Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Hiyo research ya Finland, mwanamme rijali mikidinda kwa kuwa nimemuangalia Zena, mwanamke mzuri wa kuchorwa, mwenye maumbile ya kuvutia , kwenye gazeti la SANI, hilo linamaanisha huyo katuni Zena ni mtu kweli?
Nioneshe tafiti iwe na wanaume wote mabwabwa, rijali, wenye dini etc wakidinda kwanza.

Hio tafiti imehusisha pande zote mbili wenye dini na wa sio na dini, ingehusisha wenye dini tu logic yako inge Apply ila hapo imehusisha wasio na dini. Na huo uwoga haujakuja voluntary upo invonluntary kuonesha kwamba miili yetu ipo programmed hivyo irespective ya akili yetu inafikiria vipi.
 
Siyo kufuru.
Kwa sisi wenye mwili tunaona kama kifo ni adhabu.
Kiuhalisia kifo ni mabadiliko tu ya binadamu kutoka stage moja kwenda nyingine.
Kama Mungu anaamuru ufe ki uhalisia ni jambo jema kabisa.

Aliyekuleta anakupeleka katika dalaja lingine ambolo ni bola zaidi.

Mfano. Mtoto anapozaliwa analia sana hataki kuja diniani kwa kulizoea tumbo la mama yake na kuona ndio sehemu sahihi yakuishi.

Akisha zaliwa baada ya muda anaona kumbe kule tumboni kulikuwa hakuna maana. Maisha mazuri ni haya ya sasa ya kula samaki na maziwa.

Ndivyo kilivyo kifo, ni kizuri sana mimi nitakapo karibia kufa nitawaambia waliobaki "Sitaki mtu anililie" nitaandaa bajeti ya Kusheherekea Kifo changu na Bia zitakuwepo.

Najua naenda sehemu nzuri zaidi ya hapa nilipo.
Ni mtu mjinga peke yake ndiye atakaesema kuwa kifo hakitishi.Kifo kinauma na kinatisha maana ni mwanzo wa maisha ya milele kwa maana hakuna tena kufa baada ya kufa ila matukio yajayo mbeleni ndio yanatisha. Je utakuwa miongoni mwa waliofaulu ama waliofeli??
 
So unakubali kumuamini mungu ni morality?
Hapana, hujasoma links zinakuambia kwamba morality inatokea naturally tu, haihitaji Mungu?

Let's say tupo katika ulimwengu ambao hauna Mungu.

Huko zamani kulikuwa na jamii zinazokubali morality, na jamii zisizokubali morality.

Jamii zisizokubali morality zikauanauana, zikamalizana. Hazikuwa na morality ya kukataza kuuana.Vizazi vyao havikuendelea kwa sababu kutoamini morality hakustawishi jamii, kunamaliza jamii.

Kwa upande mwingine, jamii ambazo ziliamini katika morality, ziliweza kustawi. Zikarithisha watoto morality kupitia mafunzo na kwa njia ya genetics.

Baada ya miaka mingi sana, ikaonekana kwamba jamii zisizoamini morality zimetoweka, zimeuana uana, zimepotea zimebaki jamii zinazoamini morality.

Watu ambao hawakujua historia hiyo, wakawa wanajiuliza, kwa nini watu wana morality? Kwa nini wanajua hiki kibaya hiki kizuri? Wana conclude lazima Mungu yupo na kawapa hiyo moral compass.

Wakati Mungu hahitajiki kuelezea hii natural morality.
 
Kuna wakati watu wengi waliamini jua linazunguka dunia.

Je, hilo lilifanya kuwa jua linazunguka dunia kweli?

The truth is not democratic useme kwamba watu wengi tukisema jua linazunguka dunia, basi itakuwa kweli jua linazunguka dunia.
Sijasema wingi wa watu msinilishe maneno pls.

Nimeongelea wingi wa sign.
 
Hapana, hujasoma links zinakuambia kwamba morality inatokea naturally tu, haihitaji Mungu?

Let's say tupo katika ulimwengu ambao hauna Mungu.

Huko zamani kulikuwa na jamii zinazokubali morality, na jamii zisizokubali morality.

Jamii zisizokubali morality zikauanauana, zikamalizana. Hazikuwa na morality ya kukataza kuuana.Vizazi vyao havikuendelea kwa sababu kutoamini morality hakustawishi jamii, kunamaliza jamii.

