Kwanini Kikwete hakumshauri Samia amteue Prof. Mwandosya kuwa Makamu wake wa Rais?

Kwanini Kikwete hakumshauri Samia amteue Prof. Mwandosya kuwa Makamu wake wa Rais?

Wanyakyusa wako blessed sana and very wise. Ukigombna na mnyakyusa basi jua wewe ndio mkorofi
Mkuu unaonekana hujapambana na Wanyakyusa wa Kyela unawasema Wanyakyusa wa Tukuyu! Tukiwa shuleni mgomo ulikuwa unaanzishwa na Wanyakyusa wa Kyela. Wakisema Aiseeeee, ujue mgomo unaanza!😅😅😅

By the way, Prof. Mwandosya ni Mnyakyusa wa Tukuyu, na Dr. Mwakyembe Mnyakyusa wa Kyela. Unaona tofauti eeh?
 
Mkuu unaonekana hujapambana na Wanyakyusa wa Kyela unawasema Wanyakyusa wa Tukuyu! Tukiwa shuleni mgomo ulikuwa unaanzishwa na Wanyakyusa wa Kyela. Wakisema Aiseeeee, ujue mgomo unaanza!😅😅😅

By the way, Prof. Mwandosya ni Mnyakyusa wa Tukuyu, na Dr. Mwakyembe Mnyakyusa wa Kyela. Unaona tofauti eeh?
John Mwakangale aliyetajwa kwenye Long Walk to Freedom alikuwa ni wa wapi?
 
Mwandosya na ujeuri wake, kiburi na Kujifanya ana akili nani amuweke?

Yule ni Mr.Haambiliki angemsumbua Rais..
Hapana, kwa sababu sio yeye ambae angekuwa anaambiwa bali yeye ambae anamwambia Samia, na Samia angekuwa na uhuru na uwezo wa kukubali anachoambiwa au kukataa
 
Lakini kama una habari za ndani utakumbuka kwamba climax ya yote ilikuwa ni Prof. Mwandosya kuamrisha meli iliyoleta mafuta machafu ya TIPER iondoke nchini ndani ya masaa 24, kitu ambacho Kikwete alipinga akidai wasamehewe.
Kwa namna Serikali ya Tanzania inavyofanya kazi, karibu mkuu hawezi kuwa na power ya kutoa 24hrs meli iondoke. Yaani ultimatum ya 24hrs na ikizingatia yuko against na Waziri. Katibu mkuu anaweza kutengeneza biti na mabishano ya hapa na pale lkn si kutoa saa 24 meli iondoke Tanzania (bila maelekezo ya Waziri au Rais).
 
Kwa namna Serikali ya Tanzania inavyofanya kazi, karibu mkuu hawezi kuwa na power ya kutoa 24hrs meli iondoke. Yaani ultimatum ya 24hrs na ikizingatia yuko against na Waziri. Katibu mkuu anaweza kutengeneza biti na mabishano ya hapa na pale lkn si kutoa saa 24 meli iondoke Tanzania (bila maelekezo ya Waziri au Rais).
Okay. Labda tuseme hakulazimika kutoa masaa 24 bali alisema piga ua hiyo meli isingeshusha mzigo wake TIPER. Kumbuka, TBS na wipimanji wengine walishasema ile crude ilikuwa sio ya standard na specifications za TIPER, kwa hiyo hata asingewapa masaa 24 wangefanya nini, wakae tu wakisubiri huruma za Prof. Mwandosya? Prof. yeye alisimamia ripoti za vipimo vya quality ya crude na specifications za TIPER, wakati Kikwete alitaka wafanye waiver na kuwasamehe kwa kuleta substandard crude oil. Management ya TIPER ilikuwa inalalamika kuwa hata huko nyuma walikuwa wanalazimishwa kupokea substandard crude. Na hichi ndio kilimuudhi Prof. Mwandosya, kwamba Kikwete siku zote alijua walikuwa wakileta crude isiyofaa. Kikwete akajitetea mtoto wa Mkulu alikuwa na hisa katika huo mzigo. Prof. Mwandosya akasema nonsense, hata angekuwa Mkulu mwenyewe asingeruhusu crude ipakuliwe. Unaona palivyokuwa patamu?

Hiyo issue bwana ilienda hadi Ikulu, lakini ilikuwa awkward sana kusuluhishwa Ikulu kwa sababu za personal interests. Ila meli iliondoka. Serikali ya wakati ule wee isikie tu. Kina Prof. Mwandosya ambao wanafuata ethical principles wasingedumu kwenye ile serikali. Kikwete mtoto wa mjini yeye alijifitisha popote pale, akiangalia upepo.

