Huwezi kulinganisha Ulaya na kwetu, wao maendeleo yao yamekuwa pole pole mpaka kufikia hapo walipo. Sisi maendeleo yetu yameanza baada ya wao kuja afrika kututawala.

Wao walikuwa wakichoma moto wachawi katika karne ya 16, sisi leo karne ya 21 tunauwa watu kwa uchawi.

Vile vile sera zetu na mifumo yetu ya ujamaa na kujitegemea na kuwa na chama kimoja ndiyo umetudumaza kabisa. Iweje tuwe tumepata uhuru kipindi kimoja na Indonesia na Malaysia na leo wao wametuacha mbali sana kiuchumi na sisi hatujijui hatujitambui?

Rushwa iliyokithiri bila ya wakosaji kuchukuliwa hatua

Mengine bado nafikiri
 

Kuna matatizo matatu makubwa Tanzania siwezi kuelezea kwa undani hapa
(1) Mfumo- Serikali ni kubwa sana na watu kila wakipata tatizo wanataka serikali itatue. Kuna vitu vingi ambayo serikali isingetakiwa kufanya kama Tanesco na ATC. Lazima tuelewe serikali ikitumia pesa kwenye ATC ni hiyo hiyo pesa ingeweza kwenda kwa walimu. Hata kama Chadema wakichukua nchi bila kubadilisha mfumo Tanzania haitaendelea.
(2) Rushwa- Lazima tuwe na sheria ngumu na kali zaidi kwenye rushwa. Mahakama ni lazima iogopwe.
(3)Uongozi- Hatuna viongozi wabunifu wa mbinu za kutatua matatizo. Hili ni hata upinzani hatujawahi kusikia "big ideas" Tanzania kwa muda mrefu. Nyerere pamoja na matatizo yake alikuwa na bid agenda mfano JKT. Sasa hatujasikia hata kiongozi mmoja kuja na idea kubwa kama Wanavyuo kufundisha kawa wakati wa JKT, au kuweka "Six Sigma" kwenye idara za serikali.
(4) European Mentality- Watanzania wengi wanafikiria kama wa Europeans lakini Tanzania siyo ni kubwa hivyo ni vigumu kufanya vitu kama Europe. Mfano Kwasababu europe ni ndogo ni rahisi kwao kuwa na hospitali moja kubwa maana kila mtu anaweza kwenda hospitali kama iko karibu. Tanzania ni kubwa na watu wengi wako vijijini vilevile madoctor ni wachache! sasa badala ya kutaka kuwa Europe tuje na namna ya kutatua matatizo yetu wenyewe kama kuwa na Mobile Hospitals. Hii ni system ambayo madoctor wanakuwa wanaenda vijijini kwa special trucks na kutibu watu na kutoa chanjo. Hii haitahitaji madoctor kujengewa nyumba au kuwa na hospitali kubwa kila mahali kitu ambacho hatuwezi. Hii itapunguza wauguzi kwa % kubwa sana. Barabara ni mfano mwingine tunajenga barabara ndogo kama Europe wakati sisi tunaendesha mbali na tuna nafasi ya kutosha. Hawa wa European wanatushauri kama ilivyo kwao na sasa tuna barabara nyembamba. Nenda nchi kubwa kana USA uone barabara zao ni kubwa sana lakini Tanzania na viongozi wamengangania sana european ssystem ambayo haitafanikiwa Tanzania.
 