Kwa upande mwingine, jamii ambazo ziliamini katika morality, ziliweza kustawi. Zzikarithisha watoto morality kupitia mafunzo na kwa njia ya genetics.

Baada ya miaka mingi sana, ikaonekana kwamba jamii zisizoamini morality zimetoweka, zimeuana uana, zimepotea zimebaki jamii zinazoamini morality.

Watu ambao hawakujua historia hiyo, wakawa wanajiuliza, kwa nini watu wana morality? Kwa nini wanajua hiki kibaya hiki kizuri? Wana conclude lazima Mungu yupo na kawapa hiyo moral compass.

Wakati Mungu hahitajiki kuelezea hii natural morality.
Still kiraga hujajibu utafiti wangu ninachoona hapa unahamisha tu Magoli, si watoto wote ni Moral upright, kuna watoto wamepinda vibaya mno, ila watoto kumuamini mungu ni Universal wawe wa kishua, wa uswazi, wa Marekani, wa Somalia etc.
 
Nioneshe tafiti iwe na wanaume wote mabwabwa, rijali, wenye dini etc wakidinda kwanza.

Hio tafiti imehusisha pande zote mbili wenye dini na wa sio na dini, ingehusisha wenye dini tu logic yako inge Apply ila hapo imehusisha wasio na dini. Na huo uwoga haujakuja voluntary upo invonluntary kuonesha kwamba miili yetu ipo programmed hivyo irespective ya akili yetu inafikiria vipi.
Tafiti yako wapi inasema morality inatokana na Mungu?
 
Still kiraga hujajibu utafiti wangu ninachoona hapa unahamisha tu Magoli, si watoto wote ni Moral upright, kuna watoto wamepinda vibaya mno, ila watoto kumuamini mungu ni Universal wawe wa kishua, wa uswazi, wa Marekani, wa Somalia etc.
Sasa hapa una disprove point yako ya morality, umeileta mwenyewe, halafu unaivunja mwenyewe.

Sasa Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wotte karuhusuje watoto wengine wapinde hivyo?

Umeona tafiti zinazosema kwamba morality ni natural, haihitaji Mungu?

Tafiti zako wapi zinasema morality inatokana na Mungu?

Maana ni kitu kimoja kusema watoto wanazaliwa na morality, na kitu tofauti kusema morality inatokana na Mungu.

Hata kama watoto wanazaliwa na morality, je, hilo ni uthibitisho kwamba morality hiyo inatokana na Mungu?

Unaunganishaje watoto kuzaliwa na morality na morality kutoka kwa Mungu?
 
Nikuulize wewe uliehamisha magoli na kuingiza mambo ya morality na utafiti haujaongelea
Wewe ndiye umeanza kuleta habari ya "innate religion", ambayo ndiyo hiyo hiyo ya morality.

Au hujui Kiingereza?

Sasa wewe umeleta hoja ya "innate religion", ukasema inaonesha Mungu yupo.

Mimi nakwambia hiyo ni natural morality tu, na haihitaji Mungu kuielezea, na hizi hapa tafiti zinasema hilo.

Halafu unaniambia mimi ndiye niliyeleta hoja ya "innate religion"/ natural morality hapa?

Do you even know that unachokiita "innate religion" na natural morality ni kitu kile kile?
 
Bible hiyo inatetea wizi na uuwaj pia mungu kaua watu pia kwenye bible
Mungu haui watu.
Bali anawachukua na kuwa weka katika hatua nyingine.

Mi ugomvi wangu ni hii imani ambayo watu wenye dhambi wanawaua watu wengine wenye dhambi kwa kisingizio cha wamemkosea Mungu.

Hakuna Binadamu ambaye hatendi dhambi ndio maana Mungu katoa fursa ya kutubu kwake na ameahidi kusamehe.

Kuchinja binadamu mwenza kwa kisingizio cha dini ni vitendo vya kishirikina kabisa.

Mungua ashatoa amri USIUE.
 
Hii ni dhambi gani unaweza kufafanua ? Na Je Shetani alitenda hii dhambi au ni kiburi chake yaani msamaha upo ila hautaki ?

