Kwanini Walimu wengi ni maskini hapa Tanzania?

Kwanini Walimu wengi ni maskini hapa Tanzania?

Usiwepende kufanya generalization haraka haraka

Tumia akili wakati mwingine sio emotions
mzee, majority ni wahuni tu. sisi wengine tumesoma kwa effort zetu waalimu wamefanya kazii ndogo sana. nakumbuka kipindi fulani nipo form six, ticha mmoja wa history sijui nini, akawa anafundisha anananiki desa la nyirenda ambalo mimi nimeshalitafuna lote, shule moja huko KIlimanjaro. mimi nikawa siandiki wala nini. akaja kwa fujo ati ananivamia kwanini siandiki? nikamwambia mimi notes hizo zote ninazo na nimeshazisoma...alinichukia hadi namaliza. uzuri ni kwamba nilifaulu vizuri sana. kama wewe ni mwalimu, majoirty mpo hivyo.
 
Upo sahihi, kwa mwalimu mwenye degree anaeanza ni 430,000. Sasa hiyo ukigawa kwa siku 30 exactly per day unaingiza 14,333/=
Sasa hicho ni kipato cha mtu wa kawaida sana ambaye ukimuona mtaani utamdharau mfano mchoma mahindi au bodaboda.
Kinacholeta mwalimu afeli maisha na mchoma mahindi atoboe ni life expenses.
Hapa mwalimu atataka apange nyumba ya laki kwa mwezi, kiwi kila siku, msosi nyama kwa sana. N.k
Lakin huyu dereva boda atapanga chumba cha 30 elfu na maisha ya kawaida ndo maana ataweza kutoboa maisha na kuongeza kipato.
Ushaur kwako mwalimu, jiongeze kwa huo mshahar wako, ile jion pika uji tembeza au supu kwa maeneo ya mjini ila kwa vijijn unaweza ukalima mazao mbalimbl ya muda mfupi na kwa malengo ya muda mrefu nenda Iringa huko panda miti ,patachichi, chai n.k baada ya miaka kadhaa we ni don.!
Mwalimu wa ngazi ya degree anaanza na gross ya 720,000 to 730,000
 
Mwalimu wa ngazi ya degree anaanza na gross ya 720,000 to 730,000
waalimu wangekuwa wanapata hivyo wangesumbua sana. hata hivyo, wenye degree ni wachache mno ukilinganishana wa primary school na sekondary kwa hao wenye diploma walioungaunga, na bado wakiwa shuleni wanatutesea watoto wetu.
 
jiongeze .....kuwa sharp.....umaskini ni akili yako....kama unaweza kufundisha watoto wetu, na wakatusua...huwezi jiuliza wewe umekwama wapi....jiongeze kieleimu na fikiria kipato kingine nje ya mshahara.........ila mchezo wenu wa kutuharibia watoto...laana inawasonga.....mhame ccm...
Idiot, SI walimu wote NI wa kuume!!

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Mimi ni mwalimu hali yangu ya uchumi sio nzuri sana kulinganisha na watu w kada nyingine, tatizo lipo wapi maana hata walimu wenzangu hali zao sio nzuri, tunakosea wapi walimu
Tatizo lenu walimu mnawaza bifu na wanafunzi tu ndiyo sababu
 
ila hiyo haiondoi ukweli kwamba ualimu kwa africa ni kada ya watu waliofeli. ukifeli form four, unaenda chuo cha ualimu. ukifeli form six unaenda chuo cha ualimu. ile cream nzuri ndio inaendela mbele. kwani uongo? sasa mfano mtu amefeli kwenda kidato cha juu, na unampa afundishe english, ambayo hata yeye haijui? no wonder tumejifunza kiingereza tulipofika chuo kikuu.
Kama div 4 ni kufeli basi ualimu ndio kada iliyochukua wanafunzi wenye kaunafuu kuliko kada zingine!

Ngazi ya cheti, wakiume walikuwa wanachukuliwa mwisho IV.27 na wakike mwisho point 28 wakati kada zingine walichukuliwa mpaka wenye 29(wakiume ) huko huko kwenye vyuo vya serikali..

Au ulikuwa mdogo sana wakati huo hata usiyajue hayo?
 
Kama div 4 ni kufeli basi ualimu ndio kada iliyochukua wanafunzi wenye kaunafuu kuliko kada zingine!

Ngazi ya cheti, wakiume walikuwa wanachukuliwa mwisho IV.27 na wakike mwisho point 28 wakati kada zingine walichukuliwa mpaka wenye 29(wakiume ) huko huko kwenye vyuo vya serikali..

Au ulikuwa mdogo sana wakati huo hata usiyajue hayo?
acha kujifariji, chuo gani hicho? unaweza kwenda form six kwa division four point 26? tutajie shule ishughulikiwe mapema. tuje university, mwalimu gani wa degree ambaye hakuanza na diploma alipata division one point 3,4,5,6 au hata 8 tu. tutajie.
 
Huh, umespendi ukiwa mnafanyaje?
tumefundishwa na waalimu miaka saba tukiwa primary, miaka minne tukiwa sekondari, na miaka minne tukiwa advanced. piga hesabu hiyo, 7+4+2= ngapi? au wewe ulikuwa unafikiria nini mzee kwenye akili yako. manake kimtokacho mtu ndicho kilichoujaa moyo wake.
 
Posho na mishahara midogo na muda mwingi mnakua kazini pia kwa mtumishi wa umma hasa mwalimu ukifanya ka biashara tu lazima kazini wakuwekee longolongo
 
tumefundishwa na waalimu miaka saba tukiwa primary, miaka minne tukiwa sekondari, na miaka minne tukiwa advanced. piga hesabu hiyo, 7+4+2= ngapi? au wewe ulikuwa unafikiria nini mzee kwenye akili yako. manake kimtokacho mtu ndicho kilichoujaa moyo wake.
Hilo linatosha kuwajua walimu?
 
acha kujifariji, chuo gani hicho? unaweza kwenda form six kwa division four point 26? tutajie shule ishughulikiwe mapema. tuje university, mwalimu gani wa degree ambaye hakuanza na diploma alipata division one point 3,4,5,6 au hata 8 tu. tutajie.
Hivi umeelewa kweli nilichokiandika?

Sent from my SM-J105H using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Upo sahihi, kwa mwalimu mwenye degree anaeanza ni 430,000. Sasa hiyo ukigawa kwa siku 30 exactly per day unaingiza 14,333/=
Hapana hauko sahihi..
Mwalimu mwenye Degree akianza Kazi leo analipwa TGTS D1 = 710,000/= CCM wakikata anabaki na 545,000/=

Mwenye Diploma ni 450,000 (TGTS E1)
CCM wakikata anabaki na 415,000/=

#YNWA
 
Back
Top Bottom