VICIOUS CIRCLE OF POVERTY OR A COUNTRY IS POOR BECAUSE IT IS POOR

Poverty is a great curse. It is the biggest hurdle in the way of economic development. Ranger Nurkse in ''Problems of Capital Formation in Underdeveloped Countries'' describes 'vicious circle of poverty as the basic cause of under-development of poor countries. According to him, a country is poor because it is poor. Being poor, a country has little ability or incentive to save. The low of saving leads to low level of investment and to deficiency of capital. The low of investment leads to low level of productivity. When the productivity per worker is low, the real income will obviously be low and so there poverty and vicious circle is complete.
On the side of demand when people have low real income the demand for goods is bound to be small. In the small size of market, there is no incentive of invest in real or human capital. When the rate of investment is low, the productivity of the factors of production is bound to be low. Low productivity leads to low per capital income which is rapidly absorbed by the rising population growth. The country, therefore, remained poor.
The vicious circle of underdevelopment
Lower per capita incomes make it extremely difficult for poor nations to save and invest, a condition that perpetuates low productivity and low incomes. Furthermore, rapid population growth may quickly absorb increases in per capita real income and thereby may negate the possibility of breaking out of the underdevelopment circle.

How to break this vicious circle of poverty?
Remaining poor is certainly no crime. The accepting of poverty and allowing it to continue is certainly a crime. Briefly, the vicious circle of poverty can be broken in developing countries including Tanzania by adopting following measures.

(1) Increase in savings.

The vicious of circle of poverty can be broken by making serious efforts in increasing the volume of real savings both at the level of in development the govt. The govt. can also mobilize foreign savings for capital formation country.

(2) Higher per capital growth rate.

The per capital growth rate should be higher than the rate of growth of population. This objective be achieved by increasing the level of employment in the country and reducing the rate of population growth. If the rate of increase in real per capital income is the same as the rate of growth of population, the real income per person will remain unchanged.

(3) Efficient use of natural resources.
The less developed countries (LDC) are not making the efficient use of the natural resources available to them. At present the multi national companies (MNCs) of the advanced countries are exploiting these resources more for their own economic benefits. The economic advantages of the natural resources must pass on to the benefits of the poor masses of the LDCs.

(4) Employment of human resources.

Many of the less developing countries including Tanzania are faced with serious unemployment problem. The quality of labour force is also poor. The low level of literacy, malnutrition, absence of proper medical care etc are all barriers to economic development Effective measures have to be taken for sufficient investment in human capital to break the poverty barrier of the LDCs.

(5) Increasing the stock of capital goods.
The LDCs can come out of the vicious circle pf poverty if the wealthy class is motivated to make their savings available for investment in productive activates rather than using their wealth on the purchase of urban real estates, precious metals etc.

(6) Technological advance.

The people in less developed countries (LDCs) can break the poverty barrier by adopting and applying advance technologies which are appropriate to the resources available to them.

(7) Role of the advanced nations.
T

he advanced nations san help the less developed countries in breaking the poverty barrier by:
(i) expanding volume of trade with them.
(ii) increasing the flow of private and public capital in basic infrastructure.
(iii) provision of direct aid in basic social sectors such as education, health etc.
(iv) provision of soft loans for development.
(v) writing off loans.
(8) Role for the government. The government in the less developed country is in the key position to deal effectively with social institutional obstacles to growth and breaking out the vicious circle of poverty. It can greatly root out political corruption and bribery. It can provide incentives to save and invest. It can increase agricultural production by introducing effective land reforms in the country.
 
Nchi yetu ni maskini kwa sababu idadi kubwa ya raia wake kama wewe hawajui kwa nini nchi hii ni maskini hivyo kupelekea kutojua nini cha kufanya.

Mkuu, Nchi hii sio Maskini! Ila wananchi ndio Maskini!
Matatizo watu kuwa maskini ni mengi mno pamoja na haya ndiyo yanayosababisha;
1 ccm
2 Ujinga
3 Ubinafsi
4 uongozi dhaifu
unaweza ukaongeza!
 