Kwahio ni kwamba kama vile watu wanakuwa brainwashed kuridha na chochote kile..., Yaani kama enzi za utumwa ambapo kuna watu walikuwa wanafurahia sana kuwatumikia Ma-Bwana zao yaani hata ukiwapa uhuru wanaona wanapungukiwa ?

Je unaona hilo ni sahihi yaani kuridhika hata kama kuna kunyonywa sio kwa utashi wako bali kwa kuondolewa utashi ?!!!
Shirki (ushirikina) ni miongoni mwa madhambi makubwa! Na ni dhambi kubwa kuliko madhambi yote unayoyajua wewe.Kuiba,kuua,kuzini,kusema uongo,kusengenya n.k hakufikii ukubwa wa hii dhambi.

Shirki (Ushirikina) ni kitendo cha kumuwekea Mungu washirika katika masuala yote ya Ibada.

Mfano ukiamini kuwa kuna kitu,mtu au jini anaweza kukupa wewe riziki kama/Pamoja au zaidi ya Mungu. Hapa unakuwa umemuwekea Mungu mshirika. Mfano unaumwa au una matatizo ila ukaenda kumuomba babu yako aliyezikwa miaka mingi iliyopita kaburini akusaidie kukuponya au kukutatulia matatizo yako ,hapa unakuwa umemfanya babu yako kuwa nae ni Mungu pamoja na Mungu.Hivyo umemfanyia Mungu kuwa ana mshirika.

Au ukaitakidi kuwa mizimu au miti (mibuyu) ukienda kuiomba ina uwezo wa kukutatulia matatizo yako hapa unakuwa umefanya ushirikina.

Au unamatatizo ukaensa kwa mganga akupigie ramli na kuwaomba majini wakusaidie kukutatulia matatizo yako ya biashara,kupata mali au watoto....hapa unakuwa umefanya shirki. Unakuwa ni Mshirikina.

Au nafsini kwako ukiwa na itikadi kuwa kuna Mungu zaidi ya mmoja kama walivyo wahindi na mabudha.Huo unakuwa ni ushirikina.

Ina maana kuwa umeshajitoa katika imani ya Mungu mmoja apasae kuabudiwa peke yake.

Mfano mzuri ni pale Unapokuwa na biashara kisha ukamuajiri mtu akuuzie bidhaa zako...yule mtu akauza vizuri kisha pesa yako yote akaichukua na kwenda kumpa mtu mwingine ambaye huna share nae katika umiliki wa biashara yako.Na ukimuuliza why kafanya hivyo ,anakujibu kuwa hakuna ubaya kumpa mtu mwingine pesa yako kwani ww na yule wote ni sawa!...

Je unaona ubaya wa hii kitu?? Ni wazi kuwa utachukizwa na jambo hilo na ikiwezekana unaweza hata kumuadhibu huyo mfanyakazi wako kwa tendo alilolifanya.

Hii ndio SHIRKI (ushirikina)


Ni mada pana sana.Ushirikina una matawi yake mengi tu. Ila kiufupi huo ndio uhalisia wa dhambi ya SHIRKI.

Iwapo mtu atakufa akiwa na dhambi hii pasi na kutubia kwa mola wake ajue kuwa MUNGU haisamehi kamwe na amemuharamishia pepo mtu ambae atakufa hali ya kuwa ni mshirikina.
 
Hii logic ilishakuwa debunked na hii statemnt.

"Who paint the painter?"

Sababu picha imechorwa haimaanishi mchoraji amechorwa.

Sababu binadamu Ametengenezwa haimaanishi Mungu nae Ametengenezwa, Simple Logic.
That is not how debunk works

Tunaweza kusema hivyo hivyo hata kwa vitu vingine ambavyo hautakuwa tayari kukubali kuwa havijaumbwa

Naweza kusema ulimwengu hauna chanzo, kuhoji chanzo cha ulimwengu unakuwa unafanya kosa la kuuliza mchoraji wa mchoro amechorwa na nani.

Utakubali?

Kama jibu litakuwa ni kinyume basi lazima tukubaliane dhana ya painter ni mbinu ya kukimbia uwajibikaji wa kujibu hoja
 
Kwanini Shetani hawezi kusamehewa na kuokoka?

Kuna asili tatu tu...
Mungu, Malaika na Binadamu.
Mungu huwa hakosei lakini malaika na binadamu wanaweza kukosea.

