Kwanini Walimu wengi ni maskini hapa Tanzania?

Kwanini Walimu wengi ni maskini hapa Tanzania?

Mimi sio mwalimu ila nadhani zifuatazo zinaweza kua ni sababu kwa kiasi kikubwa;-
  1. Mishahara midogo. Kada ya ualimu ni miongoni mwa kada zenye mshahara midogo ukilinganisha na kada nyingine. Nakumbuka mwalimu mwenye shahada gross salary yake ni 730,000 sasa hii ikikatwa inabaki almost 400,000k. Gharama za maisha yani nyumba, nauli, usafiri, ada za watoto, umeme, chakula, n.k inakua ni shida.
  2. Kukosekana kwa posho. Katika maofisi mengi kumekuwepo na posho mbali mbali na watumishi wengi wananufaika sana na hizi posho. Mojawapo kubwa kabisa ni posho ya kazi za ziada. Yani ukifanya kazi kuzidi masaa yanayokubaliwa kiutumishi unakua subject to compensation. Ila sasa huko kwa walimu hakuna posho ya over time, hakuna house allowance, hakuna transport allowance etc. Kukosekana kwa hizi posho kunafanya walimu waishi mshahara to mshahara. Na kwakua mshahara ni mdogo, wanajikuta katika ukata
  3. Kukosekana kwa safari. Kwenye maofisi mengi kuna vijisafari safari vya hapa na pale vya training, workshops, seminars, technical commitees na kadhalika. Safari katika kada ya ualimu ni chache sana na unakuta wanachaguana mkuu wa shule au makamu wake au academic officers. Ndani ya miaka mitatu possibility ya mwalimu kusafiri na kulipwa per diem ni ndogo sana na safari yenyewe utakuta ni ya muda mfupi haizidi wiki.
  4. Kukosekana mianya ya kupiga dili. Walimu wateja wao ni wanafunzi. Hakuna dili yoyote hapo. Kwanza elimu ya siku hizi ni bure. Hakuna motisha wala hakuna mzazi atakupa laki mbili kama zawadi kwa kumfundisha mwanae vizuri. Kuna watu huko bandarini wana mijengo Mbweni kwa hizi dili ndogo ndogo za hapa na pale.
  5. Kutochangamka. Walimu wengi hua hawako sharp kwenye harakati nyingine za kimaisha ukiachana na kazi. Wengi wanakua busy kukimbizana na wanafunzi unakuta mtu yuko job had saa kumi na moja jioni anawapa wanafunzi wachelewaji adhabu wakati huo hana hata genge la kuuza nyanya pale home au wanafunzi watano wa kupiga pindi after work.





Nimechokoza mada
Point ya 5 uko sahihi sana, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wanaboa mno.
 
Swala ni kuamua tu kwa sababu hamjaamua kuwa MATAJIRI.. acha hio dhamana nenda kajiajiri utaondokana na UMASIKINI.. na unaonekana hicho unachokifanya haujakipenda unaanzaje kuwa TAJIRI.. au kipato cha kati. Kuna kilimo, biashara tofauti tofauti.. ACHA KULALAMIKA FANYA MAAMUZI UFANIKIWE.. uondokane na UMASIKINI USIOUTAKA
 
Mwalimu wa shule gani ?inategemea na shule na elimu yako.
 
Jamaa ni wajinga sana.
Mimi mlinzi wa taasisi moja hivi ya serikali. Posho ya headmaster ambayo ni laki 2 Mimi napewa hiyo kama nauli.
Bado posho zingine , badala ya kudai haki zao wao wanajiona sehemu ya serikali
Nadhani kipato kidogo kinachangia,
 
Soma fani nyingine Kama uhasibu ,biashara kwa muda wako. omba recartegorization mkuu au hamia idara nyingine nje ya ualimu.
Asome degree nyingine, hata Open university kwa mfano uchumi then hamia omba uhanie idara ya mipango kama mchumi.

Serikali zinawadharau sana walimu wetu Nakumbuka Kuna Rais mmoja hapa Tanzania aliondoa kitu inaitwa allowance. Shame!

Ikiwa kama kulikuwa na maslahi yyt kwa nchi au mtu binafsi basi ilikuwa ni laana kwa mtu huyo. Wanafanya kaz iliyotukuka kwa taabu sana.
 
jiongeze .....kuwa sharp.....umaskini ni akili yako....kama unaweza kufundisha watoto wetu, na wakatusua...huwezi jiuliza wewe umekwama wapi....jiongeze kieleimu na fikiria kipato kingine nje ya mshahara.........ila mchezo wenu wa kutuharibia watoto...laana inawasonga.....mhame ccm...
si wanajilipa kwa migegedo na wanafunzi. Bikra unlocker🤣😂🤣😂
 
Mimi ni mwalimu hali yangu ya uchumi sio nzuri sana kulinganisha na watu w kada nyingine, tatizo lipo wapi maana hata walimu wenzangu hali zao sio nzuri, tunakosea wapi walimu
tatizo ulijui? ngoja nikwambie tatizo ni MIKOPO MIKOPO MIKOPO nimerudia mara 3. watimishi mnakopa sana bila kuongeza uzalishaji isipokuwa mahitaji ndiyo yanaongezeka
 
sawa
Tatizo hakuna.
Mishahara duni ndio source ya umaskini kwa watumishi wa umma Tanzania.
Taasisi zingine mishahara duni ila kuna posho karibu aina 3, na wizi wa kutosha.
Walimu mkaibe chaki na muuze maandazi kwa wanafunzi mtatoboa.
Nyie endeleeni kuwa waaminifu muhakikishe CCM inaendelea kukaa madarakani.
Walimu wengi wapumbavu.
wapumbavu kabisa, wanapenda sifa na vielehele
 