Tanzania ni maskini kwa sababu hizi hapa
i)Kulindana kwa wanaofuja mali zetu
ii)Ujinga
iii)Uoga wa kujaribu
iv)Kukosa viongozi shupavu na makini
v)Kuwaabudu wazungu kutoka ukolono mpaka sasa
vi)Wasomi kuendelea kuuza nchi yao bila uchungu wowote et
 
Zakumi,

Sasa namwelewa Mwanakijiji alipozungumzia swala la UMASKINI kwa sababu tunaviumiza vichwa vyetu ktk kutafuta tafsiri na mazungumzo badala ya kuweka nguvu hizi ktk utekelezaji maana hakuna tafsiri ya UMASKINI ktk UCHUMI zaidi ya matokeo ya uwezo mdogo ktk kupata maendeleo. Ni hali halisi ulonayo regardless of what You have in store na ndio maana nikasema kamauna njaa wakati chakula kipo ndani ya friji huwezi kusema huna njaa ati nimeshiba wakati tumbo lako ni empty.

Labda ktk mfano huo huo naweza kusema kwamba Ulimbukeni wetu ulotokana na kutawaliwa ndio uliotuponza kiasi kwamba chakula kipo ghalani toka mahindi, mchele, mtama na mawele isipokuwa tunataka chakula cha Mlimani City na Shoppers ambacho kiko tayari chenye hadhi ya kimataifa na kieleezo za Utajiri.. bila kujua thamani kubwa ya mahindi na mawele tuloyaacha maghalani ambayo wazungu wanakuja tena kwetu kuyataka kutokana na wao kuthamini Organic.

Hapa nikiwa na maana kwamba tuna all economic resources ambazo zinaweza kabisa kutuondoa ktk umaskini (njaa) lakini sii chakula tunachokitaka na tunatumia nguvu kubwa ktk Imported good ili kujibadirisha sisi tuonekane sawa ama kama wazungu. Sisi tunashindwa kukubali reality, na kama nisemavyo kila siku WATU na MAZINGIRA ndio focus kubwa ya neno maendeleo. Maendeleo sio watu pekee bali mazingira yao pia na wlaa huwezi kuita utajiri in aconomic term ikiwa mazingira ni mabaya. Hivyo policies zote zinapowekwa hutazama kuboresha vitu hivi vyote na sii kimojawapo.

Huyo Mmasai sisi tutamwita tajiri kwa sababu tunazithaminisha hizo ng'ombe zake 500 ktk bei za soko na kutoa namba zinayomweka Mmasai ktk utajiri au laa, lakini maadam mazingira yake yapo ktk hali mbaya utajiri wake unabakia tumbo tupu kwa sababu kuwepo kwa ng'ombe hawa na kuthaminishwa kwake bila kubadirisha maisha na mazingira yake utajiri huu ni mtupu. Na ndio maana huyo mmasai hana habari kwamba yeye ni tajiri japokuwa ana ng'ombe 500 sawa na sisi wenye dhahabu ambazo hazibadilishi maisha wala mazingira yetu. Huyu Masai sii Fukara bali ni Maskini kwa sababu umaskini unakusanya hali na mali za watu na mazingira kiuchumi. Na pia tukumbuke kwamba huyu Mmasai mwenye ng'ombe 500 ni kati ya 1% ya Wamasai wenye utajiri au ana represent ktk kundi la 1% ya wafugaji. Bado Tatizo la uzalishaji na usambazaji ktk mgao wa keki unatushinda.

Navyofikiria mimi, tukiondoa leo neno maendeleo basi bila shaka hata neno maskini litapotea japokuwa fukara na tajiri yatabakia kwa sababu inawahusu WATU tu na sio mazingira waliyopo. Na ktk umaskini ndio unakuta vitu kama elimu vinachangia sana kutambua mahusiano ya watu na mazingira ktk uboreshaji wake ili kukidhi mahitaji yetu, ni kama kusema utatumiaje mazingira ulonayo ili kukidhi mahitaji yenu. Na neno uchumi linatokana na elimu ya kuelewa, kutambua na kupima production, distribution, and consumption of goods and services. Maadam jamii zetu zinakua na mahitaji yanayozidi kupanda wakati uwezo wa kutosheleza mahitaji haya unazidi kupungua, ndipo neno maskini linapochukua nafasi kama kipimo cha kushindwa na hivyo kusema Umaskini ni matokeo ya kushindwa kukidhi mahitaji yetu.

