Kwanini Tanzania hakuna daily briefing juu ya Corona virus pandemic?

Kwanini Tanzania hakuna daily briefing juu ya Corona virus pandemic?

Tokea tarehe 22/04/2020 Rais wetu, John Magufuli, alipofanya kikao maalum na viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, kuhusiana na ugonjwa wa COVID 19, tumeshuhudia kimya kizito kwa upande wa mamlaka za utoaji taarifa wa Tanzania Bara ya maambukizi mapya na vifo vinavyotokana na ugonjwa huo

Tukumbuke pia katika kikao hicho tulimsikia Rais wetu, akipiga "mkwara" mzito, kuwa haridhishwi na namna taarifa zinazotolewa na wizara ya Afya, kuhusu maambukizi mapya na vifo vinavyotokana na ugonjwa huo wa corona

Tulishuhudia pia akifanya "mini reshuffle" kwa kumwondoa aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Afya na kumteua mwingine

Tumeshuhudia waziri wa Afya, Ummy Mawalimuambaye amekuwa akitupa "updates" za ugonjwa huo, akipata ghafla "kigugumizi" baada ya kikao hicho cha Mheshimiwa Rais kwa kutoweza tena kutupa taarifa zinazohusiana na ugonjwa huo

Ndipo hapo tunapomuuliza waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, nini kimekutokea hadi usitishe kutupa "updates" za maendeleo ya ugonjwa huo nchini?

Tunashuhudua kwenye nchi jirani za Zanzibar, Kenya na nchi nyingine za mbali za Uingereza na Marekani wakitoa "updates" za ugonjwa huo kila siku.

Tunafahamu pia kuwa Taifa la Tanzania limetoka kwenye maombi mazito ya kumlilia Mungu wetu atuepeshie na janga hili la corona.

Tunadhani ni muhimu sana kwa wananchi kuendelea kupewa "updates" za ugonjwa huo za kila siku, kama yafanyavyo mataifa mengine.

Ikiwa hakuna maambukizi mapya wala vifo, basi ni vyema waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, akawa anatipatia "daily briefing" na sisi wananchi turejeshe utukufu kwa Mungu wetu, kwa kutuondolea janga hili la corona

Kwa kuendelea kukaa kimya kwa serikali, kunatoa mwanya kwa wananchi wasilitakia mema Taifa letu, kwa kutangaza wao taarifa wanazozijua wao za maambukizi mapya na vifo vinavyotokea nchini kutokana na ugonjwa huo wa corona

Naziomba mamlaka zinazohusika za wizara ya Afya zitujibie utata huu wa suala nyeti sana la ugonjwa wa corona hapa nchini, ili sisi wananchi zituondolee hofu kubwa inayotukabili hivi sasa kuwa wananchi wa Taifa hili, hususani wa Jiji la Dar, wanapukutika kwa wingi sana

Ni lazima pia tuwajulishe watawala wetu kuwa kupewa taarifa za maendeleo ya ugonjwa huu wa corona siyo hisani kwa watawala wetu, bali ni kitu cha LAZIMA kwa wananchi wake
Mkuu Mystery, kwanza naunga mkono hoja.
Pili kwa ruhusa yako, naomba kutumia hoja za bandiko lako hili kama mbegu ya kuoteshea bandiko langu fulani.

Enzi za zamani, mambo ya kutoa habari kwa upande wa serikali ilikuwa iko huru kutoa habari au kutotoa, ikijisikia kutoa habari, inatoa, ikijisikia kutotoa habari, haitoi na hakuna yoyote mwenye mamlaka ya kuiuliza.

Lakini kuanzia mwaka 2016, Tanzania tumepitisha sheria ya haki ya kupata habari, the right to information act, ambapo sasa kupata habari ni haki, sio favours, serikali inawajibika kutoa habari za kweli kwa wananchi, hiki kinachoendelea sasa kwenye utoaji wa habari za maendeleo ya ugonjwa wa Corona, ni kinyume cha sheria. Watanzania wana haki ya kupata habari, unless rais atangaze hali ya hatari, sheria zote na haki zote zinasimama!.
P
 
1588131738390.png

Dada usiku wa kuamkia leo makaburi ya ununio kwa kondo wamezikwa Watu Zaidi ya 58 waliokufa kwa corona.
 
Back
Top Bottom