Kwanini wanajeshi wanapenda sana kukopa vitu ovyo?

Kwanini wanajeshi wanapenda sana kukopa vitu ovyo?

Hii imekuwa kero sana baadhi ya wanajeshi wamekuwa wakikopa madukani na hawarudishi vitu na pengine hutumia ubabe wao kutokulipa hata unakuta ukimpeleka polisi ana achiwa tu maana hutumia kazi yao kujiona wakubwa kwa wenzao yaani wanapewa pesa kubwa kila mwezi lakini huishia kwenye pombe na kukopa hovyo sana wanajeshi badilikeni
🤣sawa mkuu tumeskia
 
Hata ingekuwa wew kaka lazima udai haki yako
Sikatai wewe kudai haki yako, naona unaongeza mdai, mwanzo ulilalamikia kukopwa, baadae tena wanamshika mkeo makalio, mimi nimetilia shaka tu hayo madai yako, yanaweza kuwa ya uongo kwa nia ya kuwachafua mbele ya jamii, hivi kumshika mke wa mtu makalio mbele ya mume wake siyo jambo dogo, nashangaa ulikaa kimya, ukitagemea mloge je na kama ni mchawi.

Kule juu nimekulaumu kwa sababu unajua, wanajeshi hawarejeshi deni, kwanini uwakopeshe, mbaya watu wenyewe wanakushikia mkeo makalio.
 
Kaka nakaa mtaa wenye madini mengi sana mbona wengine wananilipa kwa wakati ila huyu mmoja ndo ananifanya mimi kama nyani anipi pesa yangu kwa wakati.
Ndiyo maana Ulipohama mada, ukaandika mkeo wanamshika makalio, nikajua unaandika uwongo, umepishana lugha na mmoja, ukaamua kuwachafua wote.
.
Sasa umedhitisha mwenyewe wengi wanakulipa tena kwa wakati, ispokua huyo mmoja tu.
Haya naenda kubet mimi naona hapa huna hoja, maana watu, hatana maduka, lakini kuna watu tunawadai kwa mrefu tu.
 
Nina marafiki polisi,uhamiaji. A zimamoto na wanajeshi wanalipwa allowance nyingi katikati za kisheria tena kama una familia ndo unapewa hela nzuri maana asiye na familia anapewa 300000 hapo baada ya week unapokea mshahara ila card zao zimeshikiliwa micro credit
Punguza ujuaji wakati haujui,eti asiye na familia hulipwa 300,000.Unajua maana ya ration allowance wewe?
 
Bro pole sana nishamjua mlengwa Mimi nimesoma nae advance alinizima pesa ya raman imagine msela wangu kabisa yule wa kupiga nae pindi na comb moja PCB lakin anashindwa kutoa 50000 ya ramani huku nilimfanyia fear sio bei zake lakin alinizungusha nikaamua nimchane na namba nikafuta sijui wana shida gan hawa watu
Mimi kuna mmoja namdai milioni 7, zilikuwa za kulipia mafundi site, nilisimamia nyumba yake na nimeshamkabidhi na amehamia tayari since 17 october mwaka jana.

Hilo deni la malipo ya mwisho lina mwaka sasa ni kupigwa kalenda tu, mbaya zaidi ni jirani yangu kabisa nyumba zinatazamana , nashindwa kumuwashia moto kutokana na huu ujirani.
Kuna project anataka kunipa, ndio imekuwa kisingizio kwamba tukianza project mpya ntakulipa kwanza deni lako ndio tuendelee.
Mi namuangalia tu...
 
Back
Top Bottom