Kuna jambo moja hunikera sana mimi japokuwa halikubaliwi na Watanzania wengi..nalo ni matumizi ya Lugha ya kiswahili. Tumejenga utamaduni wa kuiga hadi lugha ili kuwahudumia watanzania wasiojua kiingereza!..Hii kitu kweli haikukaa sawa. Hivi kweli tunatumia lugha kama means of communication baina ya wananchi au na kina nani?. Sasa matokeo yake mashirika yote nchini utakuta ma CEOs, board members na executive officers ni wageni ambao wataajiri Watanzania wanaozungumza lugha yao hao ma TX ili ku serve Watanzania ambao hawajui kiingereza. Hii kweli hatufanyi kinyume?

Kwa nini nafasi zote za juu ktk ashirika yatu zichukuliwe na wageni ambao hawawezi kuwasiliana na wananchi ila kwa kumtumia Mtanzania anaye ajiriwa kama mkarimani baina ya mgeni na Watanzania halafu hata huyo Mtanzania anapoichukua kazi ile hafahamu kwamba yeye anatumiwa kama mkarimani ila naye anakuwa mzungu ktk mawasiliano kuwataka walio chini yake na wananchi wazungumze kiingereza..

Inakuwaje Wachina wanapoingia nchini inawachukua onlt miezi sita au mwaka wanazungumza kiswahili na sio kiingereza kuwasiliana na wananchi lakini MKenya atakuja Tanzania na kupewa wadhifa na nafasi kubwa kwa sababu anazungumza kiingereza, pengine hana elimu kuliko Mchina au Mtanzania..Na mwisho nawaacha na swali jingine, kwa nini nchi zote zinazotumia lugha ya kigeni ambayo sii yao ndio wako nyuma ktk maendeleo?. Hakuna Mhindi wala Mchina asiyejua kusoma na kuandika Kichina hadi maofisini mwao vitu vimeandikwa Kichina au kihindi lakini sisi hata matangazo yetu yameandikwa kiingereza ilihali ni asilimia chini ya 20 ndio wanazungumza kiingereza. Hapa mlengwa wa matangazo hayo ni nani > Unamtangazia nani?
 

Mkandara,

Hata nchi zinaotusaidia zina tafsiri ya kwanini sisi ni masikini. Wanaweza kusema kuwa kipato cha wastani cha mTanzania ni chini ya dollar moja ya kiMarekani kwa siku.

Ndani ya nchi tunaweza kuwa na tafsiri ambayo itatumika kupima maendeleo yetu. Kutokuwa na tafsiri ndio sababu ya nchi kuwa na mipango mingi isiyo na matokeo yoyote yenye kuweza kufanyiwa tathmini. Na kutokuwa na tafsiri imefanya watu wapende mambo yenye kuwapa status katika jamii kuliko kufanya vitu vyenye kuboresha maendeleo.

Napenda unielewe kuwa tafsiri hiyo sio lazima ieweke mpaka ngazi za chini za kijamii. Lakini kwa watu wenye kushika madaraka na wasomi, ni muhimu kuwa na tafsiri fulani ya kuanzia.

Kwa mfano, tunaweza kusema kuwa mtanzania mwenye maisha bora ni lazima aishi au familia yake iishi kwenye nyumba ya kudumu ambayo ina vyumba vitatu. Yenye huduma za choo na maji safi. Na wakazi wa nyumba hiyo wasizidi saba.

Ukichukua tafsiri hii ya maisha bora. Utaona familia nyingi za kitanzania kwa kutumia rasimali chache na tena zinazopatikana ndani ya nchi wanaweza kufikia ubora wa maisha.

Na baada ya muda fulani unaweza kuongeza kuwa nyumba hizi ziwekewe umeme au ziwe karibu na barabara na mashule.