Ndio maana akawaambie kwa confidence mno, mie bwana ni lecturer wa UDSM. Nilikuwa appointed kuja wizarani kutokana na utaalamu wangu, haikuwa political appointment. Kama mnaona si-fit kwenye domain yenu acha nirudi zangu chuoni kufundisha vijana. Msitegemee leo nitakuwa Katibu Mkuu Nishati, kesho mnipeleke Wizara ya Utamaduni na Michezo sijui! Wapo Makatibu wakuu wa namna hiyo, ambao ukatibu mkuu ni career, lakini sio mimi. Yaani kwa kauli hii nilimpenda Prof Mwandosya - aliwapa vidonge vyao🤣🤣🤣🤣
 
..Mark Mwandosya ni msomi wa kweli sio mbabaishaji.

..huyu ni mmoja wa " Tanzania One " wa miaka hiyo.
Kwa sasa tuna tatizo la Bunge la Ulaya kusema ile pipeline ya mafuta kati ya Tanzania na Uganda isijengwe. Yaani Prof. Mwandosya ni mtu muafaka wa kutusaidia katika hili. Huyu January Makamba hataweza lolote hapo, kwanza hana charisma na confidence ya kuwaweka sawa hawa watu wa Bunge la Ulaya. Nani atamsikiliza? Abaki akijibu hoja za mambo ya Crane za Nyerere Hydopower project na kwa nini umeme unakatika, local stuff.
 
Yaan hii nchi imechoka sana.Kikwete ni failure wa muda wote .Yupo tu kwa ajili ya katiba mbozi ya Nyerere.Leo ndio awe mshauri ?Tunazid kuanguka kwa ajili ya huyi Mzee asiyejitambua
Sasa mtu kama Jiwe eti akawa Rais
 
Kwa sasa tuna tatizo la Bunge la Ulaya kusema ile pipeline ya mafuta kati ya Tanzania na Uganda isijengwe. Yaani Prof. Mwandosya ni mtu muafaka wa kutusaidia katika hili. Huyu January Makamba hataweza lolote hapo, kwanza hana charisma na confidence ya kuwaweka sawa hawa watu wa Bunge la Ulaya. Nani atamsikiliza? Abaki akijibu hoja za mambo ya Crane za Nyerere Hydopower project na kwa nini umeme unakatika, local stuff.

..sidhani kama ni mgogoro mkubwa kiasi hicho.

..kwanza makampuni ya hukohuko EU yanahusika ktk ujenzi.

..pili njia itakapopita hilo bomba ni rafiki zaidi kwa mazingira na gharama kuliko lingepitia Kenya.

..muelekeo ya Kenya kuna miinuko na vyanzo vingi vya maji kwa hiyo hatari kwa mazingira na gharama zitakuwa kubwa.

..naamini ni suala la kupeleka wawakilishi wetu huko EU kuwatotoa wasiwasi wadau wetu wa maendeleo.

..tatizo tuna watawala wanaochukia kuulizwa au kuhojiwa kwa maamuzi yoyote wanayoyafanya. They are very good at making decisions but pretty bad at justifying or explaining them.
 
..sidhani kama ni mgogoro mkubwa kiasi hicho.

..kwanza makampuni ya hukohuko EU yanahusika ktk ujenzi.

..pili njia itakapopita hilo bomba ni rafiki zaidi kwa mazingira na gharama kuliko lingepitia Kenya.

..muelekeo ya Kenya kuna miinuko na vyanzo vingi vya maji kwa hiyo hatari kwa mazingira na gharama zitakuwa kubwa.

..naamini ni suala la kupeleka wawakilishi wetu huko EU kuwatotoa wasiwasi wadau wetu wa maendeleo.

..tatizo tuna watawala wanaochukia kuulizwa au kuhojiwa kwa maamuzi yoyote wanayoyafanya. They are very good at making decisions but pretty bad at justifying or explaining them.
Umemsikia Museveni alivyoongea? Tayari anakebehi na kusema hivi visichana vidogo huko Ulaya leo vinataka kutuambia nini cha kufanya?

Sasa katika mambo ya diplomasia hatuendi hivyo. Huwezi kuwa confrontational na hizi nchi ukashinda. Always diplomacy inashinda, na ndio maana suala la rada Prof. Mwandosya aliliweza kirahisi sana.
 
Mi naona angeitumia elimu yake kuinufaisha nchi ili wanaosoma waone manufaa ya elimu.
 
