Kwanini wafanyabiashara wakubwa wakutane na Rais Ikulu badala ya Waziri husika Wizarani?

Kwanini wafanyabiashara wakubwa wakutane na Rais Ikulu badala ya Waziri husika Wizarani?

Akili kisoda sana,mambo hayo ya watu kupotezwa umeanza kuyaona leo?
Mbona hata ujambazi na wizi wa sasa mnajitetea kua haukuwahi kuisha nchini Tangu enzi?
Ujinga tu umetamalaki kichwani mwenu
hata kama yalianza zamani wewe unaona bora yaendeleee? ndio mana Mungu kawachapa pigo.
 
Maneno ya aina hii huwa yananipa picha kwamba kuna watu munatafuta raha ya maisha ambayo haipo dunia hii. Na munachukia viongozi kwa manufaa binafsi tu! Tunapojadili suala la kitaifa huwezi fikia hatua ya kuruhusu rais awe mwizi wakati jamii ya dunia hii, wizi unakubalika kwa watu wapuuzi tu. Hata kama alimnyonga mzazi wako, ifikie kiwango ujiulize kama mzazi alikuwa mtu wa maana kiasi gani.
Kwa samia ndio hamtaki kwa yule Jini Jiwe ndio mlitaka atawale milele?? hayo ndio manufaa ya kitaifa?? Malofa nyie
 
Mbona kipindi kile akina Rostam wameenda kuonana na ile maiti ya chato hamkuyasema haya

Mwacheni mama aipeleke nchi mahala salama kutoka kwenye ile diversion aliyokuwa anatupeleka bwana Mayanga/majanga

magufuli kafa, ila bado ana thamani kubwa kuliko wewe uliye hai , hapo sasa Sijui nani ni maiti
 
DU, watu kwa kubadiri topic, nani kasema Dangote ni mkumbozi wa Tanzania? Kuna andiko hata moja limesema hivyo? Tusiwekeane maneno mdomoni tafadhari.

Tangu 2012 uko JF, bado uko kiwango hiki cha majadiliano! Ni wewe uliyesifia ajira za Dangote;

Watu wengi bado tunaishi maisha ya KIJIMA sana aise; hivi bado kuna mtu hajui faida za wawekezaji katika nchi? Magufuli mwenyewe ali straggle sana kuwapata wawekezaji, sema matendo yake yalikua yanawafukuza; tunajua Dangote alitaka kufunga kiwanda chake, aliitwa na Magufuli Ikulu wakayamaliza but bado ni kama uzalishaji wake ulikua unasua sua, kaongea na watu wa Barrick baada ya yeye mwenyewe kuwachanganya, kina Rostam Aziz hadi waliondoka nao nchini but he called them back, kafanya sana vikao na wafanyabiasha wa ndani na wa nje but huenda wawekezaji/wafanya biashara walikua wanaona maneno yake na matendo yake vilikua vinapingana na waka decide otherwise.
Moja kati ya faida za wawekezaji ni AJIRA kwa Watanzania, tumelalamika ugumu wa ajira kipindi cha mwendazake, unajua sababu kubwa ni nini? Serikali haina uwezo wa kuajiri wataalamu wote, wengine wataajiriwa sekta binafsi, ndio hao wawekezaji au wafanyabiashara.
Faida ya pili ndio hiyo mambo ya kodi na dividends kwenda serikalini, ukiwaondoa wafanyabiashara hayo mengine yatatokea and hence hata hizo kodi tunazo sema zimefikia Tilion zita drop na ujambazi/wizi unaweza kuongeza. Tuache mawazo ya KIJIMA, tufikirie kisasa, duniani kote serikali zinatengeneza mazingira mazuri kwa wafanyabiashara/wawekezaji, halafu sisi na mawazo yetu ya KIJIMA tunawaona kama wanyonyaji, stupid

Ukasifia na kazi yake nzuri hadi kushusha bei unayoita bei chee;
Nimeishia darasa la hapa na pale but that doesnt mean kwamba sijui faida za uwekezaji. Hivi hujui baada ya Dangote kuanza uzalishaji bei ya cement nchini ilishuka? Dangote aliwapa sana changamoto wazalishaji wengine; ngoja nikupe hi nyingine; Cement ya Tanzania kwa sehemu kubwa iliokua inapatikana sokoni ilikua ile ya class 32.5, Dangote akawa anamwaga mzigo wa class 42.5 kwa bei chee, ndio sasa na kina Simba, Twiga nao ikabidi waji align na soko, zikaanza hizo sijui twiga plus, mara twiga extra nk. Bado utananmbia, Dangote hana faida?
Bei chee! Jinga wewe huyu ni mjomba wa Tanzania!
 