Kuhusiana na matumizi ya lugha. Mzungumko mzima wa uchumi haulengi watanzania wa kawaida. Hivyo umuhimu wa lugha yetu wenyewe unakuwa haupo. Lakini mChina, mHindi au Mwarabu anapokuja Tanzania anakuja kufanya biashara na watanzania wa kawaida. Hivyo yeye kuelewa lugha yetu anaona kuna faida.
 
Mzunguko gani mkuu wangu ikiwa Wajerumani wanaongea wote kijerumani na kiingereza ni baadhi ya watu tu hao hawana mbona kusema hivyo kuwa uchumi wao haulengi wajarumani!. Nenda India, China na duniani kote wanaona umuhimu wa kutumia lugha zao ktk mawasiliano na hujifunza za kigeni ktk maswala kwa sababu ndogo kabisa ya mawasilinao tu ya kawaida..Ukienda Ujarumani toka gari unayoendesha, mitambo ya viwandani, maofisini, microwave, radio magazeti TV station ni Kijarumani tupu na sio wao tu sehemu zote nilizowahi kutembelea.

Hakuna nchi inatumia lugha ya Kigeni ktk mawasilino ndani ya nchi yake isipokuwa nchi maskini ambazo hatujaendelea na tunazidi kuwa maskini. Huoni kama tayari tumekubali matokeo ya Utumwa wa fikra na pengine kikwazo cha maendeleo yetu kutoweza kuwasiliana sisi wenyewe..Utaendeleza vipi kilimo kama msomi wako kasomea Kilimo kwa kiingereza akienda kwa mkulima anashindwa kumwelekeza Mkulima kwa kiingereza maana mkulima hajui kiingereza, na Huyo msomi anashindwa kujieleza kwa kiswahili?. Sasa utaweza vipi kuzalisha kilimo ili kujitosheleza ikiwa mwanzo tu tumegota ktk mawasiliano baina yetu wenyewe..

Leo kule FB kwa Mwanakijiji nimeandika hivi, Ebu wabunge wetu waende vijijini wakaombe kura za wananchi kwa kiingereza tuone kama wataeleweka!..Hata Hii JF iwekwe kwa kiingereza tuone kama itapata umaarufu huu. Kwa hiyo kuendelea kwa JF na kufanikiwa kwa JF au wabunge kunatokana na lugha kwanza inayotumika baina ya makundi wanaolengwa. Maendeleo ya Tanzania hayamlengi mgeni isipokuwa sisi wenyewe na sisi ndio tutakaoijenga Tanzania. Sioni sababu kabisa ya mashirika yetu ku hire wageni kwa sababu ya kiingereza ili hali walengwa - consumers hawazungumzi lugha hiyo. Huu ni ulimbukeni kufikiria kwamba mgeni anayezuungumza kiingereza atakuwa na ufanisi wa kazi ama kuongeza uzalishaji..Hii kasumba mbaya sana.

Hao wageni tunafanya biashara nao ambao duniani kote kila mmoja wao ana lugha yake na anaithamini, sisi ombaomba ndio hubadilisha lugha zetu tunapokutana nao lakini sio wao. Alipokuja Waziri mkuu wa China alizungumza Kichina akawa na mkarimani wake akitafsiri sio kiswahili bali kiingereza! wakati huyo huyo Waziri mkuu wa Mchina akienda France ataongea Kichina na Mfaransa ataongea Kifaransa wakarimani katikati haukna aliyelazimika kutumia lugha ya mwenzake na the all Europe na jumuiya yao, ni asilimia ndogo sana kwa kila nchi wanazungumza kiingereza tena as a second language wala hakuna uhalisia wa matumizi ya lugha kama tunavyofikiria sisi.