Okay. Labda tuseme hakulazimika kutoa masaa 24 bali alisema piga ua hiyo meli isingeshusha mzigo wake TIPER. Kumbuka, TBS na wipimanji wengine walishasema ile crude ilikuwa sio ya standard na specifications za TIPER, kwa hiyo hata asingewapa masaa 24 wangefanya nini, wakae tu wakisubiri huruma za Prof. Mwandosya? Prof. yeye alisimamia ripoti za vipimo vya quality ya crude na specifications za TIPER, wakati Kikwete alitaka wafanye waiver na kuwasamehe kwa kuleta substandard crude oil. Management ya TIPER ilikuwa inalalamika kuwa hata huko nyuma walikuwa wanalazimishwa kupokea substandard crude. Na hichi ndio kilimuudhi Prof. Mwandosya, kwamba Kikwete siku zote alijua walikuwa wakileta crude isiyofaa. Kikwete akajitetea mtoto wa Mkulu alikuwa na hisa katika huo mzigo. Prof. Mwandosya akasema nonsense, hata angekuwa Mkulu mwenyewe asingeruhusu crude ipakuliwe. Unaona palivyokuwa patamu?

Hiyo issue bwana ilienda hadi Ikulu, lakini ilikuwa awkward sana kusuluhishwa Ikulu kwa sababu za personal interests. Ila meli iliondoka. Serikali ya wakati ule wee isikie tu. Kina Prof. Mwandosya ambao wanafuata ethical principles wasingedumu kwenye ile serikali. Kikwete mtoto wa mjini yeye alijifitisha popote pale, akiangalia upepo.

Ndio maana akawaambie kwa confidence mno, mie bwana ni lecturer wa UDSM. Nilikuwa appointed kuja wizarani kutokana na utaalamu wangu, haikuwa political appointment. Kama mnaona si-fit kwenye domain yenu acha nirudi zangu chuoni kufundisha vijana. Msitegemee leo nitakuwa Katibu Mkuu Nishati, kesho mnipeleke Wizara ya Utamaduni na Michezo sijui! Wapo Makatibu wakuu wa namna hiyo, ambao ukatibu mkuu ni career, lakini sio mimi. Yaani kwa kauli hii nilimpenda Prof Mwandosya - aliwapa vidonge vyao🤣🤣🤣🤣
Mkuu,wakati haya yanatokea,wewe ulikua umejibanza wapi unasikilizia?
 
Juzi hapa ilitangazwa kwamba Prof. Mwandosya ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa EWURA. Wengi walishangaa kwa nini Prof. Mwandosya kaletwa kutoka hali ambayo wengi wetu tulidhani ni ustaafu na kurudi kuwa Mwenyekiti wa EWURA.

Lakini hatupaswi kushangaa. Uteuzi wa Prof. umetukumbusha pia kwamba wakati Mkapa akikabiliwa na sakata la ununuzi wa rada toka Uingereza, ni Prof. Mwandosya alipewa jukumu la kuliweka sawa jambo hilo, hadi kukawa na joke kwamba Prof. Mwandosya alim-charm yule mwanamke wa Uingereza aliyekuwa akitutuhumu vikali hadi akabadilika na kusema "it wa a very wise decision by Tanzania to buy the radar!"

Na pia kwa mlio na ufahamu, wakati uhusiano kati ya Kiwete na Kagame umeharibika sana hadi Kagame kutishia kumpiga Kikwete ni Prof. Mwandosya alitumwa Rwanda kwenda kuweka mambo sawa.

Na labda niwaambie siri nyingine, wakati Kikwete anaona anashambuliwa kila kona kwa kuwa raisi dhaifu, ni Prof. Mwandosya aliitwa ofisi ya Raisi kama waziri asie na wizara maalum na kuwa mshauri wa karibu wa Kikwete. Matokeo tukayaona, ghafla Kikwete akaanza kuonekana kuwa na busara sana nchini na nje ya nchi. Ilifikia hatua watu wakasema unajua Kikwete aliwahi kugombea uraisi angegombea awamu ijayo maana busara zimekuja mwishini mwa awamu yake, bila kutambua kuwa kulikuwa na busara za Prof. Mwandosya nyuma ya utendaji wa Kikwete katika sehemu kubwa ya awamu ya mwisho ya uraisi wake.