Hivi umeona kejeli wapi? Just for your info umeshajiuliza kwa nini wako group ya kupata referral visa kabla ya kuingia TZ.

Na legitimate business za West Africa hapa Tanzania unaelewa undani wake? Mimi naongea with facts.
Tatizo dangote ni mweusi mwenzetu ndio maana maneno yamekuwa mengi angekuwa mhindi au mzungu wala msingepiga hizi kelele za kujifanya mna uchungu sana na nchi.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Ulikuwa na mawazo sawa na haya wakati Magu akikutana na akina Rostam au hata huyo Dangote hapo Ikulu?!

Unaweza kueleza hapa utofauti wa Dangote aliyekuwa amekutana na Magu na Dangote aliyekutana na SSH ili tuamini Dangote huyu anayekutana na SSH ni mwando tu wa kuturudisha kwenye uchuuzi lakini Dangote yule wa Magu alikuwa ni wa kutupeleka kwenye industrial nation!

View attachment 1797748

Hapo juu ni Mwenyekiti wa Bharti Enterrprise!!

Haya sasa... tofauti ya ukutanaji huu wa sasa ni ipi ukilinganisha na ule wa zamani hadi uone huu wa sasa unataka kuturudisha kwenye uchuuzi?!
Uliona popote nilipoandika humu JF nikiyashabikia na kuyashangilia matukio hayo?

Lakini usitake kulazimisha nionekane kama mpinzani wa uwekezaji wa aina yoyote nchini mwetu kwa kutaka kukidhi matakwa yako.

Kama hukusikia nikiweka msimamo wangu wazi kwa matukio hayo, huo ndio ushahidi kuwa niliyaunga mkono?

Lakini hata kama ningeunga mkono, rekodi ya huyo mtu inajulikana katika eneo hili la uwekezaji, hata kama alikuwa anadanganya, lakini rekodi ipo, kwamba aligombania maslahi ya nchi.

Ninachosikia pekee sasa hivi ni "Nafungulia nchi"; haijulikani inafunguliwa toka kifungo kipi na ni vigezo vipi vitakavyoambatana na kufungua huko.

Walanguzi kama wewe mnaipenda sana lugha ya namna hiyo, ndiyo maana unapapatikia sana hali hii ya kutupeleka kwenye uchuuzi usiokuwa na mipaka.
 
Fuatilia changamoto anazopitia Dangote kwenye kiwanda chake cha saruji (cement) huko mtwara, kuna somo linaitwa mjasiriamali na yanayomzunguka 'the entrepreneur and his environment ' tumepitia kwenye sera zisizo tabirika (policy uncertainty) huwezi kupanga namna ya kukuza biashara kwa sera ambazo hazina muelekeo 'you can not plan business growth with policy uncertainty' wafanya biashara wengi waliumizwa na hicho kikosi chenu cha 'task force ' kazi ya ziada inahitajika kurudisha imani ya wawekezaji na wafanya biashara na ndicho anakifa fanya Mama
"...na ndicho anakifanya mama"
Marekebisho ya hizo sera mbovu yalifanyika wakati gani; hebu eleza hili kidogo.

Ni yeye mwenyewe kazirekebisha, au kuna utaratibu wa kufanya kazi hiyo?
 
Tunavutia wawekezaji lakini njia za kuwekeza na Sheria za uwekezaji haziko Ikulu.

Tunazo Wizara na ofisi zinazohusika. Kwa kuwa marais wetu wameamua kuwa ni waalikaji wa wawekezaji, nawaona Mawaziri na wahusika wengine wakikaa pembeni na kufanya kazi za sekretari, kukopi kumbukumbu za mikutano na ahadi za Rais. Hii haifai. Leo Dangote, kesho wawekezaji wa Ulaya, kesho wachina, wahindi, Wakenya, n.k. mpaka lini hali hii?

Sasa Ikulu ni ya wafanyabiashara, wakiitwa wawekezaji. Ni vigumu kwa mkulima mashuhuri kufika Ikulu. Rais hajakutana na kundi lolote la waajiliwa wake; iwe Jeshi, waalimu, idara ya afya, nk.