Na swala la Kipimo cha Umaskini kuhusiana na pato la mwananchi mimi huwa siliwekei maanani sana ikiwa hiyo Dollar moja ingemwezesha mtu kununua chakula kwa siku nzima isingekuwa na maana kwetu... lakini sivyo kwa sababu kinacho thaminishwa ni pato la taifa kwa fikra za kusadikika hata kama ni asilimia 1 tu ndio wenye kushika asilimia 99 ya utajiri huo..
 
We mtu utamaduni wake unamwambia kuzaa watoto wengi na kuwa na wake/ ng'ombe wengi ndio utajiri.
Nchi yake tajiri kiasili na wala nakuwa na historia ya ushindani mkubwa.

Halafu unataka kumpangia utajiri kwa minajili ya kizungu.

Unafikiri anaweza kuwa tajiri?
 
Kwa maana hiyo, nadhani hili ndio tatizo letu kujibu tafsiri hizi:- Ikiwa fukara kinyume chake ni Tajiri. Je Maskini kinyume chake ni nini?..
 
Wakuu Kiranga na Mkandara, wenzetu ndo maana walikuja na indicators kama vile GDP nk ili kuweza kuelezea hii kitu.

Kwa upande mwingine pia, hatuwezi kuiondoa serikali/viongozi kwenye equation ya umasikini.

Kama kuna great amount of unequal distribution of the nations wealth, na kama kuna athari zinazotokana na kuwa nyuma kimaendeleo zinazotokana na mambo kama rushwa nk, then unakutana na matatizo ya umasikini uliokitihiri.

Umasikini uko kila mahali kwenye jamii mbali mbali humu duniani, lakini ni wa tofauti kwa levels tu,(ndiyo maana pia kuna matajiri zaidi ya matajiri wengine).Just kama ilivyo kuwa kuna masikini zaidi ya masikini wengine.

Kuna masikini ambao hata mlo, nguo pa kulala hawana nk hapa tunazungumzia kwa ujumla serikali kushindwa kutoa huduma muhimu kwa jamii kama vile kuwasaidia wasiokuwa na kazi nk.

Kwa wenzetu kwa kiasi kikubwa masikini wa aina hiyo ambao ni homeless nk, basi utakuta wana historia ya matatizo ya kisaikolojia na matumizi ya madawa, kwa marekani utakuta ni wale maveterans wa vita. Na pia hawawezi kukosa msaada na wanaweza kurecover na kurudi kwenye shughuli za uzalishaji, hawakuwepo huko kwenye matatizo ya umasikini kwasababu hakukuwepo na kazi za kufanya.

Lakini kama unakuta kuna watu wanakufa kwa kukosa mahitaji muhimu ya maisha, basi huo ndo umasikini wenyewe.

Nina uhakika kabisa tunaweza kuondokana na umasikini kwasababu tuna resources za kutosha kuweza kuwa na taifa lenye mafanikio, tatizo ni uongozi.Hilo hawatakaa waweze kulipinga, wao ndo wametufikisha hapa tulipo, potential tunayo, viongozi hatuna.
 
Kwa maana hiyo, nadhani hili ndio tatizo letu kujibu tafsiri hizi:- Ikiwa fukara kinyume chake ni Tajiri. Je Maskini kinyume chake ni nini?..

Fukara kinyume chake ni tajiri? Toa maana ya fukara unavyoelewa wewe.
 
Nyani Ngabu,
Mkuu tupe wewe sababu zake na sio ile ya Miafrika ndivyo Tulivyo! nadhani kubadilishana mawazo kunaweza kuchangia sana tukubali makosa au mapungufu yetu.

Kwa nini Afrika kusini mwa jangwa la sahara ni maskini? Na kwa nini Afrika Kusini (nchi) ni tajiri kushinda nchi zingine za Afrika?

Bila wazungu kulowea kule unadhani Afrika Kusini ingekuwa hapo ilipo sasa?
 