Na hivi, ni Watanzania wangapi wanatambua kuwa dira ya maendeleo aliyotumia Raisi Mkapa kutukwamua kiuchumi (TANZANIA DEVELOPMENT VISION 2025) ni matokeo ya kazi ya Prof. Mwandosya baada ya kuambiwa na Raisi Mkapa asimamie utayarishaji wake? Najua wengi hawakujua hili kwa sababu ilipokamilika iliandikwa imeandaliwa chini ya Planning Commission, bila kueleza iliandaliwa chini ya usimamizi wa Prof. Mwandosya

Na tunaomfahamu Prof. Mwandosya, tunajua kwamba katika nyanja za kimataifa, alikuwa kinara wa majadiliano ya mkataba wa mabadiliko ya tabia nchi ulioitwa Kyoto Protocol, kiasi kwamba alisifiwa sana juu ya uwezo wake wa kuchambua mambo na Raisi Clinton wa Marekani, pamoja na Al Gore. Wakati huo Prof. Mwandosya alikuwa msemaji wa kundi la G77 & China, lakini hakuwa na madaraka yoyote serikalini Tanzania, jambo ambalo lilimfanya Raisi Clinton wa Marekani amshangae sana Mkapa kutomtumia ipasayo Prof. Mwandosya katika serikali yake - na ndipo Prof Mwandosya "alipoamriwa" na Mkapa akagombee ubunge.

Ndio maana imesemwa kwamba katika mambo ambayo hutakaa umdanganye Prof. Mwandosya ni mambo ya mikataba. Hapo kina Prof. Kabudi na degree za sheria zao weka kando kabisa!

Na wakati fulani Prof. Mwandosya akiwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji, kulikuwa na mbinu za nchi ya Misri kubadilisha makubaliano ya matumizi ya mto Nile ili kuinufaisha zaidi Misri. Ilibaki kidogo sana nchi za Mto Nile kutia sahihi mkataba huo mpya pale ambapo Prof. Mwandosya aliibuka tena na kuziamsha nchi nyingine juu ya vipengele kwenye makubaliano hayo mapya ambavyo vingezikandamiza. Kwa sababu ya uchambuzi wake huo, nchi zote za Mto Nile ziliwagomea Misri kuweka sahihi makubaliano hayo mapya. Hadi leo Misri hawataki kabisa kusikia habari za Prof. Mwandosya kwa kuwa wanamuona kuwa mtu aliewanyang'anya tonge mdomoni!

Na labda pia wengi waligundua kwamba mara tu baada ya Prof. Mwandosya kuteuliwa kuwa Mweyekiti wa EWURA, bei ya mafuta ilishuka kiasi tofauti na matarajio ya wengi, na wengi wamekuwa wakijiuliza kama ilikuwa ni utendaji wake kama Mwenyekiti wa EWURA uliosababisha kutoa ahueni kwenye bei za mafuta nchini.

Sasa kuna mengi juu ya Prof. Mwandosya naweza kusema hapa, lakini acha haya yatoshe kwa sasa ili kuweka backdrop ya swali langu. Kwa nini Kikwete hakumshauri Samia amteue Prof. Mwandosya kuwa Makamu wa Raisi?

Swali langu pia linaendana na maoni ndani ya humu JF juu ya uteuzi wa Dr. Mpango kama Makamu wa Raisi. Kwa ujumla wengi wa wana JF hawaridhishwi kabisa na Dr. Mpango kuwa Makamu wa Raisi, hasa ukizingatia matukio ya hivi karibuni yaliyomhusu Dr. Mpango.

Sasa je, Kikwete hakukumbuka kwamba angalau Makamu wa Raisi wa Samia awe mmojawapo wa wagombea wa uraisi wa awamu ya Magufuli? Maana kama Prof. Mwandosya angekuwa Raisi badala ya Magufuli, hadi leo hii angekuwa ni raisi katika awamu yake ya mwisho. Je, inawezekana pia Kikwete hakumpendekeza Prof. Mwandosya kuwa Makamu wa Raisi kutokana na ile issue ya "majina ya mfukoni"?

Kwa tunaomfahamu Prof. Mwandosya, ukiachia mbali porojo za humu JF, kama angekuwa ndio Makamu wa Raisi chini ya Raisi Samia, Tanzania tungeenda mbali sana na uongozi wa Raisi Samia ungeonekana ni bora na ungemfanya maarufu kwa scale ile ya Nyerere - mama wa Taifa! Na naweza kudiriki kusema inawezekana kabisa, Kikwete alitambua wazi kama Prof. Mwandosya angekuwa Makamu wa Raisi wa Samia, basi Kikwete angekuwa na influence kidogo sana kwa Samia, au asingekuwa na influence yeyote!

Kwa hiyo naweza kusema kwamba katika hili ni wazi ubinafsi ulizidi maslahi ya nchi. Raisi Samia alipigwa chenga katika kuteua Makamu wa Raisi. Prof. Mwandosya angemfaa sana na tusingekuwa na habari za kulishwa samaki waliooshwa kwenye maji ya maiti!
Kwa hiyo makamu wa Rais aliyepo hafai ? Kila mtu na wakati wake.
 
Back
Top Bottom