa wasomi
Ardhi ni Mali ya umma, na Rais ndo amekabidhiwa kama msimamizi thus wote tumekodishiwa kutumia tena kwa muda maalum. Ndo mana kuna hati za miaka 33, 99 ndo mana tunalipa kodi. Ukipata muda pitia sheria ya, Ardhi ya mwaka 1999 na maboresho yake.
 
... wewe sasa una-diverge; hoja hapa ni sahihi kulipa kodi ya ardhi? Kwamba kuna misuse ya kodi hiyo ni topic nyingine kabisa! Let's be focused vinginevyo mjadala huu utakuwa hauna mwelekeo unaoeleweka.
Ana changanya! Hakuna anaepinga kodi! Tatizo unachukua kodi kwenye nini!
Mfano kodi ya mifugo, kodi ya ardhi, kodi ya jengo zote hizi hazina tija kabisa ni wizi!

Already existing on its nature! Kwanini uombe kodi!
Zamani kulikuwa na kodi ya kichwa! Vyote hivi ilikuwa ni unyama wa hali ya juuu! VIFUTWE VYOTE
 
Mfumo wa dunia wa Kiutawala, wanachuma mpk kwenye kazi ya Uumbaji wa Mungu.
Sheria za kidunia, Ardhi ni mali ya Serikali pamoja na vyote vilivyopo chini na juu yake isipokuwa bhangi
Quid plantue solo solo cediit
 
Back
Top Bottom