Hakuna pahala mzungu atapaendeleza na kuishi kama si yeye mwenye ku call shots, SA utajiri walionao ni kiumbe gani asingetaka kuishi?however walizidisha(apartheid) ndo maana, mbona sehemu nyingi tu mzungu bado anatawala indirectly kwasababu anaishi humo?

Mfano Jamaica na sehemu nyingi tu.

Ndo historia ilivyo, they came out on top from the begining, lakini haina maana kuwa we are inferior kwasababu we are a certain race.

Mugabe na Zimbabwe ni mfano hai kabisa kuwa wakikutolea nje ni mbaya.

Hata SA wenyewe waliwekewa vikwazo na US na wengineo vya kiuchumi ndo wakakubali mabadiliko na kwamwachia Mandela nk.
 
Ukweli ndo huo, wazungu ndo wenye ku call shots, ukijidai kujuwa huendi mahali.

Mwafrika hajui kuwa kuondokana na umasikini ni vita literally!
 

Mkandara,

Uchumi wa Tanzania unaoendeshwa kiserikali haumlengi mtanzania katika mzunguko wake. Na mfano mkubwa ni ziara za rais wako. Kama angejua kuwa solutions zinaweza kupatikana Tanzania, angezumza na wananchi wake kwa kiswahili kama vile wakati anapoomba kura.
 


Kiranga,

Hicho ndicho kitu cha kwanza nilichomwambia Mkandara. Lakini hili kuendelea kuongea naye ikabidi ni-moderate msimamo wangu.

Kuna viongozi Tanzania, wamesoma na wanaelewa ubora wa maisha ni nini. Lakini wakichota pesa serikalini, wanakwenda makwao kununua ngo'mbe, kuoa wanawake na kuwa na watoto wengi. Wanafanya hivyo kwa sababu hivyo ndio vitu vinavyowapa status katika jamii zao.

Tukirudi kwenye maendeleo ya kijamii, kila jamii ni dynamic na inaiga. Korosho na mazao mengine ya biashara yalikuwa hayana asili ya Tanzania. Lakini kwa sababu yalikuwa yanatoa kipato, watu wakaanza kuiga.

Kama watu wanaweza kuiga vitu vinavyowezekana katika jamii zao, juhudi zifanyike kuwaonyesha vitu gani wanaweza kuvifanya katika mazingira yao. Kwa mfano ujenzi wa nyumba za kudumu zenye kutumia materials yanayotokana katika sehemu husika ni kitu kinachowezekana.

Kuwa na choo ni kitu kinachowezekana. Kuwa na maji within a walking distance ni kitu kinachowezekana sehemu nyingi za Tanzania.
 
Nguruvi3, mara nyingi huwa nadhani wewe ni alias ya Dr Slaa, many times michango yako inakuwa kama the real Slaa, inawezekana siye, however i admire youre ideas many times!
Nakubaliana all the way na analysis yako.
 
Nguruvi3, mara nyingi huwa nadhani wewe ni alias ya Dr Slaa, many times michango yako inakuwa kama the real Slaa, inawezekana siye, however i admire youre ideas many times!
Nakubaliana all the way na analysis yako.

Jmushi1 and Nguruvi2,

Siku zisije mkawa very dissapointed. Dr Slaa anaweza kuchaguliwa kuwa rais na akamaliza muda wake nchi ikiwa bado masikini.

Wanafalsafa wa uchumi wamesha-prove kuwa uongozi ni kitu muhimu but it isn't the only prerequisite for development. Africa ina-nchi zaidi 40, na huwezi kusema kuwa katika nchi zote hizi hajawahi kutokea kiongozi mzuri.

Nyerere mliyemtumia kwenye mifano, tulikaa naye na aliongoza kwa miaka 23 na watu tulimchoka.

Kwanini mzungu ambaye ni dikteta, mnyonyaji, kupe, mla rushwa anaweza kuja Afrika na kujenga nchi wakati mwaAfrica mwenye kukaribia utakatifu jasho linamtoka?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…