Mimi sio mwalimu ila nadhani zifuatazo zinaweza kua ni sababu kwa kiasi kikubwa;-
  1. Mishahara midogo. Kada ya ualimu ni miongoni mwa kada zenye mshahara midogo ukilinganisha na kada nyingine. Nakumbuka mwalimu mwenye shahada gross salary yake ni 730,000 sasa hii ikikatwa inabaki almost 400,000k. Gharama za maisha yani nyumba, nauli, usafiri, ada za watoto, umeme, chakula, n.k inakua ni shida.
  2. Kukosekana kwa posho. Katika maofisi mengi kumekuwepo na posho mbali mbali na watumishi wengi wananufaika sana na hizi posho. Mojawapo kubwa kabisa ni posho ya kazi za ziada. Yani ukifanya kazi kuzidi masaa yanayokubaliwa kiutumishi unakua subject to compensation. Ila sasa huko kwa walimu hakuna posho ya over time, hakuna house allowance, hakuna transport allowance etc. Kukosekana kwa hizi posho kunafanya walimu waishi mshahara to mshahara. Na kwakua mshahara ni mdogo, wanajikuta katika ukata
  3. Kukosekana kwa safari. Kwenye maofisi mengi kuna vijisafari safari vya hapa na pale vya training, workshops, seminars, technical commitees na kadhalika. Safari katika kada ya ualimu ni chache sana na unakuta wanachaguana mkuu wa shule au makamu wake au academic officers. Ndani ya miaka mitatu possibility ya mwalimu kusafiri na kulipwa per diem ni ndogo sana na safari yenyewe utakuta ni ya muda mfupi haizidi wiki.
  4. Kukosekana mianya ya kupiga dili. Walimu wateja wao ni wanafunzi. Hakuna dili yoyote hapo. Kwanza elimu ya siku hizi ni bure. Hakuna motisha wala hakuna mzazi atakupa laki mbili kama zawadi kwa kumfundisha mwanae vizuri. Kuna watu huko bandarini wana mijengo Mbweni kwa hizi dili ndogo ndogo za hapa na pale.
  5. Kutochangamka. Walimu wengi hua hawako sharp kwenye harakati nyingine za kimaisha ukiachana na kazi. Wengi wanakua busy kukimbizana na wanafunzi unakuta mtu yuko job had saa kumi na moja jioni anawapa wanafunzi wachelewaji adhabu wakati huo hana hata genge la kuuza nyanya pale home au wanafunzi watano wa kupiga pindi after work.





Nimechokoza mada
No 5 umenena vijijini kuna fursa nyingi Sana kupitia mikopo yao wanaweza wakafanya biashara hata ya kukusanya mazao na mifugo kuuza mijini na kutoa mijini bidhaa za mahitaji ya siku kwa jumla na kusambaza vijijini.
True TANZANIA nzima Hakuna mzazi mtoto wake kafanya vizuri amewahi kwenda kuwashukuru walimu.
 
Muhimu walimu wajiongeze pili waache kuisaidia ccm kuiba kura ndio chanzo cha laana ya maisha yao. Unaposhiriki dhuluma na wewe ni sehemu ya dhuluma na dhuluma sio baraka.
Nchi ni watu na sio chama. Vyama vitapita nchi ipo Sana.
 
Police na walimu acheni kuisaidia ccm kuiba kura Ili mpate baraka toka kwa Mola Ili maisha yenu yasiwe ya laana. Thamani yenu nyie ni wakati wa uchaguzi tu baada ya hapo ccm haina habari nanyi.
Viongozi wote wa nchi hii wanatoka kwenye ualimu kwann awaboreshi maisha yenu hali nao walikuwa walimu. Jibu ni kwa sababu mnashiriki dhuluma.
 
Hii inaukweli na wakistaafu ndio inasikitisha, cha kujivunia kwao huwa hawazeeki hawa watu wapo vilevile miaka yote
 
Mimi ni mwalimu hali yangu ya uchumi sio nzuri sana kulinganisha na watu w kada nyingine, tatizo lipo wapi maana hata walimu wenzangu hali zao sio nzuri, tunakosea wapi walimu
Hii inawahusu hadi walimu wa chuo yaani lectures?
 
Mimi ni mwalimu hali yangu ya uchumi sio nzuri sana kulinganisha na watu w kada nyingine, tatizo lipo wapi maana hata walimu wenzangu hali zao sio nzuri, tunakosea wapi walimu
Wewe ndio maskini usiwahusishe wengine..

Tena kama kituo chako cha Kazi ni mjini utaishia kuwa maskini milele unless uwe na akili ya biashara ambayo huna.
 
Wewe ndio maskini usiwahusishe wengine..

Tena kama kituo chako cha Kazi ni mjini utaishia kuwa maskini milele unless uwe na akili ya biashara ambayo huna.
Umaskini wangu huenda ukawa ni utajili kwako, njoo dm nikutume instagram kwangu ujue nipoje nimelata hili hapa ili lijadidiliwe ili lisaidie wengine
 
Back
Top Bottom