Shetani kwa asili ni malaika, mwanzoni alikuwa malaika mwema, Lusifa "mbeba nuru", alikuwa na nafasi mbinguni, lakini uovu ukachipuka moyoni mwake, akawaza na akataka kuwa kama Mungu yaani naye aabudiwe (Isaya 14, Ezekiel 28), kimsingi, alitaka kufanya mapinduzi, Biblia katika Ufunuo 12:7-9 inasema, kukawa na vita mbinguni.
Malaika waliomuunga mkono Shetani wakapigwa pamoja na Shetani mwenyewe wakaangushwa hadi chini wakafukuzwa mbinguni, Yesu alimwona Shetani akianguka kama umeme. Baada ya hayo Lusifa akageuka kuwa mkuu wa giza yaani Shetani na malaika waliomuunga mkono wakageuka kuwa malaika waovu yaani majini.

Sasa, Shetani na majini, wote wana asili ya umalaika, hawawezi kusamehewa na kuokoka kwa sababu MUNGU ALIPOKUJA KUOKOA HAKUFANYIKA KUWA MALAIKA BALI ALIFANYIKA KUWA MWANADAMU. Mwandishi wa Waebrania anasema, Maana ni hakika, (Yesu) hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu. Ebr 2:16 SUV

Kwahiyo, malaika akipotea, anapotea milele, Biblia inasema kuhusu hili kwamba, Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu. Yud 1:6 SUV

Habari Njema ni kwamba, damu iliyomwagika msalabani ilikuwa ya Mungu-mwanadamu, siyo Mungu-malaika, ndio maana ina uwezo wa kukuokoa mwanadamu, MWANADAMU UNAOKOLEWA KWA KUAMINI KUWA DAMU ILIYOMWAGIKA NI KWAAJILI YA KUSAMEHE DHAMBI ZAKO. Amini hilo sasa, na wewe uliyeamini tayari usifanye dhambi makusudi maana yake unakuwa unaikanyaga damu ya agano na kumfanyia jeuri Roho wa neema.

Mambo haya niliyosema, yaani mambo ya wokovu, hata malaika wanatamani kuyaishi, wokovu ni mtamu mnooo unawatamanisha hata malaika. Kama Biblia isemavyo;

.... mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.
1 Petro 1:12 NEN

Oscar Wissa
 
Kama kawaida yenu enyi mliokufuru, kufanya kejeli dhidi ya waliomuamini Mungu. Hamna jambo jipya mtakuja kulifanya ambalo baba zenu waliowatangulia ktk kukufuru hawakulifanya. Huwa mnarudi yale yale ila karibu mtakuja jua. Mwanadamu umri wako ni mchache sana.
Kwani Mungu aliumba Majini Mashetani na watu kwa sababu gani ?
Si ili wamwabudu sasa kwao kumrudia Mungu kama walimkosea kuna shida gani.?
 
Sasa hapa una disprove point yako ya morality, umeileta mwenyewe, halafu unaivunja mwenyewe.

Sasa Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wotte karuhusuje watoto wengine wapinde hivyo?

Umeona tafiti zinazosema kwamba morality ni natural, haihitaji Mungu?

Tafiti zako wapi zinasema morality inatokana na Mungu?

Maana ni kitu kimoja kusema watoto wanazaliwa na morality, na kitu tofauti kusema morality inatokana na Mungu.

Hata kama watoto wanazaliwa na morality, je, hilo ni uthibitisho kwamba morality hiyo inatokana na Mungu?

Unaunganishaje watoto kuzaliwa na morality na morality kutoka kwa Mungu?
Wewe ndiye umeanza kuleta habari ya "innate religion", ambayo ndiyo hiyo hiyo ya morality.

Au hujui Kiingereza?

Sasa wewe umeleta hoja ya "innate religion", ukasema inaonesha Mungu yupo.

Mimi nakwambia hiyo ni natural morality tu, na haihitaji Mungu kuielezea, na hizi hapa tafiti zinasema hilo.

Halafu unaniambia mimi ndiye niliyeleta hoja ya "innate religion"/ natural morality hapa?

Do you even know that unachokiita "innate religion" na natural morality ni kitu kile kile?
Nakujua wewe mzee wa kupindisha mambo sipo hapa kubishana blah blah tafiti hupingwa na tafiti, mimi nimeleta tafiti yangu nzuri tu na kuweka Citation, sio tu imetoka university kubwa Oxford bali imetumia researcher wengi na nchi nyingi.