Imekuwa ni rahisi sana Dangote kufika Ikulu kujadili uwekezaji wa kiwanda kimoja tu. Kuna udhaifu gani unaotafutwa Ikulu? Ni kugawa shares za kiwanda kama tulivyowahi sikia?

Huu sasa umekuwa mtindo wa kudumu kwa marais wetu wa CCM.
MATAGA bwana!!eti mwekezaji mwenye kiwanda kimoja tu!!kwa akili yako unafikiria kuwa muwekezaji mkubwa ni yule mwenye viwanda vingi?hiyo tsh.trilion.1.7 kwenye huo uwekezaji wake ni ndogo?!!kwani aliyewakimbiza /kujenga mazingira yasiyotabirika ya biashara si alikuwa RAIS?Basi ni RAIS huyo huyo ndio anayeweza kujengea taswira mpya kwa hao wawekezaji.Yaani jamaa lile sijui hata lilitoka wapi
 
Tunavutia wawekezaji lakini njia za kuwekeza na Sheria za uwekezaji haziko Ikulu.

Tunazo Wizara na ofisi zinazohusika. Kwa kuwa marais wetu wameamua kuwa ni waalikaji wa wawekezaji, nawaona Mawaziri na wahusika wengine wakikaa pembeni na kufanya kazi za sekretari, kukopi kumbukumbu za mikutano na ahadi za Rais. Hii haifai. Leo Dangote, kesho wawekezaji wa Ulaya, kesho wachina, wahindi, Wakenya, n.k. mpaka lini hali hii?

Sasa Ikulu ni ya wafanyabiashara, wakiitwa wawekezaji. Ni vigumu kwa mkulima mashuhuri kufika Ikulu. Rais hajakutana na kundi lolote la waajiliwa wake; iwe Jeshi, waalimu, idara ya afya, nk.

Imekuwa ni rahisi sana Dangote kufika Ikulu kujadili uwekezaji wa kiwanda kimoja tu. Kuna udhaifu gani unaotafutwa Ikulu? Ni kugawa shares za kiwanda kama tulivyowahi sikia?

Huu sasa umekuwa mtindo wa kudumu kwa marais wetu wa CCM.

Wanafiki wakubwa hajusema wakati wa Magu sasa kila kitu mnatafuta mabaya hata ya kutuletea kazi
 
Tunasubiri muda wake uishe,afanye haraka na hao wawekezaji wake. Tumerudi kuwa shamba la bibi.

Mngetusikiliza kuhusu Corona badala ya kuweka ushabiki mzee wenu angekuwepo sasa muda wa washamba umekwisha tupeleke taifa mbele. Nawasalimia kwa jina la mungano wa Tanzania
 
Tunavutia wawekezaji lakini njia za kuwekeza na Sheria za uwekezaji haziko Ikulu.

Tunazo Wizara na ofisi zinazohusika. Kwa kuwa marais wetu wameamua kuwa ni waalikaji wa wawekezaji, nawaona Mawaziri na wahusika wengine wakikaa pembeni na kufanya kazi za sekretari, kukopi kumbukumbu za mikutano na ahadi za Rais. Hii haifai. Leo Dangote, kesho wawekezaji wa Ulaya, kesho wachina, wahindi, Wakenya, n.k. mpaka lini hali hii?

Sasa Ikulu ni ya wafanyabiashara, wakiitwa wawekezaji. Ni vigumu kwa mkulima mashuhuri kufika Ikulu. Rais hajakutana na kundi lolote la waajiliwa wake; iwe Jeshi, waalimu, idara ya afya, nk.

Imekuwa ni rahisi sana Dangote kufika Ikulu kujadili uwekezaji wa kiwanda kimoja tu. Kuna udhaifu gani unaotafutwa Ikulu? Ni kugawa shares za kiwanda kama tulivyowahi sikia?

Huu sasa umekuwa mtindo wa kudumu kwa marais wetu wa CCM.
Raia wa kawaida angekutana na viunzi 1000 kisha anakata tamaa wakati ndiye mwenye-nchi ambaye biashara yake, kula kwake, kuuguzwa kwake, kusafiri kwake, kununua bidhaa kwake, kulima mazao ya chakula na na biashara ndio KODI endelevu inayoifanya serikali kuwa hai na kutanua misuli huku yenyewe ikijiimarisha kwenye fahamu kuu tano za kimamlaka ili kuendelea kutawala.

1. Kusikia lakini wanaweka pamba masikioni
2. Kuona lakini wanapuuzia kwakuwa wananchi inawezekana ni washamba
3. Kunusa hatari na usalama lakini wakipima hadhi ya mtendewa ambaye ndie mwenye-nchi
4. Kuhisi wanapendwa au kuchukiwa bila ushahidi halisia kutoka kwa wenye-nchi
5. Kugusa kwa uthubutu wa kuhakiki hatari au usalama na pengine kuogopa kugusa kisichogusika kwa hofu ya kupoteza uungwaji mkono na wenye-nchi

Raia akiwa na dukuduku ambalo limesababisha changamoto ya kukata tamaa na maisha baada ya kudhulumiwa au kukutana na viashiria vya rushwa ili tatizo lake litatuliwe anaambiwa aanzie kwa mjumbe, mwenyekiti mtaa/kitongoji/shehia, mtendaji, mkuu wa wilaya, DAS, DED, RAS, DC, RC, WZR nk bila mafanikio yoyote. Akiomba nafasi kuonana na kiongozi mwenye mamlaka ya juu wasaidizi wanampigisha kona za kimizengwe hadi anapoteza imani na kutelekelzaq azma yake.

Tajiri akionekana kwa hisia unanusa pafyumu lakini mlalahoi anahisiwa anawweza kuhatarisha usalama-maajabu sana!!!

*Kwa hiyo ni rahisi sana kwa NGAMIA kupenya kwenye tundu la SINDANO kuliko TAJIRI wa mali (sio tajiri wa akili, hekima, busara na maarifa) na SIFA za KUJIKWEZA.
 
Tunavutia wawekezaji lakini njia za kuwekeza na sheria za uwekezaji haziko ikulu! Tunazo wizara na ofisi zinazohusika. Kwa kuwa marais wetu wameamua kuwa ni waalikaji wa wawekezaji, nawaona mawaziri na wahusika wengine wakikaa pembeni na kufanya kazi za sekretari, kukopi kumbukumbu za mikutano na ahadi za rais. Hii haifai. Leo Dangote, kesho wawekezaji wa Ulaya, kesho wachina, wahindi, Wakenya, n.k. mpaka lini hali hii?

Sasa ikulu ni ya wafanyabiashara, wakiitwa wawekezaji. Ni vigumu kwa mkulima mashuhuri kufika ikulu. Rais hajakutana na kundi lolote la waajiliwa wake; iwe Jeshi, waalimu, idara ya afya, nk. Imekuwa ni rahisi sana Dangote kufika ikulu kujadili uwekezaji wa kiwanda kimoja tu! Kuna udhaifu gani unaotafutwa Ikulu? Ni kugawa shares za kiwanda kama tulivyowahi sikia? Huu sasa umekuwa mtindo wa kudumu kwa marais wetu wa CCM

Tunasubiri muda wake uishe,afanye haraka na hao wawekezaji wake. Tumerudi kuwa shamba la bibi.

2766199_FB_IMG_1620411212769.jpg
 
Ogopa sana Technolojia, mtoa mada kule juu ana matatizo sana. Ana imani za kishamba kuwa ili kupata uwekezaji, unatakiwa na sera za NGUNGULI, mambo ambayo yamepitwa na wakati. Hizi enzi ni za utandawazi, utajikuta unaogelea peke yako. Dunia hii ni ya uwekezaji(narudia uwekezaji na siyo uchuuzi)!
Falsafa za kichuuzi na kujitenga zimeonesha kushindwa, kifo cha mende!
Wanyonge ni wengi (kama alivyokuwa akiwaita meko)ni wapiga kura wazuri sana, ila uchumi wa nchi unaendeshwa na watu wachache(matajiri)huo ndio ukweli sasa aliwaaminisha wanyonge kuwa adui wao ni tajiri!!!
 
"...na ndicho anakifanya mama"
Marekebisho ya hizo sera mbovu yalifanyika wakati gani; hebu eleza hili kidogo.

Ni yeye mwenyewe kazirekebisha, au kuna utaratibu wa kufanya kazi hiyo?
Swali fikirishi Nyumba ikiwa na ufa utasubiri ibomoke?
 
Wanyonge ni wengi (kama alivyokuwa akiwaita meko)ni wapiga kura wazuri sana, ila uchumi wa nchi unaendeshwa na watu wachache(matajiri)huo ndio ukweli sasa aliwaaminisha wanyonge kuwa adui wao ni tajiri!!!
"Tanzania hakuna matajiri,wanaoitwa matajiri ni wapigaji"
 
Back
Top Bottom