Wewe unajibu tafiti na hoja mfu mwanzo umesema wamefundishwa kitu ambacho si sahihi sababu hio tafiti ime take into consideration hio issue, then umeleta tafiti nyengine kabisa zisizohusiana na nilicholeta mimi.

Stay on point pls
 
Wewe hujui kitu kuhusu maandiko!! Naona umenukuu andiko kutoka ktk kumbukumbu la torati ila nikikupa maandiko yahusuyo sheria kwenye biblia yako utageuka na kuyakataa kwamba yamepitwa na wakati.
Wewe unayejua maandiko basi tufundishe.
 
Nakujua wewe mzee wa kupindisha mambo sipo hapa kubishana blah blah tafiti hupingwa na tafiti, mimi nimeleta tafiti yangu nzuri tu na kuweka Citation, sio tu imetoka university kubwa Oxford bali imetumia researcher wengi na nchi nyingi.

Wewe unajibu tafiti na hoja mfu mwanzo umesema wamefundishwa kitu ambacho si sahihi sababu hio tafiti ime take into consideration hio issue, then umeleta tafiti nyengine kabisa zisizohusiana na nilicholeta mimi.

Stay on point pls
1. Tafiti yako wapi imesema morality/ innate religion imetoka kwa Mungu?

2. Mimi nimekuweka tafiti zinazosema kwamba morality ni matokeo ya natural evolution, na haihitaji Mungu kuielezea.
 
Hapana, hujasoma links zinakuambia kwamba morality inatokea naturally tu, haihitaji Mungu?

Let's say tupo katika ulimwengu ambao hauna Mungu.

Huko zamani kulikuwa na jamii zinazokubali morality, na jamii zisizokubali morality.

Jamii zisizokubali morality zikauanauana, zikamalizana. Hazikuwa na morality ya kukataza kuuana.Vizazi vyao havikuendelea kwa sababu kutoamini morality hakustawishi jamii, kunamaliza jamii.

Kwa upande mwingine, jamii ambazo ziliamini katika morality, ziliweza kustawi. Zikarithisha watoto morality kupitia mafunzo na kwa njia ya genetics.

Baada ya miaka mingi sana, ikaonekana kwamba jamii zisizoamini morality zimetoweka, zimeuana uana, zimepotea zimebaki jamii zinazoamini morality.

Watu ambao hawakujua historia hiyo, wakawa wanajiuliza, kwa nini watu wana morality? Kwa nini wanajua hiki kibaya hiki kizuri? Wana conclude lazima Mungu yupo na kawapa hiyo moral compass.

Wakati Mungu hahitajiki kuelezea hii natural morality.
Mzee morality inarithishwa kwa genetics?
 
Ni mtu mjinga peke yake ndiye atakaesema kuwa kifo hakitishi.Kifo kinauma na kinatisha maana ni mwanzo wa maisha ya milele kwa maana hakuna tena kufa baada ya kufa ila matukio yajayo mbeleni ndio yanatisha. Je utakuwa miongoni mwa waliofaulu ama waliofeli??
Mimi kifo hakinitishi.
Nilikuja sina kitu na nitaondoka bila kitu.
Na nakujua ninakoenda.

Duniani hakuna cha ajabu ambacho naweza kukililia.

Ukiwa na hekima kidogo tu huwezi kuogopa kifo.
Na kuna watu wanaomba kufa baada ya muda flani.
Wengine wanajenga makaburi yao kabisa ya kuzikiwa.

Ni watu waoga pekee wanao ogopa kifo.
 
Mzee morality inarithishwa kwa genetics?
Kwani haiwezekani kwa mtu kuwa mtu wa hasira hasira, mtu mgomvi mgomvi, mtu mwenye matatizo ya akili yanayomfanya asijali morality, matatizo yaliyo katika level ya genetics, kumrithisha mtoto wake matatizo hayo hayo ya kutojali morality kwa kupitia hizo genetics?

Hujui kwamba matatizo mengine ya morality yanaendana na matatizo ya magonjwa ya akili, ambayo yanarithishwa kama vile unavyoweza kurithi magonjwa mengine kama kisukari, sickle cell etc?
 
Back
Top Bottom